Ukiunganisha dot ndo utaelewa: Alitolewa Kakoko bandarini akatolewa Chamriho ujenzi, akatolewa Kalemani Nishati n.k

Mkuu Kichuguu kukosoa na kusifia ni haki yako na ni haki ya kila mmoja.

Naheshimu maoni yako, lakini Rais ana haki ya kuamua nani na nani afanye naye kazi,
Sababu ni zake.
Wala rais halazimishwi kuja hapa kututangazia sababu za kufanya mabadiliko.
Istoshe, wizara za nchi siyo maalum kwa mtu furani kwa kuwa alifanyakazi na furani, ni maamuzi ya rais.
Wala uongozi wa nchi siyo mali ya mtu mpaka iwe ya urithi.
Watu wakarithi mali siyo uongozi.
Endeleeni kulalamika, lakini kazi za nchi zitafanywa na kila mtanzania mwenye sifa.
Comment yako yote iko sahihi lakini bado inakubaliana kabisa na dukuduku za na mtoa hoja ambaye ingawa pia ni speculative. Kama wewe unarithi serikali ambayo mlikuwa pamoja, siyo kuwa uchaguzi umapita na unaanza kuondoa watu mliokuwa nao pamoja bila sababu yoyote ila tu kwa sababu ya utashi na powers ulizonazo harafu kukaanza mambo yasiyoeleka sawasawa kama haya ya bandari ya Bagamoyo ambayo ilikuwa shelved na uliyemrithi, ni wazi unaruhusu speculations kama alizotoa mto mada. Iwapo mama angeshinda uchaguzi akaanza kusuka upya serikali ningeelewa, ila yeye alirithi serikali iliyoachwa na aliyefariki. Hiyo ni tafsiri mbaya ya katiba na abuse ya powers za presidency. Ndiyo maana marekebisho ya katiba ni ya muhimu sana sasa than ever, kwa kuwa kuna somo la ziada tumelipata.
 
Nasema hivo kwa sababu zifatazo:
Kwanza mara tu baada ya Rais Samia kuingia alifanya mabadiliko bandarini akidaiwa kuwa Kakoko ni fisadi na akawekwa chini ya uchunguzi ambao mpaka leo hakuna kilichoelezwa kwa undani tofauti na propaganda! Naweza kuamini kuwa Kakoko alitolewa pale kutokana na msimamo wake tayari kuhusu bandari ya BAGAMOYO amabayo alikuwa anaipinga sana!
Pili Rais Samia alifanya mabadiliko katika vizara ya ujenzi kwa kumtoa Chamriho hili nalo ukiliangalia kwa umakini Chamriho amekuwa katibu mkuu wa wizara ya ujenzi kwa mda mrefu kwa hiyo katika majadiriano ya bandari pendwa ya Msoga team BAGAMOYO alihusika kwa sehemu kubwa na ukizingatia tayari bandari hiyo ulikuwa ishaanza kupata mkwamo team ikaoma hata huyu Eng Chamriho anaweza kuwa kikwazo akawekwa pembeni bila sababu zenye mashiko!
Tatu ukitizama mabadiliko ya hivi karibuni ya kumtoa Kalemani bado utagundua mi mwendelezo wa kuwaondoa watu waliokiwa na msimamo wa kizalendo juu ya mikataba mibovu, hapa unaweza kuona Waziri wa sasa Makamba akifanya mikutano mingi na wawekezaji katika sekta ya gesi, kwa upande mwingine licha ya makamba kupingana na ujenzi wa bwawa la Mwl Nyerere lakini bado kupewa uwaziri ili kutimiza mision ambayo tayari ishapangwa na watawala ya awamu hii ya Sita hususani kwenye eneo la Gesi,eneo ambalo awamu ya nne ilituletea janga kubwa kwa mkataba wa ovyo wa gesi ya mtwara ambayo hata wana Mtwara wenyewe hawajui inafaida gani mpaka leo!
Nne mda si mrefu mtaona mabadiliko pia katika wizara ya nishati na madini sio kwa sababu waziri ni mbovu ila kwa sababu kuna vitu haviendi sawa vya kundi fulani la watu! Siku za hivi karibuni Waziri Biteko amekuwa akishutumiwa kwa ufisadi usio bayana akihusishwa pia na upotevu wa tanzanite kule mererani n.k yote hayo ni dalili kuwa hatakiwi kwenye hiyo wizara na bila shaka Waziri Mchengerwa amabaye huko utumishi alidokeza kuhusu uchunguzi juu ya wizara hii!
Hitimisho,Ikumbukwe kuwa nchi hii sio ya CCM na Sio ya team Msoga, haya yote yanayofanyika ya kuja kuwadanganya watanzania hususani kwenye mradi wa bandari ya BAGAMOYO ni hatari kubwa kwa hapo baadae kama yatafanyika bila umakini mkubwa,Serkali hii asidhanie kuwa watanzania ni wajinga kiasi hicho cha kuruhusu ujenzi wa bandari ambayo utaathiri bandari zetu hususani bandari ya Dar es salaam!
Wewe hizo ni hisia zako tu hazina uhalisia wowote. Mbona ndugai anasema haoni sababu kwanini bandari ya Bagamoyo ilikataliwa. Kwahiyo huoni hao wanaofufua wapo sahihi?
 
Comment yako yote iko sahihi lakini bado inakubaliana kabisa na dukuduku za na mtoa hoja ambaye ingawa pia ni speculative. Kama wewe unarithi serikali ambayo mlikuwa pamoja, siyo kuwa uchaguzi umapita na unaanza kuondoa watu mliokuwa nao pamoja bila sababu yoyote ila tu kwa sababu ya utashi na powers ulizonazo harafu kukaanza mambo yasiyoeleka sawasawa kama haya ya bandari ya Bagamoyo ambayo ilikuwa shelved na uliyemrithi, ni wazi unaruhusu speculations kama alizotoa mto mada. Iwapo mama angeshinda uchaguzi akaanza kusuka upya serikali ningeelewa, ila yeye alirithi serikali iliyoachwa na aliyefariki. Hiyo ni tafsiri mbaya ya katiba na abuse ya powers za presidency. Ndiyo maana marekebisho ya katiba ni ya muhimu sana sasa than ever, kwa kuwa kuna somo la ziada tumelipata.
Leo mnaikosoa Katiba kwa kuwa imewagusa!!
Mwendazake alisema Katiba siyo kipaumbele chake ingawa Ilani ya chama chake imeitaja katiba na majumuisho yake.
Wakati huo hamkusema lolote, mlipiga makofi.

Mkuu kichuguu, wewe ni mmoja wa memba ninaowaheshimu hapa jf, hasa kutokana na michango yako, lakini katika hili sikubaliani nawe.
 
Leo mnaikosoa Katiba kwa kuwa imewagusa!!
Mwendazake alisema Katiba siyo kipaumbele chake ingawa Ilani ya chama chake imeitaja katiba na majumuisho yake.
Wakati huo hamkusema lolote, mlipiga makofi.

Mkuu kichuguu, wewe ni mmoja wa memba ninaowaheshimu hapa jf, lakini katika hili sikubaliani nawe.
Kama unaniheshimu basi hujawahi kusoma posts zangu hapa kuhusu mapungufu ya katiba yetu na umuhimu wa kuyarekebisha. Inabidi upitia mlolongo mrefu kuanzia mwaka 2007! Kuna mambo mengi niliyokubaliana na Magufuli na kuna ambayo sikukubaliana naye, pitia tena post zangu za kuanzia mwaka 2017 untanielewa vizuri. Baadhi ya watu hapa wako too monolithic kuwa you are either on the side of Magufuli or on our side; watu tunaotumia logic hatuko hivyo. Magufuli alifanya mambo mengi sana mazuri kwa nchi ingawa pia alifanya mambo kadhaa mabaya; hakuwa malaika.
 
Hao waliokuwepo walishawahi kujibu kuhusu upotevu wa Trillion 1.5 kwenye ujenzi wa airport Chattle?
Hivi hizi hela zingekuwa zimeliwa kikweli kweli, na ubora wa teknolojia ya sasa mgekuwa kweli mmechelewa kuweka ushahidi namna zilivyoliwa hatua kwa hatua?
 
Statement yako ya mwisho imenena jambo ambalo niliambiwa siku nyingi zilizopita lakini sikutaka kuliamani na wala sijawahi kuliandika. Lisemwalo lipo?
Ndio kinachoenda kutokea ni swala la muda tu 😎
 
