Ukombozi wa dhati

MUHOGOJ

Member
Sep 13, 2011
11
3
Ndugu wana JF, tumeshuhudia Chadema wakitoa kauli kali na ngumu kuwa CCM imeamua kutumia umafia wake wote kuhujumu democrasia nchini, kuanzia vyombo vya dola, wakuu wa mikoa, wilaya na viongozi wa kata, tarafa na vijiji. Wako yatari kwa lolote, hata kama ni kuua, kujeruhi, kutishia, na kudhalilisha utu wa binadamu ili mradi waendelee kutuibia, kutunyonya, na kutukandamiza. Kama ni kweli taarifa iliyotolewa na viongozi wa Chadema kuhusu yaliyojiri kwenye kambi ya Singida, sasa uvumilivu wa watanzania utakuwa umefika ukingoni. Nimetafakari mambo haya ambayo yananiumiza sana, kiasi cha kushawishika kujiunga humu ili tuelimishane.

  1. Hela zinazotumika kugharimia kambi hizo kufundisha majangili na majambazi, fedha zinazotolewa kama rushwa, fedha zinazotumika kununua tindikali, madawa ya kulevya, sindano (ili mradi tuu kuwakomoa Chadema)n.k ni za sisi walipa kodi. Yaani natoa kodi yangu af ndo inatumika kuniua, kunijeruhi na kunitishia usalama wangu endapo sitaipigia kura CCM!!!!!! Mungu wangu!!!!!!!!
  2. Eti, Mwigulu, Nape au Mukama, "Hawa vijana mliowafundisha ujambazi baada ya uchaguzi mnaendelea kuwapa mishahara kama askari au? Au ndo wanaachwa solemba mpaka uchaguzi mwingine uje tena.? Kama ni hivyo, hatuoni kuwa baada ya uchaguzi wanabadilika kuwa majambazi kabisa? Maana wameshafundishwa mbinu.
  3. Je mtanzania kuwa mtumishi wa serikali maana yake ni kuwa mpambe wa CCM hata pale ambapo mtu hataki? CCM ya leo bado inadhani tuko kwenye mfumo wa chama kimoja enzi za Nyerere na Mwinyi? Mnataka watanzania waamini kuwa mmejisahau au ni kiburi chenu cha kujifanya miungu watu? Mtu kuwa mwalimu, mfanyakazi wa benki, au nafasi nyingine yoyote ya serikali ni dhamanana ya CCM? Ni fadhila? Msipotujibu maswali haya hakika yenu your count down imekuja.
  4. Ombi langu kwa Chadema, tuko nyuma yenu ila mtuambie mbinu mbadala za kutatua matatizo yafuatayo, tuko tayari kuchangia hata kwa gharama yoyote.
    • Pawepo na movement ya kuwafikia wananchi wa vijijini na kuwaelimisha haki zao za msingi. Mikutano ya hadhara ya siku moja kukusanya watu maelfu haitatosha. Tunahitaji tuwe na watu watakaosambaa vijijini wakae kwa muda huko wawaeleweshe raia ambao wanateseka na vitisho vya CCM.
    • Tunahitaji social media ambayo itakuwa na coverage kubwa zaidi ya kuwafikia watanzania wote (TV na magazeti). Wadau wengi hapa JF wako tayari kusapoti
Kwa leo naishia hapa kama kuna wadau wana hoja waongezee hapo.
 
{Tunahitaji social media ambayo itakuwa na coverage kubwa zaidi ya kuwafikia watanzania wote (TV na magazeti). Wadau wengi hapa JF wako tayari kusapoti]

Hili ndilo la Msingi
 
Hata wamarekani wamefanikiwa kwa kutumia Media...wasi wasi wangu ni kupata media ambayo haina chembe za U CCM
 
Sijui hawa viongozi wetu wa cdm hili la kuanzisha media wanalichukuliaje!ilianza cku nyingi na wengi tulikuwa tayari kutoa support lakini hakuna tamko lolote linalotolewa!Amkeni Chadema,tupeni mwongozo!
 
Mkuu swala lipo ndani ya katiba na huu uhuni wa hii katiba ndio unafanya watanzania wanakwenda kufanya kazi tbc kupigia magoti ccm wakiogopa kufkuzwa kazi, lingine ni swala la leseni za kuanzisha biashara za utangazaji, hazitolewi bila kupiga magoti ccm. The fact is tukiondoa ujinga wa hii katiba na hao jamaa ikulu, we will be free in did. Free at last .... Free at last!

Angalia communism china hakuna tofauti na ccm. The key ni ku-control the people so you can rule and abuse them...
Communism in China

Hata wamarekani wamefanikiwa kwa kutumia Media...wasi wasi wangu ni kupata media ambayo haina chembe za U CCM
 
Mkuu swala lipo ndani ya katiba na huu uhuni wa hii katiba ndio unafanya watanzania wanakwenda kufanya kazi tbc kupigia magoti ccm wakiogopa kufkuzwa kazi, lingine ni swala la leseni za kuanzisha biashara za utangazaji, hazitolewi bila kupiga magoti ccm. The fact is tukiondoa ujinga wa hii katiba na hao jamaa ikulu, we will be free in did. Free at last .... Free at last!

Angalia communism china hakuna tofauti na ccm. The key ni ku-control the people so you can rule and abuse them...
Communism in China

sasa hiyo ndio safi... umeona leo hii china leval iliyofikia...??!!
 
Ndugu wana JF, tumeshuhudia Chadema wakitoa kauli kali na ngumu kuwa CCM imeamua kutumia umafia wake wote kuhujumu democrasia nchini, kuanzia vyombo vya dola, wakuu wa mikoa, wilaya na viongozi wa kata, tarafa na vijiji. Wako yatari kwa lolote, hata kama ni kuua, kujeruhi, kutishia, na kudhalilisha utu wa binadamu ili mradi waendelee kutuibia, kutunyonya, na kutukandamiza. Kama ni kweli taarifa iliyotolewa na viongozi wa Chadema kuhusu yaliyojiri kwenye kambi ya Singida, sasa uvumilivu wa watanzania utakuwa umefika ukingoni. Nimetafakari mambo haya ambayo yananiumiza sana, kiasi cha kushawishika kujiunga humu ili tuelimishane.
  1. Hela zinazotumika kugharimia kambi hizo kufundisha majangili na majambazi, fedha zinazotolewa kama rushwa, fedha zinazotumika kununua tindikali, madawa ya kulevya, sindano (ili mradi tuu kuwakomoa Chadema)n.k ni za sisi walipa kodi. Yaani natoa kodi yangu af ndo inatumika kuniua, kunijeruhi na kunitishia usalama wangu endapo sitaipigia kura CCM!!!!!! Mungu wangu!!!!!!!!
  2. Eti, Mwigulu, Nape au Mukama, "Hawa vijana mliowafundisha ujambazi baada ya uchaguzi mnaendelea kuwapa mishahara kama askari au? Au ndo wanaachwa solemba mpaka uchaguzi mwingine uje tena.? Kama ni hivyo, hatuoni kuwa baada ya uchaguzi wanabadilika kuwa majambazi kabisa? Maana wameshafundishwa mbinu.
  3. Je mtanzania kuwa mtumishi wa serikali maana yake ni kuwa mpambe wa CCM hata pale ambapo mtu hataki? CCM ya leo bado inadhani tuko kwenye mfumo wa chama kimoja enzi za Nyerere na Mwinyi? Mnataka watanzania waamini kuwa mmejisahau au ni kiburi chenu cha kujifanya miungu watu? Mtu kuwa mwalimu, mfanyakazi wa benki, au nafasi nyingine yoyote ya serikali ni dhamanana ya CCM? Ni fadhila? Msipotujibu maswali haya hakika yenu your count down imekuja.
  4. Ombi langu kwa Chadema, tuko nyuma yenu ila mtuambie mbinu mbadala za kutatua matatizo yafuatayo, tuko tayari kuchangia hata kwa gharama yoyote.
    • Pawepo na movement ya kuwafikia wananchi wa vijijini na kuwaelimisha haki zao za msingi. Mikutano ya hadhara ya siku moja kukusanya watu maelfu haitatosha. Tunahitaji tuwe na watu watakaosambaa vijijini wakae kwa muda huko wawaeleweshe raia ambao wanateseka na vitisho vya CCM.
    • Tunahitaji social media ambayo itakuwa na coverage kubwa zaidi ya kuwafikia watanzania wote (TV na magazeti). Wadau wengi hapa JF wako tayari kusapoti
Kwa leo naishia hapa kama kuna wadau wana hoja waongezee hapo.
Post ya kwanza halafu unaanza na ushuzi.
 
{tunahitaji social media ambayo itakuwa na coverage kubwa zaidi ya kuwafikia watanzania wote (tv na magazeti). Wadau wengi hapa jf wako tayari kusapoti]

hili ndilo la msingi

sikatai hoja yenu ya media lakini mnawajua watanzania?
Mkianzisha tv, vijijini waliko wapiga kura, ccm hawajapeleka umeme na wala mipango si ya leo na kibaya zaidi ka watanzania wengi tv ni anasa, ukiwa na tv ni tajiri kabisa. Namaanisha wengi tv hawana, na hawataweza kununua achilia mbali kusikiliza hbr za kiukombozi. Wengi watakimbilia ze comedy na tamthiliya za wazungu.

Kwa upande wa magazeti, wa vijijini watasoma wale wenye nia ya kubadilika. Hata kama yatagawiwa bure(kwani yakiuzwa hayatanunulika) wengi wtayatumia kufungia vitumbua, andazi na bajia. Wengine watatumia kufungia unga, kwani mtakuwa mmewasaidia.

Maoni yangu ni kuwa na movement endelevu, wapatikane wanaharakati kila kijiji, wapewe semina na wawezeshwe kuwafikia wananchi kwa kufanya home to home vist, makongamano na mikutano mbalimbali.

Katika mikutano hiyo, elimu ya uraia itatolewa kwa upana, na wengi watapata kuzitambua haki zao.

Lingine ni kuwafikia wanafunzi wa kada zote, kwani tukiwekeza huko kesho tutakuwa na mtaji mkubwa.

Nyingine ni kuanzisha harakati za misi..................
 
sijui hawa viongozi wetu wa cdm hili la kuanzisha media wanalichukuliaje!ilianza cku nyingi na wengi tulikuwa tayari kutoa support lakini hakuna tamko lolote linalotolewa!amkeni chadema,tupeni mwongozo!

nadhani hata wao wanapenda suala hilo sema tu yawezekana wamekwama mahala
 
Tatizo hapa si media coverage,muelewe watanzania wengi ni wavivu kusoma especialy magazeti,mtu akiona story kwenye gazeti anataka umhadisie inasemaje na wala si kusoma,kuhusu tv mkumbuke mjini tu umeme ni ishu sembuse huko vijijini ambao ndio walengwa wakuu,vijiji vingi havina umeme na wala havina dalili ya kupata,my take, labda viandaliwe vikosi kazi kila wilaya na viwezeshwe ambavyo vitaingia kijiji baada ya kijiji ya kijiji, nyumba kwa nyumba,mtu kwa mtu, kutoa elimu nya uraia sambamba na kufungua matawi
 
Hakuna Mtanganyika wa leo ambae hajakoswakoswa na udhalilishaji wa umaskini tuliodhaninishwa na CCM. Sisi sio maskini lakini tuliambiwa kuwa sisi ni maskini na CCM huku wao wakichuma bila jasho. Sisi tufanye kazi kwa bidii ili wao wakiokota tu!. Mtanganyika wa leo anajua kwa nini haitaki CCM. by assumption 80% wameshabadilika japo shule hizi za voda fasta za kidhalilishaji zimetuweka pazuri kidogo kujua mbivu na mbichi. Ndo maana baada ya wao kujua hilo unakuta tunapambanishwa katika imani (dini) zetu. Tuwe macho nalo hilo!! Haiitaji elimu pana sana maana ukilala na njaa somo tosha!!
 
kuna kitu ambacho CCM wamekirithi toka chama kimoja ambacho ndo kimekuwa ni msingi wa mafanikio yao vijijini si kingine bali ni mfumo wa mabalozi wa nyumba kumi. Mabalozi hawa ndo Engine ya ccm ni watu wanaotumika kama toileti paper wakati wa uchaguzi lakini wananguvu ya ushawishi hasa kwa akina mama huko vijijini. Watu hawa hutembea kila mji na kukaa na akina mama na mara nyingi ccm hutuma kanga na Tshirt kwa mabalozi ili kuwafikia hawa watu.

Kama CDM inataka kuwa na mtandao mzuri mpaka vijijini ni lazima waanzishe mfumo unaofanana na huu unaowalenga hasa vijana wa vijijini na akina mama wa ambao wana Elimu japo ya darasa la saba. Akina mama wasiojua kusoma ni ngumu kuwashawishi maana hawajui chochote zaidi ya KIJANI. Hawa sio wengi na muda wao unapita ila chadema lazima iwekeeze kwa vijana huko vijijini ambao ndo nguvu ya umma. Vijana wanaweza kuwabadilisha hawa akina mama na hata kuzuia rusha za kanga na Tshirt zisipelekwe vijijini maana vijana wana nguvu hiyo.

Kama CDM wanataka kuwa chama cha kutawala ni lazima hili lifanyike kabla ya uchaguzi wa serikali za mitaa 2014. Upinzani umekuwa haufanyi vizuri kwenye hizi chaguzi Either kwa kutokujua kuwa hizi ndo zinzjenga msingi wa ushindi katika uchaguzi mkuu.

Kijiji kinapokuwa na viongozi wa serikali ambao ni wapinzani tayari ni ushindi kwenye uchaguzi mkuu katika eneo hilo.

CDM ni lazima wajipe malengo kila mbunge katika jimbo lake ya kwamba anawavutia vijana wote kuwa CDM na kuunda vikosi kazi vya vijana kuhubiri cdm nyumba kwa nyumba.

Tunaamini CDM ni chama cha ukombozi na nadhani kila mtu mwenye nia njema na nchi hii yuko tayari kuchangia harakati hizi kwa kutoa sehemu kidogo ya kipato chake.

Mimi binafisi niko tayari kutoa sehemu ya kipato changu kwa ajiri ya ukombozi huu na naamini hata Mungu atatubariki kwa kufanya hivyo.

Tunatarajia uongozi wa CDM utayafanyia kazi mapendekezo haya.

Mungu ibariki Tanzania na watu wake waliowema!
 
ni wazo la maana, ubaya wake ni kuwa mfumo huo unaweza kukifanya chama kuwa busy na mfumo wa kutawala badala ya kujikita kupigania maendeleo ya nchi na wananchi. ni wazo tu wajameni,
 
wapinzania huwa hawakosekani na tz tupo hapa tulipo kwa sababu wajinga ni wengi! naunga mkono hoja
 
<font size="4"><b><font color="#800080"><span style="font-family: comic sans ms"><br />
sikatai hoja yenu ya media lakini mnawajua watanzania?<br />
Mkianzisha tv, vijijini waliko wapiga kura, ccm hawajapeleka umeme na wala mipango si ya leo na kibaya zaidi ka watanzania wengi tv ni anasa, ukiwa na tv ni tajiri kabisa. Namaanisha wengi tv hawana, na hawataweza kununua achilia mbali kusikiliza hbr za kiukombozi. Wengi watakimbilia ze comedy na tamthiliya za wazungu.<br />
<br />
Kwa upande wa magazeti, wa vijijini watasoma wale wenye nia ya kubadilika. Hata kama yatagawiwa bure(kwani yakiuzwa hayatanunulika) wengi wtayatumia kufungia vitumbua, andazi na bajia. Wengine watatumia kufungia unga, kwani mtakuwa mmewasaidia.<br />
<br />
Maoni yangu ni kuwa na movement endelevu, wapatikane wanaharakati kila kijiji, wapewe semina na wawezeshwe kuwafikia wananchi kwa kufanya home to home vist, makongamano na mikutano mbalimbali. <br />
<br />
Katika mikutano hiyo, elimu ya uraia itatolewa kwa upana, na wengi watapata kuzitambua haki zao.<br />
<br />
Lingine ni kuwafikia wanafunzi wa kada zote, kwani tukiwekeza huko kesho tutakuwa na mtaji mkubwa.<br />
<br />
Nyingine ni kuanzisha harakati za misi..................</span></font></b></font>
<br />
<br />

mkuu pamoja na hayo ianziswe redio hihaijalishi kipato hadi mwenye kipato cha chini atapata matangazo mikutano yote itangazwe live itasaidia kubadilisha watu kwa wakati 1
 
kuna kitu ambacho CCM wamekirithi toka chama kimoja ambacho ndo kimekuwa ni msingi wa mafanikio yao vijijini si kingine bali ni mfumo wa mabalozi wa nyumba kumi. Mabalozi hawa ndo Engine ya ccm ni watu wanaotumika kama toileti paper wakati wa uchaguzi lakini wananguvu ya ushawishi hasa kwa akina mama huko vijijini. Watu hawa hutembea kila mji na kukaa na akina mama na mara nyingi ccm hutuma kanga na Tshirt kwa mabalozi ili kuwafikia hawa watu.

Kama CDM inataka kuwa na mtandao mzuri mpaka vijijini ni lazima waanzishe mfumo unaofanana na huu unaowalenga hasa vijana wa vijijini na akina mama wa ambao wana Elimu japo ya darasa la saba. Akina mama wasiojua kusoma ni ngumu kuwashawishi maana hawajui chochote zaidi ya KIJANI. Hawa sio wengi na muda wao unapita ila chadema lazima iwekeeze kwa vijana huko vijijini ambao ndo nguvu ya umma. Vijana wanaweza kuwabadilisha hawa akina mama na hata kuzuia rusha za kanga na Tshirt zisipelekwe vijijini maana vijana wana nguvu hiyo.

Kama CDM wanataka kuwa chama cha kutawala ni lazima hili lifanyike kabla ya uchaguzi wa serikali za mitaa 2014. Upinzani umekuwa haufanyi vizuri kwenye hizi chaguzi Either kwa kutokujua kuwa hizi ndo zinzjenga msingi wa ushindi katika uchaguzi mkuu.

Kijiji kinapokuwa na viongozi wa serikali ambao ni wapinzani tayari ni ushindi kwenye uchaguzi mkuu katika eneo hilo.

CDM ni lazima wajipe malengo kila mbunge katika jimbo lake ya kwamba anawavutia vijana wote kuwa CDM na kuunda vikosi kazi vya vijana kuhubiri cdm nyumba kwa nyumba.

Tunaamini CDM ni chama cha ukombozi na nadhani kila mtu mwenye nia njema na nchi hii yuko tayari kuchangia harakati hizi kwa kutoa sehemu kidogo ya kipato chake.

Mimi binafisi niko tayari kutoa sehemu ya kipato changu kwa ajiri ya ukombozi huu na naamini hata Mungu atatubariki kwa kufanya hivyo.

Tunatarajia uongozi wa CDM utayafanyia kazi mapendekezo haya.

Mungu ibariki Tanzania na watu wake waliowema!

Hawana muda kusoma mapendekezo wako bize kupiga wakuu wa wilaya wanawake ok

Haya mapendekezo yanahitaji pesa nyingi sana na cha-demu hatujapewa ruzuku na serikali ya ccm..tufanyeje?

Isitoshe katibu mkuu wetu anahitaji malipo manono ..so please vuta subira mkuu tuandamane kwanza ili tuweze kupata per-diems..ok.
 
Back
Top Bottom