Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,339
- 51,864
UKIWEZA TOFAUTISHA HAYA BASI UMEKOMAA NA UTAKUWA UMEFANIKIWA
Kwa Mkono wa, Robert Heriel
1. UHAI Vs Uzima
Uhai independent Variable
Uzima ni dependent Variable
Unaweza ukawa hai lakini usiwe Mzima
Lakini huwezi kuwa Mzima bila uhai.
Uhai unahusu kuishi kwa ujumla, uzima ni mahususi kwa kuwa na afya njema.
2. PUMZI Vs HEWA
Pumzi ni Nishati ya kumfanya kiumbe awe Hai
Hewa ni Maada ya mkusanyiko wa gesi. Itembeapo huzalisha upepo.
Pumzi huhusishwa na gesi ya Oksijen, ni kusema nishati ya uhai iitwayo pumzi imehifadhiwa kwenye gesi ya Oksijeni
3. AKILI Vs ELIMU
Akili hukupa uhai
Elimu hukupa uzima
Yaani Akili ndio inakufanya uishi wakati elimu inakufanya uishi kwa namna ipi(nzuri)
Akili haina mipaka, elimu ina mipaka, ni mahususi.
4. UZURI Vs UREMBO
Uzuri upo akilini mwa mtu, huanzia ndani kwenda nje, na kamwe uzuri hauwezi anzia nje kwenda ndani..
Urembo upo mwilini, upo nje, hauwezi ingia ndani bali upo nje siku zote.
Uzuri upo siku zote, urembo unabadilika badilika kulingana na wakati na mazingira.
5. WEMA Vs MSAADA
Wema hauna malipo
Msaada una malipo huitwa Hisani/Fadhila.
Wema wenye malipo huitwa Msaada. Hii ni kusema wema unaweza kuwa msaada, ila msaada hauwezi kuwa wema.
Wema hauumi
Msaada unauma hasa pale usipolipwa Hisani.
Ukiona ulitenda jambo fulani kwa mtu alafu ukaumia kisa hakurudisha hisani iwe ya kukwambia Ahsante, jua wewe ni mtoa msaada, huna wema.
Yesu alisema hakuna aliyemwema isipokuwa MUNGU, hata hivyo hatujakatazwa kujitahidi kuwa wema. Ndio maana Vitabu vya dini vinatusihi tujitahidi kuwa wema.
6. GIZA Vs USIKU
Giza lipo akilini/fikarani
Usiku Upo machoni.
Panaweza kuwa usiku lakini mtu akaona Nuru kutokana na akili yake kuwa na Nuru.
Giza linamfanya mtu asione hata kama ni mchana
Usiku hamfanyi mtu asione.
7. NURU Vs MCHANA
Nuru ipo akilini/ Fikarani
Mchana upo machoni
Panaweza kukawa mchana lakini mtu asione kwa sababu akili yake haina Nuru.
8. THAMANI Vs GHARAMA
Thamani ni ulazima wa kitu au jambo
Gharama ni umuhimu wa kitu au jambo
Thamani hulenga watu wote kwa sababu ni jambo//kitu cha lazima.
Gharama hulenga watu wa wachache kwa sababu sio cha lazima.
Vitu vya thamani ni kama vile Ardhi, Hewa,, Mwanga wa jua, Maji kwani watu wote bila hivyo hatuwezi kuendeea kuishi
Vitu vya Gharama ni kama vile Majumba mazuri, Magari, Simu, Vito cha thamani kama dhahabu n.k.
Maisha huwa magumu pale ushindwapo kutofautisha thamani na gharama.
9. UPENDO Vs MAPENZI
Upendo upo Rohoni na moyoni
Mapenzi yapo mwilini na akilini.
Upendo hauishi kwa sababu umezaliwa rohoni, ni mtamu kwa sababu unaishi moyoni.
Mapenzi hayadumu kwa sababu yamezaliwa akilini, na yanatesa kwa sababu yanaishi mwilini..
Kadiri maumbile ya mwili yanavyobadilika ndivyo mapenzi yanavyobadilika, lakini mabadiliko hayo hayaathiri Upendo kwani Roho ya mtu haibadilikagi ni ile ile tangu amezaliwa mpaka atakapoondoka.
10. WAKATI Vs MUDA
Wakati hauishi
Muda unaisha
Wakati hauna usiku wala mchana
Muda unao usiku na mchana
11. UTIMILIFU Vs UKAMILIFU
Utimilifu bila kuwa na kasoro, nyoofu iliyotimia.
Ukamilifu ina pande mbili kuwa na kasoro au kuwa nyoofu.
Kuna watu wanasema Hakuna mwanadamu Mkamilifu, sio kweli, Binadamu ni wakamilifu katika kukosea au katika kupatia. Wapo binadamu waliokuwa wakamilifu kwa kupatia yaani kutenda mema bila kutenda mabaya kama vile AYUBU.
Ayubu 1:1
1 Katika nchi ya Usi paliishi mtu ambaye aliitwa Ayubu. Mtu huyu alikuwa hana hatia, naye alikuwa mkamilifu; alimcha Mungu na kuepukana na uovu.
Kwa leo niishie hapa
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Iringa Mjini
Kwa Mkono wa, Robert Heriel
1. UHAI Vs Uzima
Uhai independent Variable
Uzima ni dependent Variable
Unaweza ukawa hai lakini usiwe Mzima
Lakini huwezi kuwa Mzima bila uhai.
Uhai unahusu kuishi kwa ujumla, uzima ni mahususi kwa kuwa na afya njema.
2. PUMZI Vs HEWA
Pumzi ni Nishati ya kumfanya kiumbe awe Hai
Hewa ni Maada ya mkusanyiko wa gesi. Itembeapo huzalisha upepo.
Pumzi huhusishwa na gesi ya Oksijen, ni kusema nishati ya uhai iitwayo pumzi imehifadhiwa kwenye gesi ya Oksijeni
3. AKILI Vs ELIMU
Akili hukupa uhai
Elimu hukupa uzima
Yaani Akili ndio inakufanya uishi wakati elimu inakufanya uishi kwa namna ipi(nzuri)
Akili haina mipaka, elimu ina mipaka, ni mahususi.
4. UZURI Vs UREMBO
Uzuri upo akilini mwa mtu, huanzia ndani kwenda nje, na kamwe uzuri hauwezi anzia nje kwenda ndani..
Urembo upo mwilini, upo nje, hauwezi ingia ndani bali upo nje siku zote.
Uzuri upo siku zote, urembo unabadilika badilika kulingana na wakati na mazingira.
5. WEMA Vs MSAADA
Wema hauna malipo
Msaada una malipo huitwa Hisani/Fadhila.
Wema wenye malipo huitwa Msaada. Hii ni kusema wema unaweza kuwa msaada, ila msaada hauwezi kuwa wema.
Wema hauumi
Msaada unauma hasa pale usipolipwa Hisani.
Ukiona ulitenda jambo fulani kwa mtu alafu ukaumia kisa hakurudisha hisani iwe ya kukwambia Ahsante, jua wewe ni mtoa msaada, huna wema.
Yesu alisema hakuna aliyemwema isipokuwa MUNGU, hata hivyo hatujakatazwa kujitahidi kuwa wema. Ndio maana Vitabu vya dini vinatusihi tujitahidi kuwa wema.
6. GIZA Vs USIKU
Giza lipo akilini/fikarani
Usiku Upo machoni.
Panaweza kuwa usiku lakini mtu akaona Nuru kutokana na akili yake kuwa na Nuru.
Giza linamfanya mtu asione hata kama ni mchana
Usiku hamfanyi mtu asione.
7. NURU Vs MCHANA
Nuru ipo akilini/ Fikarani
Mchana upo machoni
Panaweza kukawa mchana lakini mtu asione kwa sababu akili yake haina Nuru.
8. THAMANI Vs GHARAMA
Thamani ni ulazima wa kitu au jambo
Gharama ni umuhimu wa kitu au jambo
Thamani hulenga watu wote kwa sababu ni jambo//kitu cha lazima.
Gharama hulenga watu wa wachache kwa sababu sio cha lazima.
Vitu vya thamani ni kama vile Ardhi, Hewa,, Mwanga wa jua, Maji kwani watu wote bila hivyo hatuwezi kuendeea kuishi
Vitu vya Gharama ni kama vile Majumba mazuri, Magari, Simu, Vito cha thamani kama dhahabu n.k.
Maisha huwa magumu pale ushindwapo kutofautisha thamani na gharama.
9. UPENDO Vs MAPENZI
Upendo upo Rohoni na moyoni
Mapenzi yapo mwilini na akilini.
Upendo hauishi kwa sababu umezaliwa rohoni, ni mtamu kwa sababu unaishi moyoni.
Mapenzi hayadumu kwa sababu yamezaliwa akilini, na yanatesa kwa sababu yanaishi mwilini..
Kadiri maumbile ya mwili yanavyobadilika ndivyo mapenzi yanavyobadilika, lakini mabadiliko hayo hayaathiri Upendo kwani Roho ya mtu haibadilikagi ni ile ile tangu amezaliwa mpaka atakapoondoka.
10. WAKATI Vs MUDA
Wakati hauishi
Muda unaisha
Wakati hauna usiku wala mchana
Muda unao usiku na mchana
11. UTIMILIFU Vs UKAMILIFU
Utimilifu bila kuwa na kasoro, nyoofu iliyotimia.
Ukamilifu ina pande mbili kuwa na kasoro au kuwa nyoofu.
Kuna watu wanasema Hakuna mwanadamu Mkamilifu, sio kweli, Binadamu ni wakamilifu katika kukosea au katika kupatia. Wapo binadamu waliokuwa wakamilifu kwa kupatia yaani kutenda mema bila kutenda mabaya kama vile AYUBU.
Ayubu 1:1
1 Katika nchi ya Usi paliishi mtu ambaye aliitwa Ayubu. Mtu huyu alikuwa hana hatia, naye alikuwa mkamilifu; alimcha Mungu na kuepukana na uovu.
Kwa leo niishie hapa
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Iringa Mjini