Ukosefu wa dawa hospitalini = Serikali imefilisika?

QUALITY

JF-Expert Member
Sep 27, 2010
853
115
Wapendwa wana JF,

Ninayo masikitiko makubwa kuwataarifu kuwa jana nilifanya utafiti mdogo wa hali ya upatikanaji wa dawa katika hospitali zetu za umma. Hospitali za serikali Kyela, Rungwe, Kinondoni, Temeke na Ilala, zaidi ya 70% hazikuwa na dawa.

Nilienda hospitali iliyoko manispaa ya temeke physically iitwayo vijibweni ambapo hawakuwa na hata panado, hawana drip hata moja, dawa za malaria (mseto) hakuna, gloves hakuna, vifaa vya kujifungulia (kule matenity ward) hakuna!

Nikaondoka nikaenda kituo cha afya cha Kigamboni karibu na kituo cha polisi. hawana dawa yoyote. wanacoweza kufanya ni kukuandikia karatasi tu na kukutuma uende kutafuta dawa mahali popote. Kwa taarifa yak0 hata vyeti (printed cards) hakuna kwa hiyo wanakata makaratasi ya kawaida ndiyo wanayotumia kuandikia.

Nikatoka hadi hospitali ya Ilala, hakukuwa na dawa.

swali: Je hii si dalili kuwa serikali yetu imefirisika?
karibu kwa critical thinking

Quality
 
Mkuu hilo ni la kweli juzi tulikuwa na mgonjwa temeke hosp hatuweza kupata hata hiyo panadol hali inatisha !
 
hamna dawa mkuu.utafiti wako upo sahihi.mi nimeenda pale kurasini hospital ya polisi pale baracks hawana dawa kabisa.wanakuandikia uendekununua mtaani.mtaani unakutana na madawa feki.safari hii tutakoma.mia
 
Wapendwa wana JF,

Ninayo masikitiko makubwa kuwataarifu kuwa jana nilifanya utafiti mdogo wa hali ya upatikanaji wa dawa katika hospitali zetu za umma. Hospitali za serikali Kyela, Rungwe, Kinondoni, Temeke na Ilala, zaidi ya 70% hazikuwa na dawa.

Nilienda hospitali iliyoko manispaa ya temeke physically iitwayo vijibweni ambapo hawakuwa na hata panado, hawana drip hata moja, dawa za malaria (mseto) hakuna, gloves hakuna, vifaa vya kujifungulia (kule matenity ward) hakuna!

Nikaondoka nikaenda kituo cha afya cha Kigamboni karibu na kituo cha polisi. hawana dawa yoyote. wanacoweza kufanya ni kukuandikia karatasi tu na kukutuma uende kutafuta dawa mahali popote. Kwa taarifa yak0 hata vyeti (printed cards) hakuna kwa hiyo wanakata makaratasi ya kawaida ndiyo wanayotumia kuandikia.

Nikatoka hadi hospitali ya Ilala, hakukuwa na dawa.

swali: Je hii si dalili kuwa serikali yetu imefirisika?
karibu kwa critical thinking

Quality

Utafiti wako ni batili, mimi nipo MSD Dodoma.
 
Utafiti wako ni batili, mimi nipo MSD Dodoma.

tuwekee picha hapa na utoe maelezo ya kusema utafiti ni batili.msd dar wanalia itakuwa huko dom.na wewe kuwepo msd dodoma sio kigezo cha kupatikana kwa dawa au wewe kuwepo huko kuna uhusiano gani na uwepo au ukosefu wa madawa?.hata ungesema upo msd makao makuu.mia
 
tuwekee picha hapa na utoe maelezo ya kusema utafiti ni batili.msd dar wanalia itakuwa huko dom.na wewe kuwepo msd dodoma sio kigezo cha kupatikana kwa dawa au wewe kuwepo huko kuna uhusiano gani na uwepo au ukosefu wa madawa?.hata ungesema upo msd makao makuu.mia

mkuu alijua mtatishika labda.. hivi kwanini hospitali nyingi mbele yake yaani kwenye milango mikuu kuna kuwa na maduka ya dawa sio ndio ile janja ya nyani..
 
Utafiti wako ni batili, mimi nipo MSD Dodoma.

Sasa naelewa kwa MSD wanachemsha...kumbe mmeja akina Mwita huko (utani huu umekaa kisiasa zaidi na sio kitaaluma!)..

Pamoja na serikali kutokidhi mahitaji ya dawa kwa kila mtanzania...lakini nadhani kuna tatizo kubwa pale MSD, kubwa sana! Kuan kipindi nilikuwa na wafadhili katika vita dhidi ya malaria kwa kina mama wajawazito, tukapitia vituo kadhaa vya huduma za afya vya serikali Morogoro vijijini, hakukuwa hata na SP tu kwa ajili ya IPTp. Wafadhili wale wakajitolea wanunue dawa kibao (SP ni cheap sana), kasheshe tulipofika wizara ya afya wakatuuliza kwani mmeambiwa hatuna SP? Wakatupeleka MSD central store...SP zimejaa tani kwa tani...wakati mama zetu/wake zetu/dada zetu wanakufa kwa malaria in pregnancy! Mwita, play your part...acha kuchonga tuu kuhusu Chadema hapa JF kazi hamtaki kufanya!
 
Utafiti wako ni batili, mimi nipo MSD Dodoma.

MSD siyo hospitali. Kama mna dawa katika stoo zenu, wagonjwa waanakufa mahosptalini, basi ninyi hamfai. Bahati nzuri wengi waliofika katika hospitali zote hawakupata dawa. hata drip moja hakuna!!!!!!!
 
Sasa naelewa kwa MSD wanachemsha...kumbe mmeja akina Mwita huko (utani huu umekaa kisiasa zaidi na sio kitaaluma!)..

Pamoja na serikali kutokidhi mahitaji ya dawa kwa kila mtanzania...lakini nadhani kuna tatizo kubwa pale MSD, kubwa sana! Kuan kipindi nilikuwa na wafadhili katika vita dhidi ya malaria kwa kina mama wajawazito, tukapitia vituo kadhaa vya huduma za afya vya serikali Morogoro vijijini, hakukuwa hata na SP tu kwa ajili ya IPTp. Wafadhili wale wakajitolea wanunue dawa kibao (SP ni cheap sana), kasheshe tulipofika wizara ya afya wakatuuliza kwani mmeambiwa hatuna SP? Wakatupeleka MSD central store...SP zimejaa tani kwa tani...wakati mama zetu/wake zetu/dada zetu wanakufa kwa malaria in pregnancy! Mwita, play your part...acha kuchonga tuu kuhusu Chadema hapa JF kazi hamtaki kufanya!

Wamezidi longo longo. Wanafurahia kuwepo kwa dawa MSD hadi zitaexpire!
 
Wapendwa wana JF,

Ninayo masikitiko makubwa kuwataarifu kuwa jana nilifanya utafiti mdogo wa hali ya upatikanaji wa dawa katika hospitali zetu za umma. Hospitali za serikali Kyela, Rungwe, Kinondoni, Temeke na Ilala, zaidi ya 70% hazikuwa na dawa.

Nilienda hospitali iliyoko manispaa ya temeke physically iitwayo vijibweni ambapo hawakuwa na hata panado, hawana drip hata moja, dawa za malaria (mseto) hakuna, gloves hakuna, vifaa vya kujifungulia (kule matenity ward) hakuna!

Nikaondoka nikaenda kituo cha afya cha Kigamboni karibu na kituo cha polisi. hawana dawa yoyote. wanacoweza kufanya ni kukuandikia karatasi tu na kukutuma uende kutafuta dawa mahali popote. Kwa taarifa yak0 hata vyeti (printed cards) hakuna kwa hiyo wanakata makaratasi ya kawaida ndiyo wanayotumia kuandikia.

Nikatoka hadi hospitali ya Ilala, hakukuwa na dawa.

swali: Je hii si dalili kuwa serikali yetu imefirisika?
karibu kwa critical thinking

Quality
Sasa kama Serikali imeshindwa kuziendeleza hizo Hospitali kwanini wasiwape watu Binafsi waka ziendeleza hizo Hospitali? Jamani Serikali inawauwa watu wake kidogo kidogo, bora waseme tu hospitali za bure hakuna kuna hospitali za kulipia tujuwe kuwa Serikali imeshindwa kuwahudumia wananchi wake ahhhh jamani tutafika kule tunakokwenda?
 
Back
Top Bottom