Ukitaka kuua taifa na utaifa, wanyime watu uhuru wa kuhoji na kutowa mawazo yao

doriani

Member
Nov 24, 2019
42
38
Ukitaka kuuwa taifa na utaifa, wanyime watu uhuru wa kuhoji na kutowa mawazo yao. Ukitaka kuuwa Demokrasia, wanunue wabunge na wawakilishi wa watu waungane na watawala, wape marupurupu mazuri kutokana na kodi za watawaliwa, wapige msasa wageuke kuwa tabaka maalumu lisiloweza kuhojiwa au kukosolewa, wafanye kuwa waione kazi ya ubunge na Uwakilishi kuwa kazi ya kudumu kwa udi na uvumba, wape nyenzo za kulinda nafasi zao. Mshahara na posho nono, pencheni na kifuta jasho mwishoni mwa kipindi chao, katikati ya umaskini uliokithiri.

Tangaza demokrasia na utawala bora kwa jina tu kuvutia misada kutoka nje na wawekezaji. Wagawe wabunge na Wawakilishi kwa misingi ya hoja za Chama Tawala na hoja za wapinzani katika misingi kama hoja hizo ni za manufaa kwa taifa. Endesha serikali kwa usiri mkubwa ili watu wasijuwe yanayotendeka,wasitukizie kwa kila jambo.

Sahau kabisa lugha ya mtu mdogo na maskini, kwani hana cha kukupa wala kuchagua katika taifa, hapo utakuwa umepanuwa ufa kati ya walionacho na wasio kuwa nacho.

Zikemee Mahkama na Bunge kwa maamuzi usio ya penda wewe. Wakemee waandishi kwa kuandika mambo yanayowaamsha jamii. Jifanye kuwa taifa ndio wewe na wewe ndio taifa. Hapo utakuwa umefanikiwa kujiundia bomu la kukulupukia wewe mwenyewe.

Wazee wanatwambia madaraka yote Hulevya, lakini madaraka makubwa Hulevya zaidi, mtu mpe madaraka atayatumia vibaya, lakini mpe madaraka makubwa zaidi atayatumia vibaya zaidi.

Katika kipindi hiki cha utanda wazi, haitupasi kuzichukulia kelele za watu wadogo kama kelele za watu wasio na maana la kutwambia. Hatupaswi kutangaza demokrasia na utawala bora juu ya mapaa ya nyumba kwa sababu tu ya kuvutia misada.

Hali hiyo imepelekea raia kuwaigopa watawala na watawala wanawaogopa raia. Watawala wanaogopa kuulizwa, na raia wanaogopa kuuliza.
 
Kawe Alumni. Mbona una kosa nidhamu ya mjadala au lugha yapili kwako ni lugha ya waswahili ambayo wewe kwko sio lugha yako? Kubweka kwenu kwa lugha yenu ya asili manayake nini mwenzangu? Kwani wewe wa Mkoa gani ukinambia nitakufahamu vyema bila ya kulijibu suala nililokuuliza maana ni tajuwa mpaka tabia yako, chakula chako, mavazi yako na mwenendo mzima wa maisha na tabia zako ila unambie umetokea mkoa gani na kama utaficha kunambia basi nitakuhisabu kuwa ni mtu dhaifu sana. "kubweka"
 
Democracy
Africa ni majanga tuu,Hata uwape katiba kutoka Mbingini,
-Mwafrika si mtawala,wala hafai kuwa kiongozi wa wenzake.
-Sioni hata nchi moja Afrika iliyo na nafuu,
-Tazama Kule Libya,Wale jamaa waliochanganya damu na waarabu ,wamechagua democracy ya kuuwana wenyewe kwa wenyewe kuliko kuwa chini ya Beduwi (Ghadafi) aliye wapa kila wakitakacho
-Kama bara la Afrika tutahitaji Uongozi uliotukuka,tuwaite wazungu au waarabu wawe watawala wetu.
-Tunaweza kuwaajiri kwa mikataba maalumu.Kama mae part tu
-Kwa sisi tuliotawaliwa na Muingereza twendeni kwa Malkia tumombe atupe Mjuku wake aje atutawale ili nchi yetu ipige hatu.
-Kwa rasilimali hizi tulizonazo,tukipata kiongozi Bora ,basi ndani ya muda mfupi neema itaenea kwa raia wote.
-lakini kwa kuendelea kuwatawalisha hawa jamaa zetu ambao hawanaga hata historia ya uongozi na hawajawahipo kuwa na CV ya Kuweza kuongoza hata kikundi cha watu kumi,Lazima taifa liendelee kudidimia.
 
Back
Top Bottom