Ukweli kuhusu waasisi wa TANU na harakati za kupigania uhuru

Status
Not open for further replies.
..kuna makundi mengi sana ambayo yalishiriki ktk harakati za uchaguzi ambayo yanaweza kutoa malalamiko kama haya anayoyatoa Mohamed Saidi.

..mfano mmoja wa makundi hayo ni VYAMA VYA USHIRIKA. vyama hivyo vilikuwa mstari wa mbele ktk harakati za uhuru, lakini Mwalimu alikuja kuvivunja na kuunda mamlaka za mazao.

..kwa mtizamo wangu Mohamed Saidi anaelezea mchango wa wananchi wa mikoa ya Pwani, haswa dsm, ktk harakati za uhuru. personally nimesoma makala zake nikachukua yale ya msingi na kupuuza yale yasikuwa ya msingi.

..waandishi toka maeneo mengine ya Tanzania/Tanganyika hawazuiwi kuandika vitabu na makala kuelezea michango ya wazee wao ktk harakati za kugombea uhuru. kitu kibaya wanachoweza kufanya ni kupuuza michango ya ndugu zao wa maeneo mengine ya nchi yetu.

..waumini wa madhehebu mbalimbali nao wana ruksa ya kuandika ushiriki wa madhehebu yao ktk harakati za uhuru. kwa mfano, nilisoma makala za Padri mmoja mkatoliki akielezea urafiki wake na Mwalimu, na jinsi wamisionari wakatoliki walivyokuwa wakimfadhili wakati wa harakati za kugombea uhuru. makala hizo zilitoka kwenye blog ya Issa Michuzi.

..vilevile kuna Wahindi,Wazungu, etc etc walioshiriki harakati zile. hawa nao wanapaswa kuandika kuhusu mchango wao. why not? tena hawa wanaweza kuwa na malalamiko makubwa-makubwa kwasababu Mwalimu alikuja kutaifisha mali zao.

..tumchukulie Mohamed Saidi kwamba ameandika kitabu chake kutokana na elimu na uelewa wake. tatizo ni kwamba in recent yrs ni yeye peke yake aliyejishughulisha kutafiti na kuandika historia yetu. wangekuwepo waandishi wengine nina hakika wananchi tungeweza kupata picha nzima ya nini kilitokea ktk harakati za kutafuta uhuru.
jokaKuu,
Umesema jambo la maana sana. Watanzania tuache uvivu wa kusoma vitabu na tujitume kuandika vitabu. Wakati Mwalimu anaingia mamlakani kulikuwa na ombwe la elimu, usomi, utafiti, kila kitu. Lakini inaonekana kuna wanaomlaumu Mwalimu eti alijaribu kupotosha historia ya uhuru wa Tanganyika. Hapana. Huyu huyu Mwalimu tulimtegemea atuundie serikali, atujengee shule, hospitali, na pia atuandikie historia yetu? Saa ngapi? Ni kweli historia ya kwanza ya harakati za Tanganyika iliandikwa na wazungu. Lakini sasa tumesoma, utafiti tunauweza, sources zipo, tujitahidi tuandike na kujazia au kusahihisha pale Mohammed Said alipokosea. Utafiti hauna kikomo na historia si moribund. Juzi nimeshangaa kusoma mahali jinsi mabaharia wa Massachussetts walivyomsaidia Jemadari Washington. Historia hii haifundishwi shuleni hapa Marekani, lakini ukifanya utafiti kidogo utaipata.
 
Lole Gwakisa,

Mkuu unazungumza vitu gani haswa mbona sikuelewi?

Ni wewe uloandika haya:-

1.Kwanza kabisa ukoloni haukusababisha waislamu wasisome, kutosoma ni kutokana na waislamu wenyewe.
Wakoloni waliingia nchini with their own vested interests. Na ndio maana sehemu nyingi tu nchini ambako wakoloni hawakuweka makao maendeleo ya kielimu hata leo ni duni sana.

Mimi nikujibu vizuri kuhusiana na wakoloni kwa maana kwamba wewe kwako mkoloni ni mzungu ambaye ulidai aliendeleza sehemu walizoweka makao yao na dhahiri ukitumia udhaifu wa waislaam wenyewe kutokwenda shule kwanza...hapo ulikuwa na lengo la kupotosha na kuwahusisha maendeleo ya wakoloni na wakristu waliotaka kwenda shule.

Maneno kama haya yanathibitisha maelezo ya watu kama kina Mohammed said kwamba wakristu hawakupingana na wakoloni na ndio maana waliweka kambi zao kwao na sio kwa Waislaam ambao pengine wali resist.
Sasa ukweli ni upi? - Toka Mjarumani hadi Muingereza wote kambi zao kubwa zilikuwa Pwani na hasa Dar -es -Salaam ambayo ilikuwa Capital ya tawala zote zilizopita. Huko mashambani walioweka kambi ni makanisa na sii watawala wenyewe..

Kisha baada ya kutoridhika na maelezo yangu ukaja na objection zako ktk kifungu cha maelezo yangu kwamba yali lack merit.. na Ukaandika yafuatayo:-

2. Waarabu walifika Bagamoyo,Kilwa,Msasani na hat huko Uguja miaka ya 1100, na baadaye 1600-1800.
Ningeomba nielimishwe Mkandara mkuu ,kwa utumwa nilionao, elimu ya maana hawa waarabu waliyoi-inculcate kwa jamii ya watu waliowakuta katika maeneo hayo.
Baada ya maeneo haya hebu twende sehemu nyingi nchini ambazo waarabu ambao (walikuwa waislamu) walituama kwa miaka mingi sana kabla ya hat ya uhuru. Sehemu za Ujiji,sehemu za Zanzibar,Kilwa Lindi,Pangani nk.

Sasa kutokana na majibu kama haya yoote yakihusisha Ukoloni na ukristu, Waarabu na waislaam ndio nikakujibu tena kukufahamisha ukweli wa athari za utumwa wa mawazo pale mtu anapofikiria kwamba Uaarabu ndio Uislaam au ukoloni (uzungu) una represent Ukristu pasipo kujua fika asili ya watu hawa na dini.. Na hakika ktk maelezo yangu ya mwanzo nilizungumzia pia kuhusiana na Mohammed Said kuwa na fikra hizo hizo za kuwahusisha waarabu na tamaduni zao na Uislaam.

