Ukosekanaji wa Haki kwenye Mhimili wa Mahakama, kunaweza kuwa kunachangiwa na Majaji/Mahakimu wenye uwezo mdogo kubaini haki?

Wanabodi, hili ni bandiko la kitambo, hoja yake ni uwezo mdogo wa baadhi ya majaji na mahakimu wetu kuwa na jicho la tatu, jicho la ndani, jicho la roho kubaini haki.

Hoja hii inathibitishwa na kinachoendelea ndani ya mhimili wa Mahakama sasa. Jaji Mkuu Prof. Ibrahim Juma, ametimiza umri wa kustaafu kwa mujibu wa sheria tangu Juni 15, lakini kufuatia kukoseana majaji Rufaa wenye uwezo wa kushika nafasi ya Jaji Mkuu, imebidi Jaji Mkuu Prof. Ibrahim Juma aongezewe muda kidogo wakati wa kumuandaa mrithi wake.

Hivyo hoja yangu hii inapata nguvu!, yaani licha ya kuwepo majaji kibao wenye sifa za kuwa Jaji Mkuu, lakini bado hawatoshi, hali inayopelekea Jaji Mkuu aliyemaliza muda wake, kuongezewa muda mpaka mrithi muafaka apatikane.

Kuongezewa muda huku, kukamuibua Jaji Stella Mugasha Profesa Ibrahim Juma kuendelea kuwa Jaji Mkuu, Rais Samia anavunja Katiba ya JMT? hivyo na mimi nikashauri Jaji Mugasha Apewe Maua Yake Kupinga Uvunjifu wa Katiba Ukomo wa CJ, ila Mbona Hili ni Dogo Tuu, Kubwa ni Katiba Yetu Imenajisiwa! Why Wako Kimya?!.

Kuna vitu watu tunasema humu, wana wanapinga!. Majaji Rufani wenye sifa za kuwa Jaji Mkuu, wangekuwepo wa kutosha, kusingelikuwa na need kumuongezea muda CJ aliyemaliza muda wake!.
P
Yaani tuna Majaji vilaza ?
 
Yaani tuna Majaji vilaza ?
Kiswahili ni kigumu sana!, kwenye bandiko hili kuna issue yoyote ya ukilaza?.

Hapa tunazungumzia kutosha!, unaweza kuwa na sifa zote na umekidhi vigezo vyote na bado ukawa hutoshi!. Ma JR wote wana sifa na vigezo vya kuwa CJ, lakini bado CJ ameongezewa muda!, do you know what does this mean?.
P
 
Wanabodi, hili ni bandiko la kitambo, hoja yake ni uwezo mdogo wa baadhi ya majaji na mahakimu wetu kuwa na jicho la tatu, jicho la ndani, jicho la roho kubaini haki.

Hoja hii inathibitishwa na kinachoendelea ndani ya mhimili wa Mahakama sasa. Jaji Mkuu Prof. Ibrahim Juma, ametimiza umri wa kustaafu kwa mujibu wa sheria tangu Juni 15, lakini kufuatia kukoseana majaji Rufaa wenye uwezo wa kushika nafasi ya Jaji Mkuu, imebidi Jaji Mkuu Prof. Ibrahim Juma aongezewe muda kidogo wakati wa kumuandaa mrithi wake.

Hivyo hoja yangu hii inapata nguvu!, yaani licha ya kuwepo majaji kibao wenye sifa za kuwa Jaji Mkuu, lakini bado hawatoshi, hali inayopelekea Jaji Mkuu aliyemaliza muda wake, kuongezewa muda mpaka mrithi muafaka apatikane.

Kuongezewa muda huku, kukamuibua Jaji Stella Mugasha Profesa Ibrahim Juma kuendelea kuwa Jaji Mkuu, Rais Samia anavunja Katiba ya JMT? hivyo na mimi nikashauri Jaji Mugasha Apewe Maua Yake Kupinga Uvunjifu wa Katiba Ukomo wa CJ, ila Mbona Hili ni Dogo Tuu, Kubwa ni Katiba Yetu Imenajisiwa! Why Wako Kimya?!.

Kuna vitu watu tunasema humu, wana wanapinga!. Majaji Rufani wenye sifa za kuwa Jaji Mkuu, wangekuwepo wa kutosha, kusingelikuwa na need kumuongezea muda CJ aliyemaliza muda wake!.
P
Inawezekana pia waliopo hawaoneshi utiifu kwa mama, kwahiyo watafanya kweli na ukweli hautakiwi. Bora awepo zimwi unayemjua kuliko malaika usiyemjua
 
Wanabodi kuanzia sasa, kwenye hoja zangu ninazoibua, zile ambazo zimepatiwa majibu nitakuwa natoa update ya hoja husika na jibu la hoja iliyopatiwa majibu.
Na ikitokea nimetoa hoja kuhusu jambo lolote, hilo jambo likitokea, nitakuwa nakumbushia tuu.
Kwenye bandiko hili nilitoa hoja kuhusu uwezo wa majaji wetu kuwa na jicho la ndani la kubaini haki.

Hoja hii imeleta matokeo chanya ambayo nimeyaeleza hapa
Msikilize Rais Samia anesema nini kuhusu majaji
P

Justice must not only be done, but must be seen to be done!.
Jee hii hukumu ya leo, kuhusu issue ya DPW na Bandari zetu, haki imetendeka?. Jee imeonekana kutendeka?.
P
 
.Kwa maoni yangu, tatizo la msongamano wa kesi, sio idadi ya majaji na mahakimu, bali ni ubovu wa sheria zetu na uwezo mdogo wa baadhi ya majaji na mahakimu kukosa jicho la roho kubaini hatia, na udhaifu wa vyombo vyetu vya upelelezi.
Bandiko hili ni la siku nyingi ila kwa hii issue ya Dr. Slaa kuzungumza kupindua serikali, na kushikiliwa kwa tuhuma za uhaini, kwa kusikiliza tuu yale matamshi ni sedition case na sio treason, naamini bandiko kama hili litawasaidia vyombo vyetu vya uchunguzi kuwa na jicho la haki na kuwatendea haki. Kama kuna mtu yoyote anaamini Dr. Slaa alitaka kupindua serikali, na kama serikali inapindulika kwa matamshi tuu, then s/he needs h/is/er head seriously be examined!.
P
 
View attachment 1841771View attachment 1841772

Wanabodi,

Kama kawaida yangu, kila siku za Jumatatu, huwaletea makala za "Kwa Maslahi ya Taifa", ambayo huchapishwa na gazeti la Nipashe la Jumapili, ambazo ziko kwa mtindo wa maswali, majibu ya maswali hayo, utayapata wewe mwenyewe, na kisha tutawatafuta wahusika, ku balance hii mada, hivyo kwa mada hizi za mhimili wa Mahakama, mtu wa kubalance tuhuma hizi ni Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma.

Baada ya makala kuhusu Ofisi ya DPP, wiki hii, naugeukia Mhimili wa Mahakama.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati akiwaapisha Majaji wapya 28 wa Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani, Rais Samia alisema na hapa ninanukuu

“Tatizo la ucheleweshwaji wa kesi katika Mahakama zetu bado lipo, kama mnavyosema Wanasheria haki inayocheleweshwa ndio haki inayokataliwa, hivyo ni imani yangu kuwa baada ya upatikanaji wa Majaji hawa ucheleweshaji wa kesi Mahakamani utapungua na hatimaye haki kupatikana kwa wakati,” alisema Mhe. Rais Samia.

Rais Samia akaendelea kwa kuitaja Ibara ya (107) A ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Mamlaka ya utoaji haki ni Mahakama, “hivyo jukumu lililopo mbele yenu ni kubwa sana, basi ni vyema mkatekeleze majukumu yenu mliyopewa kwa uaminifu, mkaongoze vyema na mkaongozwe na utu na nafsi zenu katika kuwatumikia wananchi,” Mwisho wa kunukuu.

Kwa upande wake, Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma alimshukuru Mhe. Rais kwa uteuzi wa Majaji hao wapya huku akiwa na imani kuwa idadi hiyo italeta mabadiliko makubwa ambayo yataonekana mara moja.

Jaji Mkuu, Prof. Juma alisema “Mhe. Rais napenda nichukue fursa hii kukushukuru kwa kutupatia Majaji hawa, idadi hii itasaidia kupunguza mzigo wa mashauri kwa Majaji waliopo na hivyo kusaidia kuleta mabadiliko ambayo yataonekana mara moja,” alisema Mhe. Jaji Mkuu.

Prof. Juma, aliendelea “Mhe. Rais idadi ya Majaji inapanda na kupungua kulingana na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kustaafu kwa Majaji pamoja na Majaji wengine kupangiwa majukumu mbalimbali, hivyo bado tunaomba kuendelea kupatiwa Majaji kadri nafasi zinapopatikana ili kuendelea kutoa huduma ya haki kwa kuwa wananchi wengi kwa sasa wanafahamu haki zao na hivyo kufungua kesi kwa wingi,” alieleza Jaji Mkuu.

Kwa vile hoja yangu ya makala hii ni kuangazia uwezo mdogo wa baadhi ya Majaji na Mahakimu wetu, kutokuwa na jicho la ndani, lenye uwezo wa kuona haki, kunakochangia ucheleweshaji wa kesi na ukosefu wa haki, naomba kutoa historia fupi ya maisha yangu na jicho la ndani.

Mimi Paskali Mayalla, zaidi ya kuwa mwandishi wa habari na mtangazaji, mimi pia mtu wa mastori, yaani stori teller, hivyo kwa wapenzi wa mastori, unaweza kufuatilia sehemu hii ya Mastori ya Pasco Mayalla, ila wewe kama sio mtu anayependa mastori, unaweza ku skip hii segment ya mastori
Mastori ya Pasco Mayalla

Lengo la simulizi hii ni kuwadurusu baadhi ya majaji na mahakimu wetu, jee wana uwezo wa kubaini hatia kwa kutumia jicho la ndani?, jee kwenye utoaji wa humuku zao, wanazingatia "utu na nafsi"?, na sio kutegemea tuu vifungu vya sheria na ushahidi pekee?. Ili jinai itendeke ni lazima kuwepo kwa mambo mawili, actus reus (kitendo cha jinai) na mens rea, (nia ya kutenda jinai). Jee mfumo wetu wa kupata majaji na mahakimu wetu, unahusisha amplitude test kubaini uwezo wa hao majaji na mahakimu kutumia jicho la ndani la utu na nafsi kubaini nia ovu ya kutenda jinai?. Jibu ni hapana!.

Tanzania ili mtu kuwa hakimu, ni kwanza kuhitimu shahada ya sheria, na kuomba ajira ya uhakimu, kwenye kuajiriwa, kupitia Tume ya Kuajiri ya Mahakama iliyo chini ya Jaji Mkuu, ila kwenye hadidu za rejea, hakuna amplitude testi yoyote kupima uwezo wa waombaji kuwa na jicho la ndani la kubaini jinai, na matokeo yake ndio baadhi ya hawa mahakimu kwenye mahakama zetu wenye uwezo mdogo, na matokeo yake ni kwa baadhi yao, kutokuwa na uwezo wa kutoa hukumu za haki huku wengine wakituhumiwa kula rushwa!. Udhibitisho wa tuhuma hii ya uwezo mdogo wa mahakimu wetu kutoa hukumu za haki ni mlolongo wa rufaa, na matokeo ya rufaa nyingi kukubaliwa.

