Ukuta kama wa Berlin wajengwa Tanzania kwa pesa za watanzania

Mimi nimekulia eneo ambapo buzwagi ipo nakumbuka kipindi tunasoma shule ya msingi tulikuwa tunapita buzwagi hapo na wanafunzi wenzangu tunakwenda kucheza mpira KIJIJI cha jirani cha Mwime ya ILINDI sasa njia hiyo imefungwa na ndipo ulipo mgodi ambao sisi kama wananchi hatuna faida nao hata kidogo tunaloa vumbi kila kukicha ni tabu tupu hapa Kahama dhahabu yetu imegeuka kuwa mauti yetu sasa magonjwa kama kansa yanatunyemelea tumekwisha masikini Tanzania uliyetukuka sasa unanyong'onyea.
 
lile beleshi la dhahabu alilohongwa mkapa lipo wapi? KARAMAGI kuanzisha kampuni ya simu inaitwa 4G ndiye aliyesaini mkataba wa kuuzwa buzwagi hotelini ulaya
 
MIMI Kinachoniuma ni hiyo salary difference kati ya mzawa na mgeni ilihali wanafanya kazi sawa but tatizo la tofauti ya mishahara kati ya wageni na wazawa ni kubwa sana karibu kila kampuni cha ajabu huyu waziri wa ajira anafanya kazi gani kama wazungu wanakuja kuchomelea vyuma bongo?
Ndo sababu nliwahi sema ajira zimejaa tanzania lakini watanzania hatuajiriwi sasa cjui huyu anaetoa work permit kwa wachomeleaji kutoka nje ni nan?
 
Wewe nyumbani kwako hakuna ukuta? mbona Mwadui kuna ukuta hamjasema?

Ukuta wa Mwadui uko sehemu gani? Mwadui ina njia nyingi sana na hakuna ukuta. Acha uongo. Mi ningeshauri Buzwagi waweke na bati juu ili vumbi lisiathiri mji wa Kahama
 
Nyumbani kwangu sijajengewa na wageni.inashangaza kuona wazungu wanajenga ukuta eti kuwazuia wenyeji wasichukue madini.Mwadui huwa nafurahi sana nikisikia WABESHI wameingia kuchukua mawe

Na Wabeshi hawazuiwi kwa ukuta
 
Inashangaza nini? hao wenyeji walikuwa wapi siku zote? na hakuna sehemu zingine kuchimba nadini isipokuwa hapo walipokwisha pewa hao wawekezaji?

Wacheni ushamba, hakuna mtu atawekeza mifedha yote hiyo halafu awache wazi mje kumuibia, Kuweni wakweli wa nafsi zenu.
Ikiwa wewe nyumbani kwako unawaogopa ndugu na jamaa zako wakitanzania wasikuibie, ulitaka mgeni awache wazi? tena naona wamechelewa ilikuwa waweke hizo kuta siku ya kwanza walipokabidhiwa hiyo sehemu.

Kweli waswahili wanasema aliyezowea vya kunyonga vya kuchinja haviwezi.
Kama hamtaki wachimbe, ni simpo tu. Waambieni ondokeni, wawashitaki (kama Dowans) muwalipe gharama na faida waondoke zao, halafu nyinyi mchimbe na fedha zake msizione ziwe zinalipiwa madeni mpaka miaka 200 ijayo. Mnanshangaza.

Washauri Magamba wenzako wafunge huo uwanja wa ndege wa Buzwagi. Kwa usalama wa 3% yetu.
 
Magamba matatu, tafadhali usichanganye kuwa wa TZ wote ni wizi, unaposema "sababu ni kuwa kampuni inahisi wataz wanaiba mali zao" nadhani ungesema wanahisi "wezi" wanaiba mali zao. Na pia sizani kama kwa kuhisi tu wangefanya yote hayo, nna uhakika wameshaibiwa na ndio maana wanafanya hivyo, kujilinda wao nafsi zao na mali zao...

Mnazungumzia Tanzania yenu ipi? Kama ni hii siyo yetu, ilikwisha pigwa mnada siku nyingi na wajanja. Sisi sote ni watumwa wao hivyo huo mshahara tunaopata ni fadhila tu.
 
