Ukweli mchungu kuhusiana na mradi wa Stiegler's Gorge

mnengene

JF-Expert Member
Nov 21, 2011
4,089
6,273
Ni hivi watu wengi wanaandika bila kuujua ukweli.

Ukweli ni kwamba kabla ya mradi wowote mkubwa kutekelezwa lazima kifanyike kitu kinachoitwa Environment Impact Assessment.

Ukweli ni kwamba serikali iliunda team iliyojumuisha maprofesa nguli kufanya Environment Impact Assessment ambapo serikali yetu iliwalipa fedha kufanya kazi hiyo.

Ukweli ni kwamba team hiyo ilifanya kazi hiyo na kuandika ripoti yake ambayo ilieleza kwamba madhara ya kwnye mazingira kama mradi huu ukitekelezwa yatakuwa makubwa sana hivyo wakashauri mradi huu usitekelezwe na wakashauri serikali ijikite kwenye kuzalisha umeme kwa kutumia gesi ambayo inapatikana mtwara kwani uzalishaji wa umeme kwa kutumia umeme hautakuwa na madhara kwenye mazingira kama mradi wa stiglers gorge.

Sasa bana ripoti hii iliwasilishwa kwanza wizara inayohusika na mazingira ya bwana January.

Waziri akakubaliana na ripoti naye akaifoadi ikulu.

Bwana kolichotokea almanusura huyu jamaa apoteze kazi.

Ukweli ni kwamba jiwe alimuita akamtukana sana kwanini amekubaliana na ushauri wa hao maprofesa na kisha akamtupia ripoti yake .

Isingekuwa aibu ya jiwe akifahamu jinsi January alivyomfanyia figisufigisu ya kutengeneza matokeo yaliyomsaidia kumuweka madarakani pale mlimani city huyu january alikuwa afukuziwe mbali.

Sasa twende kwenye hoja, kwa nini serikali yetu inakataa repoti ya timu ya iliyoiunda na kuilipa ifanye kazi na wao wakafanya na wakashauri.

Mbona Serikali hiii hii haitoi vibali vya kuendeleza miradi ambayo environment impact assessment zimeshauri kwamb arhari za mradi ni hasi.

Kuna msemo wa kiingereza unaoheshimika sana unaosema "no research no right to speak"

Research imefanyika imeeleza mradi ni mbaya kwenye mazingira watu bila hata kufanya research nyingine wanakurupuka kuukataa ushauri wa wataalamu.

Tusiwalaumu sijui bunge la ujerumani , mimi binafsi siungi mkono kupangiwa mambo yetu na hao wajerunani.

Ukweli ni kwamba mradi huu ulikataliwa kwanza na timu yetu sisi wenyewe watanzania iliyohusisha maprofesa wataalamu ambao mwisho wa siku kama kawaida ya jiwe ukitoa mapendekezo tofauti na mtazamo wake unaitwa sio mzalendo au sijui umetumwa na mabepari.

Aina hii ya uongozi ya kukataa mapendekezo ya wataalamu ni mojawapo ya element za utawala wa kidikteta.
 
Ni hivi watu wengi wanaandika bila kuujua ukweli.
Mbona hujaweka ukweli mkuu, hiyo ripoti ulishaiona wewe au unasikiasikia tu kama hao wasiojua? Nimesoma bandiko lote, lakini hata wewe naona unasikiasikia tu kuhusu hiyo ripoti.

Sikubaliani na Magufuli kama kaamua tu yeye mwenyewe kama kawaida yake ya kutumia mabavu. Lakini hata kama hiyo ripoti ipo kweli na hao wataalam waliona madhara ya mradi huo, lingekuwa jambo zuri kuitoa hiyo ripoti watu waisome na kuijadili. Bado Magufuli angekuwa na uwezo wa kushawishi ripoti iwekwe pembeni kwa sababu anazoona ni za lazima mradi ufanyike kwa manufaa ya taifa. Na mimi ningekuwa mmojawapo wa kuunga mkono hatua hiyo, kwa sababu naamini mradi huo una manufaa makubwa kwa taifa, na hizo sababu za uharibifu wa mazingira athiri yake ingeweza kupunguzwa katika 'design' ya mrada wenyewe.

Kwa hiyo taarifa yako hapa bado ni 'hearsay', na hasa ukifikiria Magufuli kaingia 2015, hiyo 'study' ya wataalam hao iliteuliwa na nani, lini na ilifanya kazi kwa muda gani. Je hata magazeti hayakuweza kutoa habari yoyote juu ya utafiti huo ukatuwekea hapa tusome? Hata majina tu ya waliohusika katika utafiti huo.

Ukweli ni kwamba serikali iliunda team iliyojumuisha maprofesa nguli kufanya Environment Impact Assessment ambapo serikali yetu iliwalipa fedha kufanya kazi hiyo.

Ni akina nani hawa maprofesa, una jina hata la mmoja wao? Ni nani aliyewateua na lini?

Ukweli ni kwamba team hiyo ilifanya kazi hiyo na kuandika ripoti yake ambayo ilieleza kwamba madhara ya kwnye mazingira kama mradi huu ukitekelezwa yatakuwa makubwa sana hivyo wakashauri mradi huu usitekelezwe na wakashauri serikali ijikite kwenye kuzalisha umeme kwa kutumia gesi ambayo inapatikana mtwara kwani uzalishaji wa umeme kwa kutumia umeme hautakuwa na madhara kwenye mazingira kama mradi wa stiglers gorge.
Kamati na ripoti unayoiandika hapa iliteuliwa na kufanya utafiti wake" baada ya Magufuli kutaka bwawa lijengwe" au kamati hiyo iliteuliwa kabla na kuandika ripoti yake kabla ya kutangazwa na Magufuli kuhitaji mradi huo ufanyike?
Mimi sioni kumbukumbu za uteuzi wa kamati wakati Magufuli alipotangaza nia ya ujenzi wa mradi huo. Kama wewe unazo kumbukumbu hizo tuwekee hapa tuzione.
 
Sikio la kufa siku zote alisikii dawa...tena kasharuhusu watu walime ndani ya mita sitini kwenya ardhi oevu na wajenge na kuchunga kwenye hifadhi za wanyama pori wetu...tanzania ijiandae kuwa jangwa kama darful
Kumbuka msukuma hana kitu kinachoitwa kutunza mazingira. Miti na uoto asili sio issue kwake.
Labda kutunza ng'ombe.

Mimi ndukiiiiii....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi nimeosoma ripoti ya WWF kuhusu mradi huu, kama katiba tuu imeweza kukanyangwa na tuko ok kabisa, what is EIA compared?.

Kwenye hili mimi naungana na serikali yetu kuwa Tanzania is a sovereign state, tutaamua mambo yetu wenyewe bila kuingiliwa au kupangiwa na mataifa ya nje.

Natolea mfano wa mradi wa Kamba Samaki, shrimp farming kwenye Rufiji Delta, ulipitishwa vizuri tuu, lakini kabla ya utekelezaji, mashirika ya kimataifa ya mazingira yakaja na EIA nyingine, tukapigwa stop mradi ukafa. Hoja ya wanamazingira ni kilimo kile kingeathiri uoto wa asili wa mikoko.

Ukiangalia cost benefits na value benefits za mradi na faida za mikoko, mikoko are nothing compared.

Kama ulifuatilia issue ya Kihansi Hydro Electric Project, mradi ulichelewa sana kwa hoja ya vyura wa Kihansi hadi Marekani walipokubali kuwa relocate wakahamishwa, mradi ulipokamilika wakarudishwa. Ukiangalia faida za nchi inayohitaji umeme na faida ya vyura ni nothing compared.

Sasa kwenye Stieglers ni vile vile wanataka kutupangia, kule nyuma waliweza kwa sababu fedha walikuwa wanatoa wao. Kwa Stieglers, watakwama kwa sababu this time around fedha ni zetu.
Hili jambo niliisha lizungumza sana humu
Hawa WWF wakafie mbali!, kwa sababu uamuzi kuhusu Mradi huu, umeishafikiwa, hivyo uhamasishaji wa mjadala huu ni too little too late!.

Hoja za msingi za WWF ni hizi
  1. Mradi huu utaathiri Selous Game Reserve ambayo ni moja ya World Heritage Sites hivyo ujenzi katika eneo hili utaathiri ecology ya Selous kwa kuathiri mazingira, yatakayoathiri uchumi na maisha ya watu, hoja hii inakuwa defeated na manufaa ya Mradi huo ukilinganisha na athari za Mradi huo, manufaa ni makubwa mara 1000 kuliko athari!.
  2. Eneo litakalotumika ni kilomita za mraba 1,200km2, hivyo kulifanya kuwa bwawa kubwa kuliko yote eneo la Afrika Mashariki, hivyo litakausha maziwa madogo madogo yote ya jirani, litaathiri utalii, na kukomba fertility yote ya Ardhi ya eneo hilo hadi kwenye Delta ya Rufiji Delta, hivyo kuua samaki, na kuathiri uvuvi wa Kamba samaki na kamba koche unaotegemewa ka watu 200,000 wa eneo hili, pia hoja hii inapigwa chini kwa hoja kuwa Tanzania tuna maeneo mengi ambayo ni waste land, what is km za mraba 1,200?. Hao watu 200,000 watakaothiriwa na Mradi huo ni nini ukilinganisha na Wamasai wanaishi ndani ya eneo la hifadhi ya Loliondo ambao hawaruhusiwi kulima, bali wanalishwa bure?. Kwa vile faida za Mradi ni kubwa, serikali inaweza kuwaambia watu hao 200,000 wasilime na badala yake watalishwa bure maisha yao yote, hivyo Mradi uendelee!.
  3. Mradi unaelezwa unakwenda kinyume cha mikataba ya kulinda World Heritage ambayo Tanzania tumesaini, this also is nothing!, Tanzania tumesaini mikataba kibao ya kimataifa ya haki za binaadamu na kila siku serikali inakiuka mikataba hiyo, kama rais Magufuli, ameikanyaga katiba alioapa kuilinda, what are the chances kuheshimu mikataba ya kimataifa kama itatuzuia kupata manufaa, to hell with mikataba ya kimataifa at the expense of development.
  4. Mradi huo utaazuia tani milioni 16.6 za virutubisho vya Ardhi kwa mwaka, hivyo kusababisha mmomonyoko wa Ardhi kwenye Delta ya Rufiji, hii pia sio hoja, kwa ukubwa wa ardhi ya Tanzania, shughuli za kibinaadamu kama uchimbaji wa madini, unaleta athari kubwa zaidi za kimazingira na kusababisha sio tuu mmomonyoko Mkubwa wa Ardhi, bali kutuachia mahandaki mengi na makubwa Zaidi kuliko hizo tani milioni 16.6 kwa mwaka, hivyo Mradi utaendelea!.
  5. Hoja kuwa Mradi huo utaathiri sio tuu Mbuga ya Selous, bali pia Delta ya Rufiji na Bonde la Mto Kilombero, hapa tena tunaangalia faida za Mradi na kulinganisha na athari za kimazingira, then faida za Mradi ni kubwa kuliko athari!, Mradi utaendelea!.
  6. Hawa wazungu na wana mazingira ni watu wa ajabu sana, nakumbuka walivyotucheleweshea Mradi wa Kihasi kwa ajili tuu ya vyura wa Kihansi hadi Marekani walipokubali kuwahamisha vyura hao hao kuwahifadhi nchini Marekani, kisha kuwarudisha ndipo Mradi ukapitishwa!, yaani vyura walikwamisha mradi muhimu, ujinga huu walimfanyia Nyerere na Mwinyi, lakini kwa Magufuli, watagonga mwamba!.
  7. Hata Mradi wa Kamba Samaki kwenye Delta ya Rufiji, ulikwamishwa na wanamazingira kwa hoja kuwa Mradi huo utaathiri hifadhi ya miyombo!, what is miyombo compared to manufaa ya kiuchumi?.
  8. They can just go to hell, kama katiba ya Tanzania imekanywagwa for the expense ya maendeleo, rais Magufuli aliruhusu tuachane na na hizi EIA katika kupushi Tanzania ya Viwanda, hivyo sasa hapa ni kazi tuu, hakuna cha mazingira, world heritage wala cha nini, Tanzania tunataka Umeme wa kutosha kuendeshea Tanzania ya viwanda!
Hoja zote hizo ni katika kulinda kitu kinachoitwa the sovereignty of our nationalism kwamba Tanzania ni ya Watanzania, tuna uhuru wa kupanga mambo yetu kwa manufaa yetu bila kuingiliwa na mtu mwingine yoyote, hivyo hawa WWF, wasituingilie!.

Lakini on the other hand, kiukweli kabisa japo mimi sio mchumi, lakini sera za uchumi za serikali ya Magufuli ni sera za ajabu sana!.
  1. Huu Mradi wa Umeme wa Stglers Gorge ulizungumzwa tangu Enzi za Nyerere na haukutekelezwa kutokana na hixo hizo environmental concerns na mpango wa Tanzania Power System Master Plan (2016 update), umeonyesha Mradi huu ndio the last option kama miradi mingine mikubwa itashindikana, Mradi wa priority ni Umeme wa kutumia gesi, lakini sasa Magufuli kaingia, mara ghafla hatuzungumzii tena Mradi wa Umeme wa gesi, sasa Mradi huu ndio kipaumbele!, kipaumbele for what?.
  2. Japo ni kweli, the cheapest power generation projects ni hydropower projects, lakini Tanzania hatujifunzi tuu, kutokana na global warming na mabadiliko ya tabia nchi, kuendelea kutegemea Umeme wa maji ni very unpredictable, Richmond ilisababishwa na hii over dependency on hydropower, hivyo kulipotokea ukame, kilichotukuta sote tunakijua!, sasa gesi tunayo tena ya kutosha, na Umeme wa gesi, japo ni expensive kuliko hydro ni cheap kuliko diesel generation, kwa nini tusijikite kwenye gesi yenye uhakika, tunataka kuzamisha matrilioni ya Fedha kwenye pata potea nyingine ya kutegemea mvua?.
  3. Maajabu ya uchuni wa Magufuli pia yapo kwenye kuishadadia sana hii SGR, kama tumekuwa na reli mbili ya meter gauge ya Kati na Tazara, zote zina under perform, tumeanzisha bandari kavu ya Isaka ili ipokee mizigo ya Rwanda, Burundi na DRC, lakini haifunction na reli ya kati ipo, tena hadi eneo la ICD ya Rwanda watu wanalima tuu mahindi!, hii SGR italeta miujiza gani?.
  4. Uchumi wa Tanzania unategemea kilimo, hivyo Tanzania ya kweli ya viwanda, ni Tanzania ya agro processing industries, tunahubiri Tanzania ya viwanda, bila kuinua sekta ya kilimo, hivyo viwanda ni malighafi gani ya kuendesha Tanzania ya viwanda kama sekta ya kilimo ni totally neglected, Magufuli yuko bize kununua ndege na kujenga miundombinu, what has ndege, barabara za juu kwa juu, uwanja wa ndege wa Chato, na hii SGR has to do with sekta ya kilimo?.
Mimi bado nasisititiza, Kupata Maendeleo ya Kweli, Tanzania Inahitaji Systems Not Dramas, Ze Comedy na One Man Shows!.

Tuache Siasa ktk Uchumi: Wachumi tuelimisheni Dhambi ya Fixed Deposit na Faida ya Fedha Kukaa tu BoT

Uchumi wa Magufuli: Precision Air Yapumulia Machine. Yapunguza Wafanyakazi 136!

Mnatambua kuwa baadhi ya Maamuzi ya Magufuli yanaligharimu Taifa kiuchumi?

Priorities Zetu Nini?. Dola Milioni 300 Zinatosha Kununua Smelter, Jee Tununue Au Tuzitumie Kwa Mahitaji Muhimu Zaidi?.

P
Uzalendo wa kweli wa nchi yako ni pamoja na kusupport mipango kamambe
ya maendeleo ya nchi yako hata kama mipango hiyo itasababisha maumivu kwa walio wengi as long as itakuwa na faida kubwa kitaifa huko baadae.
P
 
Kelele za chura hazimzuii ng'ombe kunywa maji. Nyie na hao mabeberu wa WWF tuacheni tujenge bwawa letu tuzalishe umeme nafuu. Hakuna miradi wowote usiokuwa na madhara kwa mazingira. Kwenye kuchimba dhahabu hawapigi kelele kwa sababu makampuni yao ndiyo yananufaika. Kwenye kuchimba uranium hawapigi kelele kwa sababu nchi zao ndo zinanufaika. Sisi tukitaka kuzalisha umeme, kelele kila kukicha. Kwanza sehemu inayoathirika ni 2% tu ya mbuga yote ya selous game reserve!
 
Mimi nimeosoma ripoti ya WWF kuhusu mradi huu, kama katiba tuu imeweza kukanyangwa na tuko ok kabisa, what is EIA compared?.

Kwenye hili mimi naungana na serikali yetu kuwa Tanzania is a sovereign state, tutaamua mambo yetu wenyewe bila kuingiliwa au kupangiwa na mataifa ya nje.

Natolea mfano wa mradi wa Kamba Samaki, shrimp farming kwenye Rufiji Delta, ulipitishwa vizuri tuu, lakini kabla ya utekelezaji, mashirika ya kimataifa ya mazingira yakaja na EIA nyingine, tukapigwa stop mradi ukafa. Hoja ya wanamazingira ni kilimo kile kingeathiri uoto wa asili wa mikoko.

Ukiangalia cost benefits na value benefits za mradi na faida za mikoko, mikoko are nothing compared.

Kama ulifuatilia issue ya Kihansi Hydro Electric Project, mradi ulichelewa sana kwa hoja ya vyura wa Kihansi hadi Marekani walipokubali kuwa relocate wakahamishwa, mradi ulipokamilika wakarudishwa. Ukiangalia faida za nchi inayohitaji umeme na faida ya vyura ni nothing compared.

Sasa kwenye Stieglers ni vile vile wanataka kutupangia, kule nyuma waliweza kwa sababu fedha walikuwa wanatoa wao. Kwa Stieglers, watakwama kwa sababu this time around fedha ni zetu.
Hili jambo niliisha lizungumza sana humu

Uzalendo wa kweli wa nchi yako ni pamoja na kusupport mipango kamambe
ya maendeleo ya nchi yako hata kama mipango hiyo itasababisha maumivu kwa walio wengi as long as itakuwa na faida kubwa kitaifa huko baadae.
P
Inahitaji akili kubwa sana kuchakata bandiko lako ili kupata rangi yako Halisi Mkuu.
 
Mimi niseme wazi kuwa katika hili namuunga mkono rais wetu ... Yaani hizo hasara wanazozisema hao watu wa mazingira sioni kama zinalingana na faida tutakazozipata kwa mradi huo kuendelea... Rai yangu ni kuwa mradi huu ukamilike haraka sana kabla hajaja rais mwingine ambae hatujui kuwa atakuwa na msimamo gani katika hili ...
 
Mimi nimeosoma ripoti ya WWF kuhusu mradi huu, kama katiba tuu imeweza kukanyangwa na tuko ok kabisa, what is EIA compared?.

Kwenye hili mimi naungana na serikali yetu kuwa Tanzania is a sovereign state, tutaamua mambo yetu wenyewe bila kuingiliwa au kupangiwa na mataifa ya nje.

Natolea mfano wa mradi wa Kamba Samaki, shrimp farming kwenye Rufiji Delta, ulipitishwa vizuri tuu, lakini kabla ya utekelezaji, mashirika ya kimataifa ya mazingira yakaja na EIA nyingine, tukapigwa stop mradi ukafa. Hoja ya wanamazingira ni kilimo kile kingeathiri uoto wa asili wa mikoko.

Ukiangalia cost benefits na value benefits za mradi na faida za mikoko, mikoko are nothing compared.

Kama ulifuatilia issue ya Kihansi Hydro Electric Project, mradi ulichelewa sana kwa hoja ya vyura wa Kihansi hadi Marekani walipokubali kuwa relocate wakahamishwa, mradi ulipokamilika wakarudishwa. Ukiangalia faida za nchi inayohitaji umeme na faida ya vyura ni nothing compared.

Sasa kwenye Stieglers ni vile vile wanataka kutupangia, kule nyuma waliweza kwa sababu fedha walikuwa wanatoa wao. Kwa Stieglers, watakwama kwa sababu this time around fedha ni zetu.
Hili jambo niliisha lizungumza sana humu

Uzalendo wa kweli wa nchi yako ni pamoja na kusupport mipango kamambe
ya maendeleo ya nchi yako hata kama mipango hiyo itasababisha maumivu kwa walio wengi as long as itakuwa na faida kubwa kitaifa huko baadae.
P
Shukrani kwa kumrekebisha mleta mada. Nafikiri kakaririshwa tu. Wewe umeisoma taarifa lakini mleta mada yeye huenda hata jalada la taarifa wala jina la taarifa hiyo haijui.
 
Mimi nimeosoma ripoti ya WWF kuhusu mradi huu, kama katiba tuu imeweza kukanyangwa na tuko ok kabisa, what is EIA compared?.

Kwenye hili mimi naungana na serikali yetu kuwa Tanzania is a sovereign state, tutaamua mambo yetu wenyewe bila kuingiliwa au kupangiwa na mataifa ya nje.

Natolea mfano wa mradi wa Kamba Samaki, shrimp farming kwenye Rufiji Delta, ulipitishwa vizuri tuu, lakini kabla ya utekelezaji, mashirika ya kimataifa ya mazingira yakaja na EIA nyingine, tukapigwa stop mradi ukafa. Hoja ya wanamazingira ni kilimo kile kingeathiri uoto wa asili wa mikoko.

Ukiangalia cost benefits na value benefits za mradi na faida za mikoko, mikoko are nothing compared.

Kama ulifuatilia issue ya Kihansi Hydro Electric Project, mradi ulichelewa sana kwa hoja ya vyura wa Kihansi hadi Marekani walipokubali kuwa relocate wakahamishwa, mradi ulipokamilika wakarudishwa. Ukiangalia faida za nchi inayohitaji umeme na faida ya vyura ni nothing compared.

Sasa kwenye Stieglers ni vile vile wanataka kutupangia, kule nyuma waliweza kwa sababu fedha walikuwa wanatoa wao. Kwa Stieglers, watakwama kwa sababu this time around fedha ni zetu.
Hili jambo niliisha lizungumza sana humu

Uzalendo wa kweli wa nchi yako ni pamoja na kusupport mipango kamambe
ya maendeleo ya nchi yako hata kama mipango hiyo itasababisha maumivu kwa walio wengi as long as itakuwa na faida kubwa kitaifa huko baadae.
P
Kwa mtu anayetumia umeme hapa Tanzania na ukikumbuka kupigwa kwa gesi utakubaliana na pasco na kumdharau hoja dhaifu ya mnengene
 
Mimi nimeosoma ripoti ya WWF kuhusu mradi huu, kama katiba tuu imeweza kukanyangwa na tuko ok kabisa, what is EIA compared?.

Kwenye hili mimi naungana na serikali yetu kuwa Tanzania is a sovereign state, tutaamua mambo yetu wenyewe bila kuingiliwa au kupangiwa na mataifa ya nje.

Natolea mfano wa mradi wa Kamba Samaki, shrimp farming kwenye Rufiji Delta, ulipitishwa vizuri tuu, lakini kabla ya utekelezaji, mashirika ya kimataifa ya mazingira yakaja na EIA nyingine, tukapigwa stop mradi ukafa. Hoja ya wanamazingira ni kilimo kile kingeathiri uoto wa asili wa mikoko.

Ukiangalia cost benefits na value benefits za mradi na faida za mikoko, mikoko are nothing compared.

Kama ulifuatilia issue ya Kihansi Hydro Electric Project, mradi ulichelewa sana kwa hoja ya vyura wa Kihansi hadi Marekani walipokubali kuwa relocate wakahamishwa, mradi ulipokamilika wakarudishwa. Ukiangalia faida za nchi inayohitaji umeme na faida ya vyura ni nothing compared.

Sasa kwenye Stieglers ni vile vile wanataka kutupangia, kule nyuma waliweza kwa sababu fedha walikuwa wanatoa wao. Kwa Stieglers, watakwama kwa sababu this time around fedha ni zetu.
Hili jambo niliisha lizungumza sana humu

Uzalendo wa kweli wa nchi yako ni pamoja na kusupport mipango kamambe
ya maendeleo ya nchi yako hata kama mipango hiyo itasababisha maumivu kwa walio wengi as long as itakuwa na faida kubwa kitaifa huko baadae.
P
Hujui thamani ya mazingira mpaka siku uwe na jangwa kama sudani au mali.

Tanzania ina options nyingi za kutengeneza umeme. Kwanini msifikirie Solar? Wind Turbines? Gas? Hizo zote ni sustainable means to get electricity without the expense of environment.

Fanya yote ila usichezee mazingira. Kizazi kinachokuja kitajuta.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom