Ukosefu wa ajira kwa Vijana: Lowassa atabiri vita Tanzania...

Kuna mkutano moja wa kimataifa ulifanyika na kuhudhuriwa na wawakilishi wa wizara ya kazi. Jamaa walikuwa wanawakilishi matokeo ya utafiti wao nikawa napigwa butwaa na findings zao. Jumla ya vijana wanaomaliza shule kuanzia primary, secondary na vyuo vikuu only 3% of the population ndio wanaajiriwa kila mwaka. Inamaanisha 97% YA VIJANA HAWANA KAZI Hii figure ni hatari sana na inatisha. Hebu jisomee mwenyewe power point presentation ya watafiti hao katika link hapo chini.

http://info.worldbank.org/etools/docs/library/135839/Tanzania.pdf

Tanzania kazi za kufanya zipo, nafasi za kazi zipo (zipo zinazotumilka na zipo zilizolala tu), nafasi za ajira zipo ila hazifikiki. Kwa hiyo tatizo ni sera, ndio maana kuna ukosefu wa ajira na kazi kwa watanzania wengi vijana. Hapa ndipo pa kutumia akili, hili tatizo linawezekana kabisa kupunguzwa kwa kiasi kikubwa kama sio kuliondoa kabisa. Bahati mbaya hadi sasa mheshimiwa anasema tu kuna tatizo na halina budi kutatuliwa, labda kwake ni mapema muno kusema litatuliweje (anaficha sera?)
 
With the picture painted by an overwhelming reactions to this thread, it is undeniable that Lowassa is in line of succeeding JK. In Tanzanian politics, it is always difficult to anticipate who will become who in the future. Matters turn worse after seeing that very same clerics who once severely condemned Lowassa over Richmond scandal are now exploited to clear him. This is just validating a common statement that politics is ''inscrutable dirty game''
 
Msanii huyu Mkuu kanuia kwamba ni lazima amalize awamu yake. Hajali kabisa nchi itakuwa katika hali gani hapo atakapomaliza awamu yake 2015.

Halafu kinachoudhi zaidi ni kwamba ni kama vile ameziba masikio kabisa hasikii malalamiko ya Watanzania kuhusu hali mbaya ya nchi yetu.
 
Huyu jamaa anachokochoko,mbona alipokuwa waziri hatukusikia hizi ngonjera sasa yupo nje ndio anaona? au anataka kusema viongozi waliokuwepo hawana uwezo wa create ajira mpya bila yeye, haya JK jibu na hilo.
 
Labda tutambue wakati wa serikali ya Sumaye tatizo la ajira lilikuwaje,ilipokuja serikali ya Lowasa lilipungua?Now Pinda Limeongezeka?LOWASA Anatafuta sababu,alifanya nini kucreate ajira?

Hali ilivyo inahitaji BUSARA zaidi ya kusema ukweli!

Lowasa ni tatizo kubwa sana katika jamii ya kitanzania kuliko hata kikwete!

Naafiki!

Huyu kaamua atoke na issue ya vijana anadhani itampeleka ikulu kweli watanzania tunayo kazi sitarajii huyu jamaa kuungwa mkono na vijana maana ameshiriki kuwatesa na sasa anataka kuwatumia atimize malengo yake

Lowasa anatumia AKILI lakini hana BUSARA! Ameongea ukweli usio na Busara hata kidogo!! Kuujua ukweli si issue ..hata yeye can not handle what he pointed and expressed so well ..This make the matter even worse..cause he is worse naturally!!

Ajira kwa vijan kwani yeye ndo kaona tatizo leo? Ninavyofaham yeye kama mwkilishi wa wananchi ameishauri nini serikari au hata raisi rafiki yake. Nothing wizi tu... What a prezda fisad aiyekuwa na aibu. With me mchango wake tumeupokea but for u prezda ashindwe kwa jina la yesu

... Naafiki .. Mchango upokelewe ... na Yesu afanye vitu vyake on this issue!!

Yes, Man Made Money and, in turn, Money Made Man Mad! Kama poor peasants wanavyokiwezesha Chama Cha Magamba kuendelea kuwa madarakani kwa pupewa kofia, kanga, fulana, na ubwabwa, ndicho hiki tunaanza kukiona kwa Kanisa Katoliki (kanisa lenye heshima kubwa duniani) kutaka kutumiwa kama kondomu kwa sababu ya "Money"!!!! Kanisa Katoloki limegeuka kuwa kichaa. Shame on you!!!

... Siamini wala sioni nianzie wapi ...kuona ..kanisa ..litumike kupitishia ukweli mkubwa kama huo ..lakini usio na busara ..na hata mtoa mada mwenyewe knows kwamba ..cant change that truth!! ..Smart, clever BUT NOT Intelligent ...and this is really SHAMEFUL!!

Hatudanganyiki!!!

... I also tend to believe so!! Time and space wont allow kudanganyika any longer!!

Watanzania tuwe macho na hili fisadi papa!

Hii ni muhimu sana!! ... Nafikiri itatekelezwa!!

Kuwa na AKILI bila busara za UTU na UBINADAMU ... Ni Tatizo linaloikuba dunia yote kwa kasi ya haraka! Lakini viongozi wote NGULI wenye akili nyingi sana lakini wasio na utekelezaji kwenye nyaja ya UTU na UBINADAMU wanapukutika na kuangamia kwa AIBU na kasi ya Ajabu. Kuwa na AKILI za kutosha kunaweza kukupatia PhD! Lakini si lazima Uwe na UTU na UBINADAMU kwakuwa unaakili inayoweza kundika mtihani wa PhD!

Iko hivi Baba mwenye PhD , anayewahi kufika nyumbani akala chakula cha watoto, akanawa akawa wa kwanza kupanada kitandani wa kwanza kulala huko anakoroma na watoto wakarudi nyumbani wakakosa chakula na kulia kwa mayowe kama wale vijana wa Mbeya...hakumuondolei Baba huyo PhD Yake kwani ganda bado liko ukutani. Hakumfanyi Dingi Kutokuwa na AKILI. Lakini UTU na UBINDAMU wake Bure kabisaa! Akili ya Phd 100% na Utu na ubindamu 0%. Hafai kuwa Baba,hafai kuwa kiogozi, mbunge waziri wala Rais!

Mawaziri wangapi ndani ya baraza wana PhD na akili nyingi sana? Dosens.. Wanakula chakula cha watoto kivipi? Wanasaini mikatataba mibovu ...wawekezaji wanapata faida ya 100% kwa mika 100 ijayo na Yeye mwenye PhD na Akili nyigi sana ..anapewa RV 4 new model 2. Moja ya Mkewe na Moja ya Kwake. Kwani hiyo inamuodolea Phd Yake ? No! Akili Mingi ...Utu/Ubindamu..0%

Lowasa ametumia Akili yake vizuri sana hapo kanisani kuuweka hadharani ukweli mkubwa sana! Hilo halinipi tatizo ... Vipi kuhusu chakula cha watoto wazalendo wananchi wa kitanzania? Utu na Ubinadamu wake ndio unasukuma na kuipa akili, fikra na matendo mwelekeo wa anachokifanya! Mwelekeo wa KIUTU ambao ndio chimbuko la Taifa liitwalo Tanzania. Utanzania ni UTU, Utanzania ni Ubinadamu na asiye na sifa hizo za KIUUNGU na akae kando kwenye kuutafuta UONGOZI waTaifa hili. Kwani HIZI NI ENZI MPYA!!!
 
Hawa ccm wasitufanyie kaujanja ujanja ili kutupumbaza WATANZANIA
kazi yao ni kutumia polisi kupiga risasi za moto raia
kwa maana hiyo vita tayari kati ya polisi na raia wema
LOWASSA ni jeuri
 
Invisible, Watanzania ni watu wa ajabu sana na naweza kukuhakikishia hakuna msafi. Hivyo Lowassa hana tofauti na watanzania wengi. Rostam na Lowassa wametukanwa mafisadi lakini Symbion inamezewa mate. Akina Mwakyembe wanajiita wapambanaji lakini wakipewa uwaziri huwasikii tena. Chadema wanajifanya wapambanaji wa ufisadi lakini wao ndio wa kwanza kupeleka muswada bungeni wa kuomba maposho zaidi. Waadilifu ni wachache sana Tanzania kila mmoja ni mchumia tumbo tu usijiumize kichwa mkuu. Tumejaa unafiki na uongo ndio maana tunadharaulika na hata majirani zetu na jumuiya ya kimataifa.
...Nilitaka kuuliza, nikaacha, ngoja niulize. Hivi, katika woooote wanaomwandama PM. Lowasa kuwa ni fisadi, nani kati yao si fisadi. Wengi wao ni mafisadi wakubwa kabisa.

...Heri nusu shari, kuliko shari kamili.
 
Hiki kipande ni kwa mujibu wa World Bank...Yani nusu ya wananchi wa Tanzania ni miaka 15 ama chini...Tuliona picha za kule Mbeya jinsi ambavyo asilimia kubwa ya waliokuwa front lines na chupa za maji nk ni vijana wenye kati ya umri huo...

Kuanzia sasa,na miaka mitano ijayo pandora box litafunguka na mshike mshike lazima iwepo given un equal distribution of wealth.Tena huku serikali ikimilikiwa na watu binafsi...Tuombe uzima mtaona...Hizi ni data za 2010!

Halafu kingine cha ajabu sijawahi kuona unemployement rate ya Tanzania...Economy indicator ya muhimu tu ambayo sisi hatuaitambui.

jmushi1 umeongea kitu cha maana sana, katika serikali inayoongozwa na self serving people ambao wao kimbilio lao ni kutumia dola huwezi ona wanatoa data zinazowaweka kitanzini. Vingozi wa nchi makini huwa wanaangalia future generation sisi wetu wanaangalia own current benefits. Huwezi kujenga taifa imara kama viongozi hawana uwezo wa kufikiri matokeo ya watu kukosa ajira. Obama halali anahangaika na kuongeza ajira japo anakutana na vikwazo vya kisiasa sisi viongozi wetu ndiyo kwanza wanakula bata.

Hili bomu wasomi makini kama akina Suleiman Ngware waliliona siku nyingi sana kuwa huwezi salimika kama unasomesha watu ambao ajira zao hujui zitatoka wapi. Kwa mtu yeyote mwenye akili kwa sasa IKULU si mahali pa kukimbilia hata kidogo, ni dhahiri bomu hili kama halijamlipukia JK basi ajaye ni lazima limlipukie. Kuna mambo ambayo JK anaweza kuyafanya yakaiokoa nchi na jambo kuu kwa sasa ni kuacha mchakato wa katiba ufanywe na wananchi ili tuwe na uhuru wa kuwaweka na kuwatoa viongozi wanaoonekana hawafai. Ila kama lengo ni kulinda masilahi ya CCM basi n dhahiri kuwa ukosefu wa ajira + wananchi kulazimishwa kuwekewa vingozi ambao hawakuwachagua kutaongeza kasi ya moto huu.

Nchi kama marekani pasipokuwa na uhuru wa kuchagua viongozi wao na kuwatosa wale wasio wataka haitawaliki kabisa kwa jinsi ilivyo na mgawanyiko, japo wao employment rate yao ni sawa na unemployment rate yetu (yaani 91% employed in USA, 91% unemployed in Tanzania)
 
Jumapili ya tar.20.11.atafanya harambee Makambako mtaa wa Mjimwema.Tunasubiri hayo mamilioni.Wikina!
 
itanoga wiki nzima, Nape atakapokilinda chama dhidi ya kauli hii ya E.L

huku Wasira aki-defend serikali kwa upande mwingine

watoto wa uvccm(na riz-1) wakimlinda baba wa rafiki yao
 
Namuunga mkono Lowassa kwa alichokisema(tatizo la ajira kwa vjana) walau aliwahi ibua wazo la kutiririsha maji toka ziwa victoria to as far as Dodoma kuwezesha kilimo cha umwagiliaji, that could have been an employment! kubwa tu kwa mikoa ambayo maji yangepita. Jijini Dar tu vjana wengi wanalima mchicha na kumwagilia japo kwa maji machafu wanajipatia kipato
 
Ni kwasababu wana amini alijiuzulu kumlinda JK madarakani pamoja wao kuamini pia kuwa utendaji umepunguwa kwenye serikali yao magamba baada ya mambo hayo.
...Imani ni silaha kali kuliko zote. Ikitumika vibaya, ina maafa makuu.

...Nategemea itatumika vizuri.
 
Kama kawaida yetu badala ya kuangalia ideas zaidi tunakuwa distracted na politics za personalities. Lowassa stinks and all, we all -those of us with unbiased eyes- know that. But even the village madman must be listened to as there is no monopoly on wisdom. And on this one, I am afraid as much I am inclined to dislike Lowassa, his words are prophetic. Whether opportunistic so or not is another matter and I do not think that matters that much at this point anyway. He provided a very daring "big picture" outlook that is right on the money. Of course in politics everything is calculated and I wouldn't put it past him that he is calculating something, but that is not the point. The point is, are his words meritorious or not? Do they carry an undisputable sense regardless of the motive?

The answer to both questions is a resounding is YES.

Ukiondoa siasa zote, na ku deal na kauli ya Lowassa tu - how naive of me-, this is a no brainer. The old adage says "Idle mind is the devil's playground".

As much as I don't put much stock in the actual devil, the logic behind is sound. To quote Rabelais, nature abhors a vacuum and the lowest common denominator/ lowest energy level will always occupy such an emptiness. Sadly this low almost always happens to be permeated by quests for social justice that are full of a revolutionary zeal (rightly or not) and war will easily be justified as not only the right thing, but an honorable obligation, Patrick Henry style.

The Governor of the Central Bank of Nigeria just said the same thing in retrospect in the wake of all these "Boko Haram" killings happenning in Nigeria, he said the real problem is not religious zealotry, but economic opportunities.

Ukichanganya udini, ongezeko holela la watu (Tanzania imekuwa projected kuwa nchi ya 5 kwa watu wengi duniani by 2100 at 316m, long shot projections admittedly, but still panapofuka moshi...) ukosefu wa ajira, tofauti kubwa kati ya matajiri na watu wa kipato cha kawaida na ukosefu wa elimu huwezi kushangaa sana maneno ya Lowassa (Again, I am not a Lowassa fan by any hue by the way, but I give credit where it is due nonetheless).

Walipo wa-Nigeria leo ndipo tunapoenda kesho.
 
Kwa mara nyingine tena Edo amerudia kauli yake juu ya tatizo la ajira kwa vijana kuwa ni bomu linalosubiri kulipuka. Amezungumza hayo akiwa kwenye harambe ya kanisa huko Mwanza.

Hili litakuwa pigo kubwa sana kwa serikali LeGeLeGe ya mzee wa kaya na bila shaka hili litawagharimu sana,na mpk hapo lile neno linatimia ya kwamba "UKIONA MAYOYA UJUWE KALIWA" Anaweza ikawa ni mbinu yake ya propaganda ya 2015.
 
Baada ya uchaguzi mkuu wa chama 2012 tunamaliza kesi kwa kumpa u chifu wa Kabila la wasukuma pale Bujora EL 2015 CCM.

Dickson usitumie kabila la wasukuma vibaya, umepanga na nani kumpa huo uchifu?. sasa kwa taarifa yako haupati sasa huo uchifu hata afanye nini. msitugeuze wajinga.
 
Back
Top Bottom