Mkuu ninachokisema kinaonekana kwa kila mtanzania anayepita barabara ya kuelekea kahama kutoka Shy na siyo kuwa ni kitu kilichojificha kuwa hadi kiundiwe tume ili wapate ushahidi, ni ukuta unaoonekana waziwazi, na una urefu wa kama mita 5 juu na material yanayotumika ni zege tupu, kila kipande kinachotengenezwa na kubandika kina umbo la mraba wa kama mita 5 kwa 5 nadhani unanielewa.
<br />
<br />
na bado kuna seng'eng'e ya umeme na CCTV
 
Inashangaza nini? hao wenyeji walikuwa wapi siku zote? na hakuna sehemu zingine kuchimba nadini isipokuwa hapo walipokwisha pewa hao wawekezaji?

Wacheni ushamba, hakuna mtu atawekeza mifedha yote hiyo halafu awache wazi mje kumuibia, Kuweni wakweli wa nafsi zenu.

Ikiwa wewe nyumbani kwako unawaogopa ndugu na jamaa zako wakitanzania wasikuibie, ulitaka mgeni awache wazi? tena naona wamechelewa ilikuwa waweke hizo kuta siku ya kwanza walipokabidhiwa hiyo sehemu.

Kweli waswahili wanasema aliyezowea vya kunyonga vya kuchinja haviwezi.

Kama hamtaki wachimbe, ni simpo tu. Waambieni ondokeni, wawashitaki (kama Dowans) muwalipe gharama na faida waondoke zao, halafu nyinyi mchimbe na fedha zake msizione ziwe zinalipiwa madeni mpaka miaka 200 ijayo. Mnanshangaza.

Dah, kuna wakati unaweza usione kabisa. Hapo kwenye red. Well, amewekeza kweli vitu vyenye thamani. Hilo halina ubishi, lakini ukweli ni kwamba hicho wanachochimba ambacho ndo urithi wetu kina thamani kubwa kuliko hayo madudu yao. Urithi unaondoka so easily, watu wanapaza sauti kuutetea FF unashangaa!!!!!!!!!!!!!!!!!!? What a miss.........
 
Kinachonisikitisha ni kauli kuwa mabosi wa mgodi hawawezi kula au kulala Kahama kwani hakuna hoteli zenye hadhi yao. Je watu laki 5+ waliozunguka mgodi hawana thamani kulingana na hao mabosi. Go and return, Dar to Kahama daily tena kwa ndege
 
Jamani hii nchi imejaa madini sehemu nyingi tu! Zingine hazijaanzwa kuchimbwa.
Kwa nini tumeshindwa kwenda huko na kuchimba?
Kwa nini siku zote tunasubiri mzungu aje kutufanyia mambo yetu alafu tunaanza kulalamika?

Guys, ladies, please let us stop whining and take action. Action as in kwenda huko ambako wazungu hawajaanza kuchimba tukachimbe tuone kama tutaweza.

Secondly, I am sure Barrick is building the wall to avoid the Mara scenario.
Acha wajifungie tu humo humo.

What we can complain about, it perhaps better pay for our brothers and sisters if indeed they are underpaid. But knowing most of us Watanzania, huwa wazito sana kazini alafu tunashangaa kwa nini mwenzetu analipwa zaidi. Tuanze kuchapa kazi.
Pia, we can also complain about better terms as in what does the country or community gets from these companies.
Shule na hospitals ni responsibility ya serikali but Barrick can do it in kind. Never obligated.

In short, STOP WHINING and DO SOMETHING!
 
Mtoa mada ushukuriwe kwa taarifa:
nilikuwa sijui kama kuna foregners hapa Tz wanaofanya kazi nyepesi sana ambazo watanzania wanazimudu. Hii inadhiirisha ni kwa kiasi gani sheria zetu(za tanzania) hazina makali au zipo kwa watanzania walalahoi and not otherwise; mi nashangaa-kuna utaratibu wa Vibali vya kufanya kazi nchini na mashariti yako wazi, sasa inawaje hao wachomeleaji wanaolipwa Tsh. Milioni 20 kwa mwezi ila hali watanzania wanaofanya kazi hiyohiyo wanalipwa Tsh laki 3.5. Ni hatari watanzania wenzangu: Lakini ngoja tulifanyie kazi.
 
