ukosefu wa uadilifu kwa viongozi ndo tatizo la maendeleo yetu!

ex-sinner

New Member
Jan 21, 2011
1
0
hamjambo wana jamii!?

napoifkiria miaka hamsini iliyopita tangu tupate uhuru mpaka leo hii naona ni jambo la ajabu kwelikweli kuwa katika level hii ya maendeleo tuliyonayo, kwa hiyo mara nyingine naamua kusema ni vema watu kukaa chini wakaanza kujiuliza kwa nini hali iko hivi na je nini kifanyike ili tujikwamue hapa tulipo! binafsi nimegundua kikubwa kukosekana kwa uadilifu miongoni mwa viongozi na umma kuogopa kuwawajibisha kwa kuwanyima kura zao kipindi cha uchaguzi! nimejaliwa kuwa karibu na viongozi na pengine kuishi pamoja nao!Wengi ni watovu wa nidhamu, wazinzi, walevi, wenye lugha chafu na mengine mengi mno ya ajabu, wasiojali kabisa maisha yetu sisi raia wa ajabu, na kwa kiasi kikubwa hawamaanisha yale wanayoyahubiri majukwaani! hivyo naona ni wakati sasa wakuwajua viongozi tunaowachagua vema kabla hatujawapa dhamana za uongozi wa taifa letu!
 
Back
Top Bottom