Na kwa kuweka record sawa Biashara ya watumwa ilifanywa na wakoloni woote toka waarabu hadi Wazungu. Waarabu walikusanya watumwa kutoka ndani ya nchi (Utawala wa Sultan) na hata huko Afrika ya magharibi, na kuwauza kwa wazungu ambao waliwasafirisha nchi za makoloni yao huko Amerika ya kusini na kaskazini.
Mnada mkubwa wa watumwa Unguja ulikuwa ktk maeneo ya kanisa na hata huko Kenya, Ghana na Bukina Faso biashara ilikuwa hivyo hivyo.. Yaani Market place kama Kariakoo illitawaliwa na wazungu, na hao waarabu kila siku wanajaribu sana kuikwepa kwa kusingizia waarabu kwa kila baya.

nashukuru tu kwamba umekubali kutotumia wakoloni kama ndio mifano ya dini zetu, pengine Ukristu uliletwa na Wazungu lakini sii Uislaam na waarabu, kwani waarabu wote waliotawala Tanzania walikuwa dhehebu tofauti na dhehebu la Waislaam wa Tanzania toka nchi hii imekubali dini hiyo.. Wa Oman wana dhehebu tofauti na waislaam wa Bongo...
 
Lole Gwakisa,

Mkuu unazungumza vitu gani haswa mbona sikuelewi?
Mkuu naona we are beating around the bush, though we seem to be arguing about the same thing over and over again.
Nitapitia mada zangu ili nijaribu kuonyesha kinaga ubaga ile poitn niliyoipinga sana ya Mohammed Said kuhisiana na lawama zake kwa Mwalimu kuwa sababu ya waislamu kutosoma.Kitu ambacho si kweli.
Tukianzia hapo naona tutaelea offtakes nyingine.
Nina ka flu and read ya in the mornin
Ciao!
 
Mkuu naona we are beating around the bush, though we seem to be arguing about the same thing over and over again.
Nitapitia mada zangu ili nijaribu kuonyesha kinaga ubaga ile poitn niliyoipinga sana ya Mohammed Said kuhisiana na lawama zake kwa Mwalimu kuwa sababu ya waislamu kutosoma.Kitu ambacho si kweli.
Tukianzia hapo naona tutaelea offtakes nyingine.
Nina ka flu and read ya in the mornin
Ciao!
Sijakupinga sehemu nyingine yeyote isipokuwa pale uliposema wakoloni sio sababu ya waislaam kukosa elimu isipokuwa wao wenyewe ndio hawakwenda shule. Na nikasema haya sii maneno ya kweli kwani mimi mwenyewe nilikuwa victim wa mfumo wa mkoloni..nikaishia hapo hadi wewe uliporudi na kupinga maelezo yangu kuwa hayana merit.

Mkuu sote ni binadamu, huteleza au hufanya makosa ktk kujieleza wakati hukumaanisha hivyo au ulivyofundishwa ndio imepelekea kuamini hayo. JF ni uwanja wa kukosoana, kufahamisha na hakika mimi nimekosolewa sana humu na kukubali kwamba info nilizokuwa nazo hazikuwa sahihi na nikajifunza. Uzuri wa JF kwa kila anayekupinga humwaga ukweli hivyo hata wale tusiojua ukweli huokoteza...
 
Inasikitisha kweli kuwa hivi sasa kila Tom, Dick and Harry anaota ndoto ya kupata umaarufu kwa kumtupia madongo Mwalimu na kuona fahari kwa kujaribu kulichafua jina lake. Ukweli ni kuwa Mwalimu alitenda kile alichohubiri na dunia inamtambua hivyo na inampa heshima kwa msimamo wake thabiti. Moja wa wanafunzi wake kabla hajalewa madaraka, Pius Msekwa kwenye mada yake inayopatikana mtandaoni anasema hivi kuhusu mchango wa Mwalimu katika harakati za kupigania uhuru.
Two examples may be cited here that illustrate Mwalimu Nyerere’s exemplary powers of persuasion.

  • The first is his success in convincing the delegates to the TANU annual conference of 1958 to make the difficult decision of accepting the tripartite vote, which had been imposed by the British administration. The TANU delegates were almost unanimously opposed to the tripartite electoral rules, and actually wanted to boycott the relevant elections. Mwalimu Nyerere had been forewarned about the strong opposition to this particular issue among the delegates, so he went to Tabora fully prepared for the battle to convince them. He first asked the conference to agree to his proposal that he should not chair the conference during the discussions on that agenda, so that he could have the freedom to present his views and to argue with fellow delegates without appearing to take advantage of the authority of the Chair. When that was granted, he proceeded to argue the case for accepting the new electoral rules, and to take part in the elections, instead of staging a boycott. It was an uphill task for him, but he was able to succeed. The product of his success was the famous Tabora resolution of 1958, which is believed to have substantially changed the history of Tanganyika’s road to independence.
  • A further example of Mwalimu Nyerere’s ability to argue his case was his success in influencing the United Nations Trusteeship Council regarding the recommendations of the 1954 United Nations Visiting Mission to Tanganyika. The Visiting Mission had recommended that a time-table be drawn up for Tanganyika’s independence, and had suggested further that this could be achieved within 20 or 25 years. This section of the report was rejected by the Administering Authority. TANU received information to the effect that the European Press was also campaigning strongly for its rejection. Therefore TANU decided to send Mwalimu Nyerere to New York to argue against that campaign and to try to influence the Trusteeship Council’s decision on that matter. Although Nyerere’s endeavours did not result in the setting up of a time-table for that purpose, the fact that independence was achieved a mere seven years later, (and not the 20 to 25 years which had been suggested by the UN Visiting Mission), is clear testimony to Mwalimu Nyerere’s immense powers of persuasion.

Tulikuja kuushuhudia tena uwezo wake huu alipoweza kuutetea msimamo wake wa serikali mbili na kuwezesha kubatilishwa kwa azimio la Bunge lilowasilishwa na G55. Hapa tunapata picha ya kamanda mwenye kipaji na uwezo wa kuliongoza jeshi lake hadi ushindi upatikane. Hiyo historia haitapindishwa na malimbukeni wa leo hata siku moja - not now, not ever !
 
Sijakupinga sehemu nyingine yeyote isipokuwa pale uliposema wakoloni sio sababu ya waislaam kukosa elimu isipokuwa wao wenyewe ndio hawakwenda shule. Na nikasema haya sii maneno ya kweli kwani mimi mwenyewe nilikuwa victim wa mfumo wa mkoloni..nikaishia hapo hadi wewe uliporudi na kupinga maelezo yangu kuwa hayana merit.

Mkuu sote ni binadamu, huteleza au hufanya makosa ktk kujieleza wakati hukumaanisha hivyo au ulivyofundishwa ndio imepelekea kuamini hayo. JF ni uwanja wa kukosoana, kufahamisha na hakika mimi nimekosolewa sana humu na kukubali kwamba info nilizokuwa nazo hazikuwa sahihi na nikajifunza. Uzuri wa JF kwa kila anayekupinga humwaga ukweli hivyo hata wale tusiojua ukweli huokoteza...

I agree with you totaly Mkuu Mkandara on this ingawaje naomba nisieleweke kuwa natetea wakoloni(wa ulaya) dhidi ya wakoloni(wa uearabuni).
Nilicho kuwa napinga haswa presentation ya Mohammed Said na wenziwe ni kuweka lawama za wao kutoendelea kielimu na maendeleao kwa ujumla kwa Mwalimu na Tanu yake.Mohammed Said na wenziwe wakaenda mabli zaidi kwa kuchijukulia credit ya ukombozi wa Tanganyika na kwamba Mwalimu alikaribishwa tu katika harakati hizo.
Generally that is the gist of my rebuttal to Mohammed Said and co.
Msimamo wangu ulikuwa kupinga mawazo ya Mohammed Said kuyaona matukio ya nchi hii katika miwani ya uislamu, na kwa kuona kuwa waislamu kiujumla walionewa hasa kielimu.
Sasa hapo ndio tukaanza kutofautiana.
My argument
1 Kufika kwa wakoloni(Waarabu na Wazungu pia)
Wakoloni hawa aliyejijengea umaarufu wa kufika kwanza ni mwarabu(1100AD hadi 1800's AD)
Najua waarabu vilevile wna elimu nzuri tu kama algebra etc, pamoja na ubaharia kwa kutumia nyota.
Pamoja na kufika mapema nchi hii na kuweka makao, kulowea, sehemu walizo kaa hawakuziendeleza kielimu.Mantiki ya elimu pengine niseme ni ile elim dunia.Elimu ya kuendeleza mtu kupambana na mazimgira yake.
Na nikatoa mifano ya sehemu walizokaa, yaani Zanzibar,Pangani,Kilwa,Lindi, Msasani huko sehemu za Tabora na Ujiji.
Mimi siwalaumu kwa kulowea , nawalaumu kwa kutoleta elimu kama nilivoianisha hapo juu.
Hii ni pamoja na ukweli kuwa kwa sehemu walizokaa waarabu walioa sana mama zetu na kujiwekea uhalali wa kuishi ndani ya nchi yetu, hili silipingi hata kidogo.

Mkoloni mzungu yeye alikuja mwishoni mwa miaka ya 1800, baada ya scramble for Africa kuanza. Mkoloni mzungu alikuja na mtazamo tofauti.Yye aliona Tanganyika kama vile sisi leo tuonavyo plot au shamba ulilopewa na halmashauri ya Jiji.
Hakuona watu waliomo katika nchi hii kama watu, bali source of cheap and enforceable labour.
Mkoloni mzungu alipingwa sana na wote waliokuwepo, pamoja na ukweli kuwa huko Zanzibar Mkoloni na Mwarabu waliingia ligi moja ya kuheshimiana.
Mkoloni mzungu alichagua sehemu zake za kuishi,sehemu alizoona zinalingana na matakwa yake na biashara zake.Sas ili kuendeleza utawala wake alianzisha shule ambazo kimsingi ilikuwa kufundisha waafrika kumwendeshea biashara au utawala wake.

Sasahapo mkuu ndio tunaanza kuto fautiana.
Wakati mwarabu alikuwa na dini yake ya Uislamu, Mzungu naye aliingia na dini yake ya Ukristo. Sehemu walizo kaaa hawa wakolni(wote wazungu,waarabu) waliibadili jumuia hiyo kuingia dini zao.
Inawezekana kabisa resistance ya waarabu kwa ukoloni wa kizungu ilikuwa kutohusiana kwa aina yoyote socially na mikakati ya wazungu.
Hii inajidhihirisha hata pale Zanzibar kwani mkoloni pale alikuwapo lakini maendeleo ya kielimu bado hayakuwa makubwa sana.
Hii inaweza kuwa mada kubwa sana ya utafiti lakini ukweli ni kuwa alipokuwepo mwarabu mkoloni mzungu hakupashughulikia sana kama pale alioishi mwenyewe.

2 Ukombozi wa Tanganyika na TANU
Kiujumla waafrika waliupinga sana tawala zote zilizokuja.Tawala za kiarabu hata hivyo zilijiIdentify sana na wenyeji na kujichanganya nao baada ya muda katika sehemu walizolowea.
Historia za kupinga ukoloni wa kizungu ,za kina Mkwawa namashujaa wengine zinaonyesha wazi kupingwa kutawaliwa.
Mapambano ya enzi hizi zilikuwa za waafrika na utamaduni wao na uwezo wao dhidi ya wazungu , utamaduni wao na uwezo wao.
Nidhahiri uwezo wetu ulishindwa kuhimili uwezo wazungu.
Uanzishwaji wa TANU ulikuwa hitimisho la kuwaelewa wazungu, utamaduni wao na uwezo wao.
Pamoja na shule, vita kuu zote mbili na maendeleo ya kupata mwanga wa elimu hivi vyote vilimpa mwaafrika silaha yakuweza kupambana na mkoloni mzungu kwa kutumia itikadi yake mwenyewe.Na hapo ndio kina Mwalimu Nyerere na wenziwe wanaingia.
Mifumao ya elimu aliyo wekwa na mkoloni mzungu hata Nyere aliikuta, hakuiasisi.
Yeye Nyere alifaidika na mfumo huo wa elimu ya Mkoloni na baada ya Uhuru alijitahidi sana katika sekta ya elimu kusambaza leimu ili iwe kwa wananchi woote.

Sasa mkuu Mkandara frame work ya upinzani wangu kwa Mohammed Said and co. ni kumlaumu Nyerere kwa kutoendeleza elimu kwa WAISLAMU TU, wakati si kweli.
Mfano uliojitole wewe mwenyewe Mkuu Mkandara , ni mfano tosha kuelezea kuwa elimu ya Mkoloni mzungu ilichagua pale yeye tu(mkoloni mzungu) alipoona pana returns kwake, utawala wake na biashara zake.
Kwa bahati nzuri mimi nilikuwepo Mlimani mwaka 1978 wakati Mwalimu alikuja kuonana na wanafunzi.
Profesa Che Mponda alimuuliza swali hili
" Mwalimu tulipoonana kule Marekani uliniambia turudi nyumbani na kuiendeleza nchi yetu ya Tanzani.
Mimi nikaja na nikapata kazi hapa UDSM,Lakini hapa kuna ukabila mkubwa sana.Mkuu wa Faculty kabila moja na wakuu wa departments kabila hilo hilo sasa sisitunakereka, Utasemaje juu ya hilo."

Mwalimu akacheeka na kile kikohozi chake , lakini akajibu kwa umakini mkubwa.
Yeye ailopiata nchi hii nilikuwa na wasomi wachache sana, daktari mmoja au wawili pale muhimbili na engineer mmoja tu.
Aliendelea kuwa wakoloni(wazungu) wali jenga shule sehemu tatu kuu, Kilimanjaro,West Lake na Mbeya. Na sehemu hizo ndio unapata wasomi ingalau walioweza kuwa makarani wa kwanza.Na alisema ana makarani wengi sana toka sehemu hizo kwa vile ndio walianza kupelekewa shule na wakoloni.
Na lisema kuwa huwa inapotokea nafasi ya kazi, anaPOletewa recommendations za watu wan ofaa anakuta wa kwanza aliyesoma ni wakabila la mchagga , wa pili ni mchagga na watatu ni mchagga, wote waliosoma sana.
Na ndiyo maana akaamua kutaifisha mfumo wa elimu ili uwe wa wote, wananchi wote.
Mwalimu aliongeza kuwa sehemu kama za Tabora na Mwanza kuna kundi kubwa sana la watu, lakini ambao hwana shule kabisa na hawakujiendeleza.Akaongeza kuwa sehemu za kwao Mara wakoloni waliwachukua watu wa huko kwenda jeshini tu, nako wakijenga shule chache sana.
Na ndio maana akasema leo una kina Mwita ,Chacha na Marwa wengi jeshini lakini hawana elimu ya kutosha .Hii ni kwa vile hata jeshini makabila yaliyosomeshwa na mkoloni yalikuwa yakiongoza huko.Baada ya uasi wa 1964 Mwalimu aliongeza kusema akawapandisha vyeo wote hawa Mwita ,Marwa na Chacha ambao kimsingi bado hawajasoma.

Mwalimu altioa ushauri ambao naukumbuka hata leo.JENGENI SHULE ZA MSINGI KWA WINGI KATIKA MAENEO YENU.

Mkuu Mkandara nimeandika sana lakini nafikiri kwa sasa niishie hapo.
 
Sijakupinga sehemu nyingine yeyote isipokuwa pale uliposema wakoloni sio sababu ya waislaam kukosa elimu isipokuwa wao wenyewe ndio hawakwenda shule. Na nikasema haya sii maneno ya kweli kwani mimi mwenyewe nilikuwa victim wa mfumo wa mkoloni..nikaishia hapo hadi wewe uliporudi na kupinga maelezo yangu kuwa hayana merit.

Mkuu sote ni binadamu, huteleza au hufanya makosa ktk kujieleza wakati hukumaanisha hivyo au ulivyofundishwa ndio imepelekea kuamini hayo. JF ni uwanja wa kukosoana, kufahamisha na hakika mimi nimekosolewa sana humu na kukubali kwamba info nilizokuwa nazo hazikuwa sahihi na nikajifunza. Uzuri wa JF kwa kila anayekupinga humwaga ukweli hivyo hata wale tusiojua ukweli huokoteza...

Mkuu naamini kuwa ungesema kuwa wakoloni wamechangia kwenye ishu hii pasingekuwa na malalamiko. Najua kuna sehemu ambako waislamu walibaguliwa katika kuingia kwenye shule za misheni lakini kuna sehemu nyingine huo ubaguzi haukuwepo. Mimi nami nilisoma katika shule hizo na tulikuwa na wanafunzi wa kiislamu na mara moja kwa wiki alikuja shehe kutoa mafunzo. Kuwatupia wakoloni dhamana yote ya waislamu kukosa elimu ni kuingia kwenye mtego wa kutoa jibu rahisi kwa swali gumu. Ingekuwa hivyo basi mara baada ya sisi kupata uhuru na shule zote kutaifishwa, waislamu wangechangamkia hiyo elimu na mpaka hapa tulipo, nusu karne baadae, hii isingekuwa ishu. Mimi naamini kuwa pamoja na ukoloni (na maswihiba wake wamisheni) mila na desturi za makabila mengi ambayo yana waislamu wengi ( hususan ya pwani) zimechangia kwenye hili tatizo. Mila hizi hazina msingi katika uislamu bali tamaduni asili. Mambo ya ngoma, kuona kazi nzito ni ishara ya utwana ( kutokana na utumwa), n.k. vimechangia mno.

Lakini namna nyingine ambayo ukoloni ulichangia kudumaza elimu katika jamii ya kiislamu ni hegemony ya ukristu katika masuala ya jamii. Mpangilio wa elimu na utendaji kazi umekuwa based kwenye judae-christian traditions na hivyo kumlazimisha asiye mkristu ku-adapt. Hii inaonekana katika kutotoa nafasi ya kuswali wakati wa shule, kupumzika siku ya jumapili na jumamosi, kuchanganyika kwa jinsia katika madarasa n.k. Hivi vyote vilichangia kwenye kujenga imani kuwa elimu ya kikoloni ni elimu ya kikristu na kufanya baadhi ya waislamu kuiogopa.

