Ukosefu wa waandishi habari vijijini husababisha changamoto lukuki zilizopo huko kukosa utatuzi

Bushmamy

JF-Expert Member
Aug 18, 2019
8,851
15,265
Imezoeleka kuwa habari za vijijini zinapatikana pale kiongozi wa kitaifa akienda huko huku akiongozana na wandishi wa habari toka mjini kwa ajili ya uzinduzi wa jambo fulani kama vile Kisima, Hospital nk lakini baada ya hapo huondoka zao na kurudi walikotoka bila hata ya kuzunguka na kujua changamoto mbalimbali zilizopo vijijini huko.

Hali hii imesabababisha changamoto mbalimbali zilizopo vijijini kusahaulika kabisa,

Moja ya changamoto hizo zinaweza Kuwa ukosefu wa maji safi na salama, ubovu wa miundombinu,Kukosekana kwa Hospital, ndoa za utotoni Ukeketaji wa watoto wa kike nk.

Viongozi kupenda kusifiwa badala ya kukosolewa, hiyo nayo ni shida nyingine inayofanya Habari za vijijini kutosikika na Kutatuliwa na viongozi husika kutokana na Kuwa hawapendi Kukosolewa.

Uminywaji wa uhuru wa habari katika nchi yetu ni Moja ya Mambo yanayofanya wananchi wengi wa vijijini kutotatuliwa changamoto zao au vilio vyao kushindwa Kufika kwenye vyombo vya habari kutokana na Kuwa viongozi Wamekuwa wakiwatishia au kuwaweka ndani waandishi wa habari, na pia kuvifungia vyombo vya habari pindi wanapotumia kalamu zao kuandika changamoto zinazoikumbuka jamii fulani,au kukosoa uongozi.

Viongozi wa serikali na mashirika yasiyo ya kiserikali waangalie namna ya kuwasiaidia waandishi wa habari katika kuleta changamoto mbalimbali zilizopo vijijini kwani huko ndio kwenye mapinduzi halisi ya kimaendeleo, Taarifa za vijijini zitaamsha mapinduzi makubwa ya maendeleo nchini na pia zitafichua mengi tusiyoyajua.

3011344_Screenshot_20211124-132415.jpg
 
Nashauri! Kwa kuwa wasomi wametapakaa hadi huko vijijini, ni muda sasa wa kujitambua na kuanza kuibua changamoto za vijijini na kuzitupia katika mitandao ya kijamii.

Huko vijijini wana smartphone, wapige picha barabara mbovu na kuzipost mitandaoni.

Waandishi wa habari na vyombo vyao si wa kutegemea, kwa sababu hawako huru kutokana na njaa.

Waandishi wa habari huongozana na kiongozi kwenda kwenye ziara kijijini kwa kulipwa posho na usafiri. Usitegemee mwandishi huyo ataandika mambo hasi.
 
Nashauri! Kwa kuwa wasomi wametapakaa hadi huko vijijini, ni muda sasa wa kujitambua na kuanza kuibua changamoto za vijijini na kuzitupia katika mitandao ya kijamii.

Huko vijijini wana smartphone, wapige picha barabara mbovu na kuzipost mitandaoni.

Waandishi wa habari na vyombo vyao si wa kutegemea, kwa sababu hawako huru kutokana na njaa.

Waandishi wa habari huongozana na kiongozi kwenda kwenye ziara kijijini kwa kulipwa posho na usafiri. Usitegemee mwandishi huyo ataandika mambo hasi.

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Wazo zuri hili
 
Back
Top Bottom