Freetown
JF-Expert Member
- Apr 6, 2008
- 883
- 72
Ukubwa wa baraza la mawaziri ni ufisadi mkubwa sana, nasema hivi kwa sababu nchi zilizoendelea tena zinazochangia bajeti yetu zina baraza dogo la mawaziri kuliko TZ. Kenya nchi ambayo hakuna ubishi imetuzidi sana kiuchumi ina baraza la mawaziri 40 ambalo pia limepigiwa kelele sana na wananchi wa nchi hiyo mpaka walifanya maanadamano ambayo mwanamama aliye wahi kuwa mshindi wa Noble alipokea maanamamno hayo na kuelezea juu ya ubaya wa kuwa na baraza kubwa la mawaziri kuwa ni mzigo kwa wananchi.
Sasa kwa nchi yetu hata pale Rais alipounda baraza la mawaziri 60 halikupingwa waziwazi. umefika wakati katiba ileeze wazi kuwa tunatakiwa kuwa na baraza la mawaziri wasiozidi 20 ili kupunguza mzigo kwa wananchi ambao hali zao zinazidi kuwa mbaya kila kukicha. Najua wabunge wengine hawatafurahi kwa sababu udogo wa baraza la mawaziri utawanyima ndoto yao ya kuwa mawaziri
Tujaribu kulipia kelele hili swala jamani!!!!!!!!!!!!!!
Sasa kwa nchi yetu hata pale Rais alipounda baraza la mawaziri 60 halikupingwa waziwazi. umefika wakati katiba ileeze wazi kuwa tunatakiwa kuwa na baraza la mawaziri wasiozidi 20 ili kupunguza mzigo kwa wananchi ambao hali zao zinazidi kuwa mbaya kila kukicha. Najua wabunge wengine hawatafurahi kwa sababu udogo wa baraza la mawaziri utawanyima ndoto yao ya kuwa mawaziri
Tujaribu kulipia kelele hili swala jamani!!!!!!!!!!!!!!