Kitu kingine kilichochangia na kinachochangia ni mfumo mzima wa uongozi katika dhehebu la wasunni. Wasunni hawana centralised authority kama walivyokuwa nayo washia na wakristu. Kila msikiti unasimama wenyewe na kila shehe halazimiki kuwajibika kwa mtu mwengine. Hii imechangia katika ku-fragment nguvu zao na kuwakosesha uwezo wa kufanya mambo mengi ya kimaendeleo. Ukiangalia wa shia ( mabohora, waislamailia n.k.) wao wanawajibika kwa kiongozi mmoja amabye ameweza kukusanya nguvu zao na kufanya mambo makubwa katika nyanja ya elimu, afya n.k. Wote tunajua mchango wa Aga Khan katika elimu na shughuli za maendeleo za watu wake. Hivyo hivyo kwa madhehebu ya kikristu kama wakatoliki, waangalikana, walutheri n.k. Wote hawa wanawajibika kwa makadinali au maaskofu wao ambao nao wameweza kukusanya nguvu zao kuleta maendeleo kwa waumini wao. Ndiyo maana kuwalaumu wakristu bila kuangalia tofauti za mipangilio wa uongozi katika dini hizi ni kutokuwa makini. Kudai chombo kitakachowaunganisha waislamu kama wakristu ni kukwepa kuangalia ukweli huu maana ni vigumu sana kuwa na chombo kitakachokuwa na authority juu ya jamii yote ya kiislamu kama ilivyo kwa wakristu. Hata chombo ambacho waislamu wengi wanakikumbuka kwa majonzi ( East African Muslim Welfare Society) maana katika muda mfupi wa uhai wake kilileta maendeleo kilibebwa na Aga Khan. Sababu mojailiyochangia kifo chake ni baadhi ya waislamu wa sunni kutomkubali kama muislamu mwenzao na sabau nyingine za kibaguzi wa rangi. Kwa vile Aga Khan au mtu mwingine hakuwa na mamlaka ya kidini juu ya hawa basi chombo hicho kikafa!

Amandla.....
 
Mawazo ya kitumwa ni yale ambayo mtu hajayatoa bado, mawazo ambayo yapo kichwani kwa mtu bado. Mimi sioni tatizo kundi lolote kulalamika pindi linapoona ama kuhis halitendewi haki wakati lilitekeleza wajibu wake kama ilivyopasa. Waache waisilamu walalamike kwani wanahisi wameonewa na kupunjwa kile walichokitarajia. Jambo la msingi hapa si kutumia jazba bali kujibu hoja kwa kutumia facts na wala si kwa kutumia propaganda na prejudices zilizotufikisha hapa.

Kuna makundi mengi tu nayo yanalalamika kichinichini nayo pia naamini yanatakiwa yalalamike hadharani. Mikoa ya kusini inaugulia kutengwa, mikoa ya magharibi nayo pia, ukiwauliza hawa wote watakwambia kaskazini kunapendelewa. Naam ni kweli kunapendelewa.

Malalamiko ya waislamu pia yanaenda sambamba na hili. Mikoa inayoonekana kupendelewa ni mikoa yenye wakristo wengi kuliko waislamu, na mikoa yenye waislamu wengi, mingi kati yao ipo hoi. Hoja ya kusema mikoa hiyo ilipendelewa tangu enzi za ukoloni inakataa na inakosa mashiki pale tunapouona mkoa wa Tanga ulioendelezwa pia na ukoloni ukifa kifo cha mende.

Suala la udini lipo, tusiogope kulijadili kwani kwa kulijadili tutalisaidia taifa hili kutofanya makosa yaliyokwishwa fanywa na yanayoendelea kufanywa. Nyerere analaumiwa kwa kuwapendelea wakristo, Mwinyi analaumiwa kwa kuwapendelea waislamu, Mkapa wakristo na sasa Kikwete waislamu, na ukweli ni kwamba hata ukiangalia uteuzi wa mabaraza yao ya mawaziri na makatibu wakuu wa wizara taswira ya upendeleo wa kidini unaonekana kwa kila mmoja na baraza lake.

Jambo la msingi tujiulize kwa nini haya yanafanyika? yanafanyika kwa faida ya nani? Tusikimbilie kukataa na kuogopa kujadili hoja ngumu huku tukilifuga bomu ambalo likija kulipuka hakuta kuwa na muda wa majadiliano wala masikilizano.

Kama ukitaka kuongoa mti unachimbua mizizi basi na hili nalo tulichimbue na kweli tuweke bayana na sio kuficha
 
Mawazo ya kitumwa ni yale ambayo mtu hajayatoa bado, mawazo ambayo yapo kichwani kwa mtu bado. Mimi sioni tatizo kundi lolote kulalamika pindi linapoona ama kuhis halitendewi haki wakati lilitekeleza wajibu wake kama ilivyopasa. Waache waisilamu walalamike kwani wanahisi wameonewa na kupunjwa kile walichokitarajia. Jambo la msingi hapa si kutumia jazba bali kujibu hoja kwa kutumia facts na wala si kwa kutumia propaganda na prejudices zilizotufikisha hapa.

Kuna makundi mengi tu nayo yanalalamika kichinichini nayo pia naamini yanatakiwa yalalamike hadharani. Mikoa ya kusini inaugulia kutengwa, mikoa ya magharibi nayo pia, ukiwauliza hawa wote watakwambia kaskazini kunapendelewa. Naam ni kweli kunapendelewa.

Malalamiko ya waislamu pia yanaenda sambamba na hili. Mikoa inayoonekana kupendelewa ni mikoa yenye wakristo wengi kuliko waislamu, na mikoa yenye waislamu wengi, mingi kati yao ipo hoi. Hoja ya kusema mikoa hiyo ilipendelewa tangu enzi za ukoloni inakataa na inakosa mashiki pale tunapouona mkoa wa Tanga ulioendelezwa pia na ukoloni ukifa kifo cha mende.

Suala la udini lipo, tusiogope kulijadili kwani kwa kulijadili tutalisaidia taifa hili kutofanya makosa yaliyokwishwa fanywa na yanayoendelea kufanywa. Nyerere analaumiwa kwa kuwapendelea wakristo, Mwinyi analaumiwa kwa kuwapendelea waislamu, Mkapa wakristo na sasa Kikwete waislamu, na ukweli ni kwamba hata ukiangalia uteuzi wa mabaraza yao ya mawaziri na makatibu wakuu wa wizara taswira ya upendeleo wa kidini unaonekana kwa kila mmoja na baraza lake.

Jambo la msingi tujiulize kwa nini haya yanafanyika? yanafanyika kwa faida ya nani? Tusikimbilie kukataa na kuogopa kujadili hoja ngumu huku tukilifuga bomu ambalo likija kulipuka hakuta kuwa na muda wa majadiliano wala masikilizano.

Kama ukitaka kuongoa mti unachimbua mizizi basi na hili nalo tulichimbue na kweli tuweke bayana na sio kuficha

Ni mikoa ipi yenye wakristu wengi ilipendelewa na kwa vipi?

Ruvuma, Rukwa, Shinyanga, Mara, Manyara, Dodoma,Kagera yote ina idadi kubwa ya wakristu kuliko waislamu?

