Ukosefu wa madawa mahospitalini: Amejinyonga baada ya kufiwa na mtoto..

sosoliso

JF-Expert Member
May 6, 2009
8,539
9,462
Mwanamke aliefahamika kwa jina la Monika Mapoli (22), mkazi wa kijiji cha isima wilayani Geita, amekutwa amejinyonga juzi kwa kutumia kipande cha nguo karibu na Ofisi ya Mganga mkuu Wilaya ya Geita.
Taarifa ya mashuhuda wa tukio hilo zilisema kuwa Mapoli alichukua uamuzi huo baada ya kufiwa na mtoto wake Jumanne Philimo (2) aliekuwa amelazwa wodi namba moja katika Hospitali ya Wilaya ya Geita akipatiwa matibabu.
Ilielezwa kuwa baada ya mtoto kufariki dunia, mama huyo alitoweka wodini na kwenda kusikojulikana hadi alipokutwa amejining'iniza kwenye mti uliopo jirani na Ofisi ya Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo Dk. Omary Dihenga.
Mmoja wa mashuhuda wa tukio Petro Majiasi aliekuwa kwenye wodi hiyo alisema chanzo cha kifo cha mtoto huyo ni huduma duni za matibabu zinazotolewa hospitalini hapo ambapo tangu mtoto huyo alipolazwa hakupatiwa matibabu hadi mauti yalipomkuta.
Akizungumzia tukio hilo, Mganga mfawidhi wa Hospitali hiyo Dr. Nelson Bukuru, alithibitisha kumpokea mtoto huyo saa 7 mchana juzi akisumbuliwa na homa ya mapafu lakini kutokana na uhaba wa dawa za kutibu ugonjwa huo walilazimika kumlaza wodi ya watoto ili taratibu za kupata dawa za kutibu ugonjwa huo zikifanyika. Alisema kabla ya kupatikana kwa dawa hizo mgonjwa alifariki dunia akiwa amelazwa wodini chini ya uangalizi wa wazazi wake na katika hali ya kusikitisha kulipopambazuka walikuta mwanamke huyo akiwa amejinyonga na kuning'inia juu ya mti ulio ndani ya Hospitali hiyo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita Leonard Paul alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba Jeshi la Polisi bado linaendelea na uchunguzi..

Source: Mwananchi

Mytake..

Moja ya sababu za msingi za madaktari kugoma ni ukosefu wa vitendea kazi na dawa mahospitalini.. Mgonjwa mmoja zaidi amefariki kutokana na kukosekana dawa na kupelekea mzazi wake mwenye uchungu kuamua kujinyonga.. Hawa ni wawili tu kati ya wagonjwa wengi wanaopoteza maisha kutokana na siasa kuingiliana na utendaji.. Mungu awapumzishe kwa amani huko waliko..
 
Tunatakiwa kujua kama huyo mama pia hakuwa mgonjwa wa akili!
 
Tunatakiwa kujua kama huyo mama pia hakuwa mgonjwa wa akili!

Mgonjwa wa akili ndiyo awe na uchungu na mwanae kiasi hicho? Napata wasi wasi na wewe mwenyewe. We unaona ni sawa mgonjwa kufa kwa kukosekana dawa hospitalini?
 
Tunatakiwa kujua kama huyo mama pia hakuwa mgonjwa wa akili!

Angekataa mtoto asipewe dawa ili kumtibu tatizo lake tungesema anamatatizo ya akili, inaelekea wewe huna mtoto hivyo ujui uchungu unaoweza kumpelekea mzazi kufanya hivi. Siku nyingine usitoe comment ya namna hii, unazidisha uchungu kwa watu wanaoyaona mapungufu yanayohepukika. Tumezoea kusema kila kifo ni mapenzi ya Mungu, ila kwa jinsi huduma zetu mahospitalini tumekuwa tukimsingizia sana Mungu. Vifo vingi sana vinaweza kuhepukika kama jitihada kidogo tu zingefanyika. Mungu Ibariki Tanzania.
 
Hii ndo CCM bhana unacheza kama bip sena dawa sh ngapi tukupe hela ukatuletee
 
nakumbuka Misri mmoja alianza kwa kujichoma moto... sijui kwa TZ yetu..lakini hali ni mbaya!!madai ya msingi ya madaktari kuachwa na vivyo hivyo kwa waalimu.
 
Ajinyonga baada ya kufiwa na mtoto Send to a friend
Gazeto la Mwananchi Thursday, 02 August 2012 21:00


Salum Maige,Geita
MWANAMKE aliyefahamika kwa jina la Monika Mapoli[22],Mkazi wa Kijiji cha Isima kata ya Butundwe wilayani Geita, amekutwa amejinyonga juzi kwa kutumia kipande cha nguo karibu na Ofisi ya Mganga Mkuu Wilaya ya Geita.

Taarifa za mashuhuda wa tukio hilo zilisema kuwa Mapoli alichukua uamuzi huo baada ya kufiwa na mtoto wake Jumanne Philimo(2) aliyekuwa amelazwa wodi namba moja katika Hospitali ya Wilaya ya Geita akipatiwa matibabu.

Ilielezwa kuwa baada ya mtoto huyo kufariki dunia,mama huyo alitoweka wodini na kwenda kusikojulikana hadi alipokutwa amejining’iniza kwenye mti uliopo jirani na Ofisi ya Mganga Mkuu wa wilaya hiyo Dk Omari Dihenga.

Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo Petro Majiasi aliyekuwa kwenye wodi hiyo alisema chanzo cha kifo cha mtoto huyo ni huduma duni za matibabu zinazotolewa hospitalini hapo ambapo tangu mtoto huyo alipolazwa hakupatiwa matibabu hadi mauti yalipomkuta.

Akizungumzia tukio hilo, Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Dk.Nelson Bukuru, alithibisha kumpokea mtoto huyo saa 7 mchana juzi akisumbuliwa na homa ya mapafu lakini kutokana na uhaba wa dawa za kutibu ugonjwa huo walilazimika kumlaza wodi ya watoto ili taratibu za kupata dawa ya ugonjwa huo zikifanyika
.

Alisema kabla ya kupatikana kwa dawa hizo mgonjwa alifariki dunia akiwa amelazwa wodini chini ya uangalizi wa wazazi wake na katika hali ya kusikitisha kulipopambazuka walikuta mwanamke huyo akiwa amejinyonga na kuning’inia juu ya mti ulio ndani ya hospitali hiyo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita Leonard Paul alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi ili kubaini chanzo.


 
Tunatakiwa kujua kama huyo mama pia hakuwa mgonjwa wa akili!
yawezekana alikuwa mgonjwa wa akili lakini kilicho trigger condition yake ni hayo hapo yaliyotajwa.au tuseme na yeye alikosa dawa za kichaa
 
mgonjwa wa akili mama yako full stop.. kama burn nipate angekuwa dada yako ungesema akapimwe akili shame on u 0713 wako.

Kwanza nikuombe samahani kama comment yangu imekuudhi. Lakini pia sio vibaya kuheshimu mtazamo wa watu wengine. Watu wote hatuwezi kuwa na tafsii moja katika kila jambo. For sure, tukio linasikitisha ingawa huhitaji kuwa na darubini kuona kuwa kuna factors nyingi zinazoweza kuchangia kifo au kujinyonga kwake mbali na huduma mbovu katika hospitali zetu
 
Kwanza nikuombe samahani kama comment yangu imekuudhi. Lakini pia sio vibaya kuheshimu mtazamo wa watu wengine. Watu wote hatuwezi kuwa na tafsii moja katika kila jambo. For sure, tukio linasikitisha ingawa huhitaji kuwa na darubini kuona kuwa kuna factors nyingi zinazoweza kuchangia kifo au kujinyonga kwake mbali na huduma mbovu katika hospitali zetu
very sorry mkuu ni hasira nimeumia na comment yako but ulivyonijibu kiupole nimeumia.. sorry ndugu..plz.
 
very sorry mkuu ni hasira nimeumia na comment yako but ulivyonijibu kiupole nimeumia.. sorry ndugu..plz.

Maliyamungu, hukukosea sana kupresent hisia zako. Ndio maana pia nimeheshimu wale wote waliotofautiana na content niliyoiandika. Najua it was too short to emphasize my intention. Wote tunauchungu na jinsi nchi yetu inavyoendeshwa. Nitakuwa Mtanzania wa ajabu kama siko sensitive kiasi hicho.
 
Back
Top Bottom