Ukosefu wa ladha ya lugha ya Kiswahili kwenye mapenzi

Shukran snowhite. Mashallah nipatapo siha njema sifa zikuendee mwalimu wangu, mi bawabu tu ila tende naitia mdomoni hamad imekuwa halua! Alhamdulillah! Pema........ukipema si ........

pema usijapo pema ukipema si pema tena japo haraka haraka haina baraka nayo ngoja ngoja yaumiza tumbo ilhali subira yavuta kheri huku chelewa chelewa utakuta mwana si wako!
halula!
 
Ha ha ha, usinifanye nikakopi nikajidai nimetunga mwenyewe

Hili shairi liko kimahaba zaidi, sema watu tumekipuuza kiswahili, nacho kimetuacha
Sasa tunarudi kukilaumu

Sasa hivi kizazi cha leo, hata kuzingatia mizani na vina kwenye ushairi ni ndoto, sababu ya uchache wa misamiati tunayoijua.

Kiswahili ukikijua kinanoga hasa. Na ndo unakuwa kama Dr.Riwa ukiambiwa kwa Kiingereza unaona fake.

Tatizo la siku hizi utandawazi umechukua nafasi ya kila kitu. Watu walikuwa wakitumiana mashairi ya Kiswahili katika kutafutana uchumba, siku hizi tunamtafuta Adele sijui Rhianna!

Watu walikuwa wazuri wa kueleza hisia zao hasa za mapenzi kwenye tungo.......mcheki huyu anaelalamika. Hata ukimaliza kumsikiliza lazima umfikirie namna ya kumkubali maana inaendana na mazingira ya kikwetu zaidi



Si kitu kunipuuza, kwako tamaa sikati
Fikira sitogeuza, moyo wangu madhubuti
Nilani utavyoweza, lakini sikubanduki

Wajua nnakupenda, ndo mana waniringia
Unanifanyia inda, mapenzi kunisusia
Baada ya hichi kidonda, na moto unanitia

Nikimbie japo mwaka, nipo ninakungojea
Ukirudi nakutaka, wala sitoona haya
Kukupenda sitochoka, japo ukinizomea
 
chai ya mkandaa ni chai ya mkono mmoja!

Waoh, nisingefikiria huko kabisa. Duh, asante mwalimu!

So 'mkandaa' maana yake nini exactly, wapi tena naweza tumia hilo neno?
Naweza sema wali wa mkandaa nikimaanisha wali usio na mboga?
 
Kiswahili ukikijua kinanoga hasa. Na ndo unakuwa kama Dr.Riwa ukiambiwa kwa Kiingereza unaona fake.

Tatizo la siku hizi utandawazi umechukua nafasi ya kila kitu. Watu walikuwa wakitumiana mashairi ya Kiswahili katika kutafutana uchumba, siku hizi tunamtafuta Adele sijui Rhianna!

Watu walikuwa wazuri wa kueleza hisia zao hasa za mapenzi kwenye tungo.......mcheki huyu anaelalamika. Hata ukimaliza kumsikiliza lazima umfikirie namna ya kumkubali maana inaendana na mazingira ya kikwetu zaidi



Si kitu kunipuuza, kwako tamaa sikati
Fikira sitogeuza, moyo wangu madhubuti
Nilani utavyoweza, lakini sikubanduki

Wajua nnakupenda, ndo mana waniringia
Unanifanyia inda, mapenzi kunisusia
Baada ya hichi kidonda, na moto unanitia

Nikimbie japo mwaka, nipo ninakungojea
Ukirudi nakutaka, wala sitoona haya
Kukupenda sitochoka, japo ukinizomea

Walah, asingekuwa memba wa JF, hii kitu ningeiba (with your permission ofcourse) na kumtumia mupenzi wangu, ningepataje maujiko! LOL
 
Kwa kweli kuna kitu kinatakiwa kufanyika tena kwa jitihada za makusudi
Kiswahili kisipopewa kipaumbele kitakwisha kabisa

Nakumbuka nikiwa darasa la saba ilikuwa tunafundishwa ushairi na kuandika
Sijui kama hii bado ipo shuleni siku hizi

Kiswahili ukikijua kinanoga hasa. Na ndo unakuwa kama Dr.Riwa ukiambiwa kwa Kiingereza unaona fake.

Tatizo la siku hizi utandawazi umechukua nafasi ya kila kitu. Watu walikuwa wakitumiana mashairi ya Kiswahili katika kutafutana uchumba, siku hizi tunamtafuta Adele sijui Rhianna!

Watu walikuwa wazuri wa kueleza hisia zao hasa za mapenzi kwenye tungo.......mcheki huyu anaelalamika. Hata ukimaliza kumsikiliza lazima umfikirie namna ya kumkubali maana inaendana na mazingira ya kikwetu zaidi



Si kitu kunipuuza, kwako tamaa sikati
Fikira sitogeuza, moyo wangu madhubuti
Nilani utavyoweza, lakini sikubanduki

Wajua nnakupenda, ndo mana waniringia
Unanifanyia inda, mapenzi kunisusia
Baada ya hichi kidonda, na moto unanitia

Nikimbie japo mwaka, nipo ninakungojea
Ukirudi nakutaka, wala sitoona haya
Kukupenda sitochoka, japo ukinizomea
 
Waoh, nisingefikiria huko kabisa. Duh, asante mwalimu!

So 'mkandaa' maana yake nini exactly, wapi tena naweza tumia hilo neno?
Naweza sema wali wa mkandaa nikimaanisha wali usio na mboga?

Mkandaa kwa maana ya moja kwa moja ni mti aina ya mkoko ambao majani yake yanatumiwa kupikia chai.

Chai yake inakuwa ile watu wengine wanaita "chai ya rangi"......yaani ya kahawia iliyokuwa haijaongezwa maziwa (japo inaweza kuwa imeongezwa viungo kama tangawizi, hiliki, mdalasini)

Kwa hiyo, neno mkandaa ni mahsusi kwa chai na huwezi kulitumia kwa chakula chengine chochote ila unaweza kulitumia wakati unapofananisha vitu vyengine na chai hiyo
 
Walah, asingekuwa memba wa JF, hii kitu ningeiba (with your permission ofcourse) na kumtumia mupenzi wangu, ningepataje maujiko! LOL

Hahaha, umekubali kuwa ya Kiswahili yananoga eee! :pound:

Ila unaruhusiwa kuyabeba juu kwa juu ni tungo iliyopo kwenye nyimbo moja wapo ya taarab iliyoimbwa kabla sie hatujazaliwa!
 
manta khofu!
mahamri ntayatia tui bubu na mkate wa bafta pembeni vipi?utafaa?
kisha ntakuandalia mkekani juu nimefunika kawa yenye rangi ya samawati
halafu nakukosha mikono kisha nikukaribishe ,ukishamaliza ntakupa maji ya sharbat yenye barafu kidogo na limao kuhanikiza hirmu!

Yaani hapo nilicho elewa ni hayo kwenye bold tu, mengine yote ni 0.
 
Mkandaa kwa maana ya moja kwa moja ni mti aina ya mkoko ambao majani yake yanatumiwa kupikia chai.

Chai yake inakuwa ile watu wengine wanaita "chai ya rangi"......yaani ya kahawia iliyokuwa haijaongezwa maziwa (japo inaweza kuwa imeongezwa viungo kama tangawizi, hiliki, mdalasini)

Kwa hiyo, neno mkandaa ni mahsusi kwa chai na huwezi kulitumia kwa chakula chengine chochote ila unaweza kulitumia wakati unapofananisha vitu vyengine na chai hiyo

Thanks Gaijin, kwani nami nilifikiria ni one of the spices kumbe sikuwa mbaali saana!
 
Kwa kweli kuna kitu kinatakiwa kufanyika tena kwa jitihada za makusudi
Kiswahili kisipopewa kipaumbele kitakwisha kabisa

Nakumbuka nikiwa darasa la saba ilikuwa tunafundishwa ushairi na kuandika
Sijui kama hii bado ipo shuleni siku hizi

Hapo kwenye jitihada za makusudi, tusisubiri serikali, kwa sababu tushaona kuwa serikali hii haifanyi chochote.

Watu wengi zaidi wakionyesha shauku ya kutaka kukijua vizuri Kiswahili, basi naamini kitapiga hatua japo ndogo. Lazima kuwe na ari ya kuwa kama Mtanzania lazima Kiswahili nikijue
 
Tutaaongea biashara PM, ukinitumia shairi kama 3 hivi piemu lakini; mbona ndoa itakuwa within a month. LOL
umeona enh!mie tena kwako weye we lete tu nia mie nikufanyie mambo!navopenda kuchagua rangi za harusi mie!shurti chanikiwiti ichanganywe na rangi ya maji ya sharbati ya chungwa pamoja na zambarau au samawati!walahi tutapendezaaaje!
 
Yaani hapo nilicho elewa ni hayo kwenye bold tu, mengine yote ni 0.

ahhhhhhhhh pole maamii!huo ndo utamu wa kiswahili kunako mahaba mwali!
manta khofu ni usiwe na khofu
mahamri ni maandazi
mkate wa bafta huwa ni mlaini hivi una kuwa na ngano yako maalum
nitakuandikia maana yake nitakuandalia
samawati ni rangi ya bluu bahari
maji ya sharbati ni juice
kuhanikiza hirmu ni kukoleza harufu (nzuri)
 
ahhhhhhhhh pole maamii!huo ndo utamu wa kiswahili kunako mahaba mwali!
manta khofu ni usiwe na khofu
mahamri ni maandazi
mkate wa bafta huwa ni mlaini hivi una kuwa na ngano yako maalum
nitakuandikia maana yake nitakuandalia
samawati ni rangi ya bluu bahari
maji ya sharbati ni juice
kuhanikiza hirmu ni kukoleza harufu (nzuri)

Hicho sio kiarabu kweli? Asante mwaya ngoja niyakariri! LOL
 
Back
Top Bottom