Ukondefu unaninyima amani nifanyeje ili nipate walau vinyama kidogo

52 kwa mwanaume ni ndogo sana.. angalau 60. piga gym mara 4 kwa wiki.
 
Tafuta supu ya utumbo wa ule maziwa ule weka na pili pili na ndimu au limao na chapati zako mbili kila siku asubuhi

Mchana kula ugali samaki fresh tu na matunda

Usiku piga kitu cha wali mnyamba ,maharage au shushia mchemsho wa samaki ,kuku au ngombe na ndizi juu

Halafu piga tizi la kutanua kifua hicho huwezi nenepa wakati una kifua kama cha mbu
 
Nyama ni chakula chenye kuongeza uzito haraka, kila mlo wako kula nyama na ikiwezekana nunua nyama ya kidari.

Kula chakula na kilevi iwe wine au beer.

Baada ya siku 28 utupe mrejesho.
Uchumi hauruhusu
 
Umesema wewe una mwili mwembamba ila me naweza kuwa nimekuzidi kwa kuwa na mwili zaidi yako wewe, nakumbuka darasani nilipokuwa sekondari nilikuwa naogopwa hadi na walimu muda mwingine kunichapa tena ukizingatia mimibni mpole sana.

Ninachoshukuru sikuwahi kukufuru hata siku moja kwa kujuta hivi nilivyo, tena huwa ninapofanya mazoezi ya kukimbia asubuhi mfano naongozana na mwenye mwili mkubwa anatamani angekuwa na mwili kama wangu tena wengine wananiambia wangekuwa na mwili kama wangu wangelala tu nyumbani.

Nimeona hapo ulianza ujenzi wa ulivyo ita kibanda chako nashauri endeleza ujenzi huwenda mafanikio yakaja kuketa kwako mwili sawa na unavyotaka
 
Mawazo ya kifalafala
Acha gubu,penda kuish bila karaha,acha mawazo ya kifala fala,pata muda wa kupumzika,rizika unachopata, kula diet stahk,fanya mazoez ya kuongeza weight,HAKIKA mwili huo miez 2 mingi utambi huo unakuja
 
Acha gubu,penda kuish bila karaha,acha mawazo ya kifala fala,pata muda wa kupumzika,rizika unachopata, kula diet stahk,fanya mazoez ya kuongeza weight,HAKIKA mwili huo miez 2 mingi utambi huo unakuja
Mazoez gan ya kuongeza weight?
 
Kulewa naogopa addiction tena
Kula grand malt 1asubuhi 1mchana 1jioni na msosi usile wa mawazo. Kama unakula magengeni acha na ujipikie mwenyewe mlo wa heavy weight


Hahaah watu wanautaka wembamba, wewe unataka unene. Hahahah ila tafuta hela unene unakuja wenyewe
 
Aaah aaah wembamba jau..
Sugar mamy wanakuona mtotobukiwasilimia tu.. Hautaskia mbona hauniamkiii.....

Aaah aaah aaah tafuta chakula cha tembo ule
HABARI WAKUU.
Wakubwa kwa Wadogo salamu kwenu
Mimi ni kijana mwenye 28 years..!

Tatzo langu ni uwembamba uliopitiliza natamani walau na mimi niwe na vinyama kidogo. Nakumbuka mwaka jana niliwahi kupima uzito wangu nikawa 48kg uzito wa Jogoo la kienyeji iliniuma sana nilikaa wiki zima nikitafakari hatma ya afya yangu hadi hapo nilipoenda kupima magonjwa yote nikakutwa nipo smart sina tatzo la kiafya!

Nikaamua kujianzishia Dozi ya kula matunda kila baada ya chakula na mara kwa mara hali ambayo ilikuwa inanigalimu kila siku kutumia galama zaidi ya elfu kumi 10,000 kwa ajili ya Kuimalisha Afya yangu pia nilipata ushauri wa kula kitimoto na Bia moja kila siku! Hali ambayo sikuona shida nilikuwa nafanya hivyo hadi kujikuta nakuwa mlevi wa bia, Maana nilikuwa nakunywa bia moja kwa ajili ya Afya ila hatmae nikajikuta nakunywa bia zaidi ya 5 kwa siku maana tabia ya Bia nilikuwa nikinywa moja natamani kuongeza nyingine na nyingine hadi nikajikuta nakuwa mlevi pasipo kukusudia hali hii ilikuwa inanipelekea kukosana na watu wanaonizunguka kila nikinywa pombe nawatambia majirani zangu kuwa hawana hela na kusababisha fujo hadi nyumbani kwangu! Ikabidi nijishauri mwenyewe nakuacha dozi hii kwa sasa situmii tena.

Ila katika kumbukumbu zangu kipindi nafanya haya walau nilianza kuona mabadiliko kidogo ya afya mwilini mwangu nikaanza kutokeza kakitambi kwa mbali na kunenepa shavu na nilipopimwa uzito nilikuwa nimefikisha 60Kg hadi watu walianza kuniambia nimenenepa pasipokujua hiyo hali inaniingiza galama kiasi gani!

Nilikuwa nimeanza kunyanyua kakibanda kangu ila nilisimamisha shughuli ya ujenzi, pesa yote niliokuwa napata katika mihangaiko yangu ikawa inatumika kwa ajili ya kufanyia kile ninachokitamani, baada ya kuacha tena dozi hii kwa sasa nimepururuka vibaya mno jana nimepima uzito nakuta 52kg tu na kila kukicha nazidi kukonda tena!

Nimeamua kuja hapa ili wataalamu mnipe namna ambayo itakuwa si ghali sana ambayo nitatumia ili ninenepe huu ukondefu unaninyima michongo mingi sana!
Atakaeweza kunisaidia nipo tayari kumlipa!
 
Wanachokosea watu ni kudhan kula nyama sjui nin ndo utanenepa kunenepa kunatokana na
1.kula chakula kiingi yan haijalish nyama,dagaa ,maharage,yaan kama ni sahan bas ipitilize
2.kupumzika,yaan usifanye shuruba,mda mwing uwe umepumzika kitu ambacho si rahis
3.stress free

Hapo lazma unenepe mjomba
Daaah. Umenikumbusha kuna kipindi wife alikwenda kwao mara moja, nilikuwa najipikia ugari kubwa nakula hadi nakaribia kutapika ndo naacha, ndani ya wiki tu nikaanza kunenepa hadi sura bahati mbaya sikuendelea sana nikaacha
 
HABARI WAKUU.
Wakubwa kwa Wadogo salamu kwenu
Mimi ni kijana mwenye 28 years..!

Tatzo langu ni uwembamba uliopitiliza natamani walau na mimi niwe na vinyama kidogo. Nakumbuka mwaka jana niliwahi kupima uzito wangu nikawa 48kg uzito wa Jogoo la kienyeji iliniuma sana nilikaa wiki zima nikitafakari hatma ya afya yangu hadi hapo nilipoenda kupima magonjwa yote nikakutwa nipo smart sina tatzo la kiafya!

Nikaamua kujianzishia Dozi ya kula matunda kila baada ya chakula na mara kwa mara hali ambayo ilikuwa inanigalimu kila siku kutumia galama zaidi ya elfu kumi 10,000 kwa ajili ya Kuimalisha Afya yangu pia nilipata ushauri wa kula kitimoto na Bia moja kila siku! Hali ambayo sikuona shida nilikuwa nafanya hivyo hadi kujikuta nakuwa mlevi wa bia, Maana nilikuwa nakunywa bia moja kwa ajili ya Afya ila hatmae nikajikuta nakunywa bia zaidi ya 5 kwa siku maana tabia ya Bia nilikuwa nikinywa moja natamani kuongeza nyingine na nyingine hadi nikajikuta nakuwa mlevi pasipo kukusudia hali hii ilikuwa inanipelekea kukosana na watu wanaonizunguka kila nikinywa pombe nawatambia majirani zangu kuwa hawana hela na kusababisha fujo hadi nyumbani kwangu! Ikabidi nijishauri mwenyewe nakuacha dozi hii kwa sasa situmii tena.

Ila katika kumbukumbu zangu kipindi nafanya haya walau nilianza kuona mabadiliko kidogo ya afya mwilini mwangu nikaanza kutokeza kakitambi kwa mbali na kunenepa shavu na nilipopimwa uzito nilikuwa nimefikisha 60Kg hadi watu walianza kuniambia nimenenepa pasipokujua hiyo hali inaniingiza galama kiasi gani!

Nilikuwa nimeanza kunyanyua kakibanda kangu ila nilisimamisha shughuli ya ujenzi, pesa yote niliokuwa napata katika mihangaiko yangu ikawa inatumika kwa ajili ya kufanyia kile ninachokitamani, baada ya kuacha tena dozi hii kwa sasa nimepururuka vibaya mno jana nimepima uzito nakuta 52kg tu na kila kukicha nazidi kukonda tena!

Nimeamua kuja hapa ili wataalamu mnipe namna ambayo itakuwa si ghali sana ambayo nitatumia ili ninenepe huu ukondefu unaninyima michongo mingi sana!
Atakaeweza kunisaidia nipo tayari kumlipa!
Niwapi huko unakoishi..?? Huko mahali ambapo mtu mwenye kilo 48 analeta fujo
 
Wengi tuwakondefu either kwa mawzo au kwa kuzaikiwaa asili ila mim naamini hakuna MTU mwembamba kwa SAS pata pesa au uotee ajira ofisi nzuri utaona kuwa hakuna MTU mwembamba duniani
 
Umesema wewe una mwili mwembamba ila me naweza kuwa nimekuzidi kwa kuwa na mwili zaidi yako wewe, nakumbuka darasani nilipokuwa sekondari nilikuwa naogopwa hadi na walimu muda mwingine kunichapa tena ukizingatia mimibni mpole sana.

Ninachoshukuru sikuwahi kukufuru hata siku moja kwa kujuta hivi nilivyo, tena huwa ninapofanya mazoezi ya kukimbia asubuhi mfano naongozana na mwenye mwili mkubwa anatamani angekuwa na mwili kama wangu tena wengine wananiambia wangekuwa na mwili kama wangu wangelala tu nyumbani.

Nimeona hapo ulianza ujenzi wa ulivyo ita kibanda chako nashauri endeleza ujenzi huwenda mafanikio yakaja kuketa kwako mwili sawa na unavyotaka
Sawa wazo zuri
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom