Ukitoza kodi biashara ya kupangisha na ukaboresha ukusanyaji kodi ya majengo,huhitaji fedha za MCC

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,987
144,319
Uamuzi wa wamerekani kutunyima misaada japo utatuathiri zaidi sisi wananchi wa kawaida,bado nauunga mkono kwani utasaidia kuwa-shape watawala wetu.

Pia tutambue ili kuitoa CCCM madarakani, ni lazima tuwe tayari kulipa gharama ya mabadiliko maana hawa jamaa si rahisi kuachia madaraka kirahisirahisi tu bila mashinikizo kama haya ya MCC na mengineyo.

Hata hivyo, siamini kama nchii haiwezi kujitegemea bila msaada wa mataifa ya nje bali tatizo kubwa ni uzembe na kutowajibika ipasavyo katika kubuni na kusimamia vyanzo vya mapato.

Kwa mfano,nchi hii biashara ya nyumba za kupangisha ni biashara kubwa sana na inayolipa kweli kweli kwa wanaomiliki majumba na nyumba za kupangisha ila tu tumeshindwa kuwa na sera na sheria ya kusimamia ukusanyaji wa kodi katika eneo hili.

Kinachotakiwa ni serikali kuandaa sera na pia kutunga sheria kali itakayomlazimisha mtu yoyote mwenye kufanya biashara hii atoe taarifa TRA na katika serikali ya mtaa na kuwe na adhabu kali kwa atakaebainika kufanya biashara hii kwa siri na pasipo kufuata sheria.

Serikali inaweza pia kuwatumia wenyeviti wa vijiji,watendaji wa mitaa na madiwani katika kuwatambua wale wote wanaofanya hii biashara na serikali inaweza kutoa motisha kwa diwani,mwenyekiti au mtendaji ataekaefanya kazi hii vizuri kama vile kuwalipa kwa kamisheni kutokana na makusanyo yatakayopatikana.

Njia mojawapo ni serikali kuandaa fomu maalumu na kuzisambaza kwa watendaji na wenyeviti wa mitaa ambao nao watapaswa kuzisambaza kwa wamiliki wa nyumba au majengo katika vijiji au mitaa yao huku wakiwa na nguvu za kisheria kufanya hivyo na zitakazowalinda dhidi ya mtu yeyote yule atakaejaribu kuwakwamisha kwa namna yoyote ile katika jukumu lao hilo.

Pia kuwe na nafasi ya wamiliki kufika TRA au serikali ya kijiji/mtaa na kutoa update za kimaandishi kama ameuza nyumba au jengo lake,kama ameongeza vyumba,kama ameacha kupangisha,n.k na iwe ni kosa kisheria kutotoa taarifa hizi pale mmiliki anapofanya mabadikiko yoyote yale katika biashara yake hii.

Fomu hizi ziwe maalumu kwa watu kujaza taarifa zao kama kama vile ana ya vyumba au nyumba wanazopangisha,ukubwa wake,bei anazotoza,eneo nyumba au vyumba husika vilipo, n.k.

Mbali na fomu hizo kubeba taarifa muhimu zitakazosaidi ukusanyaji wa kodi,fomu hizi ziambatane na tamko la kisheria kuwa ni kosa kisheria kutoa taarifa za uongo na zitaje adhabu inayoweza kumpata mtu atakaetoa taarifa ya uongo katika kujaza form hizo.

Pia,serikali iongeze nguvu katika ukusanyaji wa kodi ya majengo kwa kuwashirikisha viongozi wa serikali za mitaa na kuweka bayana kuwa kila mwenyekiti wa mtaa au diwani wa eneo husika atalipwa mshahara kutokana na makusanyo ya kodi hizi ikiwemo na kodi itakayotokana na nyumba za kupangisha ila viongozi hawa wataongezewa jukumu la kusimamia ukusanyaji wa mapata haya katika maeneo yao ya kazi na iwe ni moja ya majukumu yao ya kila siku.

Eneo mojawapo ambalo serikali inaweza kukusanya mapato makubwa ni katika maeneo ambako kuna vyuo.Wanafunzi wengi wanapanga mitaani jirani na vyuo wanavyosoma na siku hizi watu wanajenga mahostel maalumu kwa ajili ya kupangisha wanafunzi na wanaingiza fedha nyingi tu pasipo kulipa kodi.

Ukiacha maeneo vilivyoko vyuo mbalimbali,kuna hili swala la mtu mmoja kumiliki fremu kibao za biashara(maduka n.k) katika jengo lake huku fremu zote au baadhi ya frame hizo akizipangisha na anakusanya kodi pasipo yeye kulipa kodi serikalini zaidi tu ya yeye kulipa property tax ya jengo lake.Bei za fremu hizi kila mtu anazijua na unatakiwa ulipe ama kwa miezi 6 au mwaka.Ni hela ngapi hawa watu wanaingiza pasipo kulipa kodi serikalini?

Nchi hii ina majumba na majengo mengi sana yaliyotapakaa nchi nzima mijini na vijijini yanayotumika katika biashara hii ya kupangisha, na nyumba/majengo haya huishia tu kulipiwa property tax wakati yanaingiza fedha nyingi pasipo kulipiwa kodi!

Hivi kweli inaingia akilini mtu mwenye fremu kibao za biashara katika jengo lake anakupangishia fremu unamlipa kodi yake kwa miezi 6 au mwaka mzima na wanakuja TRA nao unawalipa alafu tajiri huyu yeye anaishia kulipa kodi moja tu ya property tax (kodi ya jengo) wakati anazalisha mamilioni bila kuyalipia kodi?Hii haikubaliki hata kidogo.

Hata hivyo,nashauri nyumba za udongo za kupangisha huko vijjini zisihusishwe katika mpango huo kwani wengi wenye hizi nyumba wanatafuta pesa za kujikimu tu kimaisha huko wanakoishi.

Yako na maeneo mengine mengi tu kinachotakiwa ni watu wa TRA kwa kushirikiana na viongozi wa serikali za mitaa kuingia mitaani na kufanya utafiti na sio kukaa maofisini tu.
 
Mkuu,
Kama hakuna Utawala Bora huu ukusanyaji ni kazi bure.

MCC imesitishwa kutokana na nchi kutofuata misingi ya utawala bora.

Sheni hajachaguliwa na Wazanibar, hivyo hayupo kwa ajili ya wazanzibar yupo kwa maslahi ya waliomweka hapo.

So hata tukusanye kama hatuna nidhamu kwa wananchi ni kazi bure
Ntobi.
 
Kama hakuna Utawala Bora huu ukusanyaji ni kazi bure.

MCC imesitishwa kutokana na nchi kutofuata misingi ya utawala bora.

Sheni hajachaguliwa na Wazanibar, hivyo hayupo kwa ajili ya wazanzibar yupo kwa maslahi ya waliomweka hapo.

So hata tukusanye kama hatuna nidhamu kwa wananchi ni kazi bure
Ntobi.
Tuwe wakweli ni nani atie set hiyo misingi ya utawala bora? Je hiyo wanayoita misingi ya utawala bora kwao wanaitumia? Kama hawaitumii kwanini? Kuna wakati hizo nchi zinazo sisitiza utawala bora hazifanyi hivyo.
 
Mkuu,
Kama hakuna Utawala Bora huu ukusanyaji ni kazi bure.

MCC imesitishwa kutokana na nchi kutofuata misingi ya utawala bora.

Sheni hajachaguliwa na Wazanibar, hivyo hayupo kwa ajili ya wazanzibar yupo kwa maslahi ya waliomweka hapo.

So hata tukusanye kama hatuna nidhamu kwa wananchi ni kazi bure
Ntobi.

Utawala bora? nini kimefanyika Rwanda na Uganda, wamebadilisha katiba lakini Marekani kafanya nini?
 
Mmeanza kujirudi...pumbaff
Mngekuwa na akili mngekuwa wabunifu ila mnaleta viburi wakati hamjajipanga matokeoa yake wanaoteseka ni wananchi wa kawaida.Nyinyi ni laana mbinguni na duniani na ndio maana matatizo nchi hii hayaishi.
 
