Ukweli kuhusu siasa za Tanzania ‘we desire genuine results from fake political life’

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
  1. Asilimia kubwa ya watu wanaounda au kujiunga na vyama vya siasa Tanzania, hawafanyi hivyo kwa sababu ya itikadi, falsafa na sera bali ili kutafuta fursa, mengine ni yatokanayo.
  2. Wengi wanaoshabikia chama flani hawashabikii au kukiunga mkono chama husika kwa sababu wanaona chama hicho ni bora; bali kwa sababu kuna chama kingine/vingine wanavyodhani si bora.
  3. Wengi wa wanaohama kwenye vyama vya siasa si kwa sababu ya uzuri au ubaya wa vyama wanavyotoka au wanavyokwenda bali ni kwa sababu;-
    • Fursa walizozifuata kwenye chama A, hawajazipata au kuna uwezekano wa fursa zaidi kwenye chama B,
    • Wanakimbia watu/mtu flani kwenye chama wanachotoka, kwa bahati mbaya wanayemkimbia naye anaweza kuhamia wanakohamia na huko wakakutana tena.
    • Wanafuata mtu, kwa bahati mbaya wanayemfuata anaweza kuwakimbia.kwa bahati mbaya pia anayefuatwa sio kwamba anawapenda au kuwathimini wanaomfuata bali anawalia ‘timing awatumie. Wafuataji wanakuwa hawana uelewa wa wanachokifanya.
  4. Ukiona mtu anapinga jambo ,bila kujali ni hoja gani anatoa; halipingi kwa kuwa ni baya bali kwa kuwa linahatarisha maslahi yake au kundi lake. Kwa mfano, ukiona mtu anapinga dhuluma, hapingi kwa kuwa anachukia dhuluma bali kwa kuwa yeye anadhulumiwa kwa wakati huo.
  5. Ukiona mtu anatetea jambo,bila kujali uzito wa hoja zake; hatetei jambo katika uzuri wake, bali kwa sababu jambo hilo linamnufaisha au kunufaisha kundi lake kwa wakati huo.
  6. Wengi hawako tayari kusema ukweli kwa sababu ni muhimu kusema ukweli, bali kwanza huangalia ukweli huo utamnufaisha nini? Kwa msingi huo, inakuwa ni vigumu kumuamini hata yule asemaye ukweli.
  7. Kila mtu anaamini chanzo cha hali tajwa hapo juu na matatizo mengine yote msingi wake ni wenzake, sio yeye wala yeye hana la kufanya na wakati huo huo anaaimini ipo siku hizo tabia hapo juu zitabadilika bila kutaka kufikiri kivipi.
Ukweli ni kwamba hakuna kitu kitabadilika kama watu hawabadiliki, watu hawawezi kubadilika kama hawajaamua kubadilika, na hawawezi kuamua kubadilika kama kila mtu anaamini hakosei, na hauwezi kujua kama unakosea kama hauko tayari kujua.

Kwa hiyo suala ni kuuvunja huo mzunguko, hata hivyo kazi hiyo si rahisi na ndio maana hadi sasa si tu kwamba mzunguko huo upo bali unakuwa. Ijapokuwa hoja hii imekuwa na itaendelea kuwa ngumu kueleweka; huo unabakia kuwa ukweli ukiwa umeeleweka au bila kueleweka.

Tatizo kubwa linalotukabili watanzania haliko kwenye vitu vya nje bali kwenye vichwa vyetu wenyewe. Kila mtu ana ‘Fake’ huku akishangaa na kulaumu wenzake wanavyo ‘Fake’ huku kwa pamoja tukishangaa matokeo ya ‘Fake political life’ lakini pia tukiamini kuna siku ‘Fake political life’ itatupa ‘genuine results”
 
