Ukiwa na Bunge la chama kimoja, inabidi uwe na cabinet yenye watu makini sana

Kingsmann

JF-Expert Member
Oct 4, 2018
4,448
16,311
Sababu kuu ni kwa kuwa maamuzi mengi yatapita tuu bila counter-reasoning, na mtakuja kuona mazuri/madhara yake kwenye implementation ambayo ni kwenye jamii.

Sasa endapo maamuzi yenu yataleta sintofahamu kwa raia, mnakuwa mmejikaanga wenyewee, na kwa kuwa bungeni mko chama kimoja basi kamwe hamuwezi kukwepa lawama.

Mawaziri wa enzi za Nyerere hawakuwa watu wa mchezomchezo, huwezi kumlinganisha Sokoine na Majaliwa kwenye utendaji(mfano tuu). Mawaziri walikuwa ni vichwa haswa kiasi kwamba walikuwa na uwezo wa kuona mbali uzuri ama ubaya wa maamuzi wanayoyapitisha. Mawaziri walikuwa ni watu wazalendo kwelikweli, hawakuwa tayari kuona raia wanajutia kuzaliwa Tanzania.

Kamwe mawaziri wa enzi hizo hakuna ambaye angethubutu kumuambia mwananchi ahame Tanzania kama haridhishwi na maamuzi ya waziri fulani. Hakuna ambaye ana mawazo ya namna hii, na endapo angetokea waziri yeyote akatamka maneno haya japo hata kwa bahati mbaya basi kesho yake angeomba radhi na kuachia wadhifa maana ni fedheha kubwa kwa waziri kuwaambia wananchi kitu kama hicho.

Kazi kwako mama yetu, hao samaki wako bado wabichi, wakunje angali unawaweza.

maxresdefault.jpg
 
Sababu kuu ni kwa kuwa maamuzi mengi yatapita tuu bila counter-reasoning, na mtakuja kuona mazuri/madhara yake kwenye implementation ambayo ni kwenye jamii.

Sasa endapo maamuzi yenu yataleta sintofahamu kwa raia, mnakuwa mmejikaanga wenyewee, na kwa kuwa bungeni mko chama kimoja basi kamwe hamuwezi kukwepa lawama.

Mawaziri wa enzi za Nyerere hawakuwa watu wa mchezomchezo, huwezi kumlinganisha Sokoine na Majaliwa kwenye utendaji(mfano tuu). Mawaziri walikuwa ni vichwa haswa kiasi kwamba walikuwa na uwezo wa kuona mbali uzuri ama ubaya wa maamuzi wanayoyapitisha. Mawaziri walikuwa ni watu wazalendo kwelikweli, hawakuwa tayari kuona raia wanajutia kuzaliwa Tanzania.

Kamwe mawaziri wa enzi hizo hakuna ambaye angethubutu kumuambia mwananchi ahame Tanzania kama haridhishwi na maamuzi ya waziri fulani. Hakuna ambaye ana mawazo ya namna hii, na endapo angetokea waziri yeyote akatamka maneno haya japo hata kwa bahati mbaya basi kesho yake angeomba radhi na kuachia wadhifa maana ni fedheha kubwa kwa waziri kuwaambia wananchi kitu kama hicho.

Kazi kwako mama yetu, hao samaki wako bado wabichi, wakunje angali unawaweza.

View attachment 1868410
Ndio huyu?

IMG_20210723_083919.jpg
 
Back
Top Bottom