Amandla.......
 
Mambo haya yana uzuri mmoja. Huwezi kujua hatari na shida zake hadi uwe muathirika. Ukiwa hubaguliwi huwezi kujua ukweli wa mambo wala hutoshangaa kujikuta nyie wa dini moja ndio mlohodhi kila kitu. Iwe shirika au idara ya serikali. Meneja mmoja alipata kudai uthibitisho wa elimu ya Muislam kama kweli kasoma kwa kiwango kile jalada lake linavyoonyesha. Yule Muislam aloandikiwa barua ya kuleta vyeti vyake halisi kutoka vyuo vyote alivyosoma ndani na nje ya nchi akashangaa. Hakuamini macho wala akili zake. Akawa anawaza vipi huyu Mkristo mwenye diploma tu haamini vyeti vyangu wakati mimi nimemshinda kwa kisomo katika nyanja zote lakini yeye kanipita kwa mbali kwa cheo hapa shirikani? Wa kushtushwa na elimu ni nani? Ni mimi Muislam kuwa juu ya elimu yote hii nilonayo sikupanda cheo kapanda yeye Mkristo wa diploma au mimi? Basi yule Muislam akamjibu yule mkuu Mkristo barua ya mstari mmoja. Akasema je, hivyo vyeti unavyovitilia shaka umeviona katika jalada langu? Ujumbe ukawa umemfikia kwa haraka sana yule mkuu. Mambo ndiyo haya.

Lakini muhimu tujadili historia ya uhuru wa Tanganyika na mashujaa wake ambao wamefutwa katika historia yab nchi yetu. Hii ndiyo mada kuu na husika katika mjadala huu.
 
Sababu iliyotolewa na akina Nasibu Abbas ya kuwa Aga Khan si muislamu mwenzao haikuwa ya kweli na pia haikuwa sababu yao, sababu hiyo ilitengenezwa kama vile ulivyotengenezwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Mambo ya kutengenezwa katika siasa zenye kujaa ujahili ni nyingi.Kuna ajali za kutengenezwa na hata uadui wa kutengenezwa, mfano nchi moja inawza kuua watu wake makusudu na kusingizia taifa ful;ani limewaua ili lipate sabau ya kupigana vita au kuinyanga'anya nchi hiyo kitu fulani inachohitaji.

Zanzibar iliunganishwa na Tanganyika ili kuinyima haki ya kufaidi matund ya mkataba wa nchi tatu kati yao na Indonesia na Ujerumani mashariki kwa vile tu Nyerere na mataifa ya magharibi yaliingia woga kuwa Zanzibar aidha ingetumbukia kuwa nchi inayofuata taratibu na sheria za kiislamu au kuwa nchi ya kisoshalisti yenye msimamo mkali.

Hivyo ndugu yangu Fundi Mchundo unapoliangalia jambo fulani tafadhali angalia hilo jambo kwa undani na si kijuu juu kwani ukifanya hivyo utakubali kila unaloambiwa hata ukiambiwa. Utaambiwa Ulimwengu sio raia, Bashe sio raia, utaambiwa Mtu mzima kaathirika utaambiwa mengi ambayo usipoyafanyia uchunguzi na utafiti wa kina utabakia kuyaamini.

Kulikuwa na sababu maalum kabisa ya kuwatenganisha waislamu watanzania na waislamu wengine katika mataifa mbalimbali duniani.

Tafakari, Chukua hatua
 
HAHAHAHA umenifanya nicheke bila hata kutaraji kama ningecheka asubuhi ya leo. Tuanze na kuangalia kitu kimoja kimoja katika kujadili maendeleo. Tuanze na miundo mbinu ya barabara halafu tuje katika nishati. Tuanze na nkoa wenye waislamu wengi kuliko mikoa yote ukiacha Dar es salaam, mkoa ambao u karibu sana na dar Mkoa wa pwani halafu tuje na mkoa uliombali sana na dar na pia una idadi kubwa ya wakristo kama ulivyoutaja mkoa wa kagera.

Naomba nisaidie tafadhali halafu tuje mikoa ya Lindi na Mtwara na mikoa mingine miwili ya choice yako
 
HAHAHAHA umenifanya nicheke bila hata kutaraji kama ningecheka asubuhi ya leo. Tuanze na kuangalia kitu kimoja kimoja katika kujadili maendeleo. Tuanze na miundo mbinu ya barabara halafu tuje katika nishati. Tuanze na nkoa wenye waislamu wengi kuliko mikoa yote ukiacha Dar es salaam, mkoa ambao u karibu sana na dar Mkoa wa pwani halafu tuje na mkoa uliombali sana na dar na pia una idadi kubwa ya wakristo kama ulivyoutaja mkoa wa kagera.

Naomba nisaidie tafadhali halafu tuje mikoa ya Lindi na Mtwara na mikoa mingine miwili ya choice yako

Mikoa ya Rukwa, Ruvuma, Mara ina miundo mbinu bora kuliko mikoa ya Tanga, Pwani na Lindi?

Amandla.....
.
 
Mambo haya yana uzuri mmoja. Huwezi kujua hatari na shida zake hadi uwe muathirika. Ukiwa hubaguliwi huwezi kujua ukweli wa mambo wala hutoshangaa kujikuta nyie wa dini moja ndio mlohodhi kila kitu. Iwe shirika au idara ya serikali. Meneja mmoja alipata kudai uthibitisho wa elimu ya Muislam kama kweli kasoma kwa kiwango kile jalada lake linavyoonyesha. Yule Muislam aloandikiwa barua ya kuleta vyeti vyake halisi kutoka vyuo vyote alivyosoma ndani na nje ya nchi akashangaa. Hakuamini macho wala akili zake. Akawa anawaza vipi huyu Mkristo mwenye diploma tu haamini vyeti vyangu wakati mimi nimemshinda kwa kisomo katika nyanja zote lakini yeye kanipita kwa mbali kwa cheo hapa shirikani? Wa kushtushwa na elimu ni nani? Ni mimi Muislam kuwa juu ya elimu yote hii nilonayo sikupanda cheo kapanda yeye Mkristo wa diploma au mimi? Basi yule Muislam akamjibu yule mkuu Mkristo barua ya mstari mmoja. Akasema je, hivyo vyeti unavyovitilia shaka umeviona katika jalada langu? Ujumbe ukawa umemfikia kwa haraka sana yule mkuu. Mambo ndiyo haya.