  1. Asilimia kubwa ya watu wanaounda au kujiunga na vyama vya siasa Tanzania, hawafanyi hivyo kwa sababu ya itikadi, falsafa na sera bali ili kutafuta fursa, mengine ni yatokanayo.
  2. Wengi wanaoshabikia chama flani hawashabikii au kukiunga mkono chama husika kwa sababu wanaona chama hicho ni bora; bali kwa sababu kuna chama kingine/vingine wanavyodhani si bora.
  3. Wengi wa wanaohama kwenye vyama vya siasa si kwa sababu ya uzuri au ubaya wa vyama wanavyotoka au wanavyokwenda bali ni kwa sababu;-
    • Fursa walizozifuata kwenye chama A, hawajazipata au kuna uwezekano wa fursa zaidi kwenye chama B,
    • Wanakimbia watu/mtu flani kwenye chama wanachotoka, kwa bahati mbaya wanayemkimbia naye anaweza kuhamia wanakohamia na huko wakakutana tena.
    • Wanafuata mtu, kwa bahati mbaya wanayemfuata anaweza kuwakimbia.kwa bahati mbaya pia anayefuatwa sio kwamba anawapenda au kuwathimini wanaomfuata bali anawalia ‘timing awatumie. Wafuataji wanakuwa hawana uelewa wa wanachokifanya.
  4. Ukiona mtu anapinga jambo ,bila kujali ni hoja gani anatoa; halipingi kwa kuwa ni baya bali kwa kuwa linahatarisha maslahi yake au kundi lake. Kwa mfano, ukiona mtu anapinga dhuluma, hapingi kwa kuwa anachukia dhuluma bali kwa kuwa yeye anadhulumiwa kwa wakati huo.
  5. Ukiona mtu anatetea jambo,bila kujali uzito wa hoja zake; hatetei jambo katika uzuri wake, bali kwa sababu jambo hilo linamnufaisha au kunufaisha kundi lake kwa wakati huo.
  6. Wengi hawako tayari kusema ukweli kwa sababu ni muhimu kusema ukweli, bali kwanza huangalia ukweli huo utamnufaisha nini? Kwa msingi huo, inakuwa ni vigumu kumuamini hata yule asemaye ukweli.
  7. Kila mtu anaamini chanzo cha hali tajwa hapo juu na matatizo mengine yote msingi wake ni wenzake, sio yeye wala yeye hana la kufanya na wakati huo huo anaaimini ipo siku hizo tabia hapo juu zitabadilika bila kutaka kufikiri kivipi.
Ukweli ni kwamba hakuna kitu kitabadilika kama watu hawabadiliki, watu hawawezi kubadilika kama hawajaamua kubadilika, na hawawezi kuamua kubadilika kama kila mtu anaamini hakosei, na hauwezi kujua kama unakosea kama hauko tayari kujua.

Kwa hiyo suala ni kuuvunja huo mzunguko, hata hivyo kazi hiyo si rahisi na ndio maana hadi sasa si tu kwamba mzunguko huo upo bali unakuwa. Ijapokuwa hoja hii imekuwa na itaendelea kuwa ngumu kueleweka; huo unabakia kuwa ukweli ukiwa umeeleweka au bila kueleweka.

Tatizo kubwa linalotukabili watanzania haliko kwenye vitu vya nje bali kwenye vichwa vyetu wenyewe. Kila mtu ana ‘Fake’ huku akishangaa na kulaumu wenzake wanavyo ‘Fake’ huku kwa pamoja tukishangaa matokeo ya ‘Fake political life’ lakini pia tukiamini kuna siku ‘Fake political life’ itatupa ‘genuine results”
Well articulated piece of writings.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo ni Dunia nzima na siyo Tanzania tu, Mwanasiasa mkweli na aliyewatumikia Wananchi kiukweli Dunia hii alikuwa ni Adolf Hitler peke yake!
 
Hiyo ni Dunia nzima na siyo Tanzania tu, Mwanasiasa mkweli na aliyewatumikia Wananchi kiukweli Dunia hii alikuwa ni Adolf Hitler peke yake!
Sio kweli, usiseme ni dunia nzima, hili ni tatizo la kwetu. Kuna tabia mtu akiwa na tatizo badala ya kujirekebisha anajifariji kwama tuko wengi,au wote tuna tatizo hilo.

Ni sawa na unafeli mtihani, halafu unasema yaani mwaka huu, aaaaaah wote tu ni kama tumefeli, hakuna aliefaulu! wakati umefeli wewe na jamaa zako tu hahahah
 
  • Thanks
Reactions: prs
Sio kweli, usiseme ni dunia nzima, hili ni tatizo la kwetu. Kuna tabia mtu akiwa na tatizo badala ya kujirekebisha anajifariji kwama tuko wengi,au wote tuna tatizo hilo.

Ni sawa na unafeli mtihani, halafu unasema yaani mwaka huu, aaaaaah wote tu ni kama tumefeli, hakuna aliefaulu! wakati umefeli wewe na jamaa zako tu hahahah


Niambie ni wapi ambako Wanasiasa hawako jinsi ulivyoelezea Dunia hii leo hii?
 
Sijui chochote kuhusu Siasa za Mauritius lkn ninachojua kuna apartheid kati ya Wahindi na wenyeji wa Visiwani.
kama ambavyo hujui kuhusu Mauritius, kuna maeneo mengi mengineyo pia ambayo huyajui, ndio maana nakuambia si sahihi ku 'generalize' na kusema dunia nzima ndio ilivyo.
 
  • Thanks
Reactions: prs
kama ambavyo hujui kuhusu Mauritius, kuna maeneo mengi mengineyo pia ambayo huyajui, ndio maana nakuambia si sahihi ku 'generalize' na kusema dunia nzima ndio ilivyo.


Mauritius siyo perfect vinginevyo wasingepractice apartheid, unaweza kuweka nchi hapa ambayo Wanasiasa wake hawafit hizo tabia ulizoziorodhesha, mfumo wa Dunia ulivyo leo hii Wanasiasa wote ni corrupt kwa namna moja au nyingine.
 
Mauritius siyo "perfect" Wanasiasa wote ni "corrupt" kwa namna moja au nyingine.
Mkuu unachanganya mambo kweli kweli, perfection na corruption sio kitu kimoja, na tunachozungumza hapa sio perfection.

Unapozungumzia perfection unazungumza kitu kipya kabisa.
 
Mkuu unachanganya mambo kweli kweli, perfection na corruption sio kitu kimoja, na tunachozungumza hapa sio perfection.

Unapozungumzia perfection unazungumza kitu kipya kabisa.


Kwangu mimi ni sawa tu, lkn nilimaanisha orodha yako, nikiipitia sioni nchi itakayotoboa kwa Dunia ya leo, Wanasiasa wa leo wote hawafit hizo sifa, wanaweza kuzidiana hapa na pale lkn mwisho wa siku wote saws tu.
 
wanaweza kuzidiana hapa na pale lkn mwisho wa siku wote saws tu.
sasa huwezi ukasema wanazidiana hapo hapo ukasema ni sawa tu.

Any way, kwa hiyo unachotaka kusema ni kwamba hakuna kitu cha maana kinachoweza kufanywa na wanasiasa duniani, na kama ndivyo; kwa kuwa wanasiasa ndio viongozi, unasema hakuna kinachoweza kufanywa na viongozi duniani, na kwa kuwa viongozi na zao la jamii, unasema hakuna cha maana ambacho mwanadamu anaweza fanya duniani, na kama ndivyo, unachotaka kusema ni kwamba mwanadamu hafai na hana maana yoyote duniani na kama ndivyo, unataka kusema maisha ya mwanadamu duniani hayana maana? sio?

Sasa huoni mtizamo wako ni tatizo kubwa na unasadifu kile kinachozungumzwa kwenye hitimisho la mada ya msingi?
 
sasa huwezi ukasema wanazidiana hapo hapo ukasema ni sawa tu.

Any way, kwa hiyo unachotaka kusema ni kwamba hakuna kitu cha maana kinachoweza kufanywa na wanasiasa duniani, na kama ndivyo; kwa kuwa wanasiasa ndio viongozi, unasema hakuna kinachoweza kufanywa na viongozi duniani, na kwa kuwa viongozi na zao la jamii, unasema hakuna cha maana ambacho mwanadamu anaweza fanya duniani, na kama ndivyo, unachotaka kusema ni kwamba mwanadamu hafai na hana maana yoyote duniani na kama ndivyo, unataka kusema maisha ya mwanadamu duniani hayana maana? sio?

Sasa huoni mtizamo wako ni tatizo kubwa na unasadifu kile kinachozungumzwa kwenye hitimisho la mada ya msingi?


Sijasema hakuna kitu cha maana kinachoweza kufanywa na Wanasiasa Duniani bali hiyo 1-7 yako inaweza kusemwa kwa Wanasiasa wa nchi yoyote ile leo hii.
 
Hiyo ni Dunia nzima na siyo Tanzania tu, Mwanasiasa mkweli na aliyewatumikia Wananchi kiukweli Dunia hii alikuwa ni Adolf Hitler peke yake!
Azizi Mussa amesema ukweli kabisa. Labda Barbarosa ungetafakati scale ya tatizo nchini kwetu na sehemu nyingine. Kama ilivyo wizi, uchafu, ucha Mungu, Uchapa kazi nk haya mambo yapo duniani kote, lakini kila sehemu ina kiwango chake! Alichosema mwanzisha thread ni kuwa hayo matatizo hapa kwetu yameshamiri sana kufananisha na sehemu nyingine!
 
Sijasema hakuna kitu cha maana kinachoweza kufanywa na Wanasiasa Duniani bali hiyo 1-7 yako inaweza kusemwa kwa Wanasiasa wa nchi yoyote ile leo hii.
Wewe mapendekezo yako ni nini sasa kama iko hivyo unavyosema?
 
Back
Top Bottom