Ukusanyaji wa maoni baada kumaliza Zanzibar nzima

abdulahsaf

JF-Expert Member
Aug 31, 2010
858
130
Written by Zanzibar Moja // 18/12/2012 // Habari // 8 Comments


Na Ismail Jussa
MAONI KWA ZANZIBAR NZIMA:
Ukichukua mwelekeo wa maoni yote yaliyotolewa hadharani katika mikutano yote iliyofanywa na Tume ya Kukusanya Maoni ya Katiba katika visiwa vya Zanzibar unapata picha ifuatayo:
1. Waliotaka Zanzibar yenye mamlaka kamili kitaifa na kimataifa na kufuatiwa na Muungano wa Mkataba kati yake na Tanganyika ni 14,998 sawa na 65.98%.
2. Waliotaka muundo wa sasa wa Muungano (Serikali Mbili) uendelee ni 7,034 sawa na asilimia 30.94%.
3. Waliotaka Serikali Tatu ni 105 sawa na 0.46%.
4. Waliotaka Serikali Moja ni 22 sawa na 0.9%.
5. Waliotoa maoni mengine ni 573 sawa na 2.52%.

MTAZAMO BINAFSI: Inafurahisha kuona wapenda mabadiliko (progressives) katika Zanzibar kwa ujumla asilimia yao imebakia takriban ile ile 66% ambayo ndiyo iliunga mkono kuanzishwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa mwaka 2010. Kwa upande mwengine,
wahafidhina wanaokataa mabadiliko katika jamii ya Zanzibar wanazidi kupungua kutoka asilimia 33% hadi asilimia 31%.
 
Ni swali la kipuuzi; kwanini msiulize wanaotaka Zanzibar nje ya Muungano bila kufuatiwa na 'muungano wa Mkataba' na Tanganyika wako wangapi? Hiyo ndio ingewapa picha hasa ya nini kinaendelea. Haijulikani kiwango cha asilimia ya Wazanzibari wanaotaka Zanzibar huru bila Muungano na Tanganyika.
 
Tulisha kwambieni msitupigie kelele weye! Kila siku Muungano wa mkataba, sijui muungano wa ........ Kila mtu si akae zake kwake nyiee! Mmeshasema hamuutaki, kwa nini kila uchwao mko Tanganyika. Kila leo viongozi wenu hawaishi kuja Dodoma. Si wanaogopa kupoteza ajira!!!! Maalim alianza na kuuvunja. leo hii anahubiri muungano wa mkataba. hata sie hatutaki cha mkataba wala nini. Mwisho wenu pale CHUMBE weye!!!!! Halafu tuone. KAMA NI MBWAI NMBWAI BWANA!!!! Msituumize masikio yetu kila siku hapa. Mlisha elezwa njia za kuuvunja, mbona hamzi tuumii weye!!!
 
Kwa maneno mengine asilimia 65.98 ya Wanzibari hawataki 'Zanzibar huru'. Wanataka kubebana na 'koloni' Tanganyika.
 
[h=1][/h]Written by Zanzibar Moja // 18/12/2012 // Habari // 8 Comments


Na Ismail Jussa
MAONI KWA ZANZIBAR NZIMA:
Ukichukua mwelekeo wa maoni yote yaliyotolewa
hadharani katika mikutano yote iliyofanywa na Tume ya
Kukusanya Maoni ya Katiba katika visiwa vya Zanzibar
unapata picha ifuatayo:
Waliotaka Zanzibar yenye mamlaka kamili kitaifa na
kimataifa na kufuatiwa na Muungano wa Mkataba kati
yake na Tanganyika ni 14,998 sawa na 65.98%.
Waliotaka muundo wa sasa wa Muungano (Serikali
Mbili) uendelee ni 7,034 sawa na asilimia 30.94%.
Waliotaka Serikali Tatu ni 105 sawa na 0.46%.
Waliotaka Serikali Moja ni 22 sawa na 0.9%.
Waliotoa maoni mengine ni 573 sawa na 2.52%.
MTAZAMO BINAFSI: Inafurahisha kuona wapenda
mabadiliko (progressives) katika Zanzibar kwa ujumla
asilimia yao imebakia takriban ile ile 66% ambayo
ndiyo iliunga mkono kuanzishwa kwa Serikali ya Umoja
wa Kitaifa mwaka 2010. Kwa upande mwengine,
wahafidhina wanaokataa mabadiliko katika jamii ya
Zanzibar wanazidi kupungua kutoka asilimia 33% hadi
asilimia 31%.

hii ina maana CUF ni wengi kuliko CCM
 
Ni swali la kipuuzi; kwanini msiulize wanaotaka Zanzibar nje ya Muungano bila kufuatiwa na 'muungano wa Mkataba' na Tanganyika wako wangapi? Hiyo ndio ingewapa picha hasa ya nini kinaendelea. Haijulikani kiwango cha asilimia ya Wazanzibari wanaotaka Zanzibar huru bila Muungano na Tanganyika.

hadidu rejea zinataka maoni yote lazima yazingatie uwepo wa Muungano ndio maana maoni ya Wazanzibari wanaotaka Zanzibar huru bila Muungano na Tanganyika hayakuchukuliwa.
 
Kwa hesabu hiyo inaonyesha maoni yaliyotolewa na watu hadharani idadi yake ni watu 22,732. Sijui ya maandishi itakuwa wangapi. Nawashangaa wanasiasa Jussa na Mumewe Sefu kusema Wazanzibari wanataka N'kataba (Muungano wa Mkataba). Hivi ni kweli watu 14,998 wanaweza wakawasemea watu milioni moja na laki tano? Na msimamo wa CUF ni upi, Sefu anataka N'kataba wakati baraza la CUF limetoa tamko wanataka Serikali Tatu. Nawasikitikia sana Wazanzibari wanaowashabikia wanasiasa mabaradhuli.
 
kwa hesabu hiyo inaonyesha maoni yaliyotolewa na watu hadharani idadi yake ni watu 22,732. Sijui ya maandishi itakuwa wangapi. Nawashangaa wanasiasa jussa na mumewe sefu kusema wazanzibari wanataka n'kataba (muungano wa mkataba). Hivi ni kweli watu 14,998 wanaweza wakawasemea watu milioni moja na laki tano? Na msimamo wa cuf ni upi, sefu anataka n'kataba wakati baraza la cuf limetoa tamko wanataka serikali tatu. Nawasikitikia sana wazanzibari wanaowashabikia wanasiasa mabaradhuli.

ni wakati wa kuitafuta tanganyika yenu wafamaji
 
Tulisha kwambieni msitupigie kelele weye! Kila siku Muungano wa mkataba, sijui muungano wa ........ Kila mtu si akae zake kwake nyiee! Mmeshasema hamuutaki, kwa nini kila uchwao mko Tanganyika. Kila leo viongozi wenu hawaishi kuja Dodoma. Si wanaogopa kupoteza ajira!!!! Maalim alianza na kuuvunja. leo hii anahubiri muungano wa mkataba. hata sie hatutaki cha mkataba wala nini. Mwisho wenu pale CHUMBE weye!!!!! Halafu tuone. KAMA NI MBWAI NMBWAI BWANA!!!! Msituumize masikio yetu kila siku hapa. Mlisha elezwa njia za kuuvunja, mbona hamzi tuumii weye!!!

wewe inaonesha pia unautaka muungano tena ni kwa asilimia mia moja.dalili za kuukubali muungano ni kuchukia wazanzibar wanaotaka zanzibar huru.pia,wewe hutoi maoni yako juu ya muungano upi unaoutaka ila unatukana maneno kwa maneno machafu.mwisho,kama huna lakusema shut up ur mauz than talking nonesense words.shame on u.dumbs.bulshit.
 
wewe inaonesha pia unautaka muungano tena ni kwa asilimia mia moja.dalili za kuukubali muungano ni kuchukia wazanzibar wanaotaka zanzibar huru.pia,wewe hutoi maoni yako juu ya muungano upi unaoutaka ila unatukana maneno kwa maneno machafu.mwisho,kama huna lakusema shut up ur mauz than talking nonesense words.shame on u.dumbs.bulshit.

Mkuu!

Yaelekea umegusika sana, eti????!!!! Miye ntatoaje maoni kwa lidude nsilo ona maana yake? Nyie ndo mwahangaika sana nalo, kwa vile mwaliona lamitesa. Sasa mkiambiwa haya uvunjeni, mwasema tutoe maoni. Maoni gani tena wakati weye ushahitimisha yakhee???? Tushakwambieni fanyeni mtakavyo, nyie bado mwashikilia kutoa maoni. Twaambia hatuna muda wa kutoa maoni bado mwang'ang'ana na 'MKATABA'. Mbona STAKI NATAKA NYINGI YAKHE??????

Acha hasira mkuu!!!
 
Mkuu!

Yaelekea umegusika sana, eti????!!!! Miye ntatoaje maoni kwa lidude nsilo ona maana yake? Nyie ndo mwahangaika sana nalo, kwa vile mwaliona lamitesa. Sasa mkiambiwa haya uvunjeni, mwasema tutoe maoni. Maoni gani tena wakati weye ushahitimisha yakhee???? Tushakwambieni fanyeni mtakavyo, nyie bado mwashikilia kutoa maoni. Twaambia hatuna muda wa kutoa maoni bado mwang'ang'ana na 'MKATABA'. Mbona STAKI NATAKA NYINGI YAKHE??????

Acha hasira mkuu!!!

Hata tanganyika yako huitaki?
 
Ni swali la kipuuzi; kwanini msiulize wanaotaka Zanzibar nje ya Muungano bila kufuatiwa na 'muungano wa Mkataba' na Tanganyika wako wangapi? Hiyo ndio ingewapa picha hasa ya nini kinaendelea. Haijulikani kiwango cha asilimia ya Wazanzibari wanaotaka Zanzibar huru bila Muungano na Tanganyika. :confused2:
Hili si swali la kipuuzi. Anaejua maana kuelewa lugha ni kusema kuwa wanaotaka muungano wa Mkataba ni sawa na wanaotaka Zanzibar nje ya Muungano

HIvi ndi kwanza leo Zanzibar wapige kelel kuwa hawataki muungano? mtoto akililia wembe si umpe? si useme wachieni hao potelea mbali lakini kukicha MUUNGANO UDUMU HUU NDIO UPUUZI
 
Written by Zanzibar Moja // 18/12/2012 // Habari // 8 Comments


Na Ismail Jussa
MAONI KWA ZANZIBAR NZIMA:
Ukichukua mwelekeo wa maoni yote yaliyotolewa hadharani katika mikutano yote iliyofanywa na Tume ya Kukusanya Maoni ya Katiba katika visiwa vya Zanzibar unapata picha ifuatayo:
1. Waliotaka Zanzibar yenye mamlaka kamili kitaifa na kimataifa na kufuatiwa na Muungano wa Mkataba kati yake na Tanganyika ni 14,998 sawa na 65.98%.
2. Waliotaka muundo wa sasa wa Muungano (Serikali Mbili) uendelee ni 7,034 sawa na asilimia 30.94%.
3. Waliotaka Serikali Tatu ni 105 sawa na 0.46%.
4. Waliotaka Serikali Moja ni 22 sawa na 0.9%.
5. Waliotoa maoni mengine ni 573 sawa na 2.52%.

MTAZAMO BINAFSI: Inafurahisha kuona wapenda mabadiliko (progressives) katika Zanzibar kwa ujumla asilimia yao imebakia takriban ile ile 66% ambayo ndiyo iliunga mkono kuanzishwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa mwaka 2010. Kwa upande mwengine,
wahafidhina wanaokataa mabadiliko katika jamii ya Zanzibar wanazidi kupungua kutoka asilimia 33% hadi asilimia 31%.
MHeshimiwa, usichanganye mambo kati ya kura ya maoni na ukusanyaji wa maoni. Mawili haya huwezi kuyalinganisha. Kura huwa Siri na hukusanya watu wengi, tofauti na ukusanyaji wa maoni ni watu jasiri tu na wasokuwa na haya kuzungumza mbele umati wa watu ndio wanaoshiriki.
Angalia sasa Pro, Baregu, Mjumbe wa Tume na ambaye ni kiongozi kwa timu iliyokuwako katika Mkoa Mjini/magharibi alivyosema, na mnukuu 'kuwa walichokifuata Zanzibar sicho ambacho walikuwa wanakipata kutoka kwa wananchi mbalimabli visiwani humu. "Hutukuja kuchukua maoni ya aina gani mfumo wa Muungano uwe lakini ndio maoni ambayo tulikuwa tunayapata kwa wananchi wa Zanzibar," mwiso wakunukuu. Huoni kuwa Takwimu zako hazina uzito woote na maoniyaliotolewa kwa ujumla hayana maana kwa vile watu walienda nje ya mada?
 
MHeshimiwa, usichanganye mambo kati ya kura ya maoni na ukusanyaji wa maoni. Mawili haya huwezi kuyalinganisha. Kura huwa Siri na hukusanya watu wengi, tofauti na ukusanyaji wa maoni ni watu jasiri tu na wasokuwa na haya kuzungumza mbele umati wa watu ndio wanaoshiriki.
Angalia sasa Pro, Baregu, Mjumbe wa Tume na ambaye ni kiongozi kwa timu iliyokuwako katika Mkoa Mjini/magharibi alivyosema, na mnukuu 'kuwa walichokifuata Zanzibar sicho ambacho walikuwa wanakipata kutoka kwa wananchi mbalimabli visiwani humu. “Hutukuja kuchukua maoni ya aina gani mfumo wa Muungano uwe lakini ndio maoni ambayo tulikuwa tunayapata kwa wananchi wa Zanzibar,” mwiso wakunukuu. Huoni kuwa Takwimu zako hazina uzito woote na maoniyaliotolewa kwa ujumla hayana maana kwa vile watu walienda nje ya mada?

Mkuu,zanzibar wana katiba yao,kinacho wapeleka zanzibar kwenye katiba ya tanzania ni muungano na mkataba ndio maamuzi yao,muda wa kiviburuza visiwa umeisha.
 
Back
Top Bottom