Ukweli kuhusu waasisi wa TANU na harakati za kupigania uhuru

Status
Not open for further replies.
Mwanafalsafa1,
Nimemsoma sana Mohammed Said kuhusu uasis wa TANU na juhudi za uhuru wa Tanzania ziliasisiwa na Waislamu. Kwa mujibu wake, Nyerere alipochukua madaraka aliwasahau na kuwatekeleza Waislamu waliomkaribisha Dar-es- Salaam na kwenye TANU. Anakubali kuwa Waislamu walikuwa nyuma kielimu kwa sababu ya sera za ukoloni, lakini hakiri kuwa Nyerere alijaribu kurekebisha kasoro hizo. Jinsi ninavyomsoma nadhani theme yake ni kwamba kwa sababu Waislamu "walianzisha" harakati za uhuru, walistahili kuwa na bigger share of the national cake kuliko ilivyo hivi sasa, na wakristo wamechukua nafasi zote za juu nchini wakati kulikuwa na hujuma za makusudi kuzuia Waislamu wasiendelee kielimu. i.e kufutwa kwa EAWMS mna Jamat Islamiya. So this is a call to Moslems to bring about a true liberation.

Jasusi, mkuu, I always bow to your logical arguments and contents.
Lakini kwa hili la huyu Mohammed Said, presentation yake its pure Pumba through and through.
Kwanza kabisa ukoloni haukusababisha waislamu wasisome, kutosoma ni kutokana na waislamu wenyewe.
Wakoloni waliingia nchini with their own vested interests.
Na ndio maana sehemu nyingi tu nchini ambako wakoloni hawakuweka makao maendeleo ya kielimu hata leo ni duni sana.
Kumsingizia Mwalimu kuwa aliwakandamiza waislamu ni kukosa kuelewa ukweli kwa hali ya juu, Mwalimu alilaumiwa sana tena sana kwa kutaifisha shule za Missionari na kuruhusu WATU WA DINI ZOTE kusoma katika shule hizo.
Na shule hizi za Mission zilizotaifihwa si za dini moja hata zile za wahindi eg Aga Khan (Tambaza) vile vile zilichukuliwa kwa ajili ya watu wote.
Pili, si waislamu walioanzisha harakati za ukombozi.
Leo hii kule Kilwa JK amezindua sanamu ya kuwaenzi babu zetu kwa vita ya ukombozi ya Maji Maji,miaka ya 1905.Waafrika wote mashariki ya Tanganyika walishiriki.
Mifano niliyotoa awali ya kina Mkwawa, Isike ,Meli na Kimweri ni mifano tosha.
Hawa walikuwa wanatetea ustaarabu wa mwafrika.
Tatu mimi nashangaa sana kwa watu hawa kama Mohammed Said kwa kukaribisha sumu ya ubaguzi wa kidini na kuihubiri sumu hiyo.
Meya wa kwanza hapa jijini Dar, Sheikh Amri Abeid aliheshimika sana baada ya uhuru na alichaguliwa kuwa Meya wa Dar es salaam.
Alipofariki mwaka 1964 alipewa heshima isiyo ya kawaida.Kwenye mazishi alikuwepo Jomo Kenyatta,Milton Obote na viongozi wengi tu wa Tanganyika.
Na mimi nilikuwepo, ingawaje nilikuwa kijana mdogo.Mizinga ilipigwa pale kwa heshima yake.
Meya huyo wa Dar.
Hii ndio heshima aliyopewa kiongozi Sheikh Amri Abeid na haikutazamwa kwamba alikuwa muislamu au la , ila kiongozi wa Tanganyika.
Leo kwa heshima yake jina la kiwanja cha Arusha kimepewa jina lake.
Sasa mtu anapo pandikiza udini leo ni kama anaikana heshima ya muafrika ili kuendeleza udini mabao hatukua nao.
Dhana ya "kujiliberate" kama mkuu Jasusi unavyoiweka inakosa mantiki pale ambapo unatanguliza fikra ya kuonewa.
Kimsingi kufuta ujinga ilikuwa kilio cha serikali ya awamu ya kwanza baada ya uhuru.
Kilio hiki kiliitikiwa na sehemu chache sana zilizopata mwanga wa umuhimu wa elimu. Leo miaka karibu 50 baada ya uhuru kwa wengine bado ni kilio kile kile.
Ndugu zagu waislamu na waTanzania wenzangu, lazima tuwekeze katika elimu ya watoto wetu. Na hakuna mchawi wa matatizo ya kukosa elimu kwa sehemu nyingi za mikoa ya pwani na zingine nyingi tu mikoani ila kuheshimu kuwekeza katika elimu ya watoto wetu.
 
Gwakisa umeongea vizuri sana, sehemu ambazo wakoloni hawakuweka makao amendeleo ni duni sana, hii ni bada ya miaka 49 ya uhuru serikali yetu inafuata misingi ya kikoloni na sera zilezile zilizoletwa na madalali wa ukoloni. Harakati za kupinga ukoloni za kina kinjeketile, mkwa wa na wengineo wengi ilikuwa ni kupinga kuletewa na kuendeshwa na taratibu ambazo wao hawazitaki hivyo hivyo harakati za taa na tanu. Leo hapa ishi ni hii je kile wlichokipigania kina kinjeketile na kina mkwawa na wengineo pamoja na waasisi wa tanu kimepatikana? Angalau jana wamatumbi saba wamekumbukwa baada ya miaka kadhaa ya kusahauliwa na kupuuzwa na badala yake makabila mengine ndio yakaonekana ya maana hata hivi leo ndio wanapeana sehemu nono katika keki ya taifa. Gwakisa uliwahi kuwafahamu wamatumbi wengine zaidi ya kinjeketile ngwale katika mapambambano dhidi ya wakoloni. Ibrahim husein alihoji hili lakini nae alionekana hana akili akabezwa na kupuuzwa, lakini ni kitabu alichoandika huyohuyo ibrahim husein kilichopelekea kukumbukwa kwa wamatumbi wengine sita. Kama hilo limewezekana basi angalau watanganyika waambie ukweli kuhusu waasisi wa tanu na sio kutoa majina ya kiislamu kusema eti waislamu walienziwa. Kwa ninim inakuwa ngumu kwa historia kusema ukweli kuhusu waasisi wa tanu? Hili ndilo swali la msingi.
 
unajua ukiwa na jzaba si rahisi kutoa mawazo mazuri, anacholalamikia mohamed said ndicho unachokithibitisha, analalamika kukoseshwa fursa halafu kuandaliwa propaganda ili waislamu waonekane wajinga.Propaganda ya kuwa walikataa shule. Hivi enzi za Nyerere kuna mtu aliweza kukataa kitu Nyerere alichohitaji kitekelezwe? Hawa viongozi wetu wa leo pamoja na kukosa nguvu lakini wameweza kuwalazimisha wazazi wawapeleke watoto wao shuleni, je Nyerere angeshindwa kuwalazimsha waislamu wawapeleke watoto wao shuleni alipokuwa madarakani. Tuache uvivu wa kufikiri jamani
 
Mtoa hoja,
Walio changia kupata uhuru wa TANGANYAIKA ni WATANGANYIKA karibu millioni 10 wakati huo.....je unataka hao woote waandikwe kwenye historia? Halafu iweje? Tulichokitaka 1961 ilikuwa uhuru na tukaupata...tunayo katiba inayomlinda kila raia Muislamu au vinginevyo.Maswali laini kwako:
1.Je Muislamu wa leo anakwaza na nini kikatiba?Hamiliki mali?Hasomi?Hatibiwi?Haabudu?Hachagui amtakaye?Anatengwa kwa namna yeyote institutionally?
2.Tukikubali hayo atakayo huyo Dr. wako tutanufaika vipi kama nchi?
3.Hiyo historia ikibadilisha hiki kizazi kipya utakiambia nini?
4.Kama utathibitisha kuwa kweli Waislam ndio walioleta uhuru, halafu tufanyeje? Tuwafanyie pati au maulidi?
5.Tanzania(Bara) ina waisalmu kama milioni 15 na hao wengine milioni 25 ni wa imani zingine....utawapeleka wapi hawa 25m maana sasa wenye nchi kwa mujibu wako nchi ni mali ya waislamu
 
Eti suluhisho ni kuheshimu kuwekeza katika elimu ya watoto wetu, hichi ni kichekesho. Mtu hohehahe aliyenyimwa fursa toka enzi za kabala ya uhuru mpaka leo, shule bora zenye kuhitaji fedha atazimudu vipi. Hivi unajua ule mpang wa quota system katika elimu uliwekwa kwa madhumuni gani?
 
Muislamu wa leo hawakilishwi mawazo yakem ipasavyo kwani chombo kilichopo katika kuwasilisha mawazo ya waislamu si cha kiislamu ndio maana hata usimamiaji wake taasisi muhimu zinazodaiwa kumilikiwa na waislamu ni wa kusua sua. Taasisi kama vile shule hosipitali na vituo vya kulelea mayatima na wasio jiweza kam ilivyo kwa taasisi za dini nyingine mfano Rc, hivyo BAKWATA imefanya sura ya waislamu wa Tanzania kuwa wanyonge. Hii ni kwa sababu BAKWATA inapata nguvu za udhalimu kutoka serikalini.Tukitakubali ya dr wananchi wa Tanzania wtafahamu kuwa waislamu walishiriki kupigania uhuru wa tanganyika bila kujali ubaguzi wa dini, walipigania uhuru wa watanganyika hivyo dhana ya kuwa na ubaguzi wa kidini nchi itapojiunga na taasisi kama OIC si ya msingi. Waislamu wakiimarika na kuimarisha taasisi zao hawatkuwa na ubaguzi wa kidini kwa watu kunufaika na taasisi hizo hivyo taifa kiujumla litanufaika. Historia hiyo itawafany kizazi kipya kuwa bora zaidi kujua wapi walipotoka na wapi wanapokwenda na zaidi kuziona changamoto za otofauti wa kidini kama zinafaa kuenziwa au la na hat pengine kutoa wazo jipya kwa watanzania na waafrika kwa ujumla kuzitambua dini zao za asili na kuachana na dini za wayahudi na waarabu.
Hakuna aliyesema nchi ni mali ya waislamu ingekuwa hivyo Nyerere wasingemshirikisha katika TANU
 
Safari_ni_ Safari
Sina cha kuongezea maana umeshindilia boriti zote kiasi hamna haja ya kuongezea zingine. Bravo
 