Nasema hivo kwa sababu zifatazo:
Kwanza mara tu baada ya Rais Samia kuingia alifanya mabadiliko bandarini akidaiwa kuwa Kakoko ni fisadi na akawekwa chini ya uchunguzi ambao mpaka leo hakuna kilichoelezwa kwa undani tofauti na propaganda! Naweza kuamini kuwa Kakoko alitolewa pale kutokana na msimamo wake tayari kuhusu bandari ya BAGAMOYO amabayo alikuwa anaipinga sana!
Pili Rais Samia alifanya mabadiliko katika vizara ya ujenzi kwa kumtoa Chamriho hili nalo ukiliangalia kwa umakini Chamriho amekuwa katibu mkuu wa wizara ya ujenzi kwa mda mrefu kwa hiyo katika majadiriano ya bandari pendwa ya Msoga team BAGAMOYO alihusika kwa sehemu kubwa na ukizingatia tayari bandari hiyo ulikuwa ishaanza kupata mkwamo team ikaoma hata huyu Eng Chamriho anaweza kuwa kikwazo akawekwa pembeni bila sababu zenye mashiko!
Tatu ukitizama mabadiliko ya hivi karibuni ya kumtoa Kalemani bado utagundua mi mwendelezo wa kuwaondoa watu waliokiwa na msimamo wa kizalendo juu ya mikataba mibovu, hapa unaweza kuona Waziri wa sasa Makamba akifanya mikutano mingi na wawekezaji katika sekta ya gesi, kwa upande mwingine licha ya makamba kupingana na ujenzi wa bwawa la Mwl Nyerere lakini bado kupewa uwaziri ili kutimiza mision ambayo tayari ishapangwa na watawala ya awamu hii ya Sita hususani kwenye eneo la Gesi,eneo ambalo awamu ya nne ilituletea janga kubwa kwa mkataba wa ovyo wa gesi ya mtwara ambayo hata wana Mtwara wenyewe hawajui inafaida gani mpaka leo!
Nne mda si mrefu mtaona mabadiliko pia katika wizara ya nishati na madini sio kwa sababu waziri ni mbovu ila kwa sababu kuna vitu haviendi sawa vya kundi fulani la watu! Siku za hivi karibuni Waziri Biteko amekuwa akishutumiwa kwa ufisadi usio bayana akihusishwa pia na upotevu wa tanzanite kule mererani n.k yote hayo ni dalili kuwa hatakiwi kwenye hiyo wizara na bila shaka Waziri Mchengerwa amabaye huko utumishi alidokeza kuhusu uchunguzi juu ya wizara hii!
Hitimisho,Ikumbukwe kuwa nchi hii sio ya CCM na Sio ya team Msoga, haya yote yanayofanyika ya kuja kuwadanganya watanzania hususani kwenye mradi wa bandari ya BAGAMOYO ni hatari kubwa kwa hapo baadae kama yatafanyika bila umakini mkubwa,Serkali hii asidhanie kuwa watanzania ni wajinga kiasi hicho cha kuruhusu ujenzi wa bandari ambayo utaathiri bandari zetu hususani bandari ya Dar es salaam!
Kwani wao peke yaho ndio wanastahili kukaa pale milele. Na walioingia je, hawana haki hiyo? Tutolee kelele hapa.
 
Ndio kinachoenda kutokea ni swala la muda tu
Hahahahahaha, yaani kinachonichekesha jinsi mlivyopagawa na uongozi wa mama... Hivi mlikuwa tayari kuachia madaraka kweli, kama kweli angalieni tabu mnayopata. Mbaya zaidi ndio kwanza alfajiri..
 
Msitegemee mema yoyote yale katika mchakato huo ambako majizi yamepanga safu ya mashambulizi!

Mission ni bandari ijengwe wapige hela ndefu toka kwa wawekezaji wa kichina😅! Zitaongelewa story nyingi ila ni yale yale tu...

Fanikisheni dili katika zile Trillion 70 mtakula mgao wa 10 Trillion na hapo mzigo unatembea kuanzia kwa mawaziri, Ex boyfrendi wa bibi tozo pamoja na wapambe wake!
TUpo tunawazoom, pamoja na mapungufu yake ila marehemu alitufungua macho kweli! Hakuna mtu anayetaka kujivisha mabomu na kujilipua kwenye mikutano ila ikifika hatua tutaenda hapo jirani kujifunza!
 
TUpo tunawazoom, pamoja na mapungufu yake ila marehemu alitufungua macho kweli! Hakuna mtu anayetaka kujivisha mabomu na kujilipua kwenye mikutano ila ikifika hatua tutaenda hapo jirani kujifunza!
Sana yani alitufumbua macho kweli
 
Hahahahahaha, yaani kinachonichekesha jinsi mlivyopagawa na uongozi wa mama... Hivi mlikuwa tayari kuachia madaraka kweli, kama kweli angalieni tabu mnayopata. Mbaya zaidi ndio kwanza alfajiri..
Unagongwa na wachawi wewe! Yani mie sina presha hata akae miaka 100 ila madhaifu yake ntayasema mtake msitakee
 
Unagongwa na wachawi wewe! Yani mie sina presha hata akae miaka 100 ila madhaifu yake ntayasema mtake msitakee
, mkae kwa kutulia basi. Najua huna pressure yoyote ila vumilia mama agombezi wala hakufokei anafanya kazi kwa kuzingatia washauri wake halafu hakulupuki. Halafu zama za ubabe na kutunisha kifua zimepita.
 
Hivi hizi hela zingekuwa zimeliwa kikweli kweli, na ubora wa teknolojia ya sasa mgekuwa kweli mmechelewa kuweka ushahidi namna zilivyoliwa hatua kwa hatua?
Na mimi nakuuliza swali kwa teknolojia hii wameshindwa kujua Ben Saanane na Azori wako wapi?

Je wameshindwa kujua waliomshambulia Lissu mchana kweupe??

Jibu ni kuwa kulikua na vacuum kubwa sana na civic space was hugely muzzled during Jiwe's autocratic government
 
, mkae kwa kutulia basi. Najua huna pressure yoyote ila vumilia mama agombezi wala hakufokei anafanya kazi kwa kuzingatia washauri wake halafu hakulupuki. Halafu zama za ubabe na kutunisha kifua zimepita.
Spana zitaendelea kama kawaida dhidi ya uhuni wowote utakaofanyika!
We chekelea per diem za safari ila mama yenu lazma aeleweshwe
 
Back
Top Bottom