Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 22,550
- 29,626
Pamoja na ulinzi wa haki za raia kuainishwa kwenye Katiba yetu lakini jeshi la polisi wamekubuhu kusigina katiba kwa kutenda mambo ya hovyo dhidi ya watuhumiwa
1. Mawasiliano
Wananchi wengi wanaokamatwa wanazuiwa kuwasiliana na ndugu zao wawapo kituoni na hili husababisha usumbufu mkubwa kwa watuhumiwa na jamaa zao
2. Hukumu kabla ya mashtaka
Watuhumiwa wengi wa kesi ndogo ndogo kama vile wizi wa kuku, baiskeli na aina hiyo wanapigwa kikatili ili wakiri makosa yao kwenye karatasi za maelezo hivyo wengi hupelekea kupata ulemavu au kupoteza maisha
3. Mahabusu kukaa muda mrefu bila kupelekwa mahakamani
Vituoni kuna tabia ya kuzuia dhamana za baadhi ya watuhumiwa ambao wanadhaminika hadi watoe rushwa na kuna mtindo watuhumiwa wanarundikwa hata zaidi ya mwezi wakiwa vituoni huku wakikosa haki ya kujibu mashtaka au kufutiwa mashtaka yao.
4. Rushwa
Mshtaki na mshtakiwa mara nyingi huombwa rushwa ili kuweka mazingira mazuri ya mwenendo wa kesi pale kituo cha polisi.
6. Kubambikia kesi
Kwa mfano. Mtuhumiwa wa uzururaji kama anatulizwa kituoni zaidi ya wiki mbili kisha anatafutiwa robbery case ili akamuliwe fedha au apotee kabisa...
Kuna vijana wengi wanakamatwa kwa petty cases lakini wakifikishwa vituoni wanapewa "vichwa" yaani kubambikiwa kesi.
Nimeeleza kwa uchache baadhi ya kero lakini naamini wengi humu mnazo kero nyingi dhidi ya jeshi la polisi.
Jeshi letu linapaswa kujikita kwenye jukumu lake la kikatiba la ulinzi wa raia na mali zao.... ushirikiano na mahusiano mazuri baina ya polisi na raia hupelekea kupingua ama kuisha kabisa kwa uhalifu nchini.
IGP boresha jeshi lako liwe lenye tija
Uzi tayari
1. Mawasiliano
Wananchi wengi wanaokamatwa wanazuiwa kuwasiliana na ndugu zao wawapo kituoni na hili husababisha usumbufu mkubwa kwa watuhumiwa na jamaa zao
2. Hukumu kabla ya mashtaka
Watuhumiwa wengi wa kesi ndogo ndogo kama vile wizi wa kuku, baiskeli na aina hiyo wanapigwa kikatili ili wakiri makosa yao kwenye karatasi za maelezo hivyo wengi hupelekea kupata ulemavu au kupoteza maisha
3. Mahabusu kukaa muda mrefu bila kupelekwa mahakamani
Vituoni kuna tabia ya kuzuia dhamana za baadhi ya watuhumiwa ambao wanadhaminika hadi watoe rushwa na kuna mtindo watuhumiwa wanarundikwa hata zaidi ya mwezi wakiwa vituoni huku wakikosa haki ya kujibu mashtaka au kufutiwa mashtaka yao.
4. Rushwa
Mshtaki na mshtakiwa mara nyingi huombwa rushwa ili kuweka mazingira mazuri ya mwenendo wa kesi pale kituo cha polisi.
6. Kubambikia kesi
Kwa mfano. Mtuhumiwa wa uzururaji kama anatulizwa kituoni zaidi ya wiki mbili kisha anatafutiwa robbery case ili akamuliwe fedha au apotee kabisa...
Kuna vijana wengi wanakamatwa kwa petty cases lakini wakifikishwa vituoni wanapewa "vichwa" yaani kubambikiwa kesi.
Nimeeleza kwa uchache baadhi ya kero lakini naamini wengi humu mnazo kero nyingi dhidi ya jeshi la polisi.
Jeshi letu linapaswa kujikita kwenye jukumu lake la kikatiba la ulinzi wa raia na mali zao.... ushirikiano na mahusiano mazuri baina ya polisi na raia hupelekea kupingua ama kuisha kabisa kwa uhalifu nchini.
IGP boresha jeshi lako liwe lenye tija
Uzi tayari