Muislamu wa leo hawakilishwi mawazo yakem ipasavyo kwani chombo kilichopo katika kuwasilisha mawazo ya waislamu si cha kiislamu ndio maana hata usimamiaji wake taasisi muhimu zinazodaiwa kumilikiwa na waislamu ni wa kusua sua. Taasisi kama vile shule hosipitali na vituo vya kulelea mayatima na wasio jiweza kam ilivyo kwa taasisi za dini nyingine mfano Rc, hivyo BAKWATA imefanya sura ya waislamu wa Tanzania kuwa wanyonge. Hii ni kwa sababu BAKWATA inapata nguvu za udhalimu kutoka serikalini.Tukitakubali ya dr wananchi wa Tanzania wtafahamu kuwa waislamu walishiriki kupigania uhuru wa tanganyika bila kujali ubaguzi wa dini, walipigania uhuru wa watanganyika hivyo dhana ya kuwa na ubaguzi wa kidini nchi itapojiunga na taasisi kama OIC si ya msingi. Waislamu wakiimarika na kuimarisha taasisi zao hawatkuwa na ubaguzi wa kidini kwa watu kunufaika na taasisi hizo hivyo taifa kiujumla litanufaika. Historia hiyo itawafany kizazi kipya kuwa bora zaidi kujua wapi walipotoka na wapi wanapokwenda na zaidi kuziona changamoto za otofauti wa kidini kama zinafaa kuenziwa au la na hat pengine kutoa wazo jipya kwa watanzania na waafrika kwa ujumla kuzitambua dini zao za asili na kuachana na dini za wayahudi na waarabu.
Hakuna aliyesema nchi ni mali ya waislamu ingekuwa hivyo Nyerere wasingemshirikisha katika TANU

Domokaya , for your namesake, you are degenerating into an argument that smells of senseless bigotry on your part.
In your argument please take us along so that we may see your point of factual view and as such we may probably give some tips to help.
Sasa chombo chenu cha BAKWATA nani akusaidie kukiendesha?
Kama hakifai si kiueni na mtengeneze hicho kinachowafaa?
Si vyema mimi kuijadili BAKWATA maana si chombo kinachonitumikia na itikadi yake siifamu.
The issue here is there are some lazy Tanzanians, and I hope you do not for part of it, that think they can just live off the Governments taxes, just to settle the score.
Hebu jaribuni kuona wenzenu wanavyochangia maendeleo yao katika shule ,vyuo vikuu,zahanati na barabara kwa kutoa mifukoni mwao.
Na hilo unaonewa kwa kiasi gani sijui.
Unapotaka kupewa vya bure kwa kisingizio chochote kile basi hata ukikipata basi bado utalia unaonewa kwa vile hakikukutosha mpaka shibe yako.
Sasa tukiendelea kupekua zaidi mkuu Domokaya utaanza kulia na ukabila na udini kwa kwenda mbele.
 
Jengeni hoja kuimarisha BAKWATA na sio jazba...tatizo lenu mnataka muende pale Kinondoni na bakora,majambia,fatwa nk na kila mkifanya hivyo Mufti shurti aite Polisi kulinda usalama...nyie manadai BAKWATA inalindwa na serikali...hivi mimi niende pale kwa Kadinali wangu na amafimbo,makelele,majambia si ataiata Polisi pia? sasa ntasema TEC ni ya serikali au serikali inailinda amani?...si kila kitu kinasuluhishwa na confrotations
 
Domokaya,
Umeuliza maswali mawili ninayotaka kugusia. Umeuliza ni kwa nini inakuwa ngumu kwa historia kusema ukweli kuhusu waasisi wa TANU.
Hapa sijui unaposema historia unamsema nani. Historia ya Tanganyika niliyoisoma, imewataja waasisi wa TANU. Akaja Mohammed Said akashindilia kuwa waislamu ndio waliokuwa waasisi wa TANU. Sasa ulitaka historia ipi tena? Ukisoma kitabu cha Lady Listowell, The Making of Tanganyika, alijitahidi sana kuorodhesha waasisi unaolalamikia kuwa historia imewasahau. Swali la pili umeuliuza kama Nyerere angeshindwa kuwalazimisha ( the operating word hapa ni kulazimisha) waislamu kuwapeleka watoto wao shuleni alipokuwa madarakani. Nyerere alijitahidi ku level play ground ya shule kwa kutaifisha shule za mishenari ili kila Mtanganyika apate nafasi sawa. Haukuwa wajibu wake kupita nyumba kwa nyumba kuwalazimisha Waislamu kupeleka watoto wao shule. Kuna msemo wa Kiswahili, unaweza kuwapaleka ng'ombe ziwani lakini huwezi kuwalazimisha kunywa maji. Haikuwa wajibu wake kulazimisha watu wasomeshe watoto wao kama watu hao wenyewe hawaioni hiyo fursa.
 
Wakuu zangu,
habari kama hizi ni very sensitive na sii vizuri ukazichukua kwa kufikiria imani yako ili kujibu hoja iliyopo. hakika huyu Mohammed Said kazungumza mengi. Yapo ya ukweli na yapo MENGI ya uongo ama tungo ambazo kwa mwenye akili timamu ataelewa kwamba kichwa cha habari ya mabandiko yake yote ni UDINI.. Ni kuonyesha chuki yake kwa Wakristu zaidi ya kuzungumzia Uhuru na Utawala mzima wa Tanganyika au Tanzania chini ya mwalimu.

Kwa hiyo hata nyie mnapokuja hapa na kuzipitia hoja za huyu jamaa, kisha mkaiga mtindo wake kuzijibu inawaweka pia ktk nafasi mbaya zaidi kwani msomaji kama mimi ni rahisi sana kujua kwamba hata wewe unatumia UDINI badala ya facts zilizokuwepo. Hakuna mtu anayepinga kitu kisha akaandika ukweli ulikuwaje ila kwa kufikiria tu jibu sahihi ni kupingana na Mohammed Said (hearsay).

