Ukweli haupingiki; Wazanzibar tunadhulumiwa na TANESCO kwa kuwekewa makato ya ziada kwenye umeme

aleesha

JF-Expert Member
Oct 17, 2016
775
1,117
Hatimae Waziri wa nishati na Bunge limekubaliana na ukweli juu ya jinsi Wazanzibar tunavyodhulumiwa kuwekewa makato ya ziada kwenye Umeme.

Makato hayo Ni:
3% Umeme vijijini (REA)
2% Energy and Water Regulatory Authority. (EWURA)
Pia kuuziwa kwa bei ya retail price(rejareja) shirika la Zecco Kama anavyonunua Mtu binafsi.

Jana niliweka ujumbe hapa kuhusu hili jambo na jioni walikubaliana na hoja za wabunge wetu na hatimae wamekubali mpaka tarehe 25/6 hili Jambo litakuwa limepatiwa majibu.

Shukran za dhati kwa Spika Ndugai kulipa uzito Jambo hili na kukubali kwamba hii sasa linakuwa ni Jambo la Bunge zima na ukitaka serikali kulimaliza kwa muda uliowekwa.

Pia nimshukuru MH Najma Giga mbunge pekee kutoka CCM Zanzibar kuungana na wabunge wetu makini kutoka CUF kusimamia Hoja hii pamoja huku akiwaacha wabunge wengine wa ccm kama vile jambo hili haliwahusu.

Hakika utumwa wote ni mbaya lakini utumwa wa kutawaliwa kifkra ni mwisho wa uovu. Hata jambo hili wabunge wa Zanzibar walisubiri amri ya Balozi mkaazi?

Wabunge wetu pamoja na kutoitambua serikali iliopo Zanzibar lakini kwa kujali wananchi wanyonge wameamua bila kujali kuwa maslah yakipatikana Zanzibar yatapitia mikononi mwa haohao. Hapa lengo Ni unafuu kwa wananchi wetu.

Inaumiza sana tukiwa hapa bungeni unamsikia waziri wa madini wa Tanganyika akisisitiza wananchi wa Tanganyika waungiwe Umeme kwa sh 27,000/-tu. Wenzetu wana Dhahabu, gesi, almasi, na mali tele kwa tele lakini bado serikali yao inawapa unafuu huo huku kodi ya REA na EWURA wakibebeshwa wanyonge wa Zanzibar ambao vijiji vyao havijawahi kunufaika na msaada wa REA.

Tujiulize huko Zanzibar ni kiasi gani mnyonge wa Mungu inabidi apapatue kuunganishiwa Umeme? Nasikia kima cha chini Ni 18000/

Kweli tuna serikali inayowajali watu wake?
Kweli tuna wawakilishi wanaojali matatizo ya watu wetu?
Hakika inauma wachaguliwa na wananchi waliopo bungeni wanaposhindwa kutetea maslah ya Zanzibar
Wanasahau kwamba bila Zanzibar wasingeitwa waheshimiwa.

Naamini Mungu muweza anasikia kilio Na mateso ya wazanzibar Na yeye ndio tegemeo letu.
Mola wetu tuondolee udhalim huu-
Amein
 
As if sisi huku Tanganyika tunakula bata na Tanesco. Sema Watanzania tunadhulumiwa na Tanesco.
 
Hatimae Waziri wa nishati na Bunge limekubaliana na ukweli juu ya jinsi Wazanzibar tunavyodhulumiwa kuwekewa makato ya ziada kwenye Umeme.

Makato hayo Ni:
3% Umeme vijijini (REA)
2% Energy and Water Regulatory Authority. (EWURA)
Pia kuuziwa kwa bei ya retail price(rejareja) shirika la Zecco Kama anavyonunua Mtu binafsi.

Jana niliweka ujumbe hapa kuhusu hili jambo na jioni walikubaliana na hoja za wabunge wetu na hatimae wamekubali mpaka tarehe 25/6 hili Jambo litakuwa limepatiwa majibu.

Shukran za dhati kwa Spika Ndugai kulipa uzito Jambo hili na kukubali kwamba hii sasa linakuwa ni Jambo la Bunge zima na ukitaka serikali kulimaliza kwa muda uliowekwa.

Pia nimshukuru MH Najma Giga mbunge pekee kutoka CCM Zanzibar kuungana na wabunge wetu makini kutoka CUF kusimamia Hoja hii pamoja huku akiwaacha wabunge wengine wa ccm kama vile jambo hili haliwahusu.

Hakika utumwa wote ni mbaya lakini utumwa wa kutawaliwa kifkra ni mwisho wa uovu. Hata jambo hili wabunge wa Zanzibar walisubiri amri ya Balozi mkaazi?

Wabunge wetu pamoja na kutoitambua serikali iliopo Zanzibar lakini kwa kujali wananchi wanyonge wameamua bila kujali kuwa maslah yakipatikana Zanzibar yatapitia mikononi mwa haohao. Hapa lengo Ni unafuu kwa wananchi wetu.

Inaumiza sana tukiwa hapa bungeni unamsikia waziri wa madini wa Tanganyika akisisitiza wananchi wa Tanganyika waungiwe Umeme kwa sh 27,000/-tu. Wenzetu wana Dhahabu, gesi, almasi, na mali tele kwa tele lakini bado serikali yao inawapa unafuu huo huku kodi ya REA na EWURA wakibebeshwa wanyonge wa Zanzibar ambao vijiji vyao havijawahi kunufaika na msaada wa REA.

Tujiulize huko Zanzibar ni kiasi gani mnyonge wa Mungu inabidi apapatue kuunganishiwa Umeme? Nasikia kima cha chini Ni 18000/

Kweli tuna serikali inayowajali watu wake?
Kweli tuna wawakilishi wanaojali matatizo ya watu wetu?
Hakika inauma wachaguliwa na wananchi waliopo bungeni wanaposhindwa kutetea maslah ya Zanzibar
Wanasahau kwamba bila Zanzibar wasingeitwa waheshimiwa.

Naamini Mungu muweza anasikia kilio Na mateso ya wazanzibar Na yeye ndio tegemeo letu.
Mola wetu tuondolee udhalim huu-
Amein
Bure aghali,wekeni umeme wenu halafu huo ndio msitoe hata thumni na hakuna wa kuwauliza,udhalimu huku hulipi ukiambiwa lipa unasema udhalimu,bure kabisa nyie wavaa talawanda
 
Hatimae Waziri wa nishati na Bunge limekubaliana na ukweli juu ya jinsi Wazanzibar tunavyodhulumiwa kuwekewa makato ya ziada kwenye Umeme.

Makato hayo Ni:
3% Umeme vijijini (REA)
2% Energy and Water Regulatory Authority. (EWURA)
Pia kuuziwa kwa bei ya retail price(rejareja) shirika la Zecco Kama anavyonunua Mtu binafsi.

Jana niliweka ujumbe hapa kuhusu hili jambo na jioni walikubaliana na hoja za wabunge wetu na hatimae wamekubali mpaka tarehe 25/6 hili Jambo litakuwa limepatiwa majibu.

Shukran za dhati kwa Spika Ndugai kulipa uzito Jambo hili na kukubali kwamba hii sasa linakuwa ni Jambo la Bunge zima na ukitaka serikali kulimaliza kwa muda uliowekwa.

Pia nimshukuru MH Najma Giga mbunge pekee kutoka CCM Zanzibar kuungana na wabunge wetu makini kutoka CUF kusimamia Hoja hii pamoja huku akiwaacha wabunge wengine wa ccm kama vile jambo hili haliwahusu.

Hakika utumwa wote ni mbaya lakini utumwa wa kutawaliwa kifkra ni mwisho wa uovu. Hata jambo hili wabunge wa Zanzibar walisubiri amri ya Balozi mkaazi?

Wabunge wetu pamoja na kutoitambua serikali iliopo Zanzibar lakini kwa kujali wananchi wanyonge wameamua bila kujali kuwa maslah yakipatikana Zanzibar yatapitia mikononi mwa haohao. Hapa lengo Ni unafuu kwa wananchi wetu.

Inaumiza sana tukiwa hapa bungeni unamsikia waziri wa madini wa Tanganyika akisisitiza wananchi wa Tanganyika waungiwe Umeme kwa sh 27,000/-tu. Wenzetu wana Dhahabu, gesi, almasi, na mali tele kwa tele lakini bado serikali yao inawapa unafuu huo huku kodi ya REA na EWURA wakibebeshwa wanyonge wa Zanzibar ambao vijiji vyao havijawahi kunufaika na msaada wa REA.