Ili kuwa Jaji wa Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani ni Tanzania, ni kwanza kuwa mwanasheria, kisha jina lako likapendekezwa na Tume ya ajira ya Mahakama, na kupelekwa kwa rais, mtu unateuliwa kuwa jaji, napendekeza, ili Tanzania tupate majaji kama Lord Denning, tuongeze vigezo vya mtu kuteuliwa Jaji. Kila mtu anaweza kuwa mwanasheria, lakini sio kila mwanasheria anaweza kuwa Jaji. Mfano mzuri ni mtu aliyekuwa DPP kinara wa ukandamizaji wa haki, halafu mtu huyo anateuliwa kuwa Jaji, unategemea nini?!. Kama akiwa DPP alifanya madudu yote yale ambayo sasa ndio yanafumuliwa, akiwa Jaji, atatenda haki?. Unless kama wakati akiwa DPP, baadhi ya maamuzi yake ilikuwa ni kufuata maelekezo, then sasa akiwa Jaji, atakuwa Jaji mzuri, lakini kama akiwa DPP alishindwa kutenda haki, haitegemewi akiwa Jaji atatendaje haki!.

Nchi za wenzetu hadi wana vifaa maalum vya kubaini kama mhusika anasema uongo, (lie detectors), Majaji wetu na Mahakimu lazima wawe na uwezo huo, ili kuepuka kuwatesa watu kwa kuwasweka ndani miaka mingi watu wasio na hatia. Yako mazingira mtu anakutwa na ushahidi wa kuhusika na jinai fulani, na wengine hadi kuhukumiwa kunyongwa, na akiisha nyongwa ndipo ushahidi unakuja kupatikana kuwa amehukumiwa kwa makosa. Majaji na Mahakimu wetu, wakiwa na jicho la rohoni, wataweza kuiona haki na kutoa hukumu ya haki hata kama ushahidi utaonyesha kuhusika.

Kwa maoni yangu, tatizo la msongamano wa kesi, sio idadi ya majaji na mahakimu, bali ni ubovu wa sheria zetu na uwezo mdogo wa baadhi ya majaji na mahakimu kukosa jicho la roho kubaini hatia, na udhaifu wa vyombo vyetu vya upelelezi. Mfano kwa tukio kama lile shambulio la Lissu, hata sisi tuu waandishi wa habari za uchunguzi, tungehitaji IJ ya siku moja tuu, kubaini chanzo cha wasiojulikana hao, na kukitumia kama lead kuwabaini, lakini kwa vyombo vyetu vya uchunguzi ni mpaka leo hakuna taarifa zozote!.

Kwa kesi kama ya kina Rugemalila, sisi waandishi wa habari za uchunguzi, tungehitaji siku 7 tuu, kuwawekea ushahidi wote mezani, lakini vyombo vyetu vya uchunguzi, ni zaidi ya miaka 4 sasa na bado kesi haijaanza kusikilizwa!, kwenye mazingira kama hayo, hata tungekuwa na majaji 100, wangefanya nini?.

Kwa bahati mzuri, mimi nimebahatika kuwa mwanafunzi wa Prof. Ibrahim Juma, hivyo namfahamu vizuri kwa kauli, uwezo na matendo, jicho hilo la rohoni analo, na kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania, Mahakama ndio mhimili rasmi wa utoaji haki Tanzania, hivyo nina imani kubwa na Mhimili wa Mahakama chini ya Jaji Mkuu, Prof. Ibrahim Juma, licha ya changamoto za utoaji haki, inauwezo wa kuwapatia haki Watanzania.

Kufuatia mhimili wa mahakama kushiriki Maonyesho ya Saba Saba, makala ya wiki ijayo, nitawaletea ushiriki wa Mahakama kwenye Saba Saba.

Paskali
Update
Wanabodi kuanzia sasa, kwenye hoja zangu ninazoibua, zile ambazo zimepatiwa majibu nitakuwa natoa update ya hoja husika na jibu la hoja iliyopatiwa majibu.

Kwenye bandiko hili nilitoa hoja kuhusu uwezo wa majaji wetu kuwa na jicho la ndani la kubaini haki.

Hoja hii imeleta matokeo chanya ambayo nimeyaeleza hapa
Msikilize Rais Samia anesema nini kuhusu majaji
P
Don't attribute to incompetence something that can be explained by malice. Mhimili wa mahakama wanashirikiana na executive kuminya haki za raia. That simple. But the only constant in this world is change. Wataruja wee lakini watarudi chini. We will be waiting for them.
 
Bandiko hili ni la siku nyingi ila kwa hii issue ya Dr. Slaa kuzungumza kupindua serikali, na kushikiliwa kwa tuhuma za uhaini, kwa kusikiliza tuu yale matamshi ni sedition case na sio treason, naamini bandiko kama hili litawasaidia vyombo vyetu vya uchunguzi kuwa na jicho la haki na kuwatendea haki. Kama kuna mtu yoyote anaamini Dr. Slaa alitaka kupindua serikali, na kama serikali inapindulika kwa matamshi tuu, then s/he needs h/is/er head seriously be examined!.
P
Naunga mkono hoja
 
Bandiko hili ni la siku nyingi ila kwa hii issue ya Dr. Slaa kuzungumza kupindua serikali, na kushikiliwa kwa tuhuma za uhaini, kwa kusikiliza tuu yale matamshi ni sedition case na sio treason, naamini bandiko kama hili litawasaidia vyombo vyetu vya uchunguzi kuwa na jicho la haki na kuwatendea haki. Kama kuna mtu yoyote anaamini Dr. Slaa alitaka kupindua serikali, na kama serikali inapindulika kwa matamshi tuu, then s/he needs h/is/er head seriously be examined!.
P
Naunga mkono hoja
 
Wanabodi,


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati akiwaapisha Majaji wapya 28 wa Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani, Rais Samia alisema na hapa ninanukuu

“Tatizo la ucheleweshwaji wa kesi katika Mahakama zetu bado lipo, kama mnavyosema Wanasheria haki inayocheleweshwa ndio haki inayokataliwa, hivyo ni imani yangu kuwa baada ya upatikanaji wa Majaji hawa ucheleweshaji wa kesi Mahakamani utapungua na hatimaye haki kupatikana kwa wakati,” alisema Mhe. Rais Samia.

Rais Samia akaendelea kwa kuitaja Ibara ya (107) A ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Mamlaka ya utoaji haki ni Mahakama, “hivyo jukumu lililopo mbele yenu ni kubwa sana, basi ni vyema mkatekeleze majukumu yenu mliyopewa kwa uaminifu, mkaongoze vyema na mkaongozwe na utu na nafsi zenu katika kuwatumikia wananchi,” Mwisho wa kunukuu.

Kwa upande wake, Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma alimshukuru Mhe. Rais kwa uteuzi wa Majaji hao wapya huku akiwa na imani kuwa idadi hiyo italeta mabadiliko makubwa ambayo yataonekana mara moja.

Jaji Mkuu, Prof. Juma alisema “Mhe. Rais napenda nichukue fursa hii kukushukuru kwa kutupatia Majaji hawa, idadi hii itasaidia kupunguza mzigo wa mashauri kwa Majaji waliopo na hivyo kusaidia kuleta mabadiliko ambayo yataonekana mara moja,” alisema Mhe. Jaji Mkuu.

Prof. Juma, aliendelea “Mhe. Rais idadi ya Majaji inapanda na kupungua kulingana na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kustaafu kwa Majaji pamoja na Majaji wengine kupangiwa majukumu mbalimbali, hivyo bado tunaomba kuendelea kupatiwa Majaji kadri nafasi zinapopatikana ili kuendelea kutoa huduma ya haki kwa kuwa wananchi wengi kwa sasa wanafahamu haki zao na hivyo kufungua kesi kwa wingi,” alieleza Jaji Mkuu.

Kwa vile hoja yangu ya makala hii ni kuangazia uwezo mdogo wa baadhi ya Majaji na Mahakimu wetu, kutokuwa na jicho la ndani, lenye uwezo wa kuona haki, kunakochangia ucheleweshaji wa kesi na ukosefu wa haki, naomba kutoa historia fupi ya maisha yangu na jicho la ndani.

