Ukosefu wa ladha ya lugha ya Kiswahili kwenye mapenzi

Mimi hicho kiswahili cha wasemaga na hakunaga wala sikijui. Nina imani kiswahili changu kinatosha kufahamu yaandikwayo. Sisemi kama ina walakini bali haina ladha au hamasisho kwenye mapenzi nionavyo mimi, Maana kuna lugha nyingine ambazo zipo kimapenzi zaidi yaani yana sweets words kuliko kiswahili hapa simaanishi kizungu.

Kumbe unaongelea mambo ya imani? Kwamba una imani Kiswahili chako kinatosha kufahamu yaandikwayo?

Hata R. Kelly ana imani anaweza kuruka kama ndege, imani si kazi.

Nimekuuliza umesoma tenzi gani ukaiona ina mapungufu ya kukosa ladha? Hujanijibu.

Huwezi kuwa George Bernard Shaw, H.L Mencken au Edmund Wilson au hata mfungakamba za viatu vyao katika fasihi, wa kukisema Kiingereza kama hujasoma vitabu na kuweza kuchambua tenzi na riwaya. Vivo hivyo kwenye Kisahili na magwiji wake.

Nataka kuona hoja inayotokana na uchambuzi wa lugha, si maoni rejareja yanayotoka kwa watu ambaoa inaonekana wazi hata kutaja tenzi moja tu waliyosoma inawawawia vigumu.
 
Ni kweli lakini haya maneno yako kwa wachache tu tulio wengi tunajua darling, honey, i miss you n.k. Ule utamkwaji sio wote wanaojua

Umefanya utafiti upi mpaka unasema wachache ndio hutumia hicho kiswahili? Wanuka shombo wa UDSM na wenzao wa vyuoni, machangu na Bongo Movies ndio wanaotumia maneneno hayo kwa sana. Je hao wanafika zaidi ya nusu ya watanzania hadi useme wengi wetu?
 
Kiranga, povu la nini nimejibu nionavyo mimi kuhusu kiswahili na sio peke yangu ambao tunakubaliana na hili. Cha muhimu naona ni kujaribu kuheshimu hoja za watu, unasema kama vile kiswahili nimekuja kiona hapa JF.
 
Last edited by a moderator:
he he he, dah!
Sudusu ya sudusu? Ni neno la ukweli hili?

Kiukweli, kama mtu ana utajiri wa maneno ya kiswahili anaweza kutunga mashairi mazuri sana na watu wakayakubali.

Mfano ni Mwana FA, sio mzuri kihivyo kwa kiswahili, lakini ni kati ya wasanii wa kizazi kipya wanaokubalika kwa mashairi ya kiswahili hapa kwetu.

Je angewekuwa na misamiati hata sudusu ya sudusu?

Lugha hii ina ladha sana, kwanza mkiwa mnaongea kwa kiswahili halafu mtu anatumia 'i love u' au 'i miss u' inaweza ikaonekana usanii zaidi
Haswaa, precisely.

Watu Kiswahili hawakijui, msamiati hata sudusu ya sudusu hawajakimu ila haweshi kujivika uhakimu!

Ukiuliza tenzi za mapenzi walizoenzi unawatoa benzi!
 
Bora tu kunena kwa lugha maana kiswahili hola kingereza ndio usiseme!!!

Sasa hivi kuna hatari ya watu kutojua Kiswahili, Kiingereza wala lugha za makabila.

Halafu watu hawahawa wakalaumu kwamba Kiswahili hakina ladha.

Mie swali muhimu ninaloliona linazalishwa na mjadala huu ni hili la kwamba kwa nini watu hawapendi kujifunza Kiswahili?

Kuna sababu za kiuchumi/ utamaduni? Kuna sababu zilizoelemea zaidi kwenye watu kujazana mijini na kufanya lugha ikue kwa kuchukua muelekeo tofauti na "classic Swahili"?

Je ni sawa kuhalalisha matumizi mapya ya kina "tunasemaga" kwa kuzingatia lugha inatakiwa ikue "organic" au tuwe na polisi wa lugha kama walivyofanya Wafaransa na hawa wanaosema "tunasemaga" tuwapige faini kila wanapokosea (kifasihi).

Watu wasiojua tenzi waruhusiwe kusema Kiswahili hakina ladha kabla hata ya kukijua?
 
he he he, dah!
Sudusu ya sudusu? Ni neno la ukweli hili?

Kiukweli, kama mtu ana utajiri wa maneno ya kiswahili anaweza kutunga mashairi mazuri sana na watu wakayakubali.

Mfano ni Mwana FA, sio mzuri kihivyo kwa kiswahili, lakini ni kati ya wasanii wa kizazi kipya wanaokubalika kwa mashairi ya kiswahili hapa kwetu.

Je angewekuwa na misamiati hata sudusu ya sudusu?

Lugha hii ina ladha sana, kwanza mkiwa mnaongea kwa kiswahili halafu mtu anatumia 'i love u' au 'i miss u' inaweza ikaonekana usanii zaidi

Sudusu ni 1/6, sudusu ya sudusu ni 1/36. Nawasema hawa wasiojua msamiati wa Kiswahili hata kwa sehemu ya 1/36 nao wanajitutumua kukisema hakina ladha!

Soma tenzi maarufu utakutana na maneno kama hayo. Ndo maana nasisitiza kusoma Kiswahili kabla ya kukibeza.

Mtu anakandya Kiswahili huku hata hajawahi kuperuzi "Wasifu Wa Siti Binti Saad" nje ya shule, if at all !!!
 
Kiranga, huu ukuaji wa kiswahili wa sasa unatia hasira wakato mwingine.


Kuna tangazo moja la zantel wameweka barabara ya Ali Hasan Mwinyi, walivyoandika maneno huwa natamani niwe msimamizi wa kugha niwatie adabu kidogo.

Mzee kifimbo cheza wa gazeti la Sani inabidi aje mtaani.

Kuna kizazi hapa Tanzania kinaweza kisijue lugha fasaha hata moja
 
Last edited by a moderator:
Kiranga, povu la nini nimejibu nionavyo mimi kuhusu kiswahili na sio peke yangu ambao tunakubaliana na hili. Cha muhimu naona ni kujaribu kuheshimu hoja za watu, unasema kama vile kiswahili nimekuja kiona hapa JF.

Trust me, nikitoa povu hutaweza kujibu, hapo hata chafya ya kuitia madogoli ya "waungwana" bado.

Kama ulivyojibu uonavyo wewe, na mie ndo nilivyokosoa maoni yako kwamba yana walakini.Huwezi kujibu kwa ufasaha kabla ya kusoma. Hili ni jambo la msingi lisilopingika kama unaamini katika uchunguzi.

Mie kuijibu hoja yako tayari ni kuiheshimu. Ningeidharau nisingeijibu kabisa.
 
Movies.............watu wanaangalia za kiingereza, na kuiga ya kiingereza, huoni hata kunanihii watu wanafanya wayaonayo kwa movies.
Ni Movies, poor us

Mkuu u're deadly right..! Hizi movies na tamthilia za wazungu kila mahali ndio imekuwa sababu ya kuonekana maneno ya kiswahili hayana mvuto..! Maana tunayabeba ya kwao na kuyafanya yetu.. Maana hata huo utamkwaji wa hayo romantic words hata wenyewe wenye lugha yao hawaoni ndani..
Wanaotaka kujua jinci gani maneno ya kiswahili yamekaa kimahaba fanyeni mirejeo kwenye nyimbo za taarabu za akina Issa Matona.. Juma Balo.. Bi Shakila na wengineo wa zamani.. Kule mtacikia maneno ya kiswahili yenye mvuto kuliko hata hiyo English yenu..
 
Mkuu u're deadly right..! Hizi movies na tamthilia za wazungu kila mahali ndio imekuwa sababu ya kuonekana maneno ya kiswahili hayana mvuto..! Maana tunayabeba ya kwao na kuyafanya yetu.. Maana hata huo utamkwaji wa hayo romantic words hata wenyewe wenye lugha yao hawaoni ndani..
Wanaotaka kujua jinci gani maneno ya kiswahili yamekaa kimahaba fanyeni mirejeo kwenye nyimbo za taarabu za akina Issa Matona.. Juma Balo.. Bi Shakila na wengineo wa zamani.. Kule mtacikia maneno ya kiswahili yenye mvuto kuliko hata hiyo English yenu..

Tatizo ni msingi tuliopewa wa kujua lugha hii ya kiswahili. Kiswahili cha watu wa pwani ni tofauti na kiswahili cha msukuma au watu wa kaskazini. Lugha yetu imekuwa ngumu maneno ya misamiati ni adimu kuyaona labda uwe na kamusi.
 
kiswahili cha pwani na msukuma hivi kamusi tofauti??

Sasa kama kiswahili cha pwani tu tabu, je inglish ya huko mbali ilokuja kwa meli?

Tatizo ni msingi tuliopewa wa kujua lugha hii ya kiswahili. Kiswahili cha watu wa pwani ni tofauti na kiswahili cha msukuma au watu wa kaskazini. Lugha yetu imekuwa ngumu maneno ya misamiati ni adimu kuyaona labda uwe na kamusi.
 
Cause Swahili is not a romance language. On second thought what exactly is a romance language ie lugha ya mahaba?
 
Mimi mtu akiniambia ananipenda nai-feel zaidi kuliko akiniambia I love you........that's me.
maneno mengi ya kuzungu naona yamekaa kiwizi zaidi........

Wanasaikolojia wanasema kwamba maneno kama hayo yakisemwa kwa lugha ya kwanza yana uzito wa zaidi ya pale yatakaposemwa kwa lugha uliyojifunza ukubwani.
 
Cause Swahili is not a romance language. On second thought what exactly is a romance language ie lugha ya mahaba?

I take a special interest in the etymology of words and inter pollination of indo-european languages.

Ukisoma mzizi wa neno "romance" utagundua limetokana na Romans.

Kuamini kwamba kiswahili si lugha ya mahaba ni kukubali kuwa brainwashed kwamba utanashati wa kimapenzi umeanzia Roma na wahenga wake na ni lazima ufuatilie formula za magharibi. Hata kama sie hatum "miss" mtu kwa sababu ya cosmogony yetu, tunamfikiria tu, itabidi tuanze kujiuliza neno la kum-miss mtu (ambalo halipo, kwani tuna miss -in this context- vitu, sio watu, kwa watu utamaduni wetu una a spiritual mundane tradition ambayo kum-miss mtu hakuruhusiki, tunaweza kumfikiria tu)

Na kwamba Waswahili na wahenga wao hawakujua mapenzi kwa sababu hawachumiani maua February 14, hata kama wanaamini maua sehemu yake ni bustanini kwa mujibu wa mila zao.
 
Back
Top Bottom