Tatizo si kutokupewa misaada tu Bali kuwekewa vikwazo vya kiuchumi maana hili ndilo tishio haswaa maana kama nchi hatuwezi kuwa kama kisiwa kinachojitegemea kwa kila kitu....

Lakini katika jicho la pili hii mikopo na misaada ni utumwa wa karne hii kwa kuwa umekuwa kama ukomo wa fikra za viongozi wetu katika kuviendeleza vyanzo vingine vya pato la nchi ili kutengeneza uwezekano wa kujitegemea kibajeti ambapo huongeza ufanisi wa bajeti zetu pia....

Deni limekuwa likikua kwa mwendo mkali huku huduma za kijamii zikiwa hazipati afuheni inayohitajika...ningeomba watu wanaohusika wawajibishwe kwa matumizi mabovu maana hapa lazma kuna hujuma iliyofanyika..

** TANZANIA KWANZA **
 
Utawala bora? nini kimefanyika Rwanda na Uganda, wamebadilisha katiba lakini Marekani kafanya nini?

Americans are hypocrites. Eti wanataka kumchagua Donald Trump kuwa rais wao. Huyo ukimwuliza good governance ni nini atakuambia ni al qaida.!
 
Sasa haya mawazo ulikuwa umeyakalia mpaka lowasa awe rais? Ungeyakalia milele!
Nakupongeza kwa hili toka moyoni ingawa najua utaropoka tu, mdomo wako hauna breki!
 
Kwa nini mmtwishe mzigo mtu aliyejinyima kwa miaka kibao akiwa ni mtumishi wa serikali au sekta binafsi kisha akajenga nyumba yake na kuamua kupangisha ili kujikimu ukizingatia hizo pensheni wanazolipwa wastaafu ni pesa ya kununua karanga tu na hupita miezi kibao ndio alipwe.

Kwa nini usishauri marupurupu yote wanayolipwa wabunge kuanzia posho ya vikao hadi pensheni zao zipunguzwe hadi asilimia 60 na pesa hiyo itumike katika miradi ya maendeleo na ikiwezekana wabunge ambao ni mawaziri walipwe mshahara wa uwaziri tu ile pesa wanayopaswa kulipwa kama wabunge nayo ikafanye kazi ya maendeleo ya taifa na watu wake.

Na jingine la msingi ni kuwasaka na kuwashtaki wote wale waliohusika kwa namna moja au nyingine na ubadhirifu na ufisadi wa raslimali ya taifa katika kashfa za epa,richmond,dowans,meremeta radar,escrow,nk na sheria ichukue mkondo wake na mali zote walizopata kwa njia zisizo halali zifilisiwe na kitachopatikana kitumike kwa faida ya wote.Kwanza hizo kodi za majengo toka tumeanza kulipa zimefanya nini zaidi ya kuwabillionaresha kina Masamaki na wenzake?
 
Sasa haya mawazo ulikuwa umeyakalia mpaka lowasa awe rais? Ungeyakalia milele!
Nakupongeza kwa hili toka moyoni ingawa najua utaropoka tu, mdomo wako hauna breki!
Haya mawazo hatujaanza kuyatoa leo ila serikali hii ya CCM ni wabishi na walikuwa wamelewa misaada ila kwakuwa sasa wametoswa hiyo misaada, watalazikika kutafuta vyanzo mbadala vya kodi.
 
