Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,595
- 215,272
Sukari tunayoihitaji mwilini tunaipata katika vyakula tunavyokula. Chapati, majimbi, viazi, mkate vyote hivi vinatupa sukari. Unaweza kabisa kunywa chai bila sukari.
Wana historia wanasema kabla ya kugundulika kwa sukari, ingawa afya ya meno haikuwa bora kama ilivyo sasa lakini matatizo ya meno hayakuwa makubwa kama tuliyonayo leo.
Unapokunywa chai yenye sukari, inapitia mdomoni, huelewi tu madhara unayopatia meno yako. Chai bila sukari ni salama kwa meno na afya ya mwili kwa ujumla.
Fikiria pia pesa utakayo okoa utakapoacha matumizi ya sukari. Ukitembelewa na mgeni unamfahamisha kabisa mila na desturi ya nyumba yako, unaweza kuwa unatoa ushauri nasaha wa afya bila kujijua.