Ukweli kuhusu Benedict Mutungirehi na kundi la G211 pale UDSM mwaka 1994

Ndugu Subirijibu.... Nimesikitishwa sana na ujasiri wa kutetea uwoga wako na utraitor wako... mimi ni miongoni mwa G211 na ni mmoja wa viongozi tuliongoza kundi la G211 NA KUSHINDA KESI DHIDI YA CHUO... Naikumbuka sana historia hii na haitakuja kutoka kichwani pangu.... sina haja ya kurudia historia nzima hila napenda kukufahamisha haya machache kwa faida ya wana Jf na kuweka kumbukumbu sahihi..

Tuna kila sababu ya kuwaita nyinyi matraitor kwa sababu .... sheria za chuo zilieleza wazi kwamba mtihani ukichelewa au mwanachuo akichelewa kufika kwenye chumba cha mtihani kwa zaidi ya dk 30 hataruhusiwa kuingia kwenye chumba cha mtihani na vilevile mtihani ukichelewa kwa dk 30 ... wanafunzi wanaweza kutoka kwenye chumba cha mtihani unless kuna taarifa za kuchelewa kwa mtihani... Tukio lilivyotokea ni kwamba mtihani ulichelewa zaidi ya masaa 2 na bila taarifa YOYOTE.

Muonamambo,
Hapa ndipo hata anayesoma thread hii anapoona mlikosea. Ukiichukulia kama unavyoileta unaweza kudhani ni kweli mtihani ulichelewa na hakukuwa na taarifa yoyote.

Ni kweli mtihani ulichelewa. Lakini je ni kweli hukuwa na taarifa yoyote? Kama hukuwa na taarifa yoyote ulikuwa unafanya nini eneo la FOE tena mmekaa kundi kubwa mnaongelea tukio hilo?

Usidanganye watu hapa. Nimesema na haujakanusha ni kwamba mzozo huo ulianza mwezi April na mliujua. Taarifa mlishaambiwa kwamba Mathematics Department haita-liaise na Engineering first year hadi wa-apology. Hukupata taarifa hii?

OK, siku ya mtihani, tulikusanyika pale nje na tukakubaliana tusiondoke hadi tujue Class Reps wamekubaliana nini na Lecturers. Ulitaka taarifa gani wakati viongozi wako wako mazungumzoni na hujapata feedback.

Halafu unasema kuwa ni u-traitor nione aibu. Nitaonaje aibu kutetea history ambayo mmeipotosha kwa miaka mingi.

Tatizo lenu ni kwamba hata kwenye mikutano hamkutaka wenzenu tutoe hoja mkawa mnatumia ubabe na kuzomea mkipewa vipande.

Unakumbuka bwana mmoja alieleza walimu walivyowakuta darasani mkamzomea na kumuita "WA NDANI WA NDANI WA NJE WA NJE".

Lete hoja tusahishe history.

SOTE tulikubaliana ya kwamba tusiendelee na mtihani hule na kwa vile wengine walikuwa na mitihani inayofuata muda wa mchana... sasa matraitor wachache kama wewe mliendelea kufanya mtihani hata baada ya kuletwa masaa ma 3 baadaye..

Uongo ambao unapimwa kwa kitu kidogo tu. Kama wote tulikubaliana, iweje wale Class reps wakae kule ofisini waki-discuss jambo lile. Unataka kutuambia wakati Sweke, Karungubare na Kitilinga mlishawapindua mkaweka resolution yenu nyingine kabisa.

Na kama mlishakubaliana si mngeondoka mlikuwa mnasubiri nini maeneo yale huku mitihani mingine ikiwasubiri jioni. Uongo mtupu.

Hata baada ya kuendelea na mtihani, tuliokuwa nje tuliwasihi mtoke ili tuwe na msimamo wa pamoja nanyi mliweka masilahi yenu mbele kama mafisadi na kusahau masilahi ya wengi..


Ona unavyojichanganya katika jambo hili. Sasa kama sisi tulikuwa ndani ya exam room na nyinyi mlikuwa nje, mlitusihi kwa mawasiliano gani. Kwamba mlikuwa mnakuja darasani mnatutangazia halafu sisi tunakataa?

Huu ni uongo ambao kila anayejua logistics za mtihani ataung'amua. Ukiingia kwenye exam room mtu wa kwanza kukutana naye ni msimamizi au invigilator. Sasa mliwezaje kumvuka invigilator aache kusimamia exam awape muda mtangaze azama yenu kututaka tuache mtihani kisha akawaruhusu mtoke ili sisi ama tukubali ama tuache.

Ni uogo ambao hauwezekani. Kilichotokea inawezekana kweli mlikuwa mnatuma watu kuja kututoa. Lakin badala yake watu hao wakifika mlangoni wanaona kila mtu amejipinda kwenye pen wanaajiunga pia kuwa na sisi. Na bahati yenu sheria ilikuwa ni nusu saa lakini ingekuwa zaidi basi wengi tu wangechomoka huko kwenu wakaja kufanya paper maana tatizo la wengi walidhani kutokana na mzozo basi Mathematics wametukomoa ili tufeli lakini mtihani ule kumbe ulikuwa rahisi na kila mtu angefaulu.

Napenda kuwapongeza tena wana G211 kwa moyo wa kizalendo na wa kijasiri wa kuungana pamoja dhidi ya udhalimu wa chuo/serikali na kushinda ... nawatakia kila la heri kwenye shughuli zenu na mungu akipenda aweze kutuunganisha tena ili tushinde vita dhidi ya ufisadi kwani naamini bado mnaendeleza mapambano huko mliko

Hapa ndipo mlipopotoka. Nimeeleza kirefu hadi inachosha lakini lengo langu ieleweka kuwa mzozo haukuwa na sura yoyote ya kisiasa au hata kiutawala.

Mbona hata siku moja hamkutaka tuujulishe umma kwamba chanzo cha mzozo ni ile test ngumu ya vector calculus yenye curl na divergence. It was a pure academical matter and never administrative or political.
 
Muonamambo ni kweli ndio maana mlishinda kesi kirahisi.
Halafu pia sijapenda huyu bwana aka traitor anasema wazi majina ya watu huku lake lipo kapuni, mods huyu traitor anastahili ban walau ya siku 3, kwa kuwa bado analeta utraitor.
All in all, well said Muonamambo.

Niliowataja wote walikuwa public figure. Mfano kama ulikuwa kiongozi pale utaachaje kukwepwa kujulikana. Nimemtaja Phenihas Magesa, je hakuwepo kama mshiriki kwenye kesi mliyofungua.

Nimemtaja Hussein Kitilinga, Sweke, na Lugiko Karungubare kama viongozi yaani class representative wakati ule, kuna tatizo gani katika hilo.

Nimemtaja Godwin Ngwilimi ambaye ni mwanasheria sasa pale TANESCO, je hakuwa pale pembeni ya Mutungirehi katika varangati ile.

Ukiwa kiongozi hata ukiranja wa darasa moja huko primary school basi history itaandikwa hivyohivyo na watakaoipenda wataisoma hivyohivyo.

Kwanza mjiulize kwa nini nimeanzisha thread hii. Ni kwa sababu kuna thread nyingine inaelezea kwa juu sana kuhusu hili nikaona tuumwage ukweli kamili. Thread imetaja G211 na Mutungirehi.

Mbona Mutungirehi mmemtaja na nyinyi hamjitaji. Si kwamba mnaonyesha ule ubabe wenu wa FOE ambao nilidhani maisha yameubadilisha kumbe bado mko vilevile.

Tunatakiwa tuweke sawa historia. Binafsi sikupenda lilivyopotoshwa wakati uhalisi ninaujua.

Mbona nyinyi mmetuita TRAITORS kwa miaka. Tunachofanya sasa ni kuonyesha kwamba hakukuwa na kitu kilichosababisha tuitane traitor au shujaa.

Tunapigana kuondoa ufisadi. Hebu waangalie pale Bungeni akina John Mnyika, Zitto, Wenje, Halima Mdee na wenzao. Je wanatumia njia za kibabe? Huwezi kutumia ubabe kwa mtu mwenye dola na silaha zote?

Wanatumia akili zao na kanui hadi Anne Makinda hana hamu nao tena.
 
Kimbunga njoo mjadiliane na Classmates wenzako. Sisi UDSM tulipita enzi za kina Mtatiro na Mwita Mwikwabe. Hatuna cha kuchangia hapa.

Mkuu TUMBIRI jamaa kasema maneno ya kweli kabisa kabisa. Unajua kuna kitu kingine kilikuwa kule FOE, mtihani ukionekana mgumu tu basi linaanzishwa kunji la kufa mtu ili watu wakajiandae upya! Sweke alikuja kuwa presidaa wa Daruso baada ya Lenganasa aliyechikua mikoba ya Mutungihela. Story hiyo imenimumbusha mbali sana; akina Eng. Peter, Malima (huyu kwa sasa anaongoza kitengo kimoja huko serikalini). Mtoa mada safi sana kwa kuweka kumbukumbu sawa.
 
Last edited by a moderator:
SubiriJibu ;Hapa ndipo hata anayesoma thread hii anapoona mlikosea. Ukiichukulia kama unavyoileta unaweza kudhani ni kweli mtihani ulichelewa na hakukuwa na taarifa yoyote. Ni kweli mtihani ulichelewa. Lakini je ni kweli hukuwa na taarifa yoyote? Kama hukuwa na taarifa yoyote ulikuwa unafanya nini eneo la FOE tena mmekaa kundi kubwa mnaongelea tukio hilo? Usidanganye watu hapa. Nimesema na haujakanusha ni kwamba mzozo huo ulianza mwezi April na mliujua. Taarifa mlishaambiwa kwamba Mathematics Department haita-liaise na Engineering first year hadi wa-apology. Hukupata taarifa hii? OK said:
WA NDANI WA NDANI WA NJE WA NJE[/B]".

Lete hoja tusahishe history.



Uongo ambao unapimwa kwa kitu kidogo tu. Kama wote tulikubaliana, iweje wale Class reps wakae kule ofisini waki-discuss jambo lile. Unataka kutuambia wakati Sweke, Karungubare na Kitilinga mlishawapindua mkaweka resolution yenu nyingine kabisa.

Na kama mlishakubaliana si mngeondoka mlikuwa mnasubiri nini maeneo yale huku mitihani mingine ikiwasubiri jioni. Uongo mtupu.




Ona unavyojichanganya katika jambo hili. Sasa kama sisi tulikuwa ndani ya exam room na nyinyi mlikuwa nje, mlitusihi kwa mawasiliano gani. Kwamba mlikuwa mnakuja darasani mnatutangazia halafu sisi tunakataa?

Huu ni uongo ambao kila anayejua logistics za mtihani ataung'amua. Ukiingia kwenye exam room mtu wa kwanza kukutana naye ni msimamizi au invigilator. Sasa mliwezaje kumvuka invigilator aache kusimamia exam awape muda mtangaze azama yenu kututaka tuache mtihani kisha akawaruhusu mtoke ili sisi ama tukubali ama tuache.

Ni uogo ambao hauwezekani. Kilichotokea inawezekana kweli mlikuwa mnatuma watu kuja kututoa. Lakin badala yake watu hao wakifika mlangoni wanaona kila mtu amejipinda kwenye pen wanaajiunga pia kuwa na sisi. Na bahati yenu sheria ilikuwa ni nusu saa lakini ingekuwa zaidi basi wengi tu wangechomoka huko kwenu wakaja kufanya paper maana tatizo la wengi walidhani kutokana na mzozo basi Mathematics wametukomoa ili tufeli lakini mtihani ule kumbe ulikuwa rahisi na kila mtu angefaulu.



Hapa ndipo mlipopotoka. Nimeeleza kirefu hadi inachosha lakini lengo langu ieleweka kuwa mzozo haukuwa na sura yoyote ya kisiasa au hata kiutawala.

Mbona hata siku moja hamkutaka tuujulishe umma kwamba chanzo cha mzozo ni ile test ngumu ya vector calculus yenye curl na divergence. It was a pure academical matter and never administrative or political.
subirijibu:

  1. Acha kupotosha watu sheria za chuo ziko wazi kwamba mtihani ukichelewa zaidi ya dk 30 bila taarifa maalum basi mwanachuo anaruhusiwa kutoka kwenye chumba cha mtihani. mtihani wa engineering mathematics ulichelewa zaidi ya masaa 2 na taarifa pia zilichelewa zaidi ya dk 30....
  2. Kitendo cha watu kubakia FOE hakina uhusiano na taarifa ya mtihani kuchelewa ... ni kweli class reps walikuwa na discusion na uongozi kuhusu kanuni na nini kifanyike baada ya mtihani kuchelewa bila taarifa... uongozi wa chuo uliamua kuficha udhaifu wao na kuamuru mtihani ukafanywe na hata watu wachache waliopo baada ya masaa 3 nje ya muda wa kawaida wa kuanza mtihani... kuwepo kwa wanachuo FOE kuansababu nyingi kwanza ni chuo chao pili bado wengine tulikuwa tunajiandaa na mitihani mingine... sasa ulitaka tukajiandaye wapi?...
  3. habari ya mzozo wa APRIL wewe ndio unaijua na kamwe huwezi kuhihusisha na mtiani wa UE Kwani mtihani unakuja kutokana na syslbus iliyofundishwa .... hivyo ni upotoshaji mkubwa kuhusisha issue ya nyuma na mtihani wa sasa
  4. kama kweli mlikuwa mnathamini walio wengi ambao ni 211 kati yenu 72 .. basi mngetoka nje na kuungana na wenzenu lakini narudia kusema mliweka masilahi yenu mbele na kusahau kuwa mligawanywa ili mtawalike kirahisi na uzembe wa uongoozi wa chuo...
  5. napata mashaka na utetezi wako kwamba kwa nini tuliendelea kukaa FOE nimeshakwambia vilevile hatukuwa na sababu ya kuondoka kwani hapo palikuwa ni chuoni petu, pili watu tulikuwa tuanajiandaa na mtihani mingine...
  6. Suala la class reps kuzungumza na uongozi haliondoi uhalali wa hoja kwamba uongozi ulichemsha na kama sheria inavyosema kwamba mtihani ulitakiwa kuhahirishwa kutokana na kuchelewa bila taarifa yoyote... kama ilivyokuwa kwamba yoyote aliyechelewa kuingia kwenye chumba cha mtihani alikatazwa kufanya hivyo...
  7. mazungumzo ya class reps na uongozi yalikuwa ni ya lazima kwani tatizo lilishatokea na safari hii lilifanya na chuo... hivyo walitaka kujua outcomes yake..lakini haki yetu ilikuwa palepale na ndio maana tukashinda MAHAKAMANI
  8. nakupa tu ushauri wa bure kubali kiiungwana kwamba ulichemsha kwa kuwa traitor na hiyo haikupunguzii mwili wako bali inakuweka katika jamii ya watu wasioaminika kwa manufaa ya wengi...
 
..waliokosea ni viongozi/wawakilishi waliokubali mtihani uanze baada ya kuchelewa masaa 3++.

..pia lazima tukubali kwamba kuna mahusiano mabaya kati ya waalimu na wanafunzi hapo UDSM.

..hali ya kuogopana, kutishana, kuwindana, kupigana, haifai ktk mazingira ya kisomi.

Nakubaliana na wewe mkuu,

Ila kama hukuwepo labda nirudie jambo moja kulieleza. Nimeeleza kwamba unajua hawa mabwana wanaojiita G211 walitaka ionekane kaan kwamba tatizo lilianza siku ileile ya mtihani. Ingekuwa hivyo kusingetokea yale yote kwani sheria ilikuwa ni wazi kabisa kwamba dakika 30 unaweza kuondoka.

Labda nirudie narration kwamba siku hizi nasikia wamenaisha semester system ambapo University Exam unafanya ndani ya semester moja mnamalizana na somo hilo.

Siku zile haikuwa hivyo. Somo kama Engineering Maths au lolote mlikuwa mnalisoma ndani ya terms tatu. Kila term mnasoma kama 10 weeks kisha mnafanya test halafu mnafunga Chuo kwa wiki mbili, first term inaisha. Term ya pili inakuwa hivyohivyo.

Third term ilikuwa tofauti kidogo. Ni kwamba baada ya kufanya test hatukufunga bali tulikuwa tunakaa wiki mbili tunajiandaa kwa General Unversity Examination. Yaani exam inafanywa mara moja tu kwa mwaka kwa somo lolote.

Zile test tatu zilichukuliwa kama coursework for 50% weight.

Tatizo lililojitokeza hapa ni ile third term test ya Mathematics. Ndipo ikawa ngumu na fujo ikafanyika na Maths Dept wakatoa written warning kuwa hawatafundisha au kutoa exams kwa Engineering first year.

Hiyo ni April 1994 wakati University Exam tulitakiwa kufanya May 1994. Hivyo kulikuwa na gap ya more than two weeks mzozo ukijulikana upo.

Halafu hawa wanadanganya umma ili ionekane kana kwamba lilikuwa tatizo la siku ileile ya kufanya mtihani yaani May 1994. Na kwa kweli walifanikiwa sana kupata waumini wengi wa kuamini propoganda yao tena kwa miaka mingi na hadi leo bado hawaoni aibu kujiita mashujaa.

Mimi hata ningekuwa upande wao wa G211 bado ningeona aibu kwa sababu siwezi kuficha ukweli ule miaka mingi ila kuona aibu wakati nikijua kuna wengi tu wanaujua.
 
Mkuu SubiriJibu,

Umenikumbusha miaka ile ya Dhahabu UDSM! Mutungirehi alichaguliwa kwa Kishindo kuwa Rais wa DARUSO late 1993 na kuwa TRAITOR wa Magamba baada ya kupta safari ya Uholanzi au Hungary mwenye kumbukumbu sahihi atasaidia.

Siku ile aliposhushwa High table kuna kijana mmoja alisimama akasema " you were elected democratically ....now you are also rejected democratically " Nakumbuka kijana huyo then aliitwa NIPASHE. Najua Wakuu wengine kama Eliakim Maswi na Sylvester Sweke watakumbuka vema tukio hili. Sijui wamo humu au wanapita hapa?
Mkuu umenikumbusha juu ya NIPASHE. Huyu alikuwa Faculty of Education aliitwa nipashe kwa kuwa alikuwa na masikio makubwa kama kikatuni kimoja cha nipashe kilichokuwa kinatoka kwenye gazeti moja. Nilikutana naye akiwa ni mwalimu tukaliga mvinyo tukikumbuka hiyo hadithi. Sweke nilikutana naye akiwa ni mhandisi kwenye kampuni moja ya ushauri (consultancy). Enzi hizo bwana sijui kama bado zipo; rejected democratically!
 
Niliowataja wote walikuwa public figure. Mfano kama ulikuwa kiongozi pale utaachaje kukwepwa kujulikana. Nimemtaja Phenihas Magesa, je hakuwepo kama mshiriki kwenye kesi mliyofungua.

Nimemtaja Hussein Kitilinga, Sweke, na Lugiko Karungubare kama viongozi yaani class representative wakati ule, kuna tatizo gani katika hilo.

Nimemtaja Godwin Ngwilimi ambaye ni mwanasheria sasa pale TANESCO, je hakuwa pale pembeni ya Mutungirehi katika varangati ile.

Ukiwa kiongozi hata ukiranja wa darasa moja huko primary school basi history itaandikwa hivyohivyo na watakaoipenda wataisoma hivyohivyo.

Kwanza mjiulize kwa nini nimeanzisha thread hii. Ni kwa sababu kuna thread nyingine inaelezea kwa juu sana kuhusu hili nikaona tuumwage ukweli kamili. Thread imetaja G211 na Mutungirehi.

Mbona Mutungirehi mmemtaja na nyinyi hamjitaji. Si kwamba mnaonyesha ule ubabe wenu wa FOE ambao nilidhani maisha yameubadilisha kumbe bado mko vilevile.

Tunatakiwa tuweke sawa historia. Binafsi sikupenda lilivyopotoshwa wakati uhalisi ninaujua.

Mbona nyinyi mmetuita TRAITORS kwa miaka. Tunachofanya sasa ni kuonyesha kwamba hakukuwa na kitu kilichosababisha tuitane traitor au shujaa.

Tunapigana kuondoa ufisadi. Hebu waangalie pale Bungeni akina John Mnyika, Zitto, Wenje, Halima Mdee na wenzao. Je wanatumia njia za kibabe? Huwezi kutumia ubabe kwa mtu mwenye dola na silaha zote?

Wanatumia akili zao na kanui hadi Anne Makinda hana hamu nao tena.

SubiriJibu,

..tatizo hapo ni watu wazima kama Prof.Masenge kushindwa kutumia busara.

..mkutano wa wahadhiri na wawakilishi wa wanafunzi ulipaswa kupanga tarehe mpya ya mtihani.

..mimi nadhani muweke pembeni hii habari ya "traitors" na "G211" halafu mjiulize kama wahadhiri really acted like guardians and grown ups ktk kulazimisha mtihani ufanyike ukiwa umechelewa 3++ hrs.

..hapo inaonesha kabisa kwamba wahadhiri walikuwa na nia mbaya kwa kutaka kuwakosesha baadhi ya wanafunzi nafasi ya kufanya mtihani.

..UDSM wanakuja wanafunzi toka background mbalimbali na mashinikizo kibao ktk maisha yao. sasa wahadhiri na watawala wanatumia hali ya wanafunzi kuwalazimisha kutimiza matakwa yao.
 
Nakubaliana na wewe mkuu,

Ila kama hukuwepo labda nirudie jambo moja kulieleza. Nimeeleza kwamba unajua hawa mabwana wanaojiita G211 walitaka ionekane kaan kwamba tatizo lilianza siku ileile ya mtihani. Ingekuwa hivyo kusingetokea yale yote kwani sheria ilikuwa ni wazi kabisa kwamba dakika 30 unaweza kuondoka.

Labda nirudie narration kwamba siku hizi nasikia wamenaisha semester system ambapo University Exam unafanya ndani ya semester moja mnamalizana na somo hilo.

Siku zile haikuwa hivyo. Somo kama Engineering Maths au lolote mlikuwa mnalisoma ndani ya terms tatu. Kila term mnasoma kama 10 weeks kisha mnafanya test halafu mnafunga Chuo kwa wiki mbili, first term inaisha. Term ya pili inakuwa hivyohivyo.

Third term ilikuwa tofauti kidogo. Ni kwamba baada ya kufanya test hatukufunga bali tulikuwa tunakaa wiki mbili tunajiandaa kwa General Unversity Examination. Yaani exam inafanywa mara moja tu kwa mwaka kwa somo lolote.

Zile test tatu zilichukuliwa kama coursework for 50% weight.

Tatizo lililojitokez hapa ni ile third term test ya Mathematics. Ndipo ikawa ngumu na fujo ikafanyika na Maths Dept wakatoa written warning kuwa hawatafundisha au kutoa exams kwa Engineering first year.

Hiyo ni April 1994 wakati University Exam tulitakiwa kufanya May 1994. Hivyo kulikuwa na gap ya more than two weeks mzozo ukijulikana upo.

Halagu hawa wanadanganya umma ili ionekane kana kwamba lilikuwa tatizo la siku ileile ya kufanya mtihani. Na kwa kweli walifanikiwa sana kupata waumini wengi wa kuamini propoganda yao tena kwa miaka mingi hadileo bado hawaoni aibu kujiita mashujaa.

Mimi hata ningekuwa upande wao wa G211 bado ningeona aibu maana siwezi kuficha ukweli huo miaka mingi ila kuona aibu wakati nikijua kuna wengi tu wanaujua.


SubiriJibu,

..I hear u loud and clear.

..naona matatizo kila mahali kuanzia na huo mtihani ambao hakuna mwanafunzi alikuwa na uwezo wa kuufanya.

..mtihani ungekuwa umetungwa na mhadhiri tofauti na yule aliyefundisha basi hali iliyotokea ingeeleweka.

..kama umesoma nje ya Tanzania ktk level ya chuo kikuu, utakuwa shahidi kwamba hakuna mambo kama hayo ktk nchi za wenzetu.

..kwenye nchi za wenzetu lecturers r FIRM but FAIR. unakuta mhadhiri anatunga mtihani ambao unaweza kuchekecha A students, B students, etc etc.
 
Mimi nilikuwa g211, nilikuwa ndani lakini kwa kuona uchungu wa wenzangu nikatoka nje, nikawasihi wengine watoke mmmh!
 
Tatizo lilikuwa ni kukosa ujasiri na woga, wangetoka darasani wote tatizo lisingekuwepo, kosa lilkuwa la math dept!
 
Mkubwa Muonamambo,

Kwanza habari ya miaka mingi, maana controversty ya thread isitufanye tukasahau kwamba sisi ni classmates. Naamini uliko maisha yanaenda na mimi nasukuma gurudumu la maisha.

Kuna mmoja kwenye ile thread amesema waliomvua tai Mutungirehi weng sasa ni senior engineers. Ni kweli mimi ni Senior Engineer mahala fulani japo wengine nasikia mlishabadili fani.

Tuje kwenye last post yako. Kadiri post zinavyotiririka kuna kila dalili za kukubaliana na nilichosema na kilichofichwa kwa miaka mingi. Naanza kujibu point moja hadi nyingine kama ifuatavyo:

Kitendo cha watu kubakia FOE hakina uhusiano na taarifa ya mtihani kuchelewa ... ni kweli class reps walikuwa na discusion na uongozi kuhusu kanuni na nini kifanyike baada ya mtihani kuchelewa bila taarifa... uongozi wa chuo uliamua kuficha udhaifu wao na kuamuru mtihani ukafanywe na hata watu wachache waliopo baada ya masaa 3 nje ya muda wa kawaida wa kuanza mtihani... kuwepo kwa wanachuo FOE kuna sababu nyingi kwanza ni chuo chao pili bado wengine tulikuwa tunajiandaa na mitihani mingine... sasa ulitaka tukajiandaye wapi?...

Nashukuru kukubali kwamba class rep walikuwa wanajadili hilo. Hivyo sijakanushwa nimethibitisha ninasema ukweli. Lakini class reps outcome ndiyo ilikuwa resolution yetu hata kama tatizo lisingeanzia April. Kama ni kweli baadhi mlikuwa na msimamo bila kujali matokeo ya majadiliano ya class reps na Chuo, basi ni wazi tayari huo ni mgawanyiko tosha kwamba humuhumo mliojiita G211 mliona umuhimu ni sovereignity yenu na wengine walsha-surrender sovereignity kwa class reps.

Unasema kuwa mlibaki FOE kujiandaa na mitihani mingine. Huu ni uongo mkubwa unaoweza kusadikiwa na asiyejua mazingira ya pale siku ile.

Kumbuka kwamba University Exam ilikuwa inafanyika kipindi kimoja kwa Chuo kizima. Madarasa yalikuwa hayatoshi kiasi kwamba tuliowatania kwa jina la Mangwini walikuwa inawabidi kuja kufanyia exams kule kwetu FOE.

Hivyo hakukuwa na darasa lililokuwa wazi zaidi ya yale ambayo tulikuwa tufanyie exam na ambayo nyinyi na hata mimi mwanzoni tulishatoka.

Kwa ujumla mlikuwa revolution Square ndogo ya kule FOE nikiruhusiwa kuiita hivyo. Yaani kilie kilichozoeleka kufanyika kule Revolution Square pale Cafeteria ndicho kilikuwa kinaendelea.

Hakukuwa na mjadala wa masomo kujadili next subjects wakati hakuna aliyekuwa anajua whata next hasa kwa waliokuwa nje kama mimi na wewe.

Wale waliobaki ndani ndiyo ninasema wangeweza kusema walikwua wana-study for next exam.

Lakini nikukumbushe tena ni kwamba hakukuwa na makubaliano kuwa tutoke chumba cha mtihani kama mtihani utachelewa. Ndiyo maana wengine walibaki hadi Prof. Masenge alipowakuta.


habari ya mzozo wa APRIL wewe ndio unaijua na kamwe huwezi kuhihusisha na mtiani wa UE Kwani mtihani unakuja kutokana na syslbus iliyofundishwa .... hivyo ni upotoshaji mkubwa kuhusisha issue ya nyuma na mtihani wa sasa


Kwa hiyo mnataka watu waamini ilikuwa ni suala la uchelewshaji wa siku ile!! Ndiyo maana ninasema ile INTIMIDATION yenu ilifanikiwa sana watu wawe na woga wa kusimulia chanzo halisi cha suala lile. Nimesema baada ya vurugu ile Mathematics Department ikaandika kwa management ya FOE kwamba haitafundisha au kutoa Exam hadi students tu-apologise kwa kitendo cha kumfanyia fujo yule Mwalimu.

Kama hulijui hili basi pole sana labda ulikaa chumba kingine alichosimamia tutorial assistant mwingine.


kama kweli mlikuwa mnathamini walio wengi ambao ni 211 kati yenu 72 .. basi mngetoka nje na kuungana na wenzenu lakini narudia kusema mliweka masilahi yenu mbele na kusahau kuwa mligawanywa ili mtawalike kirahisi na uzembe wa uongoozi wa chuo

Kwanza hata kabla haijatangazwa hakuna aliyejua nyinyi wangapi na sisi tulikuwa wangapi. Wote tulishtukia list kwenye notice board na idadi magazetini.

Hakuna aliyekuwa na muda kujua wengi wako wapi na hii inaweza kuwa ilipelekea hilo. Kwa nini nasema hivi? In fact mtihani tulikuwa tunagawanywa kwenye vyumba zaidi hata ya vinane na kila chumba kikiwa na watu labda 30, 20 au 40.

Hivyo mtu ulikuwa ukienda unaangalia chumba chako tu na ikibidi hujui mwingine chumba chake ni kipi maana hakuna aliyejitayarisha kujua list ya vyumba vyote kwa kujiandaa na hilo.

Hivyo, iwapo ulisikia kwamba kuna watu wanafanya paper basi ulikimbilia kwenye chumba chako kuhakikisha. Na kibaya kwa mgawanyo wa vyumba hasa vile vya wazi ilionekana kabisa wanaofanya ni wengi.

Kibaya kingine ni kwamba class reps walipita kwanza vyumbani na kuona watu wanafanya paper. Waliomo ndani wakaona wazi kuwa Prof. Masenge kaleta mitihani mbele ya class reps. Sasa hapa utakataaje kufanya wakati kuna baraka zote za viongozi wako yaani wawakilishi wako katik hali ambayo hamkuwa na makubaliano yoyote ya kuukataa mtihani ukiletwa.

nakupa tu ushauri wa bure kubali kiiungwana kwamba ulichemsha kwa kuwa traitor na hiyo haikupunguzii mwili wako bali inakuweka katika jamii ya watu wasioaminika kwa manufaa ya wengi

Ona mpaka leo mko vilevile na ubabe wenu, tena uko mmoja na hunijui ID yangu na mimi sikujui ni nani naongea naye. Hebu angalia tungekuwa tuko Chuoni na wenzako wengi ingekuwaje. Lete ushawishi tuweke history sawa.


Kuhusu kushinda kesi yenu mahakamani ni kwamba mlijikita na matukio ya siku ya mtihani na lile la ugomvi wa nyuma halikuwahusu.

Ni kweli kuna ukweli kidogo hapa. Si wote waliomvamia yule lecturer baada ya ile test ngumu. Ungeniambia uzembe wa chuo kutowa-identify waliomfanyia vurugu lecture nimgekusikiliza kidogo.

Mbona sasa hamkutumia mahakama hiyohiyo kufungua kesi mlipojikita kwa wingi kumtimua benedict Mutungirehi kwa kumvuta tai na kumwangusha kana kwamba Nkrumah Hall imegeuka uwanja wa masumbwi, kisha asilimia kubwa ya G211 mkasimamishwa kwa mwaka mzima!!!
 
Umenikumbusha mbali sana!!
FoE was a place to be!! Traitors hawakupewa nafasi... na kweli Ma traitor mlikoma!!!
 
Mjadala huu na ule wa Mtungirehi umanifaidisha sana japo enzi hizo nilikuwa shule ya msingi Kimbunga nilikuwa namuhisi kama age mate wangu lakini kumbe.........
 
Last edited by a moderator:
SubiriJibu,

..tatizo hapo ni watu wazima kama Prof.Masenge kushindwa kutumia busara.

..mkutano wa wahadhiri na wawakilishi wa wanafunzi ulipaswa kupanga tarehe mpya ya mtihani.

..mimi nadhani muweke pembeni hii habari ya "traitors" na "G211" halafu mjiulize kama wahadhiri really acted like guardians and grown ups ktk kulazimisha mtihani ufanyike ukiwa umechelewa 3++ hrs.

..hapo inaonesha kabisa kwamba wahadhiri walikuwa na nia mbaya kwa kutaka kuwakosesha baadhi ya wanafunzi nafasi ya kufanya mtihani.

..UDSM wanakuja wanafunzi toka background mbalimbali na mashinikizo kibao ktk maisha yao. sasa wahadhiri na watawala wanatumia hali ya wanafunzi kuwalazimisha kutimiza matakwa yao.

Mkuu, heshima yako mbele.

Mkuu kuna jambo moja wanalopotosha hawa wenzetu. Nijichukulie mimi kwa mfano. Ukisoma nilichoeleza movement zangu zinaonyesha kwamba kwanza nilikaa darasani kisha nikatoka nje ili kujua wengine wote wameamua nini.

Hata katika hili hakuna aliyekuja kutu-organise tutoke nje kisha tufanye nini. Ulikuwa uamuzi binafsi.

Hebu angalia sababu zao hata leo wanavyosema. Wanasema 30 minutes zinakupa haki ya kutoka nje ya mtihani na kwenda kwenye shughuli zako.

Ni kweli kwamba wengine wana speed kiasi kwamba ikifika 30 minutes wanatoka na wanaenda kwenye Hall of residence au Library.

Je, tujiulize iweje tabia ibadilike siku ileile tu kwamba kwa nini tusiondoke wote baada ya kukosekana mtihani.

OK,

Tuone sasa rection baada ya kujua kwamba mtihani umeanza. Hapa ndipo vurugu kubwa zilianza.

Wazo la kwanza ilikuwa JE WENZETU WALIOONDOKA ITAKUWAJE?

Hivyo, concern ya kwanza kabisa haikuwa TUSIFANYE PAPER KWA SABABU IMECHELEWA. Cincern ilikuwa ni wale walioondoka watakuwa wame-DISCO.

Kwa ujumla hii concern ndiyo iliyonifanya nianze kufikiri kurudi kwenye mtihani. Kwamba iweje tuwahurumie watu ambao kwanza tuliwasihi wasiondoke hadi tufikie muafaka watakaotulelea viongozi wetu, lakini wao kwa ujeuri wakaondoka na kauli kwamba LIWALO NA LIWE MTIHANI UKIJA MTACHAGUA KUFANYA AU KUACHA.

Kumbe hata hawa walioondoka, walijua kuwa inawezekana paper ikaja na kukawa na option ya kufanya.

Kingie ni kwamba G211 walichelewa sana option ya kuwatoa wengine darasani. Nimesema mimi nilikaa hadi dakika 2O nje, nikatoa option hiyo wakanipuuza wakaendelea kubwabwaja pale nje hakuna resolution yoyote.

Nikaona upuuzi nikaingia kwenye mtihani. Ona sasa delay yao. Nimeingia nikafanya hadi maswali matatu yaani kama dakika 40 hivi ndipo wakaja wamegawana makundi kuingia vyumbani kuwanyang'anya watu mitihani.

Sasa kama walikuwa na haki ambayo waliishinda kweli mahakamani ni haki gani iliwaambia kwamba waje watutimue kwenye exam rooms na kuchanchana mtihiani yetu.

Ona hata baada ya kututoa kwenye exam rooms unajua ilikuwa vigumu kumu-identify ni nani TRAITOR na nani G211. Kwa sababu hakukuwa na block moja iliyokaa na kujitambua kwamba hawa walikubali resolution na wale walikataa.

Identification ilikuja kujulikana rasmi baada ya kutangazwa magazetini na kwenye notice board. Tena kuna wawili watatu hawakujulikana kama walifanya wakakumbwa na dhoruba wakawa ndani ya G211.

Binafsi siwezi kuacha kutupa lawama kwa wale walioondoka wakisema LIWALO NA LIWE MTIHANI UKIJA TUJICHAGULIE UAMUZI.

Maana hawa ndiyo ilikuwa concern ya kwanza. Vilivyobaki vyote vilikuwa ni visingizio ambayo ni rahisi kumshawishi ambaye hakuwepo kwenye tukio.
 
Umenikumbusha mbali sana!!
FoE was a place to be!! Traitors hawakupewa nafasi... na kweli Ma traitor mlikoma!!!

Mkuu,

Umenisaidia kusema point moja. Ndiyo maana zile barua tulizopewa kusema kama tulikuwa INTIMIDATED tutaje watu mimi sikusita hata chembe.

haya ninayoyaeleza humu niliandika vilevile. Mmekataza humu kutaja watu. Na kweli humu nimetaja pubclic figure of that time and place. lakini kwenye barua ile nilitaja list ya wengi tu, kwa sababu sina huruma na mtu muonevu na hasa anayenionea bila sababu ya msigi eti tu kwa sababu wako genge la wengi.

Unasema tulikoma. Lakini hukusema kwa muda gani. Mliposimamiswa nyinyi G211 mkaenda mahakamani sisi tukafunga chuo tukaenda Practical training (PT), nyinyi mkasota na kesi iliyodumu hadi late Sepetember yaani miezi zaidi ya mitatu.

Hivyo hapo sisi hatukukomeshwa nyinyi ndiyo mlisota na ikabidi mkae D'Salaam kipindi chote wakati Chuo kimefungwa na tuko PT na kisha likizo nyumbani.

Mliporudi yaani early October kweli mkatutishatisha sana kwa intimidations nyingi. Mkakosea mkatumika na watani zenu mangwini kumtimua Benedict Mutungirehi. Mkatumika kama wasukuma wa kanda ya ziwa kwa wingi wao wanavyotumika kuipa CCM kura halafu sasa wanapandishiwa bei ya pamba.

Mkafanikiwa kumvuruga Mutungirehi yaani late October. Lakini Early November 1994 tukarudishwa nyumbani na sisi baada ya mwezi tukaitwa nyinyi mkasota home mwaka mzima kama adhabu.

Tulivyorudi G211 walichoma moto T-Shirt zao hawakutaka tena lisikike tena neno hilo. Neno TRAITOR likafa kama kifo cha mende.

Wanaosoma thread hii wanaujua ukweli huu wote na hawanijui lakini wakiniona watashangaa kama kweli ningeweza kusema haya.

Ni kweli sitaji majina zaidi maana wapo G211 wengine sasa ni wakuu wa TAKUKURU tena kama watatu ninaowafahamu. Mmoja ni yule ambaye aliwahi kugombana na Polisi alipowaambia kuwa Polisi ndiyo wanaongoza kwa kuomba rushwa na hivyo mapambani ya rushwa yanakuwa magumu.

Ilimpa tatizo kauli hii.
 
Mkuu,

Umenisaidia kusema point moja. Ndiyo maana zile barua tulizopewa kusema kama tulikuwa INTIMIDATED tutaje watu mimi sikusita hata chembe.

haya ninayoyaeleza humu niliandika vilevile. Mmekataza humu kutaja watu. Na kweli humu nimetaja pubclic figure of that time and place. lakini kwenye barua ile nilitaja list ya wengi tu, kwa sababu sina huruma na mtu muonevu na hasa anayenionea bila sababu ya msigi eti tu kwa sababu wako genge la wengi.

Unasema tulikoma. Lakini hukusema kwa muda gani. Mliposimamiswa nyinyi G211 mkaenda mahakamani sisi tukafunga chuo tukaenda Practical training (PT), nyinyi mkasota na kesi iliyodumu hadi late Sepetember yaani miezi zaidi ya mitatu.

Hivyo hapo sisi hatukukomeshwa nyinyi ndiyo mlisota na ikabidi mkae D'Salaam kipindi chote wakati Chuo kimefungwa na tuko PT na kisha likizo nyumbani.

Mliporudi yaani early October kweli mkatutishatisha sana kwa intimidations nyingi. Mkakosea mkatumika na watani zenu mangwini kumtimua Benedict Mutungirehi. Mkatumika kama wasukuma wa kanda ya ziwa kwa wingi wao wanavyotumika kuipa CCM kura halafu sasa wanapandishiwa bei ya pamba.

Mkafanikiwa kumvuruga Mutungirehi yaani late October. Lakini Early November 1994 tukarudishwa nyumbani na sisi baada ya mwezi tukaitwa nyinyi mkasota home mwaka mzima kama adhabu.

Tulivyorudi G211 walichoma moto T-Shirt zao hawakutaka tena lisikike tena neno hilo. Neno TRAITOR likafa kama kifo cha mende.

Wanaosoma thread hii wanaujua ukweli huu wote na hawanijui lakini wakiniona watashangaa kama kweli ningeweza kusema haya.

