Freed Freed
JF-Expert Member
- Jun 27, 2017
- 6,198
- 6,416
Habari wadau wa JF siasa.
Kumekuwa na vuguvugu la muda mrefu wilayani Kiteto mkoa wa Manyara kuwa Mbunge wao sio raia wa nchi hii na ana asili kutoka Rwanda.
Vuguvugu hili lilibuka tangu siku nyingi Mbunge huyu akiwa kada mtiifu wa CCM akihangaikia ubunge huku akiwa AFISA KILIMO wa kata moja wilayani kiteto.
Kifupi Mheshimiwa Emmanuel Papian ni mtu wa watu mwenye kupenda watu na hujichanganya sana. Yeye anadai ni mwenyeji wa Kagera kutoka ktk jamii ya wasubi na alikuja kiteto akiwa kijana mdogo akiwa mtumishi wa Umma. Baada ya kuwa na nyota ya kupendwa tena mbali na asili yake ya huko Magharibi mwa nchi alijitosa ktk siasa za kiteto na anaipenda kiteto kuliko chochote.
Wenye chuki naye wanadai sio raia bali alitokana na kambi za wakimbizi huko kagera akiwa miongoni mwa walionufaika na huruma ya Mwl Nyerere ya kuwasaidia na kuwapa uraia watu wa nchi jirani wataabikao na misukosuko ya kisiasa huko kwao.
Hivyo wenye chuki na Mheshimiwa Papian, Mbunge wa Kiteto CCM, wapuuzwe .
Kumekuwa na vuguvugu la muda mrefu wilayani Kiteto mkoa wa Manyara kuwa Mbunge wao sio raia wa nchi hii na ana asili kutoka Rwanda.
Vuguvugu hili lilibuka tangu siku nyingi Mbunge huyu akiwa kada mtiifu wa CCM akihangaikia ubunge huku akiwa AFISA KILIMO wa kata moja wilayani kiteto.
Kifupi Mheshimiwa Emmanuel Papian ni mtu wa watu mwenye kupenda watu na hujichanganya sana. Yeye anadai ni mwenyeji wa Kagera kutoka ktk jamii ya wasubi na alikuja kiteto akiwa kijana mdogo akiwa mtumishi wa Umma. Baada ya kuwa na nyota ya kupendwa tena mbali na asili yake ya huko Magharibi mwa nchi alijitosa ktk siasa za kiteto na anaipenda kiteto kuliko chochote.
Wenye chuki naye wanadai sio raia bali alitokana na kambi za wakimbizi huko kagera akiwa miongoni mwa walionufaika na huruma ya Mwl Nyerere ya kuwasaidia na kuwapa uraia watu wa nchi jirani wataabikao na misukosuko ya kisiasa huko kwao.
Hivyo wenye chuki na Mheshimiwa Papian, Mbunge wa Kiteto CCM, wapuuzwe .