Tujiulize huko Zanzibar ni kiasi gani mnyonge wa Mungu inabidi apapatue kuunganishiwa Umeme? Nasikia kima cha chini Ni 18000/

Kweli tuna serikali inayowajali watu wake?
Kweli tuna wawakilishi wanaojali matatizo ya watu wetu?
Hakika inauma wachaguliwa na wananchi waliopo bungeni wanaposhindwa kutetea maslah ya Zanzibar
Wanasahau kwamba bila Zanzibar wasingeitwa waheshimiwa.

Naamini Mungu muweza anasikia kilio Na mateso ya wazanzibar Na yeye ndio tegemeo letu.
Mola wetu tuondolee udhalim huu-
Amein
Mkuu Eleesha, kwanza nitoe pole kwa Wanzanzibari, kutokana na tabia ya kuzoea vya bure kwa kila kitu kutaka kubebwa bebwa, itafikia mahali hata mbeleko yenyewe inaelemewa mwishowe ina hatari ya kukatika!.

Hayo malipo unayoyaita makato ya ziada
3% Umeme vijijini (REA)
2% Energy and Water Regulatory Authority. (EWURA)
, isio makato ya ziada bali ni statutory payments kwenye package ya Tanesco.

Statutory payments ziko kwa mujibu wa sheria, mtu yoyote atakayetumia huduma za Tanesco lazima ayalipe regardless anahudumiwa na REA or na Ewura kwa sababu malipo haya ni package!.

Namna pekee kwa Zanzibar kuepuka malipo haya ni kufua umeme wake mwenyewe.

Tanesco ni kampuni inayouza bidhaa, ya umeme, bei ya bidhaa hiyo ni kiasi kadhaa kwa unit moja. Kila atakayenunua bidhaa hiyo lazima alipie kiasi kilichopangwa regardless malipo mengine yanamuhusu au hayamhusu.

Katika mahangaiko ya maisha, kuna wakati niliishi UK Katika jiji la London nikifanya kazi ya kubeba box. Ukifanya kazi yoyote halali UK, ukilipwa lazima ukatwe kodi. Ndani ya kodi hiyo unayokatwa kuna hadi kodi ya kulipia BBC ndani yake. Nikasema mimi siangalii BBC, sina TV wala redio!. Nikaelezwa hayo ni malipo ya lazima haijalishi unaangalia BBC au haungalii, unasikiliza Redio au hausikilizi, maadam hiyo nyumba ina TV set na kuna watu wanaishi humo, lazima utalipia TV levy hata kama hautawasha hiyo TV mwaka mzima. It's in a package ya kodi lazima ulipe.

Hata sisi kwenye mifumo yetu kuna malipo ya SDL yanayokwenda VETA, taasisi zote za Zanzibar zilizo Bara lazima zilipe hata kama VETA sio taasisi ya Muungano. That is the package!.

Baada ya kugundulika gesi Mtwara, Dangote akajenga kiwanda cha cement Mtwara ili apate gesi kwa urais.

Tanzania tumejenga bomba la gesi kwa mkopo wa dola billion 1.2 kutoka Exim Bank ya Uchina, mkopo huo utalipiwa na gesi inayochimbwa Mtwara. TPDC kwenye kukokotoa viwango vya bei ya gesi, pia vimejumuisha gharama za kusafirisha hiyo gesi kutoka Mtwara hadi Dar ndipo wakaja na bei ya gesi ya LNG.

Dangote kagoma kulipa kwa hoja kuwa alijenga kiwanda Mtwara ili kuepuka gesi kusafirishwa. Kwa nini alipie gharama za kusafirisha gesi wakati kiwanda chake hakihitaji gesi ya kusafirishwa?. Akaambiwa that is the package price!. Akagoma!.

Akaamua kutumia makaa ya mawe ya Ngaka ikatokea hawana uwezo wa kuzalisha kutosheleza mahitaji ya kiwanda chake, hivyo akaagiza makaa ya kutosha kutoka Afrika Kusini, serikali ikapiga marufuku kuagiza makaa. Jamaa akakasirika akafunga kiwanda, hadi Magufuli alipoingilia kati kumruhusu kuchimba makaa yake na auziwe gesi kwa bei halisi bila gharama ya kusafirishwa hivyo atasafirisha mwenyewe hadi kiwandani kwake.

Vivyo hivyo kwa Zanzibar, we are very sorry for you, lazima ama mlipie umeme kwa bei iliyopangwa ama fueni umeme wenu au mtumie vibatari.

Paskali
 
Mkuu Pascal Mayalla ahasante kwa maelezo. Zaidi ya hapo wznz wajue kuwa umeme unaovushwa kuna service charge za miundo mbinu. Nani analipa?
Pesa za MCC walipewa kwa ajili ya umeme vijijini. Kiasi hicho ni kikubwa kuliko mkoa wa Tanganyika

Zeco wanakusanya bill za wateja. Wanazipeleka wapi?
Wznz wamesahau kuwa kulikuwa na ufujaji wa pesa hizo zeco?

Leo wakiambiwa katika deni la bilioni takribani 120 walipe bilioni 100 hawataki

Wanazaidi ya miaka 10 SMZ haijalipa kwavile tu wanapata bure

Kikubwa cha kuwauliza, wanaonewa! kwenye muungano wanachangia nini?

Hoja ya kutaka kila kitu bure inachosha. Wanapewa hadi bajeti bado wanadhani wanaonewa

Hao wabunge wa znz wanaosema wanaonewa wapo Dodoma kwa kodi za Mtanganyika siyo SMZ

Kuondokana na adha wafue umeme wao wa upepo au mafuta, hawalazimishwi kuchuku bara

Zaidi ya kudai hawana gharama nyingine zozote ndani ya muungano.

Halafu wznz wajiulize, nani aibie znz na kwasababu zipi. Bajeti yao nzima ni ya wizara moja tu
 
Some birds are not meant to be caged, that's all. Their feathers are too bright, their songs too sweet and wild. So you let them go, or when you open the cage to feed them they somehow fly out past you. And the part of you that knows it was wrong to imprison them in the first place rejoices, but still, the place where you live is that much more drab and empty for their departure. FREE ZANZIBAR.HAKI!
 
Wazanzibar mnapenda sana vya dezo... Mmesikka hayo malipo huku bara hatulipi? Mbona kila mtu analipa.. Kwann nyie msilipe.. Au mnatak ss wa bara tuwalipie?
 
Wazanzibar mnapenda sana vya dezo... Mmesikka hayo malipo huku bara hatulipi? Mbona kila mtu analipa.. Kwann nyie msilipe.. Au mnatak ss wa bara tuwalipie?
Wazanzibari wananufaika vipi na mikato ya REA na EWURA?
 
Mkuu Pascal Mayalla ahasante kwa maelezo. Zaidi ya hapo wznz wajue kuwa umeme unaovushwa kuna service charge za miundo mbinu. Nani analipa?
Pesa za MCC walipewa kwa ajili ya umeme vijijini. Kiasi hicho ni kikubwa kuliko mkoa wa Tanganyika

Zeco wanakusanya bill za wateja. Wanazipeleka wapi?
Wznz wamesahau kuwa kulikuwa na ufujaji wa pesa hizo zeco?

Leo wakiambiwa katika deni la bilioni takribani 120 walipe bilioni 100 hawataki

Wanazaidi ya miaka 10 SMZ haijalipa kwavile tu wanapata bure

Kikubwa cha kuwauliza, wanaonewa! kwenye muungano wanachangia nini?

Hoja ya kutaka kila kitu bure inachosha. Wanapewa hadi bajeti bado wanadhani wanaonewa

Hao wabunge wa znz wanaosema wanaonewa wapo Dodoma kwa kodi za Mtanganyika siyo SMZ

Kuondokana na adha wafue umeme wao wa upepo au mafuta, hawalazimishwi kuchuku bara

Zaidi ya kudai hawana gharama nyingine zozote ndani ya muungano.

Halafu wznz wajiulize, nani aibie znz na kwasababu zipi. Bajeti yao nzima ni ya wizara moja tu
Mkuu Nguruvi 3, tena umenikumbusha. Mtoto huwa anabebwa akiwa mchanga lakini kadri anavyakuwa na kupata akili anafikia kiwango akibebwa na yeye anajibeba hadi kufikia hataki tena kubebwa. Lakini huyu Mtoto wetu Zanzibar, sio tuu anabebwa bali anapobebwa alipaswa naye angalau kujibeba lakini ndio kwanza anajibweteka!.

Tulipounga alipaswa kuchangia uendeshaji wa muungano, nasikia alichangia mwaka mmoja tuu au miwili na mchango wake wa mwisho ni uanzishwaji wa BOT ile 1966, baada ya pale ndio basi mwendo ni wa kubebwa mwanzo mwisho. Hawachangii tena hata senti tano kuendesha muungano. Zigo lote la kuendesha Muungano ameachiwa mshirika mmoja tuu.

Tatizo sio kuchoka kuwabeba, ukibebwa angalau basi japo uwe na shukrani kwa anaye kubeba kwa kutojibweteka na kutulizana humo kwenye mbeleko ya Muungano, lakini toto hili...!, liko mgongoni limebebwa halafu lina sumbua, lina kukuruka, linaleta nyodo, kelele na ghubu hadi karaha kwa mbebaji.

Niliwahi kuwashauri
Wanzanzibar amueni moja, ama acheni kelele za muungano!, ama pigeni Kura ya Maoni, muamue moja!.

Paskali
 
Mkuu Pascal Mayalla ahasante kwa maelezo. Zaidi ya hapo wznz wajue kuwa umeme unaovushwa kuna service charge za miundo mbinu. Nani analipa?
Pesa za MCC walipewa kwa ajili ya umeme vijijini. Kiasi hicho ni kikubwa kuliko mkoa wa Tanganyika

Zeco wanakusanya bill za wateja. Wanazipeleka wapi?
Wznz wamesahau kuwa kulikuwa na ufujaji wa pesa hizo zeco?

Leo wakiambiwa katika deni la bilioni takribani 120 walipe bilioni 100 hawataki

Wanazaidi ya miaka 10 SMZ haijalipa kwavile tu wanapata bure

Kikubwa cha kuwauliza, wanaonewa! kwenye muungano wanachangia nini?

Hoja ya kutaka kila kitu bure inachosha. Wanapewa hadi bajeti bado wanadhani wanaonewa

Hao wabunge wa znz wanaosema wanaonewa wapo Dodoma kwa kodi za Mtanganyika siyo SMZ

Kuondokana na adha wafue umeme wao wa upepo au mafuta, hawalazimishwi kuchuku bara

Zaidi ya kudai hawana gharama nyingine zozote ndani ya muungano.

Halafu wznz wajiulize, nani aibie znz na kwasababu zipi. Bajeti yao nzima ni ya wizara moja tu
na nyie Tanganyika kwenye muungano munachangia nn
 
Mkuu Pascal

Juzi wamezindua kituo cha kodi cha kijitonyama wadau wakiwa TRA na ZRB
Makusanyo ya kodi ya TRA yanakwenda kuwapa 4% ya kila mwezi. Yale ya ZRB yanabaki huko

Simu zinazopigwa na watu milioni 45 ni Tanganyika, halafu kiasi kinakwenda kwa watu lakini 5
Nilidhani wangeachiwa waunde mashirika yao. Zantel walikimbia kwa soko
Sasa hapo wanalalamika wanaonewa

Hiyo 3% ya REA ikiondolewa Tanesco ikawa charge service za infrastructure wataweza?

Kinachoshangaza wao ni wazuri sana wa kudai, na wabovu sana wa kuchangia
Nani atuonyeshe bajeti ya znz ya mambo ya ndani, ulinzi, mambo ya nje, shughuli za muungano n.k. Hao wabunge wakidai REA ingependeza wakaitaka SMZ iwagharamie kushiriki shughuli za Tanganyika ambazo nyingi haziwahusu

Wabunge wanaolalamika wanalipwa posho na mishahara ya Tanganyika.
Kwa mwezi mmoja gharama zao ni kubwa kuliko deni wanalodaiwa. Hawaoni

Katika kubebwa kunakokirihisha ni pale wanapopewa HESLB za wanafunzi wao bure kutoka TRA ambayo wanadai mgao pia. Halafu hawalipi mkopo kama wa bara! hilo kwao ni haki. Bure!

Ni wakati wa kuwaeleza ndani ya muungano si kudai tuuu kila asubuhi.
Ni lazima waonyeshe mchango wao ni nini.

Ningefurahi japo wangepewa kawizara kamoja waendeshe

Mtoto ana miaka 10 bado anataka nyonyo tu na huko Dodoma wanaona haki.
Hawamasaidi wanamdumaza. Wznz waulizwe katika muungano sehemu yao ni ipi ukiacha madai

Hili la umeme ni la biashara, kama wanaona Tanesco inawadhulumu wafue umeme wao au wachukue Mombasa! hawalazimishwi nini kinawasukuma kupiga kelele kila siku na si kutamani japo kuchangia hata kidogo
 
na nyie Tanganyika kwenye muungano munachangia nn
Tumeubeba mzima! hadi wabunge kutoka znz ni wafadika
Yaani ukizungumzia tunachangia nini inachekesha. Tumeubeba na tumebeba SMZ
Bajeti ya ZNZ inapata subsidy, halafu kila mwezi kuna 4% ya kodi za Tanganyika kwenda znz

Kwa maneno mengine znz wanaomba kodi zikusanywe sana bara, ili 4% iwe nono

Ukiacha kubeba muungano, kuna mbeleko ya mtoto.
 
Tumeubeba mzima! hadi wabunge kutoka znz ni wafadika
Yaani ukizungumzia tunachangia nini inachekesha. Tumeubeba na tumebeba SMZ
Bajeti ya ZNZ inapata subsidy, halafu kila mwezi kuna 4% ya kodi za Tanganyika kwenda znz

Kwa maneno mengine znz wanaomba kodi zikusanywe sana bara, ili 4% iwe nono

Ukiacha kubeba muungano, kuna mbeleko ya mtoto.
yaani unamainisha muungano ni Tanganyika au
 
yaani unamainisha muungano ni Tanganyika au
Hapana na ZNZ kwa jina. Muungano wa kuchangia na rasilimali ni Tanganyika aliyeubeba

Kama sivyo nieleze kitu kimoja tu ambacho znz inachangia
 
Hatimae Waziri wa nishati na Bunge limekubaliana na ukweli juu ya jinsi Wazanzibar tunavyodhulumiwa kuwekewa makato ya ziada kwenye Umeme.

Makato hayo Ni:
3% Umeme vijijini (REA)
2% Energy and Water Regulatory Authority. (EWURA)
Pia kuuziwa kwa bei ya retail price(rejareja) shirika la Zecco Kama anavyonunua Mtu binafsi.

Jana niliweka ujumbe hapa kuhusu hili jambo na jioni walikubaliana na hoja za wabunge wetu na hatimae wamekubali mpaka tarehe 25/6 hili Jambo litakuwa limepatiwa majibu.

Shukran za dhati kwa Spika Ndugai kulipa uzito Jambo hili na kukubali kwamba hii sasa linakuwa ni Jambo la Bunge zima na ukitaka serikali kulimaliza kwa muda uliowekwa.

Pia nimshukuru MH Najma Giga mbunge pekee kutoka CCM Zanzibar kuungana na wabunge wetu makini kutoka CUF kusimamia Hoja hii pamoja huku akiwaacha wabunge wengine wa ccm kama vile jambo hili haliwahusu.

Hakika utumwa wote ni mbaya lakini utumwa wa kutawaliwa kifkra ni mwisho wa uovu. Hata jambo hili wabunge wa Zanzibar walisubiri amri ya Balozi mkaazi?

Wabunge wetu pamoja na kutoitambua serikali iliopo Zanzibar lakini kwa kujali wananchi wanyonge wameamua bila kujali kuwa maslah yakipatikana Zanzibar yatapitia mikononi mwa haohao. Hapa lengo Ni unafuu kwa wananchi wetu.

Inaumiza sana tukiwa hapa bungeni unamsikia waziri wa madini wa Tanganyika akisisitiza wananchi wa Tanganyika waungiwe Umeme kwa sh 27,000/-tu. Wenzetu wana Dhahabu, gesi, almasi, na mali tele kwa tele lakini bado serikali yao inawapa unafuu huo huku kodi ya REA na EWURA wakibebeshwa wanyonge wa Zanzibar ambao vijiji vyao havijawahi kunufaika na msaada wa REA.

Tujiulize huko Zanzibar ni kiasi gani mnyonge wa Mungu inabidi apapatue kuunganishiwa Umeme? Nasikia kima cha chini Ni 18000/

Kweli tuna serikali inayowajali watu wake?
Kweli tuna wawakilishi wanaojali matatizo ya watu wetu?
Hakika inauma wachaguliwa na wananchi waliopo bungeni wanaposhindwa kutetea maslah ya Zanzibar
Wanasahau kwamba bila Zanzibar wasingeitwa waheshimiwa.

Naamini Mungu muweza anasikia kilio Na mateso ya wazanzibar Na yeye ndio tegemeo letu.
Mola wetu tuondolee udhalim huu-
Amein
Ngoja mkome wawakilishi wenu bunge la jamhuri ni kupiga makofi hata pumba
 
Back
Top Bottom