Kwa mfano nimesoma mahala mtu mmoja akisema, Wakoloni hawakuwatenga Waislaam kielimu. Huyu mtu hajui historia ya Mkoloni kwani siku zote kazi kubwa ya mkoloni popote alipo ilikuwa ni kuwatenganisha wananchi wa makoloni hayo ili apate kutawala kirahisi.. Mkoloni hutafuta weakness yenu na vitu gani vinavyoweza kuleta uhasama baina yenu na akavitumia. Elimu ilikuwa moja ya silaha zake kubwa sana ktk kuyagawa makabila au makundi ya dini..
Sasa mtu anapokuja na kudai ati Waislaam wenyewe ndio hawakwenda shule pasipo facts zinazothibitisha maelezo yake, hizi ni akili ya kitumwa kwa sababu huyu mtu sio Muislaam na hakuwepo ktk uatywala wa mkoloni tuseme yeye ni msemaji wao. Huwezi kuzungumza kwa niaba yao hali hujui kilichotokea..Na anatumia hizi lawama za mkoloni kama vile unalaumiwa Ukristu..

Mimi nimesoma shule ya msingi huko Kibara, Mwibara najua kilichonikuta mimi na ndugu zangu walionitangulia hadi mwalimu alipobadilisha mfumo wa elimu ya mkoloni msifanye mzaha hata kidogo.

Namkubali sana mkuu mwenzangu Jasusi ambaye anajua fika dhamira ya waandishi kama huyu Said. Na kibaya zaidi hatav hao waislaam wenyewe wanaposoma maandishi ya mtu huyu wanashindwa kuingia aibu zaidi kwani huyu said anatumia zaidi mila na desturi za Waarabu kuzungumzia Uislaam. Na mtu kama mimi nayeweza kujitoa ndani ya sanduku nahisi huyu Mohammed ana asili zaidi ya Kiarabu na pengine mtumwa wa mila na desturi za kiarabu kuliko Uislaam wenyewe.

Haiwezekani mtu asifie vazi la Baibui kuwa ni vazi la kiislaam hali akijua fika kwamba sii kweli isipokuwa ni vazi la waarabu tena kwa ajili ya kujilinda na vumbi pamoja na virusi vinavyoambukiza magonjwa ya macho. Ni vazi linalolingana na mazingira ya nchi zote za mashariki ya kati. hao waislaam wa Tanzania na pwani wameiga utamaduni usiohusiana kabisa na mazingira yao isipokuwa kutokana na UTUMWA.

Hata kanzu na kicho kibaraghashia kinachovaliwa sana nchini, ni utamaduni wa WaOman na kina sisi tulotawaliwa na Waoman - haihusiani kabisa na Uislaam. Sii Saudia wala nchi nyingine yeyote ya kiislaam wanavaa kofia na kanzu kama hizi zetu, isipokuwa kila makabila yao yanalo vazi yake likitofautiana na makabila mengine ya kiarabu.


Ifike wakati waislaam tukzungumzie ukweli na kutoficha jambo kwa visingizio. Hivi kweli serikali ya kwanza ya Nyerere ilikuwa haina Waislaam? hivi kweli tunaweza kumlaumu Nyerere kwa kuvunjika kwa East African Muslim Society hali tunajua fika kwamba ni kina Shaban Nassib ndio walivunja mahusiano na chombo hicho wakikipiga marufuku kufanya shughuli zao mikoa yao. Mikoa ya Bukoba (Ziwa magharibi) na Tanga zikiongozwa na Waislaam ndio mikoa ya kwanza kupiga marufuku chama hicho kujishughulisha makwao kwa sababu hawa Waislaam wenyewe walikuwa TANU na wakaona chama hicho kinawaingilia kula yao.

Tatizo la miiko na maadili halikuanza majuzi, ni tatizo sugu la kila Mwafrika mtawaliwa anapopata madaraka kidogo husahau hata dini yake. Waliokipiga vita chama cha EAMS ni pamoja na kundi kubwa la waislaam waliokuwa ndani ya chama TANU wakitaka wao kuwa watawala kama walivyoachiwa na mkoloni. Nyerere alikuwa mwiba kwa wengi sana na hakika chuki yoote hii kwa Nyerere ni kwa sababu Nyerere alikata mizizi yoote ya unyonyaji na fikra za hawa watawaliwa kufikiri kwamba kuondoka kwa mkoloni basi wamekabidhiwa rungu wao.

Yes, upo ukweli mkubwa kuhusiana na historia ya waislaam ktk jitihada za Uuru wetu, upo ukweli mkubwa wa ushirikiano baina ya Nyerere na kina Sykes kupeana mamlaka lakini hizi chuki pandikizi zinaboreshwa na watu waliotegemea kupewa nafasi ndani ya mamlaka ya kiutawala. Sii tu Nyerere aliwaweka chini waislaam, Nyerere hakuweza hata kuchukua viongozi wa juu toka makabila mengineyo kutokana na uwezo wetu kielemu. makabila yaliyokuwa yameelimika yalikuwa matatu..oooh manne na Wakerewe of course!..

Hivyo uongozi ulikwenda katika wale wenye uwezo wa kuongoza na kwa bahati mbaya au nzuri sii waislaam wala makabila 115 mengine ambayo pia wanaweza kuweka madai yao ya kubaguliwa kama waislaam. Ndugu zangu waislaam na Wakristu hizi habari za Udini haziwezi kulijenga taifa la kesho bali kutugawa zaidi pasipo kukubali na kujifunza kutokana na makosa yaliyofanyika zamani. hakuna sababu wala haja ya ku question kila kosa lililofanyika kwa mtazamo wa dini. na hakika huyu Nyerere mwenyewe kazikwa akitazama Mecca ingawa ni mila za kabila lake, kafa kajenga Msikiti hao viongozi wenu waislaam wangapi wamefanmya hivyo? huyo Mohammed said hata kuchangia tofali maisha yake hajawahi kufanya.. Hujafa hujaumbika mkuu wa ngu..

Na kwa ndugu zangu wakristu acheni ujinga.... Kwa kichuguu na Jasusi naukumbuka wimbo huu tulipokuwa shule tukitembelewa na viongozi wa kanisa.. Kagunguli mission baliyo Bapadre, baliyooo baliyooo baliyo bapadre.. makofiiiii na vigelelgele...

Nimemaliza - msema ovyo!
 
Mkandara,'
Thanks. Sina la ziada. Tanzania ni yetu sote. Tuijenge pamoja, tuondoe kasoro zinazotukabili pamoja na tudumishe mshikamano. That is the only way forward.
 
Mwingine ni Christopher Mtikila na udini wake pamoja na ubaguzi wake wa rangi. Halafu kuhusu Nyerere, alipoulizwa katika interview, "Heaven on Earth": "Was there anything positive about Nyerere?" Alijibu na kusema: "If there were any I would say. But throughout the forty-one years of his rule, I never saw one."
 
Some Muslims within the Party rose to challenge this new development. Sheikh Suleiman Takadir, Chairman of TANU Elders Council, and all Muslim body wanted the Party to discuss this problem. There were fears that the emerging Christian leadership in TANU which would obviously go into the Legislative Council would also go on to form the first independence government. It was feared that these would use Church influence to suppress Islam as a political force. This conflict threatened to split the Party. 1958 was very crucial time for TANU. For over thirty years Africans had been working towards having democratic principles established in Tanganyika. TANU in 1958 was on the verge of knocking the doors of the Legislative Council but for the problem of Christianity which was again cropping up for the second time in the Party. The majority of Muslims in TANU did not see the African Christians as posing any threat to Islam in free Tanganyika. Many saw the Christian influx into the Party’s leadership positions as a catalyst for accelerating the thrust of the struggle - a consolidation of its own strength vis-a-vis the conspiracies of the colonial state. No one saw this rapid changing pattern of Party leadership as a neutralising agent against Muslim influence in TANU. The Takadir faction which was calling for equal representation between Muslims and Christians in the party leadership and in the independence government was seen as a divisive element. Sheikh Takadir was relieved of his post in TANU, suspended and later expelled from the Party for raising the sensitive issue, which it was feared, would divide the party along religious lines and consequently slow down the tempo of the struggle.10 TANU, therefore, selected the following to contest the 1958 election: Julius Nyerere, John Keto, Nesmo Eliufoo, John Mwakangale and Chief Abdallah Said Fundikira.

imeandaliwa na MALARIA SUGU, kwa msaada mkbwa wa tTUMAIN, DOMOKAYA, JEYKEY kwa lengo la kupotosha umma wa WATANZANIA.
 
ukisha anza ku personalize katika kufanya arguement basi anza kufikiria kujipanga upya katika ujenzi wa hoja
 
Wakuu zangu,
habari kama hizi ni very sensitive na sii vizuri ukazichukua kwa kufikiria imani yako ili kujibu hoja iliyopo. hakika huyu Mohammed Said kazungumza mengi. Yapo ya ukweli na yapo MENGI ya uongo ama tungo ambazo kwa mwenye akili timamu ataelewa kwamba kichwa cha habari ya mabandiko yake yote ni UDINI.. Ni kuonyesha chuki yake kwa Wakristu zaidi ya kuzungumzia Uhuru na Utawala mzima wa Tanganyika au Tanzania chini ya mwalimu.

Kwa hiyo hata nyie mnapokuja hapa na kuzipitia hoja za huyu jamaa, kisha mkaiga mtindo wake kuzijibu inawaweka pia ktk nafasi mbaya zaidi kwani msomaji kama mimi ni rahisi sana kujua kwamba hata wewe unatumia UDINI badala ya facts zilizokuwepo. Hakuna mtu anayepinga kitu kisha akaandika ukweli ulikuwaje ila kwa kufikiria tu jibu sahihi ni kupingana na Mohammed Said (hearsay).

Kwa mfano nimesoma mahala mtu mmoja akisema, Wakoloni hawakuwatenga Waislaam kielimu. Huyu mtu hajui historia ya Mkoloni kwani siku zote kazi kubwa ya mkoloni popote alipo ilikuwa ni kuwatenganisha wananchi wa makoloni hayo ili apate kutawala kirahisi.. Mkoloni hutafuta weakness yenu na vitu gani vinavyoweza kuleta uhasama baina yenu na akavitumia. Elimu ilikuwa moja ya silaha zake kubwa sana ktk kuyagawa makabila au makundi ya dini..
Sasa mtu anapokuja na kudai ati Waislaam wenyewe ndio hawakwenda shule pasipo facts zinazothibitisha maelezo yake, hizi ni akili ya kitumwa kwa sababu huyu mtu sio Muislaam na hakuwepo ktk uatywala wa mkoloni tuseme yeye ni msemaji wao. Huwezi kuzungumza kwa niaba yao hali hujui kilichotokea..Na anatumia hizi lawama za mkoloni kama vile unalaumiwa Ukristu..

Mimi nimesoma shule ya msingi huko Kibara, Mwibara najua kilichonikuta mimi na ndugu zangu walionitangulia hadi mwalimu alipobadilisha mfumo wa elimu ya mkoloni msifanye mzaha hata kidogo.

Namkubali sana mkuu mwenzangu Jasusi ambaye anajua fika dhamira ya waandishi kama huyu Said. Na kibaya zaidi hatav hao waislaam wenyewe wanaposoma maandishi ya mtu huyu wanashindwa kuingia aibu zaidi kwani huyu said anatumia zaidi mila na desturi za Waarabu kuzungumzia Uislaam. Na mtu kama mimi nayeweza kujitoa ndani ya sanduku nahisi huyu Mohammed ana asili zaidi ya Kiarabu na pengine mtumwa wa mila na desturi za kiarabu kuliko Uislaam wenyewe.

Haiwezekani mtu asifie vazi la Baibui kuwa ni vazi la kiislaam hali akijua fika kwamba sii kweli isipokuwa ni vazi la waarabu tena kwa ajili ya kujilinda na vumbi pamoja na virusi vinavyoambukiza magonjwa ya macho. Ni vazi linalolingana na mazingira ya nchi zote za mashariki ya kati. hao waislaam wa Tanzania na pwani wameiga utamaduni usiohusiana kabisa na mazingira yao isipokuwa kutokana na UTUMWA.

Hata kanzu na kicho kibaraghashia kinachovaliwa sana nchini, ni utamaduni wa WaOman na kina sisi tulotawaliwa na Waoman - haihusiani kabisa na Uislaam. Sii Saudia wala nchi nyingine yeyote ya kiislaam wanavaa kofia na kanzu kama hizi zetu, isipokuwa kila makabila yao yanalo vazi yake likitofautiana na makabila mengine ya kiarabu.


Ifike wakati waislaam tukzungumzie ukweli na kutoficha jambo kwa visingizio. Hivi kweli serikali ya kwanza ya Nyerere ilikuwa haina Waislaam? hivi kweli tunaweza kumlaumu Nyerere kwa kuvunjika kwa East African Muslim Society hali tunajua fika kwamba ni kina Shaban Nassib ndio walivunja mahusiano na chombo hicho wakikipiga marufuku kufanya shughuli zao mikoa yao. Mikoa ya Bukoba (Ziwa magharibi) na Tanga zikiongozwa na Waislaam ndio mikoa ya kwanza kupiga marufuku chama hicho kujishughulisha makwao kwa sababu hawa Waislaam wenyewe walikuwa TANU na wakaona chama hicho kinawaingilia kula yao.

Tatizo la miiko na maadili halikuanza majuzi, ni tatizo sugu la kila Mwafrika mtawaliwa anapopata madaraka kidogo husahau hata dini yake. Waliokipiga vita chama cha EAMS ni pamoja na kundi kubwa la waislaam waliokuwa ndani ya chama TANU wakitaka wao kuwa watawala kama walivyoachiwa na mkoloni. Nyerere alikuwa mwiba kwa wengi sana na hakika chuki yoote hii kwa Nyerere ni kwa sababu Nyerere alikata mizizi yoote ya unyonyaji na fikra za hawa watawaliwa kufikiri kwamba kuondoka kwa mkoloni basi wamekabidhiwa rungu wao.

Yes, upo ukweli mkubwa kuhusiana na historia ya waislaam ktk jitihada za Uuru wetu, upo ukweli mkubwa wa ushirikiano baina ya Nyerere na kina Sykes kupeana mamlaka lakini hizi chuki pandikizi zinaboreshwa na watu waliotegemea kupewa nafasi ndani ya mamlaka ya kiutawala. Sii tu Nyerere aliwaweka chini waislaam, Nyerere hakuweza hata kuchukua viongozi wa juu toka makabila mengineyo kutokana na uwezo wetu kielemu. makabila yaliyokuwa yameelimika yalikuwa matatu..oooh manne na Wakerewe of course!..

Hivyo uongozi ulikwenda katika wale wenye uwezo wa kuongoza na kwa bahati mbaya au nzuri sii waislaam wala makabila 115 mengine ambayo pia wanaweza kuweka madai yao ya kubaguliwa kama waislaam. Ndugu zangu waislaam na Wakristu hizi habari za Udini haziwezi kulijenga taifa la kesho bali kutugawa zaidi pasipo kukubali na kujifunza kutokana na makosa yaliyofanyika zamani. hakuna sababu wala haja ya ku question kila kosa lililofanyika kwa mtazamo wa dini. na hakika huyu Nyerere mwenyewe kazikwa akitazama Mecca ingawa ni mila za kabila lake, kafa kajenga Msikiti hao viongozi wenu waislaam wangapi wamefanmya hivyo? huyo Mohammed said hata kuchangia tofali maisha yake hajawahi kufanya.. Hujafa hujaumbika mkuu wa ngu..

Na kwa ndugu zangu wakristu acheni ujinga.... Kwa kichuguu na Jasusi naukumbuka wimbo huu tulipokuwa shule tukitembelewa na viongozi wa kanisa.. Kagunguli mission baliyo Bapadre, baliyooo baliyooo baliyo bapadre.. makofiiiii na vigelelgele...

Nimemaliza - msema ovyo!

Nakufagilia mkuu kwa deliberation safi yenye nia ya kuleta umoja kati ya makundi yote ya watanzania.
I however object to your observation highlighted in red for lack of merit.
Inaweza kuwa maoni yako kama ulivyo malizia- ya msema ovyo.
Kam maoni hayo yana mantiki basi waTanzania tuna kazi kubwa sana na tutamlaumu mwalimu hata kwa mambo ya kipuuzi.
Waarabu walifika Bagamoyo,Kilwa,Msasani na hat huko Uguja miaka ya 1100, na baadaye 1600-1800.
Ningeomba nielimishwe Mkandara mkuu ,kwa utumwa nilionao, elimu ya maana hawa waarabu waliyoi-inculcate kwa jamii ya watu waliowakuta katika maeneo hayo.
Baada ya maeneo haya hebu twende sehemu nyingi nchini ambazo waarabu ambao (walikuwa waislamu) walituama kwa miaka mingi sana kabla ya hat ya uhuru. Sehemu za Ujiji,sehemu za Zanzibar,Kilwa Lindi,Pangani nk.
Si kwamba hawa watu hawakuja na elimu yao , hasha. Lakini mpaka leo hizi sehemu ziko nyuma kuielimu
Wa kulumiwa nani.Pengine ukinielimisha, Mkandara mkuu, kautumwa nilikonako katatoweka.
 
Nakufagilia mkuu kwa deliberation safi yenye nia ya kuleta umoja kati ya makundi yote ya watanzania.
I however object to your observation highlighted in red for lack of merit.
Inaweza kuwa maoni yako kama ulivyo malizia- ya msema ovyo.
Kam maoni hayo yana mantiki basi waTanzania tuna kazi kubwa sana na tutamlaumu mwalimu hata kwa mambo ya kipuuzi.
Waarabu walifika Bagamoyo,Kilwa,Msasani na hat huko Uguja miaka ya 1100, na baadaye 1600-1800.
Ningeomba nielimishwe Mkandara mkuu, kwa utumwa nilionao, elimu ya maana hawa waarabu waliyoi-inculcate kwa jamii ya watu waliowakuta katika maeneo hayo.
Baada ya maeneo haya hebu twende sehemu nyingi nchini ambazo waarabu ambao (walikuwa waislamu) walituama kwa miaka mingi sana kabla ya hat ya uhuru. Sehemu za Ujiji,sehemu za Zanzibar,Kilwa Lindi,Pangani nk.
Si kwamba hawa watu hawakuja na elimu yao , hasha. Lakini mpaka leo hizi sehemu ziko nyuma kuielimu
Wa kulumiwa nani.Pengine ukinielimisha, Mkandara mkuu, kautumwa nilikonako katatoweka.
Unarudia Upuuzi ule ule.. Kuwa maadam Waarabu walikuwa Waislaam basi ndio waliokuja na elimu pasipo kufahamu kwamba Uislaam na waarabu waliokuja ni vitu viwili tofauti kabisa..Waajemi na Mabarush walikuja Coast ya east Afrika toka karne ya kwanza wakifanya biashara way back kabla hata ya dini kuwepo duniani. Kwa hiyo sijui unaposema waarabu una maanisha wapi WaOman au?

Pili, Waarabu alipokuja mwaka 1100 walikuja fanya biashara wakiondoka na kurudi wakati wazungu walikuja kutafuta koloni za kutawala, haya ni malengo na tactics tofauti baina yao. Kisha, Zanzibar ya 1800 ilipokuja tawaliwa na Sultan (mwarabu) walikuwa na wasomi kuliko sisi Bara hadi kufikia Uhuru pamoja na kwamba sisi tulikuwa na watu wengi na shule nyingi kuliko wao.

Na hii wala sio sifa kwa Sultan kuwa na wasomi kuliko Utawala wa Mjarumani na Muingereza kwa sababu unachopima wewe ni unafuu wa kitumwa baina ya wakoloni hawa wawili, badala ya kuwa na kipimo cha elimu bora kwa wananchi wake pasipo kuwepo ubaguzi.. Sasa kama leo hao watu wa pwani wako nyuma kieleimu tuilaumu dini gani? tusiwalaumu tena wakoloni waarabu au wazungu maana hawapo tena, tujiulize sisi wenyewe imekuwaje hawa watu wa Pwani bado wako nyuma kielimu hata baada ya miaka 50 ya Uhuru wetu?

Mkuu, mtazamo wako unahusiana na rangi za watu pamoja na dini kufikia mahitimisho unayoyatoa sawa sawa na huyo Mohammed Said.. Hii ndio point yangu kuu na ndiyo inayowafanya watu kama Said kuamini kwamba maadam Nyerere alikuwa mkristu, basi bila shaka aliwakandamiza Waislaam kielimu na kibaya zaidi wapo watu kama wewe wanaamini kwamba huyu Kikwete hatufai kwa sababu ni Muslaam.
Haya ni mawazo ya kitumwa na ndio athari ya kutawaliwa kwani unafuu ndio unatumika kuwa kipimo cha maendeleo kama vile mtumwa akipewa Unyapala.

By the way nimesoma mahala umesema Sheikh Amri Abeid alikuwa Meya wa jiji ka Dar es Salaam, je, una hakika na hilo au... maanake kumbukumbu zangu zinaonyesha sivyo..sina hakika zaidi lakini nadhani Sheikh Kaluta Amri Abeid wa magomeni Mikumi alikuwa waziri wa sheria kabla ya kifo chake!
 
..kuna makundi mengi sana ambayo yalishiriki ktk harakati za uchaguzi ambayo yanaweza kutoa malalamiko kama haya anayoyatoa Mohamed Saidi.

..mfano mmoja wa makundi hayo ni VYAMA VYA USHIRIKA. vyama hivyo vilikuwa mstari wa mbele ktk harakati za uhuru, lakini Mwalimu alikuja kuvivunja na kuunda mamlaka za mazao.

..kwa mtizamo wangu Mohamed Saidi anaelezea mchango wa wananchi wa mikoa ya Pwani, haswa dsm, ktk harakati za uhuru. personally nimesoma makala zake nikachukua yale ya msingi na kupuuza yale yasikuwa ya msingi.

..waandishi toka maeneo mengine ya Tanzania/Tanganyika hawazuiwi kuandika vitabu na makala kuelezea michango ya wazee wao ktk harakati za kugombea uhuru. kitu kibaya wanachoweza kufanya ni kupuuza michango ya ndugu zao wa maeneo mengine ya nchi yetu.

..waumini wa madhehebu mbalimbali nao wana ruksa ya kuandika ushiriki wa madhehebu yao ktk harakati za uhuru. kwa mfano, nilisoma makala za Padri mmoja mkatoliki akielezea urafiki wake na Mwalimu, na jinsi wamisionari wakatoliki walivyokuwa wakimfadhili wakati wa harakati za kugombea uhuru. makala hizo zilitoka kwenye blog ya Issa Michuzi.

..vilevile kuna Wahindi,Wazungu, etc etc walioshiriki harakati zile. hawa nao wanapaswa kuandika kuhusu mchango wao. why not? tena hawa wanaweza kuwa na malalamiko makubwa-makubwa kwasababu Mwalimu alikuja kutaifisha mali zao.

..tumchukulie Mohamed Saidi kwamba ameandika kitabu chake kutokana na elimu na uelewa wake. tatizo ni kwamba in recent yrs ni yeye peke yake aliyejishughulisha kutafiti na kuandika historia yetu. wangekuwepo waandishi wengine nina hakika wananchi tungeweza kupata picha nzima ya nini kilitokea ktk harakati za kutafuta uhuru.
 
Unarudia Upuuzi ule ule.. Kuwa maadam Waarabu walikuwa Waislaam basi ndio waliokuja na elimu pasipo kufahamu kwamba Uislaam na waarabu waliokuja ni vitu viwili tofauti kabisa..Waajemi na Mabarush walikuja Coast ya east Afrika toka karne ya kwanza wakifanya biashara way back kabla hata ya dini kuwepo duniani. Kwa hiyo sijui unaposema waarabu una maanisha wapi WaOman au?

Pili, Waarabu alipokuja mwaka 1100 walikuja fanya biashara wakiondoka na kurudi wakati wazungu walikuja kutafuta koloni za kutawala, haya ni malengo na tactics tofauti baina yao. Kisha, Zanzibar ya 1800 ilipokuja tawaliwa na Sultan (mwarabu) walikuwa na wasomi kuliko sisi Bara hadi kufikia Uhuru pamoja na kwamba sisi tulikuwa na watu wengi na shule nyingi kuliko wao.

Na hii wala sio sifa kwa Sultan kuwa na wasomi kuliko Utawala wa Mjarumani na Muingereza kwa sababu unachopima wewe ni unafuu wa kitumwa baina ya wakoloni hawa wawili, badala ya kuwa na kipimo cha elimu bora kwa wananchi wake pasipo kuwepo ubaguzi.. Sasa kama leo hao watu wa pwani wako nyuma kieleimu tuilaumu dini gani? tusiwalaumu tena wakoloni waarabu au wazungu maana hawapo tena, tujiulize sisi wenyewe imekuwaje hawa watu wa Pwani bado wako nyuma kielimu hata baada ya miaka 50 ya Uhuru wetu?

Mkuu, mtazamo wako unahusiana na rangi za watu pamoja na dini kufikia mahitimisho unayoyatoa sawa sawa na huyo Mohammed Said.. Hii ndio point yangu kuu na ndiyo inayowafanya watu kama Said kuamini kwamba maadam Nyerere alikuwa mkristu, basi bila shaka aliwakandamiza Waislaam kielimu na kibaya zaidi wapo watu kama wewe wanaamini kwamba huyu Kikwete hatufai kwa sababu ni Muslaam.
Haya ni mawazo ya kitumwa na ndio athari ya kutawaliwa kwani unafuu ndio unatumika kuwa kipimo cha maendeleo kama vile mtumwa akipewa Unyapala.

By the way nimesoma mahala umesema Sheikh Amri Abeid alikuwa Meya wa jiji ka Dar es Salaam, je, una hakika na hilo au... maanake kumbukumbu zangu zinaonyesha sivyo..sina hakika zaidi lakini nadhani Sheikh Kaluta Amri Abeid wa magomeni Mikumi alikuwa waziri wa sheria kabla ya kifo chake!
Pamoja na assertions zako sahihi za awali lakini sasa unajicontradict na unarudia yaleyale niliyo yasema mwanzoni.
Tupende tusipende wewe na mimi katika nji hii mababu zetu tulitawaliwa.
Hakuna maneno makali yanayoweza kubadilisha ukweli huu.
Wakoloni ni wakoloni wawe waarabu wazungu au wachina.
Mwarabu awe wa Oman,Saudia,Muscat au kwingineko, yeye alikuja kufanya biashara tu?
Yeye alikuwa kanyaga twenda ? au ilikuwa bahati mbaya basi akaishia kusettle Pwani ya Afrika Mashariki kwa hiyo hakuwa na mipango yoyote ya kuendeleza watu wake.
Sasa hii kukaa kwao alileta manufaa gani kwa wananchi waliopo na walio wakuta.Kwa vile waarabu walichukua watumwa na kuondoka nao na asiwaendeleze wazalendo waliopo,basi waona ni afadhali sana kuliko mkoloni mzungu aliyeleta elimu ya kumtunumikia yeye katika utawala wake?
Kama ulivosema hapo awali tuchambue mada kwa makini na mimi si msemaji wa wakoloni wa kizungu kama wewe usivyo msemaji wa wakoloni wa kiarabu na kwingineko
Kwa vyovyote vile hii ni topic nzito sana na na usijaribu keweka hisia za ubagazi kwa kwenda off topic.
Sijaongelea hisia za uarabu kama rangi lakini both uarabu na ukoloni wa kizungu ni mifumo iliyoletwa kwetu kututawala,
Sasa tunapolaumu mfumo mmoja wakati mfumo mwingine ulitangulia kufika way back basi hili ndio issue yangu ya kimsingi kuwa tusimlaumu Mwalimu kwa sababu za kipuuzi.

Hilo la kumlaumu Kikwete kwa kuwa ni Mwislamu walifahamu wewe na mimi hakuna mahali nimelitaja.
Mada ya Mohammed Said nimeipinga kwa vile unaweza kuublow wide open kwa mfano mmoja tu wa kihistoria kwa kuchanganya itikadi ya imani na siasa, hilo sidhani kama lina haja ya kulirudia.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom