MKITAKA POLISI WAWAHI KWENYE TUKIO MTAANI AU KIJIJINI KWENU; WAAMBIENI CHADEMA HAWA HAPA WANATAKA KUFANYA MKUTANO
TUKIO likitokea huku Mtaani kwetu Siku hizi, huwa hatupati shida kupata msaada wa haraka kutoka Polisi, ni fasta tu wanatia timu eneo husika. Wakishuka tu kwenye Gari wanaanza kuuliza, CHADEMA wako wapi?
Wakishafika karibu yetu, ndipo tunawaeleza aina ya tukio kama ni Uvamizi, Moto, Ajali ama tukio lililotokea kwa wakati huo.
Zamani ilikuwa tukipiga simu Polisi kutafuta msaada wa haraka wanajibu kwamba, wana Mafuta kidogo sana kwenye Gari ama hawana Askari wa kutosha Kituoni kwao.
Siku hizi ukisema tu; CHADEMA hawa hapa wanataka kuhutubia Mkutano jukwaani na tayari Wananchi wameshajaa, Polisi hawa hapa ndani ya Difenda huku wakiwa na silaha nzito nzito na Mabomu kibao.
Siku hizi raha sana!
TUKIO likitokea huku Mtaani kwetu Siku hizi, huwa hatupati shida kupata msaada wa haraka kutoka Polisi, ni fasta tu wanatia timu eneo husika. Wakishuka tu kwenye Gari wanaanza kuuliza, CHADEMA wako wapi?
Wakishafika karibu yetu, ndipo tunawaeleza aina ya tukio kama ni Uvamizi, Moto, Ajali ama tukio lililotokea kwa wakati huo.
Zamani ilikuwa tukipiga simu Polisi kutafuta msaada wa haraka wanajibu kwamba, wana Mafuta kidogo sana kwenye Gari ama hawana Askari wa kutosha Kituoni kwao.
Siku hizi ukisema tu; CHADEMA hawa hapa wanataka kuhutubia Mkutano jukwaani na tayari Wananchi wameshajaa, Polisi hawa hapa ndani ya Difenda huku wakiwa na silaha nzito nzito na Mabomu kibao.
Siku hizi raha sana!