Mdogo wangu alihama zamani kwa sasa yulo Burundi, anasema hawezi kubali kuishi kwenye nchi ambayo kila mtu anasema ni tajiri halafu yeye tu peke yake ndio hauoni huo utajiri. Alipataga kibarua GGm akaambiwa salary 250,000 na ana degree akaamua kusepa> Bora awe mkimbizi kule kuliko kuendelea kuteseka kwenye nchi yake. Mm mwenyewe nikimaliza haka ka degree kangu ka Engineering naenda Sudani Kusini.
 
Fanya kazi kama mtumwa wa nchi yako kisha kabru aishi kama mfalme. Kisa, tatizo la ajira bongo.
 
Ukuta kama wa Berlin unajengwa huko Kahama na Kampuni ya kuchimba madini ya Barrick- Buzwagi, ni ukuta wenye ghalama ya juu kuliko unavyofikiri, ni mzunguko wa km zipatazo 80, ninaposema ni wa ghalama ninamaanisha kuwa ni ukuta usiotumia tofali hata kidogo, inatengenezwa ukuta wa kubandika na unabandikwa kwa crane baada ya kuwa unakamilka kwa kila kipande na kwa sasa zimeishajengwa kama km 2, kma unaelekea kahama mjini kutoka shinyanga utauona huo ukuta,

Haijawahi kutokea hata Afrika ukuta mkubwa kuliko huo, sababu ni kuwa kampuni inahisi wataz wanaiba mali zao,
Huku kiampuni ikijenga ukuta huo wa matrion ya pesa wananchi wanaouzunguka mgodi huo wa Buzwagi hawana hata hospitali, shule zinazouzunguka mgodi huo wanafunzi wanakaa chini,wananchi wanaouzunguka mgodi huo hawana hata maji, Wananchi hawana umeme huku mgodi ukiwaka umeme kila siku.

Kibaya zaidi wafanyakazi wanaofanya kazi na kuupatia faida kubwa mgodi huo na kufikia kujenga ukuta huo wa BERLIN kwa matrion ya pesa mshahara wake ni dhaifu na kama ungeweza kupata saraly slips zao ungeshangaa sana kwani bado wana kipato cha 350000 cha enzi za Chiligati huku wakiajiliwa mamia ya wazungu wachomeleaji wa vyuma na mafundi wa kawaida na kulipwa zaidi ya sh milioni 20 kwa mwezi huku kazi wanayofanya ni sawa na wazawa waliopo hapo mgodini,nilipopita kuelekea kahama nilistaajabu sana kwa jinsi huo ukuta unaojengwa kwa ghalama kubwa na baada ya kumuuliza mdogo wangu niliyeenda kumtembelea kahama anafanya kazi pale Buzwagi na kumuuliza kipato chake,niliona saraly slip yake nikashangaa sana, na akaniambia kuwa kuna watu ni mafundi wa kuchomelea tuu vyuma kutoka Afrka kusini wanalipwa zaidi ya sh milion 20 kwa mwezi huku yeye akiambulia kiasi cha 350000 kwa mwezi na wote wanafanya kazi moja,

Hiii ni serikali yangu ila kwa hili nimeamini Tanzania haiko serious na wananchi wake, sikatai kwa kampuni kubwa kama hii ya Barrick kujenga ukuta mkubwa kama huu, swali langu ni dogo tuu,
1. Je hiii kampuni inawajali kimaslahi hao wafanyakazi wanaosababisha wapate hizo faida zote????

2. Je hii kampuni inawapa wananchi wanaouzunguka huu mgodi huduma bora kama afya na elimu kulingana na faida kubwa hii wanayopata????

kuna umuhimu wa JK na serikali yake kufika 2011 jamani kwa mambo yanavyozidi kuwa hivi?
hebu tujaribu kufikiri, "una nyumba then ukamkaribisha mpangaji, kwa kumkaribisha na kwa kulialia ukakubalia kukaa bila kulipa kodi then baada ya mwezi nyumba yako haina umeme lkn anajivutia chumbani kwake, anajivutia maji chumbani kwake, anabomoa mlango na kujiwekea grill, anakataza watoto wasipite kwenye corido n.k na baba umenyamaza tu ni sawa?"
 
Magamba matatu, tafadhali usichanganye kuwa wa TZ wote ni wizi, unaposema "sababu ni kuwa kampuni inahisi wataz wanaiba mali zao" nadhani ungesema wanahisi "wezi" wanaiba mali zao. Na pia sizani kama kwa kuhisi tu wangefanya yote hayo, nna uhakika wameshaibiwa na ndio maana wanafanya hivyo, kujilinda wao nafsi zao na mali zao.

Nadhani wasingekuwa na matatizo ya kuibiwa na mengine ya kiusalama wasingeweka huo ukuta, sioni ubaya wa kujilinda na kujihami. Au ulitaka wawache wazi?

Tanzania nzima ukitembea majumba, maduka, viwanda, vina kila namna ya ulinzi kuzuwia wezi na ujambazi, kuanzia maukuta makubwa makubwa mpaka waya za umeme, walinzi na silaha za kila aina, mbwa, mageti ya chuma, madirisha ya nondo. Au huyaoni hayo? sasa cha ajabu nini ikiwa wanajenga ukuta wa kujilinda?

Kama wewe una kajumba kako ka 20 x 20 na hakana hata mali za million mbili ndani unajilinda kwa ukuta, geti la chuma, waya za umeme, mbwa wa polisi na mlinzi wa kimasai na wa Knight security. Sasa hao wenye vifaa vya mabilion na mali wanayochimba ya matrilion unashangaa nini wakijilinda?

Ndugu.. Watanzania wakiamua kuchukua kutoka katika migodi hiyo wanachukua kilicho chao baada yakuona waliokabidhiwa si lolote ila ni waporaji!! Hakuna mtu anaeiba kilicho chake mwenyewe!!!!... Hivi umesha kaa na kujiuliza kwa nini Watanzania wanavamia migodi hiyo??? Jibu ni rahisi kama A, B, C!!! Wanaona hawanufaiki chochote kutoka katika madini hayo pamoja na kuwa ni ya kwao kwa 100%!!!! Wanaozunguka migodi hiyo kama wangekuwa wananufaika wangeona faida ya kuwepo migodi hiyo na kwa hiyo wasingeivamia na hao waporaji wasingekua na haja ya kujenga ukuta mkubwa namna hiyo. Hao watanzania sio wajinga kiasi hicho kiasi waamue kuharibu kinachowanufaisha!!!
 
Wakubwa hayo ndo mambo ya makaburu!!! Wazawa wanalipwa vijimishahara kiduchu wakati hao wanaowaita ma-experts wanalipwa mishahara mikubwa mno wakati hakuna cha ajabu wanachokifanya cha ziada ukilinganisha na wafanyakazi wazawa!! Mambo hayo yapo pia Mtibwa Sugar Estate na Kilombero Sugar Estate(ILLOVO)!!! %&*@#^%$!!!
 
Acheni Ushabiki na jazba, leteni evidence hapa...

Hata hivyo nani anafahamu mkataba wao na serikali aumwage hapa...

Pili nani anafahamu wanalipa kiasi gani serikalini amwage hapa...

Tatu acheni ufinyu wa maono je, ni wao wa kuwatizama au ni wale waliowaruhusu kuwepo hapo wa kuwatizama"? Maana mi najua mwekezaji kwa lolote liwe jengo au investment lazima apate kibali cha serikali kuhusiana na development anayotaka kuifanya kwenye eneo lake....

Aliyeko huko afuatilie atujuze acheni wivu kwani hata ingekuwa wewe kwa hali ya usalama wa mgodi ungejenga ukuta, ninachotaka kujua ni nani amewaruhusu kujenga? Na mrahaba na mchango kw ajamii ni kiasi gani na kwa nani? Wazungu ni jamii ambayo sio wajinga kihivyo unaweza kukuta Mjomba wako ndio anakusanya mirahaba na michango ya jamii na kuipeleka nyumba ndogi kama sio kule kwa wengine...

Leteni evidence hapa
 
Back
Top Bottom