Ukiwa kama Mtanzania Mzalendo ukipata nafasi ya kuwa Mshauri wa Rais wa JMT je?

KakaKiiza

JF-Expert Member
Feb 16, 2010
11,555
8,552
Kama Mtanzania mwenye uzalendo na nchi yako na unapenda kuiona nchi hii inafika mahali hata ukiwa nje nchi ukisema mimi ni Mtanzania unajisikia uko kifua mbele, Je katika vitu hivi hapa chini ungemshahuri nini?

(a), Siasa za Africa Mashariki
(b), Mipaka ya Tanzania
(c), Uchumi wa Tanzania
(d), Siasa za Tanzania
(e), Uwekezaji na Mikataba kwa wawekezaji
(f), Elimu ya Tanzania
(g), Kilimo
(h), Ufugaji Tanzania
(I), Huduma za Afya nchini
(j), Ukusanyaji wa Kodi pamoja misamaha ya kodi
(k), Swala la Muungano wa Jamhuri ya Tanzania
Kwa haya machache kwa mtazamo wangu haya ndiyo yanaikwamisha hii nchi katika kujiletea maendeleo ya wananchi wake.
Ukweli ni mengi ila ukipata wasaa wakuwa mshauri wa Rais wa Jamuhuri ya Muhungano wa Tanzania utatoa ushahuri upi katika nyanja nilizozitaja hapo juu.
Kama unalakuongezea unaruhusiwa.
 
nitamshauri akubaliane na kurudishwa kwa Tanganyika, jambo lisilopingika kimtazamo toka kwa raia, na aache kushusha askari wa miamvuli kwenye sherehe anawapa raia ugonjwa wa moyo.
Kama Mtanzania mwenye
uzalendo na nchi yako na unapenda kuiona nchi hii inafika mahali hata
ukiwa nje nchi ukisema mimi ni Mtanzania unajisikia uko kifua mbele, Je
katika vitu hivi hapa chini ungemshahuri nini?

(a), Siasa za Africa Mashariki
(b), Mipaka ya Tanzania
(c), Uchumi wa Tanzania
(d), Siasa za Tanzania
(e), Uwekezaji na Mikataba kwa wawekezaji
(f), Elimu ya Tanzania
(g), Kilimo
(h), Ufugaji Tanzania
(I), Huduma za Afya nchini
(j), Ukusanyaji wa Kodi pamoja misamaha ya kodi
(k), Swala la Muungano wa Jamhuri ya Tanzania
Kwa haya machache kwa mtazamo wangu haya ndiyo yanaikwamisha hii nchi
katika kujiletea maendeleo ya wananchi wake.
Ukweli ni mengi ila ukipata wasaa wakuwa mshauri wa Rais wa Jamuhuri ya
Muhungano wa Tanzania utatoa ushahuri upi katika nyanja nilizozitaja
hapo juu.
Kama unalakuongezea unaruhusiwa.
 
Ushauri wa kumpa ni kuachia madaraka tu, maana sijawahi sikia rais duniani anasema hajui kwanini nchi yake ni masikini
 
Mimi nitamuuliza swali moja tu. IKIWA TANZANIA INA RAIS MTANZANIA NA MAWAZIRI WATANZANIA NA WANAMUDU HIZO KAZI ZAO. iweje watanzania waliobaki hawawezi kupewa kazi hata ya kupiga hotelini ? kazi zote wamechukua wahindi. wakenya na wa south. hawa wa tz ambao si mawaziri wafanye kazi gani ilhali mashamba yao mmeyagawa kwa wageni hao hao wenye kazi ?????????????
 
Honestly, Frankly, mimi sio mzalendo kabisa.

Sina cha kunifanya kuwa mzalendo kwakweli.

Tanzania hatuna cha kunifanya niwe mzalendo.
 
Hakika ningemshauri mengi kuhusu hayo uliyo yataja lakini muda umekwisha 2015 hiyo labda rais ajae.:smile-big:
 
Hakika ningemshauri mengi kuhusu hayo uliyo yataja lakini muda umekwisha 2015 hiyo labda rais ajae.:smile-big:
Bado una nafasi ya kufanya hivyo haujachelewa ukimshauri anaweza akaweka katika State road map ya 2015-2020.
 
Aache kusafiri ovyo na atulie kusikiliza kero za wananchi ili kuujenga uchumi.
 
Aache kabisa kuchezea elimu na kutumia kama mtaji wa kisiasa wamejenga marasa mengi bila ya nyumba ya mwalimu hata moja, kisa tu wapate takwimu kuwa serikali imejenga vyumba vya madara ,,,, wanawapeleka wanafunzi kidato cha kwanza wakiwa hawajui kusoma wala kuandika ili tu waje kusema tumeandikisha idadi kuwa ya wanafunzi kidato cha kwanza, wanaleta propaganda za BRN ili hali walimu wamevunjika moyo kwa kuto walipa madeni yao. Haya yote wanamfanyia mwanafunzi wa hali ya chini huku watoto wa mawazri wote wanasoma nje hii ni dhuluma mbaya sana na tuiangalie ili isiendelee baada ya 2015
 
Aache kabisa kuchezea elimu na kutumia kama mtaji wa kisiasa wamejenga marasa mengi bila ya nyumba ya mwalimu hata moja, kisa tu wapate takwimu kuwa serikali imejenga vyumba vya madara ,,,, wanawapeleka wanafunzi kidato cha kwanza wakiwa hawajui kusoma wala kuandika ili tu waje kusema tumeandikisha idadi kuwa ya wanafunzi kidato cha kwanza, wanaleta propaganda za BRN ili hali walimu wamevunjika moyo kwa kuto walipa madeni yao. Haya yote wanamfanyia mwanafunzi wa hali ya chini huku watoto wa mawazri wote wanasoma nje hii ni dhuluma mbaya sana na tuiangalie ili isiendelee baada ya 2015
Asante umeongea vitu vilivyopo na donda sugu katika tasnia ya Elimu kwani hapo pana hitaji uwajibikaji na panahita umadhubuti kwa Elimu ndo kitu cha msingi katika Taifa.
 
Wana jamvi wasalaam'
kama ningekuwa m/kiti wa hiki chama cha mapinduzi ninge fanya haya:
-kama m/kiti ningepiga marufuku safari nyingi za raisi nje ya nchi ili kuepusha matumizi mabovu ya fedha za umma.
-ningepambana na ufisadi mkubwa ulio ndani ya chama na serikali kwa kumwajibisha yeyote yule bila kujali urafiki wetu hatukukutana barabarani au vichochoroni,na kila ningeshawishi chama kitunge sheria kali za kuwasulubu mafisadi wote wanaokutikana na hatia za ufisadi.
-uongozi wa watu kama mwigulu,nape nnauye,kinana na nisingeuruhusu wala kuupa nafasi maana hawa watu wanamanukato ya rushwa,mauaji,ujangili na kukosa staha katika siasa za watanganyika wa leo.
-mawaziri kama muhongo,lukuvi,mwigulu,chiza,hawa,kawambwa,wassira,nisinge wapa nafasi ya kuteuliwa.
-ninge kataa mfumo wa kurithishana na kupeana madaraka kama ilivyo kwa,makamba jr:ritz 1,v.kawawa,h.mwinyi,g.mgimwa.
-ninge hakikisha maisha bora kwa watanzania wanayapata kwa kutumia rasimalia za ndani.
"hakika ningekuwa mwenyekti wa c.c.m taifa"
 
Wana jamvi wasalaam'
kama ningekuwa m/kiti wa hiki chama cha mapinduzi ninge fanya haya:
-kama m/kiti ningepiga marufuku safari nyingi za raisi nje ya nchi ili kuepusha matumizi mabovu ya fedha za umma.
-ningepambana na ufisadi mkubwa ulio ndani ya chama na serikali kwa kumwajibisha yeyote yule bila kujali urafiki wetu hatukukutana barabarani au vichochoroni,na kila ningeshawishi chama kitunge sheria kali za kuwasulubu mafisadi wote wanaokutikana na hatia za ufisadi.
-uongozi wa watu kama mwigulu,nape nnauye,kinana na nisingeuruhusu wala kuupa nafasi maana hawa watu wanamanukato ya rushwa,mauaji,ujangili na kukosa staha katika siasa za watanganyika wa leo.
-mawaziri kama muhongo,lukuvi,mwigulu,chiza,hawa,kawambwa,wassira,nisinge wapa nafasi ya kuteuliwa.
-ninge kataa mfumo wa kurithishana na kupeana madaraka kama ilivyo kwa,makamba jr:ritz 1,v.kawawa,h.mwinyi,g.mgimwa.
-ninge hakikisha maisha bora kwa watanzania wanayapata kwa kutumia rasimalia za ndani.
"hakika ningekuwa mwenyekti wa c.c.m taifa"

Ndio maana sio mwenyekiti , ukabaki kuwa kijana wa MBOWE na SLAA
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom