Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,395
Watu wengi wanapozungumzia kuvunjika kwa ndoa au uhusiano, sababu zinazojitokeza sana au kutajwa ni zile za ulevi, kutoka nje ya ndoa, kipato, uchafu, na mengine ya aina hiyo, lakini wanasahau kuwa kuna baadhi ya tabia zenye kukera ambazo kama zisipoangaliwa kwa makini zinaweza kuipeleka ndoa au uhusiano shimoni:
Nitataja baadhi ya tabia hizo kwa uchache ili nisiwachoshe:
1. Kujilinda- ni kitendo cha mwanandoa kutopenda kupingwa, kwa namna yoyote, hata pale inapoonekana dhahiri hayuko sahihi, atatumia muda mwingi kujitetea na kutoa mifano chungu mzima isiyo na kichwa wala miguu.
2. Kutofurahia ukimya- mwanandoa asiyefurahiya ukimya ni yule ambaye mdomo wake unamuwasha wakati wote anapenda kuongea tu, na wakati mwingine huongea utumbo mtupu. Mara nyingi watu wa aina hii hupoteza kumbukumbu ya kile walichosema au walichozungumza muda mfupi ulipita.
3. Utani ulopita kiasi- uchekeshaji ni mzuri sana katika kuboresha ndoa au uhusiano na hujenga afya kwa wanandoa unapotumiwa vizuri. Lakini pale utani unapozidi unakuwa ni kero kwa mwenzako. Utani unakuwa mzuri iwapo utatolewa kwa muda muafaka. Kuna wakati unaweza kukuta mwanandoa anatoa utani wenye kushusha na kutweza bila kujali hisia za mwenzake hii ni hatari sana katika ustawi wa ndoa. Kuna wakati unaweza kukuta mwanandoa roho yake iko juu juu pale wanapotembelewa na wageni maana anakuwa na wasiwasi kuwa mwenzake anaweza kumfanyia utani wa ajabu kabisa nakumuharibia siku na kumuabisha kwa wageni.
Nitataja baadhi ya tabia hizo kwa uchache ili nisiwachoshe:
1. Kujilinda- ni kitendo cha mwanandoa kutopenda kupingwa, kwa namna yoyote, hata pale inapoonekana dhahiri hayuko sahihi, atatumia muda mwingi kujitetea na kutoa mifano chungu mzima isiyo na kichwa wala miguu.
2. Kutofurahia ukimya- mwanandoa asiyefurahiya ukimya ni yule ambaye mdomo wake unamuwasha wakati wote anapenda kuongea tu, na wakati mwingine huongea utumbo mtupu. Mara nyingi watu wa aina hii hupoteza kumbukumbu ya kile walichosema au walichozungumza muda mfupi ulipita.
3. Utani ulopita kiasi- uchekeshaji ni mzuri sana katika kuboresha ndoa au uhusiano na hujenga afya kwa wanandoa unapotumiwa vizuri. Lakini pale utani unapozidi unakuwa ni kero kwa mwenzako. Utani unakuwa mzuri iwapo utatolewa kwa muda muafaka. Kuna wakati unaweza kukuta mwanandoa anatoa utani wenye kushusha na kutweza bila kujali hisia za mwenzake hii ni hatari sana katika ustawi wa ndoa. Kuna wakati unaweza kukuta mwanandoa roho yake iko juu juu pale wanapotembelewa na wageni maana anakuwa na wasiwasi kuwa mwenzake anaweza kumfanyia utani wa ajabu kabisa nakumuharibia siku na kumuabisha kwa wageni.