Ni kweli sitaji majina zaidi maana wapo G211 wengine sasa ni wakuu wa TAKUKURU tena kama watatu ninaowafahamu. Mmoja ni yule ambaye aliwahi kugombana na Polisi alipowaambia kuwa Polisi ndiyo wanaongoza kwa kuomba rushwa na hivyo mapambani ya rushwa yanakuwa magumu.

Ilimpa tatizo kauli hii.

Tatizo ni kuwa wewe maisha yako yote hii label ya UTRAITOR haitokutoka, ndio maana mpaka leo bado inakuandama!
 
Tatizo ni kuwa wewe maisha yako yote hii label ya UTRAITOR haitokutoka, ndio maana mpaka leo bado inakuandama!


Nyinyi ma-engineer wenzangu ndiyo ile character yenu bado mnayo hata kimaisha ya leo. Wenzenu kama Zitto, Tundu Lissu. Slaa, Halima Mdee, Wenje wanajua kujenga hoja kiasi kwamba usipokubaliana nao tuna haki ya kukuita TRAITOR.

Nyinyi hilo mmegoma kabisa kujifunza.

Mmegoma hata kufungua dictionary ili kujua ina-define vipi neno TRAITOR. Na kama English bado ni ngumu kwenu hadi leo basi angalieni kamusi inasemaje kuhus neno MSALITI.

Nyinyi kwenu jambo mnalolitaka kwa musuli kama wabeba vyuma mnataka kila mmoja alifuate. Akilikataa mnamwita TRAITOR.

Basi walau hata hayo mambo yawepo. Hili la G211 na la Mutungirehi halikuwahi kufika katika level ya unanimous decision bado mnaliita ni u-TRAITOR hadi leo.

Jengeni hoja na maamuzi yawe ya vikundi mtakubaliwa kama yana ushawishi.

Ugonjwa huu sitanii unawakumba sana maengineer wenzangu. Maofisini wakitaka jambo lao wanataka kama vile unamwita mkeo bila kujenga hoja yenye ushawishi. Msiwashangae walianza hivyohivyo tangu tukiwa chuoni.

Badala ya kujichanganya na wenzao kuongeza communication skills wao wanawaita wenzao MANGWINI.

Ona hata hapa sioni ushawishi wowote. Kubalini udhaifu. Mimi niliukubali udhaifu huo nikajizoeza sasa hivi najenga hoja vizuri tu. Si unaona mwenyew thread hii.
 
Ndugu yangu subirijibu heshima Kwako ....

Kwanza napenda kukushauri Kuwa kukubali kosa nao ni uungwana
  • Fact ni kwamba mtihani ulicheleweshwa zaidi ya Masaa 3 bila taarifa
  • fact ni kwamba math dept na uongozi wa chuo walichemsha kulazimisha mtihani ufanyike licha ya kuchelewesha
  • fact ni kwamba ilikuwa ni haki ya g211 pamoja na wewe kususia mtihani baada ya mtihani kuchelewa
  • fact ni kwamba kwa kukubali kufanya mtihani ulionyesha woga wa kupita kiasi na usaliti kwa wenzako walitaka haki itendeke. Kama mwanafunzi anaadhibiwa kwa kuchelewa Dk 30 na mtihani ukichelewa je nani aadhibiwe



  • Samahani natumia simu hivyo Siwezi kuandika zaidi. Pole kwa Dow la Kuwa traitor.
 
Subirijibu acha ku expose Uoga wako. Hivi hata mkeo akisoma hapa si atakudharau sana. FOE SPIRIT Forever
 
act ni kwamba math dept na uongozi wa chuo walichemsha kulazimisha mtihani ufanyike licha ya kuchelewesha

Kama walilazimisha, walikuwa na uwezo gani kuilazimisha management ya FOE na management ya wanafunzi. Hii kulazimisha ni hypothesis yako
Hukuwepo kwenye yale mazungumzo na class reps kwa hiyo huwezi kusema walilazimisha kana kwamba hakukuwa na demands toka pande zote.

fact ni kwamba ilikuwa ni haki ya G211 pamoja na wewe kususia mtihani baada ya mtihani kuchelewa
Sheria iliyotulinda ni kwamba mtihani ukianza ndipo sheria ya dakika 30 inatumika. Kabla ya kuanza hakukuwa na na sheria iliyosema tuitumie iwe kama haki yetu tutokomee. Ndiyo maana na wewe hukutokomea ulibaki unasubiri kwa hamu majibu ya class reps watakachokubaliana na akina Prof. Masenge wa Maths na Dean of Engineering.


fact ni kwamba kwa kukubali kufanya mtihani ulionyesha woga wa kupita kiasi na usaliti kwa wenzako walitaka haki itendeke

Hadi dakika tunafanya mtihani hakukuwa na madai ya aina yoyote ktuoka kwangu wala kwako. Na kama ni madai ya siku hiyo basi haki yetu ilikuwa ni mtihani na tungedai kwa nini hatuletewei mtihani wakati tumeshajiandaa. Hivyo hamkuwahi kuwa na madai ya kutofanyika mtihani.

Nitaongea sana kwa sababu hili mlilipotosha sana

Kama mwanafunzi anaadhibiwa kwa kuchelewa Dk 30 na mtihani ukichelewa je nani aadhibiwe

Narudia kama nilivyosema hapo juu. Ndiyo maana tulikaa kusubiri itokee nini. Kumbe unajua kuw amaswali kama hayo lazima yalete ambiguity na lazima tuwe na resolution kwa sababu hayakuwa define.

Ndiyo maana hata reslotuion mliyochukua bado ilikuwa ya kitoto. Kama kosa lilikuwa ni Maths Dept mbona hamkuli-address moja kwa moja kwa kumzuia Masenge asiendelee kusimamia mitihani badala yake mkadhani solution ni sisi wote tuonekane kama hatukufanya paper kwa kuzichana.

Kuna tofauti gani kama mlikuwa na haki mtihani uendelee na nyinyi mkaitafuta haki yenu mahakamani kwa sababu hizihzi mnazozisema humu.
 
Back
Top Bottom