Ukweli kuhusu Dini Ulipo: Je, Tumekubali Imani kwa Kufuata Mapokeo au Uelewa wa Kweli?👇🏻

Ukweli kuhusu Dini Ulipo: Je, Tumekubali Imani kwa Kufuata Mapokeo au Uelewa wa Kweli?👇🏻

Davidmmarista

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2024
Posts
2,766
Reaction score
5,677
Wadau Nina maswali machache hapa ningependa kufahamu:
1. Chanzo cha Dini: Ilianzia Wapi?
Je, dini ziliundwa na Mungu au binadamu? Je, zilitokea lini na kwa nini kila tamaduni ina dini yake? Kabla ya Uyahudi, Ukristo na Uislamu watu waliamini nini?

2. Kabla ya Yesu (na Mitume), Watu Waliamini Nini?
Biblia na Qur’an zimekuja kwa njia ya mitume, lakini kabla ya hao watu waliishi vipi kiimani? Walikuwa na dini? Walimjua Mungu vipi?

3. Sadaka Zinakwenda Kwa Mungu au Kwa Binadamu?
Tunambiwa tukitoa sadaka tumempa Mungu. Lakini pesa hizo zinabaki kanisani au kwa viongozi wa dini. Je, hizo huduma ni Mungu? Sadaka kwa miamala ya simu au benki bado ni tendo la kiroho au limekuwa biashara?

4. Maandiko Yameandikwa na Binadamu Kwa Nini Tuyachukulie Kama Neno la Mungu?
Hakuna kitabu kilicholetwa na Mungu mwenyewe. Vyote vimeandikwa na wanadamu. Je, kwa nini tuyaamini kama Neno la Mungu? Nani alithibitisha Roho Mtakatifu aliwaongoza?

5. Kwa Nini Hofu ya Moto wa Milele Hutumika Kwenye Dini?
Tunaambiwa tukikosea tutachomwa moto. Je, ni nani alishawahi kwenda huko na kurudi kutuambia? Je, hofu ni njia sahihi ya kuendesha imani? Jehanamu ipo wapi? Na mbona dini hutufundisha zaidi hofu badala ya upendo?

6. Mambo Kama Kurusha Mawe Kupiga Shetani Maana Gani Halisi?
Watu hufanya vitendo kama kurusha mawe wakisema wanampiga shetani. Je, haya ni maonyesho ya kiimani au ni ishara ya kupinga uovu? Je, tuna uhakika haya mambo si maigizo ya kiroho?

7. Je, Dini Zinajenga Hofu Badala ya Maarifa?
Wengi hushindwa kuuliza maswali ya msingi kwa hofu ya “kukufuru.” Lakini swali ni hili: Imani inapaswa kujengwa kwa maarifa au kwa hofu?

Kiranga
 
Niulize mimi swali moja baada ya jingine......kwa kifupi dini ya kweli ipo na ina majibu kamili ya hayo maswali yako ...tatizo lililopo ni hizi dini feki za kikristo na kiislamu na nyinginezo....ukijua dini ya kweli hayo maswali yako ni mepesi sana 😁
 
Niulize mimi swali moja baada ya jingine......kwa kifupi dini ya kweli ipo na ina majibu kamili ya hayo maswali yako ...tatizo lililopo ni hizi dini feki za kikristo na kiislamu na nyinginezo....ukijua dini ya kweli hayo maswali yako ni mepesi sana 😁
Dini ya kweli ndio ipi mkuu?
 
Dini ya kweli ndio ipi mkuu?
Kujua mema na mabaya kisha tenda mema na usitende mabaya hii ndiyo dini ya kweli na pure religion....kwa hii hata lile swali la waliokuwa awajafikiwa na hizi dini wataumhukumiwa vipi ? Utapata jibu ndani yake ...maana kujua mema na mabaya kuko moyoni mwa mwanadamu siyo hadi maandiko.
 
Kujua mema na mabaya kisha tenda mema na usitende mabaya hii ndiyo dini ya kweli na pure religion....kwa hii hata lile swali la waliokuwa awajafikiwa na hizi dini wataumhukumiwa vipi ? Utapata jibu ndani yake ...maana kujua mema na mabaya kuko moyoni mwa mwanadamu siyo hadi maandiko.
Yani bro siamini katika dini yeyote Mimi sio mfia dini nnachoamini Mungu yupo na njia ya kumfikia sio dini ni Imani na tabia zako.
 
Niulize mimi swali moja baada ya jingine......kwa kifupi dini ya kweli ipo na ina majibu kamili ya hayo maswali yako ...tatizo lililopo ni hizi dini feki za kikristo na kiislamu na nyinginezo....ukijua dini ya kweli hayo maswali yako ni mepesi sana 😁
Ni kweli ipo. Soma hii
 

Attachments

  • downloadfile-1.png
    downloadfile-1.png
    627.4 KB · Views: 37
Niulize mimi swali moja baada ya jingine......kwa kifupi dini ya kweli ipo na ina majibu kamili ya hayo maswali yako ...tatizo lililopo ni hizi dini feki za kikristo na kiislamu na nyinginezo....ukijua dini ya kweli hayo maswali yako ni mepesi sana 😁
Chanzo cha dini ni siasa na utapeli wa binadamu kuwatawala na kuwaibia wenzake. Vilianzia Ulaya na Mashariki ya Kati kwa dini hizi za kinyonyaji. Kwa dini nyingine, kila sehemu kulikuwa na. dini zilizouawa na hizi dini za kijambazi na kitapeli zilizojimilkisha kila kitu
 
