sinyora
JF-Expert Member
- Nov 21, 2016
- 966
- 1,622
ni kweli mkuu uwa ni kipindi kigumu sana kwa mama mtoto anakua bila baba na baba yupo hana time nae kuna muda mtu anahitaji ule upendo tu na ukaribu mwanae apate kutoka kwa baba au ndg wa baba sema wanaume wengi wanajua kukumbia kwao wanaepuka matumizi nshaptia hayo yanauma sanaNi mbaya saana...wengi wa watoto wanaokataliwa hupitia maisha magumu saana.
Imagine unaambiwa na mama baba yako alikukataa huku unaona marafiki zako wanachukuliwa na baba zao shule!!
Huyo mdada alifanya vizuri kurudi kwa mara pili kumwonyesha jamaa mtoto wake cha kusikitisha bado mwanaume hakuonyesha ushirikiano.
Unajua faida ya kurudi kwa mara ya pili??
Unaepuka kuwa mbinafsi. Kumbuka unaweza kugombana na mzazi mwenzako wewe binafsi lakini ni haki ya mtoto kumjua mama au baba yake. Hili huwa tunalisahau.
Wengi wanazilisha ego zao kwa kuwakomoa wazazi wenzao lakini literally anayekandamizwa ni mtoto...huu nauita ubinafsi.
Lingine..wanaume tunaokimbia watoto tunadhani wanawake wanahitaji vingiii. Wala sio wengi wenu kikubwa mnachohitaji hata kama hauhufumii asilimia 100 lakini unaonyesha kujali, upendo kwa mama na mtoto na kumweleza mwanamke tulichofanya hatukukosea...inatosha kabisa.
Umenifanya niandike saana.