Uko mbele kutakuwa na ndoa kweli';nahisi zitadisapia kabisa

Mwanajamvi mwenzangu mimi nahisi matatizo ya ndoa huanzia kwenye maandalizi ya ndoa zenyewe... Vijana wanakuwa wamependana vizuri kwa jinsi walivo na wamelidhika kwa uwezo wao, ndoa wazee wanataka kuonesha wana uwezo kiasi gani, hivi ina maana gani mtu mwenye kipato kidogo cha chini kumfanyia harusi ya gharama si bora kama wazazi wana hela wawape watoto za kuanzia maisha..... Tutakapofika pale kila mtu atakapokuwa na uweza kujiamini na kuishi kwa kadiri ya uwezo wake ndoa zitadumu, sababu tatizo kubwa linalopelekea kuachana ni tamaa na instability ya kipato katika familia changa!! Watu wasipojitambua vikao vya usuluhishi vitakuwa vingi sana!!
Sijakuelewa ndugu yangu wazazi umewaingizaje hapo? kwani wao ndio waliotaka kuoana? wenyewe si walishapendana kabla na kuona wanafaa kuwa mume na mke sasa.. sherehe ya kukamilisha tu tena huwa mwishoni baada ya kutoka kanisani ndio iwe tatizo..!
 
mimi naona tatizo kubwa hapa ni tabia za mabinti wa kisasa, wanakuwa wanapenda sana kushindana na waume zao, hawataki kuwa chini hata kidogo, siku zote fahari wawili hawawezi kaa zizi moja, hapo ndio shida inapokuja, mimi juzi nimemtwanga sana fiance wangu kwa tabia kama hizi, hakuna masikilizano, na sasa ni na review wazo la kumuoa. big problem
 
[. Ndoa siyo tendo la kujamiiyana kwani hili tendo ni sehemu ndogo sana ya ndoa, sehemu kubwa ya ndoa ni majukumu ya kawaida kabisa ambayo hayana uhusiano wowote na kujamiiyana hivyo haya masuala mingene lazima myajadili kwa kina kabla ya kuingia kwenye ndoa vinginevyo haya mambo ni rahisi sana kuvyunja ndoa na ndio vyanzo vingi vya migogoro ya ndoa.[/QUOTE]


vumbi umeongea point,asante.
 
Mwanajamvi mwenzangu mimi nahisi matatizo ya ndoa huanzia kwenye maandalizi ya ndoa zenyewe... Vijana wanakuwa wamependana vizuri kwa jinsi walivo na wamelidhika kwa uwezo wao, ndoa wazee wanataka kuonesha wana uwezo kiasi gani, hivi ina maana gani mtu mwenye kipato kidogo cha chini kumfanyia harusi ya gharama si bora kama wazazi wana hela wawape watoto za kuanzia maisha..... Tutakapofika pale kila mtu atakapokuwa na uweza kujiamini na kuishi kwa kadiri ya uwezo wake ndoa zitadumu, sababu tatizo kubwa linalopelekea kuachana ni tamaa na instability ya kipato katika familia changa!! Watu wasipojitambua vikao vya usuluhishi vitakuwa vingi sana!!


Ndugu kipato ni sehemu ndogo sana ya maisha ya ndoa,so sidhan inachangia kuharibu ndoa zetu
nina mfnao wa mjomba wangu kumradhi wanaomjua yuko Tacaids swaafii na mama yukoo UN
Zaidi ya miaka 10 nw wana hela chafu sio mbaya yaani imezidi ubaya.......,na leo hii wana gorofa lao masaki tatu baba yuko juu mama ya pili watoto chini na wakijisikia watoto wanaenda kw baba na mama na hutoamini kila siku wako gari moja wanapelekana kazini.......siri ya ndoa ajuaye mwenye ndoa
 
mimi naona tatizo kubwa hapa ni tabia za mabinti wa kisasa, wanakuwa wanapenda sana kushindana na waume zao, hawataki kuwa chini hata kidogo, siku zote fahari wawili hawawezi kaa zizi moja, hapo ndio shida inapokuja, mimi juzi nimemtwanga sana fiance wangu kwa tabia kama hizi, hakuna masikilizano, na sasa ni na review wazo la kumuoa. big problem



yaani unadhubutu kumtwanga mchumba wako sasa hivi? inasikitisha! na ukishamwoa itakuwaje?
 
mimi naona tatizo kubwa hapa ni tabia za mabinti wa kisasa, wanakuwa wanapenda sana kushindana na waume zao, hawataki kuwa chini hata kidogo, siku zote fahari wawili hawawezi kaa zizi moja, hapo ndio shida inapokuja, mimi juzi nimemtwanga sana fiance wangu kwa tabia kama hizi, hakuna masikilizano, na sasa ni na review wazo la kumuoa. big problem
Du kaka, hivi hapa Tz unatoka 'jamhuri' gani vile??! ulimtwanga fiancée wako!!! kazi ipo.
 
tatizo watu mnaangalia mlipoangukia badala ya mlipojikwaa,,, hebu tazameni hawa wanaooana siku hizi wengi wao mwanzo wa uhusiano wanakutana kwenye mazingira gani? Ndoa nyingi zinatengenezwa na watu wenye tamaa za muda mfupi kutoka kwa wenzao huku wakijua ndoa ni kifungo cha maisha.
 
Hili swala litazamwe pia kimazingira ya sasa na ya vipindi vya nyuma wakati ndoa zikiheshimika na kudumu.Ulimwengu wa leo vijana wana tamaa sana hasa wa kike,na wazee wetu ambao walishachuma siku nyingi wanavitolea macho hivyo vitoto na kuvimwagia mipesa kede kede,kuna wazazi pia wamewalea watoto vibaya sana hawana maadili kabisa,mtoto wa kike kupika hajui hata usafi unamshinda,pia viburi hawarekebishiki katu katu,adabu pia iko chini sana.Likija la Beijing ndio mbaya zaidi,tena nasikitika kwamba badala ya kuitafsiri kwamba ni ukombozi wa mwanamke wao wanachulia ni ushindani na usawa na wanaume,tangu lini jinsia hizi mbili zikalingana?Wazazi na viongozi wa dini watuisaidie kutufundisha misingi ya jinsia hizi mbili na majukumu yake katika maisha na swala la ndoa na majukumu yake likiwemo.
 
Kama mimi na mume wangu ukituona huko mtaani huwezi jua kama sijapata unyumba huu mwaka wa nne na bado tupo wote. im only 34 and i have sixteen years in mariage naendelea vumilia najua iko siku mungu atafungua milango. Ndoa ngumu jamani sasa hawa wa siku hizi hawawezi vumilia hii issue hata iweje labda wanaomwamini mungu.

Ukija kwa wazee wa zamani, wao walivumilia ndoa si kwamba walikuwa hawazini au kuwa na tabia kama hizo , ila kulikuwa hakuna issue kama hizi za utandawazi, simu zimekuwa ndio chanzo kikubwa cha ndoa kuvunjika cause mtu unashikwa na kithibitisho. shangazi yangu alikuwa anasema enzi hizo ndoa zilikuwa hazivunjiki sababu wanzinzi walikuwa hawashikwi
Utakuta baba na mama wa jirani wanakutana huko kwenye mipaka ya mashamba wanalima wanapeana dozi kila mtu anarudi kwake kimya. siku hizi utakuta mke wa mtu anataka kuchati na kibwana chake hata akiwa kwake.

Nilienda dodoma kutafuta msichana wa kazi ni kijijini kabisa ajabu nikaletewa halfcast wa kizungu kuuliza kulikoni mama mweusi baba mweusi mtoto mzungu! mama mwenye mtoto akasema alikuwa analima shambani akapita mzungu akasimama kujisaidia alivyomuona akamwomba mchezo kwa kumpa alfkumi kuja kushangaa anamimba kujifungua ndio huyo mtoto. Guess wat! mumewe alienda kwa wazazi akalipwa fidia ya ng'ombe mmoja na ndoa iliendelea wakaendelea kuzaa watoto wengine.so mtoto wa kizungu katikati ya watoto weusiiii na yuko kijijini.
samahani kwa post ndefu
Ndugu kipato ni sehemu ndogo sana ya maisha ya ndoa,so sidhan inachangia kuharibu ndoa zetu
nina mfnao wa mjomba wangu kumradhi wanaomjua yuko Tacaids swaafii na mama yukoo UN
Zaidi ya miaka 10 nw wana hela chafu sio mbaya yaani imezidi ubaya.......,na leo hii wana gorofa lao masaki tatu baba yuko juu mama ya pili watoto chini na wakijisikia watoto wanaenda kw baba na mama na hutoamini kila siku wako gari moja wanapelekana kazini.......siri ya ndoa ajuaye mwenye ndoa
 
Marriage is a VERY SERIOUS BUSINESS!
Naamini from the bottom of my heart kuwa dini inaplay part kubwa sana katika hili. Kama wote ni wacha Mungu na mnafuata dini kisawasawa basi mtaacha mabaya yote na mtaoana na kuishi katika misingi ya kidini kama vile Mungu anayotaka.
Kila Mume/Mke atamheshimu, atampenda, atamjali, atamsaidia, atamtii mwenzake 200%.
Kwa mtaji huo itakuwa ni heshima, upendo na amani pande zote saa zote na wakati wowote.
Hakutakuwa na cha nyumba ndogo wala serengeti boyz, wala kuvunjiana heshima ktk namna yoyote ile!!
Shetani hapendi ndoa na ndio maana watu hawazingatii maadili ya dini zetu. Zingatieni maadili ya dini zenu na myafuate mtafanikiwa ktk ndoa zenu!!
 
Hatumshikiri Mungu kwenye kumtafuta mchumba, kwenye maandalizi ya ndoa na kuiishi ndoa yeye. Tunabaki na maandalizi ya sherehe, michango na mambo yote ya mwili. lakini ndoa nzuri/bora inaanza kwenye maandalizi ya dhamira na roho.
 
Back
Top Bottom