Chanzo cha dini ni siasa na utapeli wa binadamu kuwatawala na kuwaibia wenzake. Vilianzia Ulaya na Mashariki ya Kati kwa dini hizi za kinyonyaji. Kwa dini nyingine, kila sehemu kulikuwa na. dini zilizouawa na hizi dini za kijambazi na kitapeli zilizojimilkisha kila kitu
Kujua mema na mabaya kisha kutenda mema na kuacha mabaya ndiyo wizi 🙄🙄...huo msingi wa dini nilio kueleza unapingana na unacho sema ...kwa sababu ku8bia watu ni kutenda maovu siyo kutenda mema ni kinyume ya dini ya HAKI ....Maana ya neno DINI NI 👉HAKI (ya Mungu).
Neno 👉"mtu wa dini" maana yake ni "mtu wa haki" hivyo ukitaka kujua dini na wati wa dini feki ni rahisi sana kwa sababu watakuwa kunyume na HAKI NA MEMA
 
Ni kweli ipo. Soma hii
Sasa huu upumbavu wa dini ya mudi boy na swahaba wake shetani inanihusu nini
Yani bro siamini katika dini yeyote Mimi sio mfia dini nnachoamini Mungu yupo na njia ya kumfikia sio dini ni Imani na tabia zako.
Sasa umeandika nini ? Kwani kujua mema na mabaya kisha ukatenda mema na kuacha mabaya ni Dini gani ?
 
Kujua mema na mabaya kisha kutenda mema na kuacha mabaya ndiyo wizi 🙄🙄...huo msingi wa dini nilio kueleza unapingana na unacho sema ...kwa sababu ku8bia watu ni kutenda maovu siyo kutenda mema ni kinyume ya dini ya HAKI ....Maana ya neno DINI NI 👉HAKI (ya Mungu).
Neno 👉"mtu wa dini" maana yake ni "mtu wa haki" hivyo ukitaka kujua dini na wati wa dini feki ni rahisi sana kwa sababu watakuwa kunyume na HAKI NA MEMA
Sijui kama unajua usemacho na ujuacho katika hili. Kaa na ujinga wako
 
Sijui kama unajua usemacho na ujuacho katika hili. Kaa na ujinga wako
Una akili finyu sana unatakiwa ukimbie 7kachukue kadi ya ccm samia anatafuta watu wenye akili finyu kama wewe ili aongoze nao
 
Sasa huu upumbavu wa dini ya mudi boy na swahaba wake shetani inanihusu nini

Sasa umeandika nini ? Kwani kujua mema na mabaya kisha ukatenda mema na kuacha mabaya ni Dini gani ?
Sio dini na sio kila mtu atakuwa mfuasi wa dini kwasababu hizi dini ni taasisi za binadamu tangu Dunia kuumbwa hamna dini yeyote ambayo ni default
 
Wadau Nina maswali machache hapa ningependa kufahamu:
1. Chanzo cha Dini: Ilianzia Wapi?
Je, dini ziliundwa na Mungu au binadamu? Je, zilitokea lini na kwa nini kila tamaduni ina dini yake? Kabla ya Uyahudi, Ukristo na Uislamu watu waliamini nini?

2. Kabla ya Yesu (na Mitume), Watu Waliamini Nini?
Biblia na Qur’an zimekuja kwa njia ya mitume, lakini kabla ya hao watu waliishi vipi kiimani? Walikuwa na dini? Walimjua Mungu vipi?

3. Sadaka Zinakwenda Kwa Mungu au Kwa Binadamu?
Tunambiwa tukitoa sadaka tumempa Mungu. Lakini pesa hizo zinabaki kanisani au kwa viongozi wa dini. Je, hizo huduma ni Mungu? Sadaka kwa miamala ya simu au benki bado ni tendo la kiroho au limekuwa biashara?

4. Maandiko Yameandikwa na Binadamu Kwa Nini Tuyachukulie Kama Neno la Mungu?
Hakuna kitabu kilicholetwa na Mungu mwenyewe. Vyote vimeandikwa na wanadamu. Je, kwa nini tuyaamini kama Neno la Mungu? Nani alithibitisha Roho Mtakatifu aliwaongoza?

5. Kwa Nini Hofu ya Moto wa Milele Hutumika Kwenye Dini?
Tunaambiwa tukikosea tutachomwa moto. Je, ni nani alishawahi kwenda huko na kurudi kutuambia? Je, hofu ni njia sahihi ya kuendesha imani? Jehanamu ipo wapi? Na mbona dini hutufundisha zaidi hofu badala ya upendo?

6. Mambo Kama Kurusha Mawe Kupiga Shetani Maana Gani Halisi?
Watu hufanya vitendo kama kurusha mawe wakisema wanampiga shetani. Je, haya ni maonyesho ya kiimani au ni ishara ya kupinga uovu? Je, tuna uhakika haya mambo si maigizo ya kiroho?

7. Je, Dini Zinajenga Hofu Badala ya Maarifa?
Wengi hushindwa kuuliza maswali ya msingi kwa hofu ya “kukufuru.” Lakini swali ni hili: Imani inapaswa kujengwa kwa maarifa au kwa hofu?

Kiranga
Kabla ya mitume na manabii ipo pure dini ...nayo ni kujua mema na mabaya .....kila binadamu moyoni mwake anao 7funua wa kujua mema na mabaya ...ukusoma imeandikwa 👉tazama umejua mema na mabaya katende mema ukitenda mema utapata dhawabu na pepo na ukitenda mabaya utapata dhambi na laana na jehanam
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom