Utunzaji wa nywele za asili

Apa nna Afro balaa kama la Shmateo,,ila Tatizo nywele zangu waga hazisimami nikizichana zinashuka akati ni ndefu kinyama yaani!!
 
Kwa wale ambao tuna nywele asilia a.k.a natural hair, tayari tunafahamu changamoto kadhaa tunazokumbana nazo. Kwa wale mnaofikiria kuanza kuwa na nywele asilia, karibuni sana tuendelee kujuzana namna ya kutunza nywele zetu kama tulivyopewa na Mungu

Katika mada ya leo,nitakwenda kuzungumzia vitu vya kuzingatia ili kuikuza nywele yako asilia kwa haraka zaidi. Je,unazifahamu nywele zako vizuri? Una nywele za aina gani? Zina tabia gani? Zinataka nini?

1. Kuzikubali kama zilivyo na kuzipenda.
Utasikia ..hiki kipilipili changu ni steelwire ya kimataifa, ..hakitikisiki hata upepo wa dunia yote ungevumia pande hizi. Mwingine oh.. nywele zangu kama miti ya mibuyu kichwani…hazishikiki.Tatizo ni kwamba hamjafahamiana vizuri yani wewe na nywele zako. Hata mimi niligombana nazo sana huko nyuma kabla ya kuzielewa vizuri hivyo jambo la msingi la kuzingatia katika nywele zako ni kujenga mahusiano mazuri tu na nywele zako ,zielewe, ukifikia hapo utaanza kuzipatia hata hazitakusumbua.

2. Usafi wa ngozi ya nywele na nywele zenyewe.
Nywele zenye afya huanzia kwenye ngozi safi ya nywele. Nafahamu unataka nywele zako zisidumae kwa hiyo zioshe vizuri. Wakati uliopita nilizungumzia kuziosha kwa product zilizo rafiki( ‘friendly’) . Ngozi safi ya nywele itasababisha nywele kupata njia ya kujitokeza nje kwa urahisi. Unapoziacha chafu, ule uchafu unaziba matundu ya nywele zako na kuzuia njia, kama ambavyo matundu ya uso yakiziba unapata machunusi maana uchafu unajaa basi kwa nywele hazitakua vizuri.

3. Linda unyevu wa nywele zako
Kila mtu akisikia kiu hunywa maji. Nywele zako zinahitaji kulindwa zisisikie kiu. Unapoziosha,yale mafuta asilia ya kuzilinda huondoka na uchafu. Nywele inabaki ikiwa na udhaifu fulani maana haiwezi hata kushikilia hayo maji yaliyopo vizuri, na zikikauka zinakua kavu sana. Ni vizuri kabla hazijakauka vizuri, ukazi-’condition’. Kwa nywele ambazo ni nyepesi na chache, pia kuna product za kuzisaidia ziweze kutunza vizuri unyevu na hivyo kuwa na afya nzuri.

4. Zifahamu nywele zako
Yani hapa ndo shule ilipolalia kabisaa maana ukizijua tu basi utazihudumia kwa usahihi. Unatakiwa kuangalia namna gani nywele zako zinanyonya unyevu. Unajuaje?

Chukua kikombe,kijaze maji safi.Ukipata glass itakuwa vizuri zaidi.

Chomoa unywele mmoja kichwani,hakikisha unatoka na kale kamzizi kake keupe keupe hivi.

Tumbukiza unywele wako kwenye glass yako ya maji hakikisha imeingia yote.Kama ikizama hapo hapo na hainyanyuki tena,basi nywele zako zinanyonya unyevu kwa haraka kabisa. Kama inachukua muda kuzama,au haizami kabisa,nywele zako zinanyonya unyevu taratibu au zinanyonya kwa shida .(Wala usihofu,zipo namna ya kuzifanya zinyonye unyevu kwa haraka,tutajuzana.)Ni kwamba ‘cuticle’ zake zimefunga haswa,ndio maana unyevu au maji haviingii kwa haraka.

Kwa hiyo ukifanya ‘deep conditioner’ kwa kutumia joto kama la drier lakini uwe moto mdogo sana au ufanye ‘hot oil treatment’ itakusaidia ‘cuticle’kufunguka na unyevu kupita.

Mbadala,unaweza baada ya kuosha suuza na maji ya vuguvugu halafu weka mafuta ya kimiminika.Inasaidia sana.

Mimi nina aina gani?..Nina nywele zinazonyonya unyevu haraka.

5. Mafuta ya Kupaka kichwani.
Ni ya muhimu mnoo!.Nimefanya utafiti wa kina nimeona mafuta ya nazi yanaweka afya nzuri kwa nywele aina nyingi hivyo na mimi nikaanza kuyatumia. Kwangu mimi,mafuta ya nazi ya kutengeneza mwenyewe yamenikubali sana. Japo huwa nanunua pia mafuta kama ya olive(extra virgin) na ya tea tree.

6. Kuzichambua vizuri kabla ya kuchana.
Uwe mkarimu na mwenye subira kwa nywele zako. Mimi zikijifunga huwa nazichambua kwa mikono taratibu wakati mwingine nazilowesha na maji kwa mbali halafu nachana kwa chanuo lenye mapana sio ambalo reli zake zimebanana. sio kitana. Chanuo kubwa(wide toothed comb).

7. Usizisumbue mara kwa mara na usuke mitindo ya kuzitunza zikue.
Kama unataka zikue haraka,usizisumbue sana.Unaweza ukasuka mitindo mizuri tu ukakaa nazo wiki nzima au kadri zitakavyodumu. Au upunguze kuzichana mara kwa mara lakini utafute siku kama wikiendi ukae uzichambue taratibu na vidole kuondoa mafundo.Kuchana mara kwa mara zinapukutika,zinaanguka. Zitakua lakini sio kwa kasi ya kama ukizisuka ukaziacha kwa muda.

8. Punguza matumizi ya vitu vya moto kwenye nywele zako kama pasi ya nywele na vingine vya hivyo.


Sababu hizi hupelekea nywele kukatika

Hilo ni tatizo linalowakumba, siyo kinamama pekee, pia wanaume. Hata bidhaa nyingi za vipodozi hazijaweza kuleta matokeo makubwa katika kukabiliana na hali hiyo.

Kulikoni nywele zinapotea?

Zipo sababu mbalimbali zinazochangia kupotea nywele nyingi vichwani.
Kupotea au kunyonyoka kwa nywele, kumekuwa kukielezwa na wataalamu wa viumbe, kwamba ni matokeo ya misukosuko inayovipata viumbe vyote. Sababu zinazotajwa zinajumuisha zifuatazo:-\

  • Kuwepo shida za kila mara, au za muda mfupi, lakini athari zake ni kubwa.
  • Magonjwa ya kisaikolojia ya muda mrefu.
  • Uvuta sigara.
  • Kinga ya mwili kuwa chini; magonjwa yatokanayo na virusi; mabadiliko ya homoni katika mwili; masuala yanayohusu mazingira; mabadiliko ya mzunguko wa damu katika kichwa;
  • Sababu nyingine kurithi, kuwekewa ganzi wakati wa matibabu, mlo usio sahihi; ujauzito na kunyonyesha; tabia mbaya; magonjwa ya kichwani.
  • Kukatika nywele na ujauzito
Kwanini nywele za wanawake walio wengi hukatika sana wakati wa ujauzito na baada ya kujifungua? Ni tatizo linalomkumba takriban kila mjamzito.

Wakati wa ujauzito, inaelezwa kuwa virutubisho vya afya ya mwili huchukuliwa na mtoto na kumwachia mama kiasi kidogo. Ni hali inayomuachia mama huyo uchovu.

Lakini swali la kujiuliza ni, kwanini kukatika kwa nywele hukuishii kipindi cha mimba tu, bali inaendelea hata baada ya kuzaliwa mtoto?"

Mwili wa mama baada ya kuzaliwa mtoto, unafanya kazi ya uzalishaji maziwa. Ni hali inayompunguzia mama nguvu zake.

Kwa mantiki hiyo, wataalamu wa afya wanasema, mabadiliko makubwa ya homoni katika mwili wakati wa ujauzito na baada ya kujifungua huchangia madhara kwa mama kupoteza nywele.

Sababu za wanawake kupoteza nywele nyingi, pia inaweza kusababishwa na mambo yafuatayo;-

  • Upungufu wa vitamini zaidi ya aina moja mwilini (Avitaminosis) kwa muda mrefu; Yafaa kupata hasa vitamin ‘E’ na ‘A’ wakati wa ujauzito, ili kuepuka nywele kukatika.
  • Hali mbaya ya hewa, kwa mfano joto lililopotiliza.
  • Kuwepo kemikali kali za rangi zilizoko chini ya nywele bandia za bei nafuu, vidonge vya mara kwa mara vya kemikali, matumizi ya vifaa vya kukausha nywele, bila ya kutumia vifaa vya kinga.
  • Mimba na mchakato wa kuzaliwa.
  • Pia, kupoteza nywele nyingi kunaelezwa kunachangiwa na matokeo ya matumizi ya muda mrefu ya dawa. Kwa mfano, dawa zinazosababisha kuchanganyikiwa au kupatwa ‘maruweruwe’ zijulikanazo kama ‘narcoleptics.’ Vitu vinavyozuia kukua na
    kugawanyika chembe baadhi ya aina za dawa zinazozuia kifafa na ukosefu mkubwa wa vitamini A.
    Urejeshaji nywele

Haijalishi umepoteza nywele nyingi kiasi gani, lakini ni muhimu kuanza mchakato wa tiba mara moja kwa kushauriana na daktari kupata suluhisho.Mchakato wa kurejesha nywele unahitaji muda wa kutosha, utaratibu na uvumilivu sahihi.Hivi sasa, njia za kurejesha nywele zilizopotea zinapatikana kupitia baadhi ya njia zifuatazo:
  • Ulaji wa baadhi ya vitamin.
  • Baadhi ya vifaa vya tiba vinavyoondoa madhara, tiba ya uso na ngozi.
  • Matumizi ya vipodozi maalum na dawa za tiba za kienyeji ambazo ni za nyumbani, ambazo hupikwa kulingana na mapishi ya wanafanilia wanaozifahamu kwa kina.
Aidha, baada ya upotevu wa nywele, inaelezwa ni muhimu kuanza mara moja kuchukua hatua zinazozingatia mambo kadhaa:
  • Kuboresha lishe ya vifuko vinavyoshikilia mizizi ya nywele na kimetaboliki kwa jumla.
  • Kuboresha mzunguko wa damu kwenye mishipa midogo ya damu katika nywele.
  • Kuondoa ukavu kichwani.
Kumbuka kwamba, kupoteza nywele kwenye sehemu za mwili hutokea kwa muda fulani.
Hiyo, imekuwa ikimaanisha kwamba; kwanza unahitajika utunzaji viungo vyote vya mwili kwa ujumla.
Pili, ili kurejesha hali ya zamani ya nywele na itachukua muda, wakati mwingine zaidi ya vile tunavyodhania. Lakini, kwa njia ya kawaida, japokuwa ni ngumu bado inawezekana kurejesha nywele zilizopotea.

Wanawake wengi wanaona jinsi nywele zao zinavyokatika kwa wingi, bila ya kujali baadaye itakuwaje kimwili na kihisiaNywele zinazopotea. Ikiwa kila siku mtu anapoteza nywele kati ya 50 na 150 kulingana na ulaini wa kichwa, ikiwa ni jambo la kawaida.

Kumbuka kwamba, mifuko midogo inayoshikilia nywele kichwani, hubadilika kila mara na hawezi kabisa kuzuia upoteaji wa nywele.

Inashauriwa kwamba, iwapo mtu anaona nywele zake zinapotea sana, ni muhimu akawa na wasiwasi juu ya dalili za kuwepo walakini wa afya yake.

Unajuaje nywele zinapungua?

Wanawake wengi wenye nywele ndefu wanaweza kugundua uzito wa jumla umeshuka, ila wasijue kinachoendelea.

Lakini, ili kuwa na uhakika kabisa kwamba kichwa chako kimepungua nywele kwa uwiano, hesabu idadi ya nywele zilizoanguka wakati wa mchana.

Mtu akitaka kupata matokeo sahihi zaidi, inapendekezwa kwamba asikilize kichwa chake, kwa siku moja au mbili kabla ya jaribio.

Saa za asubuhi, mtu anaweza kuhesabu nywele zilizobaki juu ya mto baada ya kulala.

Kisha hatua inayofuata, ni kwamba mtu ananyunyiza nywele kwenye chombo kisafi na ahesabu wingi wa nywele fupi nene zinazobakia. Hapo ndipo, mtu anarekodi matokeo katika kidokezo maalum.

Nyakati za mchana, kila baada ya kuchana nywele, angalia nywele ngapi zinazopotea zaidi.

Mwishoni wa siku, mtu anatakiwa asafishe kichwa chako. Nywele zinazobaki bafuni au mikononi mwako, inapaswa pia kuhesabiwa. Huo ni mchakato mbadala.

Kwa njia hiyo, mtu anajua usahihi kabisa ni kiasi cha nywele anachopoteza kila siku.
Nywele na umri

Swali lingine ni je, uliwahi kujua kwamba, kulingana na umri, matatizo ya mabadiliko ya homoni na rangi ya nywele, kiwango cha kila siku cha kupoteza nywele kinaweza kutofautiana?

Kwa vijana, hadi asilimia 10 ya vifuko vinavyoshikilia nywele juu ya kichwa, hufa wakati wa kipindi cha kupevuka.

Kwa hiyo, swali la kuulizwa daktari, ni kwamba ikiwa nywele zimekatika kwa mtoto, inapaswa kuzingatia mazingira anayoishi na utendaji wa chembe ndani za mwili wake. Usiogope kabla ya wakati, ikiwa unapambana kukabili afya ya mtoto wako.

Wakati wa makuzi ya watoto (umri kati ya miaka mitatu hadi saba), balbu nyingi za nywele ziko katika awamu utendaji kazi.

Iwapo binti yako mwenye umri wa miaka 10 bado ana upotevu mkubwa wa nywele, hiyo ni nafasi ya kufanya miadi na daktari bingwa wa eneo hilo (dermatologist) kwa ajili ya kusaidia kuondokana na tatizo hilo.

Ikumbukwe, mpito wa umri wakati wa marekebisho ya homoni, huongeza tena kiwango cha wastani cha kupoteza nywele.

Nywele na rangi
Kulingana na rangi ya asili, kila mwanamke anapoteza nywele kwa kiasi tofauti kila siku. Kwa mfano, nywele rangi ya asili zina balbu zaidi juu ya vichwa vyao - hadi 150,000.

Nywele zao ni nyembamba za kutosha nyeusi na zenye uzuri zaidi kuliko zinazojulikana kama ‘braunettes’ au rangi nyekundu.

Kiwango cha upotezaji ya wenye nywele za asili, ni kati ya nywele 100 hadi 150 kwa siku. Nywele nyekundu pia zinamilikiwa na wanawake vijana wenye rangi nyekundu-‘maji ya kunde.’
Kichwani kwa mnyama mwenye kichwa chekundu, kuna

Vifuko vinavyoshikilia nywele (follicles) 80,000. Kwa hiyo, kiwango cha kupoteza manyoya kwao hutofautiana kutoka nywele 70 hadi 90 kila siku.

Kiwango cha hasara ya kila siku kinawekwa kwenye nywele karibu 80 hadi 110.
Ushauri

Nywele zikibaki katika hali ya asili kupumua, ni bora kwa ngozi. Kwa sababu hiyo, ukitaka uwe salama, ni muhimu kuepuka mitindo ya nywele iliyokaza sana.

Mambo kadhaa muhimu katika usalama wa chakula:
Chakula kisicho sahihi. Kwa kazi ya kawaida, balbu juu ya kichwa zinahitaji nguvu si tu kutoka nje, pia ndani.

Kwa hiyo, wanawake waliozoea mlo usio na lishe nzuri, mara nyingi wanakabiliwa na tatizo la kupoteza nywele, tofauti na wale wanaokula chakula bora.

Isisahaulike kwamba, kuimarisha mlo kwa mboga, matunda na multivitamini.






View attachment 1341083



Njia za asili za kuandaa chakula cha nywele



Kitengo kinaninyanyasa sana hiki cha nywele. Kuna hii kuweka vitu vya kisasa, madawa, mawigi n.k.,Mimi sipatani na madawa na harufu za hizi mambo kabisa.Na wenzetu hicho kitengo ndo huwaambii kitu.
 
Back
Top Bottom