Kwa nini mmtwishe mzigo mtu aliyejinyima kwa miaka kibao akiwa ni mtumishi wa serikali au sekta binafsi kisha akajenga nyumba yake na kuamua kupangisha ili kujikimu ukizingatia hizo pensheni wanazolipwa wastaafu ni pesa ya kununua karanga tu na hupita miezi kibao ndio alipwe.Kwa nini usishauri marupurupu yote wanayolipwa wabunge kuanzia posho ya vikao hadi pensheni zao zipunguzwe hadi asilimia 60 na pesa hiyo itumike katika miradi ya maendeleo na ikiwezekana wabunge ambao ni mawaziri walipwe mshahara wa uwaziri tu ile pesa wanayopaswa kulipwa kama wabunge nayo ikafanye kazi ya maendeleo ya taifa na watu wake.Na jingine la msingi ni kuwasaka na kuwashtaki wote wale waliohusika kwa namna moja au nyingine na ubadhirifu na ufisadi wa raslimali ya taifa katika kashfa za epa,richmond,dowans,meremeta radar,escrow,nk na sheria ichukue mkondo wake na mali zote walizopata kwa njia zisizo halali zifilisiwe na kitachopatikana kitumike kwa faida ya wote.Kwanza hizo kodi za majengo toka tumeanza kulipa zimefanya nini zaidi ya kuwabillionaresha kina Masamaki na wenzake?
Naunga mkono mawazo yako ila ni lazima kila aneingiza fedha kulipa kodi ikiwamo wanaotengeneza fedha kupitia biashara hii ya nyumba za kupangisha.
 
Uamuzi wa wamerekani kutunyima misaada japo utatuathiri zaidi sisi wananchi wa kawaida,bado nauunga mkono kwani utasaidia kuwa-shape watawala wetu.

Pia tutambue ili kuitoa CCCM madarakani, ni lazima tuwe tayari kulipa gharama ya mabadiliko maana hawa jamaa si rahisi kuachia madaraka kirahisirahisi tu bila mashinikizo kama haya ya MCC na mengineyo.

Hata hivyo, siamini kama nchii haiwezi kujitegemea bila msaada wa mataifa ya nje bali tatizo kubwa ni uzembe na kutowajibika ipasavyo katika kubuni na kusimamia vyanzo vya mapato.

Kwa mfano,nchi hii biashara ya nyumba za kupangisha ni biashara kubwa sana na inayolipa kweli kweli kwa wanaomiliki majumba na nyumba za kupangisha ila tu tumeshindwa kuwa na sera na sheria ya kusimamia ukusanyaji wa kodi katika eneo hili.

Kinachotakiwa ni serikali kuandaa sera na pia kutunga sheria kali itakayomlazimisha mtu yoyote mwenye kufanya biashara hii atoe taarifa TRA na katika serikali ya mtaa na kuwe na adhabu kali kwa atakaebainika kufanya biashara hii kwa siri na pasipo kufuata sheria.

Serikali inaweza pia kuwatumia wenyeviti wa vijiji,watendaji wa mitaa na madiwani katika kuwatambua wale wote wanaofanya hii biashara na serikali inaweza kutoa motisha kwa diwani,mwenyekiti au mtendaji ataekaefanya kazi hii vizuri.

Njia mojawapo ni serikali kuandaa fomu maalumu na kuzisambaza kwa watendaji na wenyeviti wa mitaa ambao nao watapaswa kuzisambaza kwa wamiliki wa nyumba au majengo katika vijiji au mitaa yao huku wakiwa na nguvu za kisheria kufanya hivyo na zitakazowalinda dhidi ya mtu yeyote yule atakaejaribu kuwakwamisha kwa namna yoyote ile katika jukumu lao hilo.

Pia kuwe na nafasi ya wamiliki kufika TRA au serikali ya kijiji/mtaa na kutoa update za kimaandishi kama ameuza nyumba au jengo lake,kama ameongeza vyumba,kama ameacha kupangisha,n.k na iwe ni kosa kisheria kutotoa taarifa hizi pale mmiliki anapofanya mabadikiko yoyote yale katika biashara yake hii.

Fomu hizi ziwe maalumu kwa watu kujaza taarifa zao kama kama vile ana ya vyumba au nyumba wanazopangisha,ukubwa wake,bei anazotoza,eneo nyumba au vyumba husika vilipo, n.k.

Mbali na fomu hizo kubeba taarifa muhimu zitakazosaidi ukusanyaji wa kodi,fomu hizi ziambatane na tamko la kisheria kuwa ni kosa kisheria kutoa taarifa za uongo na zitaje adhabu inayoweza kumpata mtu atakaetoa taarifa ya uongo katika kujaza form hizo.

Pia,serikali iongeze nguvu katika ukusanyaji wa kodi ya majengo kwa kuwashirikisha viongozi wa serikali za mitaa na kuweka bayana kuwa kila mwenyekiti wa mtaa au diwani wa eneo husika atalipwa mshahara kutokana na makusanyo ya kodi hizi ikiwemo na kodi itakayotokana na nyumba za kupangisha ila viongozi hawa wataongezewa jukumu la kusimamia ukusanyaji wa mapata haya katika maeneo yao ya kazi na iwe ni moja ya majukumu yao ya kila siku.

Eneo mojawapo ambalo serikali inaweza kukusanya mapato makubwa ni katika maeneo ambako kuna vyuo.Wanafunzi wengi wanapanga mitaani jirani na vyuo wanavyosoma na siku hizi watu wanajenga mahostel maalumu kwa ajili ya kupangisha wanafunzi na wanaingiza fedha nyingi tu pasipo kulipa kodi.

Ukiacha maeneo vilivyoko vyuo mbalimbali,kuna hili swala la mtu mmoja kumiliki frame kibao za biashara katika jengo lake huku frame zote au baadhi ya frame hizo akizipangisha na anakusanya kodi pasipo yeye kulipa kodi serikalini zaidi tu ya yeye kulipa property tax ya jengo lake.Bei za frame hizi kila mtu anazijua na unatakiwa ulipe ama kwa miezi 6 au mwaka.Ni hela ngapi hawa watu wanaingiza pasipo kulipa kodi serikalini?

Yako na maeneo mengine mengi tu kinachotakiwa ni watu wa TRA kwa kushirikiana na viongozi wa serikali za mitaa kuingia mitaani na kufanya utafiti na sio kukaa maofisini tu.
Wewe hujajenga ndio maana unamwonea wivu baba mwenye nyumba unayoishi. Hili lingewezekana ikiwa kila Mtanzania angelazimishwa kujaza ritani ya mwaka ya mapato yake; kwa kufanya hivyo kila mpangaji angeweka bayana kiasi cha kodi ya nyumba anayolipa na anamlipa nani.
 
Na wapangaji tujiandae kukipa kodi kubwa. Maana siku zote end user ndiye anayeumia. Chumba cha sh 30,000 kitakuwa 50,000. Au la mkataba utasomeka kodi sh 10,000 ili tax iwe elf 4. Ilhali analipa elf 30.
 
Tatizo siyo MCC tatizo tunalogomba ni kunyimwa haki ndani ya nchi yetu! Serikali inayonyima haki siwezi kushirikiana nayo kamwe!
 
Na wapangaji tujiandae kukipa kodi kubwa. Maana siku zote end user ndiye anayeumia. Chumba cha sh 30,000 kitakuwa 50,000. Au la mkataba utasomeka kodi sh 10,000 ili tax iwe elf 4. Ilhali analipa elf 30.
Uko sawa; kama mwenye nyumba ameandikishwa kwenye kodi ya VAT; kodi ya pango ya TZS 30,000 lazima uongeze 18% ya VAT yaani TZS 5,400 hivyo mpangaji atalipa TZS 35,400 ambazo TZS 30,000 ni za mwenye nyumba na TZS 5,400 zinaenda TRA. Mwenye nyumba yeye atalipishwa kodi ya 10% yaani atalipa TZS 3,000 toka kwenye kodi ya TZS 30,000. Seriklai itapata jumla ya TZS 8,400 toka kwenye huu mwamala.
 
Na wapangaji tujiandae kukipa kodi kubwa. Maana siku zote end user ndiye anayeumia. Chumba cha sh 30,000 kitakuwa 50,000. Au la mkataba utasomeka kodi sh 10,000 ili tax iwe elf 4. Ilhali analipa elf 30.
Tatizo hii biashara imeachwa kuwa ni biashara holela kila mtu anajipangia anavyotaka.Inabidi serikali ingilie kati na kuwe na sheria ya kudhibiti biashara hii kama inavyofanya kwenye mafuta na kwenye bidhaa zingine.
 
Back
Top Bottom