Kwa bahati mzuri, mimi nimebahatika kuwa mwanafunzi wa Prof. Ibrahim Juma, hivyo namfahamu vizuri kwa kauli, uwezo na matendo, jicho hilo la rohoni analo, na kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania, Mahakama ndio mhimili rasmi wa utoaji haki Tanzania, hivyo nina imani kubwa na Mhimili wa Mahakama chini ya Jaji Mkuu, Prof. Ibrahim Juma, licha ya changamoto za utoaji haki, inauwezo wa kuwapatia haki Watanzania.

Paskali
Update
Wanabodi kuanzia sasa, kwenye hoja zangu ninazoibua, zile ambazo zimepatiwa majibu nitakuwa natoa update ya hoja husika na jibu la hoja iliyopatiwa majibu.

Kwenye bandiko hili nilitoa hoja kuhusu uwezo wa majaji wetu kuwa na jicho la ndani la kubaini haki.

Hoja hii imeleta matokeo chanya ambayo nimeyaeleza hapa
Msikilize Rais Samia anesema nini kuhusu majaji
P

Hata kama kuna kiongozi alitoa hiyo 'green light' je, hiyo peke yake inatosha kuwafanya wawe Wabunge?
Kuna taratibu za kuzingatiwa na si takwa la mtu au watu. Walikwendaje Bungeni na Form zikabaki Ufipa?

Hakuna mtu anayeweza kupeleka mtu Bungeni, ingalikuwa rahisi hivyo tusingekuwa na sheria.
Hoja ni je hawa ni Wanachama halali wa chama cha siasa?

Hii ndiyo hoja yao , walifukuzwa bila kuzingatia taratibu.
Hoja yao si kwamba walikwenda vipi Bungeni, ni uhalali wao Bungeni kupitia uanachama.

Kuna mwanasheria mmoja anayejitambulisha kama Baba Mwita, ameandika hoja nzuri sana. Mwita anasema Mahakama iliacha wajibu wake wa kutazama katiba ikaingia katika kutafuta mapungufu ya Katiba.
Mahakama ilitakiwa kuhakikisha je Katiba ya Chadema imefuatwa? Kumbuka katiba imeridhiwa na Msajili

Hoja za akina Halima Mdee ni kutosikilizwa na Baraza kuu, hawakupewa muda wa kufika na upuuzi wa namna hiyo.

Jaji anaposema wajumbe wa CC hawakupaswa kuingia Baraza kuu ni kituko, akina Halima hawakuomba tafsiri ya suala hilo. Mahakama yetu inatia shaka sana na sijui hawa Majaji hupatikana kwa utaratibu gani.

Prof angepisha wengine , amefeli

JokaKuu Pascal Mayalla
Mkuu Nguruvi3 , hili la mhimili wa Mahakama kutokutenda haki ni tatizo kubwa that needs to be addressed properly!. Niliwahi kulizungumza humu Ukosekanaji wa Haki kwenye Mhimili wa Mahakama, kunaweza kuwa kunachangiwa na Majaji/Mahakimu wenye uwezo mdogo kubaini haki?

Hii hukumu ya suala hili imenisikitisha sana, nimeiandikia kitu, na sasa siishii kwenye kuandika tuu humu, mitandaoni na magazetini, bali sasa kuanzia Jumapili hii, naanza kuzungumza public kupitia Channel Ten Kipindi cha TV, Kutoa Elimu ya Katiba, Sheria na Haki, Kuanza Jumapili Hii Kupita Channel Ten. Mahakama Zitoe Haki Hata Bila Kuombwa!.
View: https://youtu.be/ZJIKhnZCf04?si=e1S0KY-zlJOC034E

Naamini kuna vitu ambavyo haviendi vizuri na vinaendelea kwenda mrama kwasababu watu hamvizungumzi, naamini kabisa, mkivizungumzia, publically with honesty and integrity, things will change!.

P
 
Back
Top Bottom