Ukiwa na vitu hivi halafu upo hivi, Utawamaliza wanawake kwa kweli

Mtanisamehe kwa ninyi ambao ninapozungumzia maisha mazuri huwa mnakasirika. Mtanisamehe maana ndo experience niliyo nayo. ni ngumu sana kwa mtu mvuvi kuzungumzia vizuri habari za kilimo, ndio ilivyo kwangu napata shida sana kuzungumzia shida na matatizo sababu sijawahi kukutana nayo zaidi zaidi nilipokuwa mdogo mama anasema nilikuwa nasumbua sana hasa kunywa maziwa na mayai.

Jana nolitoka ofisini nikawa nimeamua nikale KFC na kufanya mizunguko kadhaa nikaja kutoke mataa ya pale Posta Akiba. Ile sehemu nishaijua kitambo kuna traffic washaifanya kitega uchumi. So wanasubiria tu ukichelewa kidogo kwenye taa ukawa unapita huku zinaishia wanakupiga mkono uwaachie chochote au wakuandikie.

Alinikamata dada mmoja jana akidai nimepita wakati taa ya njano imewaka. Mimi nilikuwa wa pili kutoka mwisho, sijui sababu ni nini akaona anikamate mimi mwenye Range Rover amwache jamaa aliyekuwa na Subaru nyuma yangu. Nimepita nikaona ananipiga mkono. Nikacheck nyuma nikaona kuna subaru nayo ipo inakuja nikajua labda anaisimamisha subaru.

Nikaamua kutii sheria bila shuruti nika indicate kushoto akanionesha nisimame pembeni ambako nipandishe nguzo za barabara. Nikagoma nikasimama barabarani ila pembeni. Mdada akaja mwenyewe kwa maringo akitingisha mwili. Alikuwa mdada mweusi mrefu kiasi,kiuno chembamba na hips zimejitokeza.

Sikuzima gari nikawa namsubiria akaaanza na kuchukua namba ya gari kuingiza kwenye kimashine chake. Baadaye akaja kuangalia kwenye kioo na mwishowe akaja kugonga akitaka nishushe kioo.Nikashusha kioo cha abiria. Alinisalimia habari yako boss@ nikamjibu kifupi tu 'salama'
afande; unajua kosa lako?
mimi : hapana
afande; umevuka wakati taa nyekundu zimewaka
mimi; si kweli. nimevuka wakati taa za kijani zimeruhusu
afande; boss unabisha na mimi nimekuona ndugu yangu... naomba leseni nikuandikie;
mimi: huna cha kuniandikia, na leseni nimeisahau ofisini ukihitaji ntakupatia ila sina kosa.
afande; unaendeshaje gari bila leseni?
mimi: fande kwani sheria inasemaje kuhusu mtu anaposhindwa onesha leseni kwa wakati huo unapohitaji?
afande; kwa hiyo umekataa kulipia kosa la kuvuka wakati wa red right (akimaanisha red light)
mimi: afande xxxx (baada ya kusoma jina lake) nachelewa kazini. sina kosa na kama una ushahidi nioneshe nilipe haraka nataka kuondoka. kama ni suala la leseni twende ofisini.
afande: fatu... naondoka na huyu mheshimiwa kwenda kituoni nakuja...
akapanda kwenye gari.
mimi: funga mkanda
afande: unanijali eeeehhh.... haya boss mjeuri
mimi: tunaenda kituoni au wapi
afande: mi njaa inaniuma unataka unizungushe mpaka wapi au unataka unipeleke kwako ?
mimi: chukua biznez kadi yangu hii nitafute jioni tuzungumze huu ugomvi wetu unaishaje nikatoa nikampa akanambia niende nikamwache pale serena hotel atanitafuta baadaye.

Jioni kweli alinitafuta amechangamka kweli na kuuliza nipo wapi ili tukutane tuongee. Yule afande nimeshamuona ni mtu ambaye kabisa ametamani kuwa na mahusiano na mimi. Usiku katuma meseji ananiita dear. Anataka nikilala nimwote n.k Aliaanza kuniuliza nisije mgombanisha na mke wangu, nilimwambia bado sijaoa.

Akataka kujua nataka kuoa mke mwenye sifa zipi anafanya kazi gani.

Kiufupi huyu dada tayari ameshakuwa ina love with either me au gari na mwonekano wangu. Najiuliza naweezaje ku date mdada mwenye akili kama hii? Huyu si ni tatizo tayari?Leo nimemtumia tsh 50,000 ya lunch. Nikamwambia nipo busy kidogo na vikao ofisini but when i am done nitamtafuta mimi mwenyewe.Kajibu meseji 'thank you love' just like that? ni mdada mzuri sikatai but kichwani nshamuona hana akili.

Ukiwa na gari kali,pesa, mwonekano mzuri utawapanga saa wanawake wapumbavu utabadili tu rangi,maumbo,makabila,dini n.k

Wanawake kuweni na akili .Sisi wengine hatupendi ku date wanawake wapumbavu maana nasikia waaambukiza upumbavu.
Nashida ya ada naomba mchango wako.
 
Shida sana... Mwanaume anaomba omba pesa akibanwa anajidai eti anamjaribu...mijinga sana hii mi CCM ndo inaanzaga hivyo hivyo imeshazoea kuomba omba rushwa.

Hili jitu ni ccm humu jf linajulikana cheki linavyoomba hela mkiambiwa wapenda bribe mnakataa utapumuliwa mkia kenge wewe!
 
Pesa napata kwa njia halali. Sijadhulumu mtu... Acha ni enjoy mkuu. Wale matrafiki nawafahamu wengi wao hawana utulivu. Kanipendea wapi ndo kaniona siku hiyo na anaanza kutaka offer ya chakula?

Jichunguze mkuu unakiburi cha pesa kilichokomaa na kuzaa dharau na unapoelekea utakosa utu. Huyo Dada inawezekana kakupenda kama binadamu wa kawaida mwenye hisia anavyoweza kumpenda lakin wewe kwenye bandiko lako unaonekana umeiashia kusoma kwa ukwasi ulionao, kama Dada huyo ni traffic police marange mangapi yanapita kwenye barabara hiyo, unafikiri Kila marange yanapopita hufanya kama alivyokufanyia?

Mapenzi yanaweza kuanzia popote na katika mazingira yoyote mkuu, niliwahi kupendwa na dada mmoja nilikuwa nauza genge la matunda yeye akiwa lecture wa chuo kikuu, alikuwa mteja wangu tu na aliifahamu kazi yangu ila Mimi nilikuwa sifahamu kazi yake nasikutaka kuifahamu alikuja kuniambia mwenyewe baadaye akataka tuwe wapenzi nikamwambia ninamchumba basi tukaishia hapo tunaheshimiana hadi leo. Kwa hiyo mkuu ni vizuri kutambua mapenzi hayaangalii chochote wapo pia matajiri wanaosumbuka kuwapata waliovutiwa nao, ni hayo tu.
 
Kama angenisimamisha kistaarabu akanambia ana tatizo au kanipenda si shida. Nlichokwazika ni kunibambikia kosa ndo maana nikaeleza yote hayo. Najua naye ni binadamu ana haki ya kupenda na kupendwa but angalia alikoanzia mpaka tukafika hapo... Ndicho kilichonikwaza..

Mkuu hawa maaskari wa barabarani sio malaika ni waajiriwa wa serikalini wana shida zao pia wana majukumu yao nao wanashawishika kama watu wengine....ila kuanika issue nzima kwa kulenga uhalisia sio nzuri sana. Kuwa askari hakumvui uanamke wake bado nae anatamani apendeze na hapo ndo naye anategemea ale kwa njia hiyo.
Ila nakusifu kwa ujasiri wako kama umeruka kishawishi hicho
 
Kama angenisimamisha kistaarabu akanambia ana tatizo au kanipenda si shida. Nlichokwazika ni kunibambikia kosa ndo maana nikaeleza yote hayo. Najua naye ni binadamu ana haki ya kupenda na kupendwa but angalia alikoanzia mpaka tukafika hapo... Ndicho kilichonikwaza..
Mkuu kila kitu lazima kiwe na gia ya kuingilia, kwa akili kama angekusimamisha na kukwambia hivyo si ungemuona chizi, lazima awe na njia ya kuingilia ambayo itaonekana ya kawaida kwa raia kumbuka pale ilikuwa ni road, lakini alipopanda ndani si akasema ana njaa, ulipompa namba si akaanza kukutext dear. Lazima atumie nafasi yake ya kazi kama starting point hapo hamna pa kulaumu hata waalimu, madaktari hufanya vivyohivyo
 
MORAL TO THE STORY: Money is everything, hata kama watu wanasema jamaa anadanganya, I dont care, who does not love to drive a VX, and the likes ?...Maisha ndio haya haya hata mimi ningekuwa napush range nisingemla trafick I would have upgraded my game...OVA..
 
Kwa haya uliyoandika inaonesha wewe si maskini... Maskini wanachukia tajiri anapozungumzia mambo ambayo yanaonesha mafanikio yake. Wanakasirika sana na kutokwa povu



Lakn wenye maisha yenu magumh amewataka radhi mapema maana kumbe jamaa nana experience na roho zenu za kimaskini zilizotamalaki chuki na husuda.
Hongera mkuu. Mm ni maskini ila sina chuki na mwenye nazo
 
Bingwa utagundua JF kuna watu wanachukia sana ukizungumzia mafanikio... Wanatokwa na povu kila sehemu.

MORAL TO THE STORY: Money is everything, hata kama watu wanasema jamaa anadanganya, I dont care, who does not love to drive a VX, and the likes ?...Maisha ndio haya haya hata mimi ningekuwa napush range nisingemla trafick I would have upgraded my game...OVA..
 
Back
Top Bottom