Lakini muhimu tujadili historia ya uhuru wa Tanganyika na mashujaa wake ambao wamefutwa katika historia yab nchi yetu. Hii ndiyo mada kuu na husika katika mjadala huu.

Kwa hiyo tunapohoji Ph. D ya Mustafa Mkullo tunafanya hivyo kwa sababu ni muislamu? Na wale wanaohoji za wakina Mary Nagu wanafanya hivyo kwa sababu hawawapendi wakristu? Ingekuwa vyeti vya waislamu wote vinatiliwa shaka na mabosi wakristu basi pasingekuwa na muislamu katika nafasi ya uongozi! Pamoja na lawama zote zinazoelekezwa kwa Ramadhani Dau sijasikia hata mmoja akihoji uhalali wa Ph.D yake. na kumbuka ni mmisheni aliyempa nafasi aliyonayo sasa hivi! Huyo ndugu yako ambaye hamtaji inawezekana alitiliwa shaka kutokana na uvaaji wake, lahfudhi yake, kabila lake, urefu au ufupi wake, jinsia yake, n.k. Na inawezekana kabisa alihojiwa kutokana na uislamu wake maana wabaguzi wapo. kama vile wakristu wengine wanavyodai wanatiliwa kauzibe na mabosi waislamu. Vyeo haviendani na elimu peke yake. Kama utendaji wako ni mbovu, kama ni mlevi n.k. basi cheo unaweza kunyimwa. Na ndio, kuna waislamu wanaokunywa. Hata unguja Zanzibar makomba wako kibao! Vile vile kiongozi yeyote makini anahoji vivuli vya shahada. Ndio maana ukienda kwenye interview mara nyingi wanadai uende na cheti halisi. Hii inafanywa kwa wote, si waislamu peke yao.

Kwa mfano, mbona tuko wakristu ambao tumeibiwa na vibaka waislamu kama vile bila shaka wako waislamu ambao nao wameibiwa na vibaka wakristui? Basi, kwa your warped logic, nasi sote tuone mkono wa udini kwenye yote haya? Unasahau kuwa kibaka haangalii dini! Yuko tayari kumtendea maovu mwenye dini yake kama alivyokuwa tayari kumtendea maovu mwenye dini nyingine. Huyo bosi unayemzungumzia kama alikuwa hajiamini na usomi wake basi hata angekuja mkristu na madigirii yake angemsumbua! Ndivyo ilivyo.

Mkuu, chuki na ubaguzi utakufikisha pabaya. Hapa hauna hoja. Tumekustukia.

Amandla......
 
Huwezi kujua anavyohisi yatima hadi nawe uwe umepoteza wazazi wako. Ikiwa utajibu kistaarabu tunaweza tukaendelea na mazungumzo lakini ikiwa lugha ndiyo kama hivi kwangu huwa naishiwa na hoja. Napenda mijadala lakini sipendi kuvunjiana heshima. Haya ndiyo mafunzo katika Uislam.
 
Mohamed Said said:
Lakini muhimu tujadili historia ya uhuru wa Tanganyika na mashujaa wake ambao wamefutwa katika historia yab nchi yetu. Hii ndiyo mada kuu na husika katika mjadala huu.

Mohamed Said,

..inawezekana usumbufu unaoupata unatokana na hisia kwamba na wewe umerudia makosa yaleyale unayojaribu kuyarekebisha. kwamba kuna mashujaa walishiriki ktk harakati za uhuru lakini hujawatambua kutokana na mchango wao.

..je, umejihakikishia ktk nafsi yako kwamba, vitabu na makala zako, vimeheshimu michango ya wanaharakati waliopigania uhuru bila kuwabagua kikabila, kidini, au kijinsia?

..je, una mipango yoyote ya kuandika vitabu kuhusu michango ya medhehebu mengine ya dini,vyama vya ushirika, jumuiya za makabila mbalimbali, wanawake, etc etc katika harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika?

NB:

..ingependeza kama mihadhara yako ungeitoa kwa wanajumuiya wote wa chuo kikuu, na siyo kwa chama cha wanafunzi Waislamu pekeyao.

..kuhusu Muislamu aliyehojiwa vyeti vyake, nadhani huo ni utaratibu wa kawaida siku hizi. kinachofanyika ni kwanza kuwasilisha VYETI, na baadaye uhakiki kufanyika kwa kuitisha OFFICIAL TRANSCRIPTS.
 
Katika "The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 -1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism, London 1998, nimejitahidi sana kueleza historia ya kudai uhuru wa Tanganyika na michango ya wazalendo walioshiriki kadri ya uwezo wangu. Kama unacho hicho kitabu soma au kwa haraka pitia faharasha ya majina (name index) utawaona hawa wazalendo majina yao na ukiingia katika kitabu utakuta habari zao.

Ama kuhusu makala zangu hazitofautiani sana na msimamo wa kalamu yangu kama nilivyoeleza hapo juu.

Bahati mbaya ni Waislam tu ndiyo wanaonialika lakini endapo nitaalikwa hata na Wakristo nitakaja na kuwaeleza kile ninachoakijua na kuamini.

Kuhusu kuhoji vyeti hilo lilisukumwa na hasad kuliko utaratibu wa kazi. Angalia kichekisho chenyewe. Huyo Afisa Mkuu aliona vyeti vya computer literacy program ambazo huyo jamaa alizisoma miaka zaidi ya ishirini iliyopita ambayo kwa sasa hazitumiki. Afisa Mkuu akawa anazidai aone ushahidi kama kweli hivyo vyeti ni kweli vimepatikana kwa kusoma. Kichekesho cha kwanza ni kuwa leo hicho cheti kilichotolewa miaka ishirini iliyopita hakina maana yoyote jinsi utaalamu wa computer ulivyopiga hatua.

Idara hiyo ilikuwa na vituko vingi. Kaachwa Muislam msichana mwenye digrii ya Uzamivu kapewa promosheni mlokole mwenye diploma. Kaachwa kupewa cheo afisa alomaliza Mzumbe 1963 enzi za Cambridge cheo akapewa jamaa ex- standard 8.

Haya ni kweli kabisa yametokea.



Ama
 
Sababu iliyotolewa na akina Nasibu Abbas ya kuwa Aga Khan si muislamu mwenzao haikuwa ya kweli na pia haikuwa sababu yao, sababu hiyo ilitengenezwa kama vile ulivyotengenezwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Mambo ya kutengenezwa katika siasa zenye kujaa ujahili ni nyingi.Kuna ajali za kutengenezwa na hata uadui wa kutengenezwa, mfano nchi moja inawza kuua watu wake makusudu na kusingizia taifa ful;ani limewaua ili lipate sabau ya kupigana vita au kuinyanga'anya nchi hiyo kitu fulani inachohitaji.

Zanzibar iliunganishwa na Tanganyika ili kuinyima haki ya kufaidi matund ya mkataba wa nchi tatu kati yao na Indonesia na Ujerumani mashariki kwa vile tu Nyerere na mataifa ya magharibi yaliingia woga kuwa Zanzibar aidha ingetumbukia kuwa nchi inayofuata taratibu na sheria za kiislamu au kuwa nchi ya kisoshalisti yenye msimamo mkali.

Hivyo ndugu yangu Fundi Mchundo unapoliangalia jambo fulani tafadhali angalia hilo jambo kwa undani na si kijuu juu kwani ukifanya hivyo utakubali kila unaloambiwa hata ukiambiwa. Utaambiwa Ulimwengu sio raia, Bashe sio raia, utaambiwa Mtu mzima kaathirika utaambiwa mengi ambayo usipoyafanyia uchunguzi na utafiti wa kina utabakia kuyaamini.

Kulikuwa na sababu maalum kabisa ya kuwatenganisha waislamu watanzania na waislamu wengine katika mataifa mbalimbali duniani.

Tafakari, Chukua hatua
Mimi nilidhani Zanzibar iliunganishwa na mainland kutokana na hofu za Karume kupinduliwa. Kama ni masuala ya cold war mbona Nyerere alivunja uhusiano na Ujerumani magharibi walipomwekea masharti ya kufunga ofisi ya ubalozi wa Ujerumani mashariki Zanzibar?
 
Kulikuwa na sababu maalum kabisa ya kuwatenganisha waislamu watanzania na waislamu wengine katika mataifa mbalimbali duniani.

Tafakari, Chukua hatua

Domokaya, domokaya, domokaya - baada ya kutoa kauli kama hii ni mwenda wazimu tu ataweza kuendelea kujadiliana na wewe, adieus !
 
Fundi Mchundo,
1. Umesema kwamba wewe ulipokuwa ukisoma (wakati wa mkoloni), ulisoma na Waislaam na Sheikh alikuwa akija kutoa mawaidha.. please naomba unipe jina la shule hiyo au hizo ili nipate kuelimika zaidi.

2. Mkuu wangu tunachozungumzia ni mchango wa Mkoloni ktk kudumaza elimu ya Waislaam, mila na desturi za watu wa Pwani hazihusiani kabisa na kukubaliwa ku register shuleni. Na hakika hadi kufikia Uhuru ni mkoa wa pwani ulikuwa na shule nyingi kuliko mikoa ya bara sasa hatuwezi kusema wazungu walikuwa wajinga kujenga shule zao pwani hali wakijua fika kwamba watu wa pwani hawapendi kusoma..

3. Mkuu wangu sababu nyinginezo naweza kuzikubali lakini pengine unashindwa kuelewa kwamba mimi mfuasi wa Sunni na hakika nimekuwa mfuasi wa dini na dhehebu hili kutokana na imani kwamba kazi ya dini ni ya kiimani na hakuna binadamu mwenye madaraka zaidi au juu ya mwingine.

All glory ni ya Mwenyezi Mungu hivyo unaponambia kwamba kudumazwa kwa elimu ya waislaam nchini kunatokana na sisi wenyewe kuchagua dhehebu la sunni nashindwa kabisa kukuelewa kwani kiutawala haikutakiwa kuwa hivyo. Utawala wowote wa nchi hautakiwi kushirikisha dini ktk maendleleo ya wananchi wake isipokuwa kiroho..

Kama umewahi kunisoma mimi huko nyuma nimekuwa mpinzani mkubwa wa swalka la AFYA na ELIMU kuachiwa vyombo binafsi kuendesha kwa sababu naamini kwamba hizi ni haki za kila binadamu na ni jukumu la mtawala kuhakikisha vitu hivyo anavipata mwananchi wake. Na ndio maana hata tunapopima maendeleo ya nchi ktk elimu au afya huwa tunalaumu utawala uliopo na sio mashirika binafsi. Tunatazama nguvu ya seriukali iliyotenga kupambana na adui hawa na sio kuwaachia missionaries ku deal la shida zetu za kidunia.

Kwa hiyo naweza kusema kwamba Waislaam wanapolalamikia swala hili ni kutokana na kwamba serikali yetu imesahau wajibu wake na kuiga baadhi ya tamaduni au ibada za dini fulani kufanya sheria kwa watu wote..Yes, ktk dunia ya leo ni kilema kikubwa kwa waumini wa sunni kutokuwa organised kwa ajili ya maendeleo yao kama walivyo Wakristu au Wahindi kina Agha Khan lakini pia kukubali kuwa na Organisation kama hizi kunawapa nguvu hawa viongozi kuwa MIUNGU WATU.

Wanakuwa wakiabudiwa jambo ambalo mfuasi wa Sunni hawezi kulikubali kiimani hata siku moja. Na ndio maana kina Shaban Nasibu wakatuletea Bakwata wakifikiria wanaweza kuwaongoza Waislaam kwa kupitia nguvu za watu ikashindikana. sasa wamekuja na mpya ya kutumia Kadhi ambayo pia imeleta utata na kufikia waislaam wa Tanzania kuanza kuwa na makundi ndani ya sunni. Mwezi unaandama ati wamsubiri Kahi mkuu aseme.... hapo ndipo mtu kama mimi sintakubaliana naye na sababu ninazo.

Yote haya yanatokana na kujaribu ku introduce mila na culture za madhehebu mengine ambayo kiimani hayakubaliki ndani ya sunni. na kama unakumbuka Mstaafu Alhajj Mwinyi alichukua kofi la kerbu alipozungumza ujinga. Hii ndio dini ya Sunni na kusema kweli malalamiko yao yooote ni kutokana nakwamba Sunni ni dini na hawana ushiriki ktk ibada zao na maswala ya kidunia. Ni kazi ya serikali kufuatilia mabo ya kidunia na dini inajihusisha na maswala ya dini tu kila mmoja wetu akiwa na nafasi sawa mbele ya Mwenyezi Mungu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom