Ukweli kuhusu WWE mieleka

kuna tofauti kati ya mieleka ya ushindan na mieleka ya burudani, mieleka ya ushindani haina mvuto sana kama ya wwe
 
Think outside the box, usiwe unachotwa kirahisi hivyo. Point ni kwamba hizo circus zao huwa scripted na zinakuwa rehearsed, betting can never turn that shit into a real sport.
So betting turned that shit into what??
 
Ulichosema kwa kiasi flani ni kweli ila hawa majamaa wana mafunzo maalumu, na unavyoona jukwaani ni halisi kabisa. Sema visa hupangwa ili kupata sababu ya kuvuta hisia za watazamani. Kama ni mfatiliaji mzuri utagundua mechi zenye washabiki wengi ni zile zinazotokana na visa na majigambo, vinginevyo mchezo usingekuwa na washabiki.

So jukwaani ni vitendo halisi (Ushahidi kutoka kwa waliofika jukwaani kutazama)
 
Hata wacheza sinema wa Hollywood wanalipwa pesa ndefu, WWE(World Wrestling Entertainment) ni maigizo tu. Kuwa 'Entertainment' na si 'Sport' au si 'Competition' ina maana ni burudani tu na si mashindano halisi wala si sport.

Finamu zimejisajiri Kama kazi za Sanaa za Maigizo.
Na waigizaji wake wanajulikana Kama
WASANII.

Mieleka ni Michezo halisi hata hapa Tanzania uliwahi kuchezwa na wachezaji Kama.
Power Mwanza
Power Bernardo
Power Shaka Zuru
Power Vuru Mroma
Power Ruvuma
Nk.
Na baadae mchezo wa Mieleka hapa TZ ukafungiwa kutokana na kukosa vigezo vya kimataifa vya kulinda usalama wa wachezaji.
Yaani
Palikosekana madaktari na matibabu ya uhakika ya wachezaji.
Palikosekana Jukwaa salama la kuchezwa Mieleka ambalo litawalinda wachezaji ( Jukwaa moja linakalibia TSH 1.bn)
Palikosekana mdhamini wa kuuendesha pambano katika viwango vinavyokubalika kimataifa.

(Kabla ya pambano la ngumi huwa mnaona mabondia wanakutanishwa ili kujitambulisha. tulio hilo linaweza kubeba mambo mengi na hata mabondia kuzichapa kavukavu kama hawazuiwa.
Katika mieleka tukio hili lipo pia, na ndipo hapo mnapoona kama Maigizo kwani katika utambulisho wachezaji wa Mieleka huwa wanakuja na wapambe wao na zinachapwa Kama kawaida na wapambe wanaingilia pambano Kama kawaida.
Au linapangwa pambano la kujitambulisha ambalo mchezaji mhusika mmoja anacheza na asiye husika, mhusika akikaribia kushinda ndipo mshindani sahihi anakuja kuingilia pambano na kumpinga mshindani mwenzake.)
Tazameni pambano la mieleka la mtu na kakake
Yaani Jeff Hard na Mark Hard lilivyoandaliwa mtaelewa.
Jeff hakutaka kucheza na kakake Hard.
Na Hard aliandaliwa pesa nyingi ili amchokoze kakake hadi wacheze kwa ahadi ya kulipwa pesa nyingi kwani wadau walitaka ndugu hao wacheze.
Mambo haya yanafanyika ili kuvutia watazamaji wengi kuingia mchezoni na kupata pesa.

MIELEKA SIO SANAA NA USANII NI MCHEZO HALISI NA WADAU WAKE TUPO
Asiyeelewa aende akaulize Baraza la Michezo Tanzania.
BMT.
Umesema kweli
 
Fulamu na Sanaa za Maigizo zinazajiriwa BASATA.
Mieleka inasajiriwa BMT.
Mwenye macho haambiwi tazama.
 
Fulamu na Sanaa za Maigizo zinazajiriwa BASATA.
Mieleka inasajiriwa BMT.
Mwenye macho haambiwi tazama.
Tofautisha kati ya mchezo wa mieleka kama inayachezwa kwenye Olympics na burudani(entertainment) za WWE.
 
Kazi za Sanaa na Maigizo zinazajiriwa BASATA.
BMT Inasajiri Michezo halisi.
Soma mada kama ilivyoletwa, inazungumziwa WWE na si mchezo wa wrestling wa mashindano.
WWE is fake,scripted and rehearsed kabla ya kuingia ulingoni. Au siku hizi WWE imesajiliwa BMT? Kkkk.....!
 
Kwa hiyo mkuu unataka kutuaminisha kuwa huwa Wana kula vyakula maalum na kadawa ili watune na si mazoez
 
Mchezo wa Mieleka ni wa Kweli.
Ila Kuna wakati wanafanya show ya just intertainment ili kutia chachu katika pambano halisi linalotarajiwa.
Mshindi wa Mkanda wa meileka analipwa pesa ndefu hadi anaponyang'anywa.
Sasa jiulizeni mzaha unafanyika vipi wakati Kuna pesa mezani ?
Kwa mfano Kuna kushindania Money in the Bank.
Yaani mshindi anawekewa kitita cha pesa mda huohuo baada ya ushindi.
Hivi unaweza kuamini umati wote ule wa Wazungu kutoa kiingilio cha kutazama Mieleka kinaingia kuangalia maigizo..!

Shindano la kugombea kupata pesa linalotokana na ghalama kubwa ya kufanya mazoezi ya Mieleka liishie kufanya maigizo..!
hujielewi
 
hujielewi
Wewe ndio hujielewi, na Wala huelewi nini kinaendelea.
Mchezo ya mieleka uliwahi kuchezwa hapa nchini Tanzania.
We sijui ulikuwa wapi wakati huo.
Wengi wanashindwa kuuelewa mchezo wa Mieleka kwakuwa wanaufananisha na mchezo wa ngumi.
Mieleka ni mchezo wa kipekee na unasheria zake.
Usipoujua utaona kama wanaigiza.
Kwani hujui aina ya Michezo ya mieleka.
Kuna shindano lenye sheria ngumu na shindano lenye sheria nyepesi yaani free style wrestling ambalo unaweza kutumia silaha kama viti nk.
Mimi ni mdau wa siku nyingi wa huo mchezo.
Kwa kuuthibitisha nenda BMT pale Taifa kaulize usibaki unapinga kitu usichokijua.
 
Wewe ndio hujielewi, na Wala huelewi nini kinaendelea.
Mchezo ya mieleka uliwahi kuchezwa hapa nchini Tanzania.
We sijui ulikuwa wapi wakati huo.
Wengi wanashindwa kuuelewa mchezo wa Mieleka kwakuwa wanaufananisha na mchezo wa ngumi.
Mieleka ni mchezo wa kipekee na unasheria zake.
Usipoujua utaona kama wanaigiza.
Kwani hujui aina ya Michezo ya mieleka.
Kuna shindano lenye sheria ngumu na shindano lenye sheria nyepesi yaani free style wrestling ambalo unaweza kutumia silaha kama viti nk.
Mimi ni mdau wa siku nyingi wa huo mchezo.
Kwa kuuthibitisha nenda BMT pale Taifa kaulize usibaki unapinga kitu usichokijua.
uongo, hujui lolote
 
Back
Top Bottom