Ukitaka kuishi vizuri Dar es Salaam ishi Kigamboni

Kigamboni (sasa ni wilaya) ni sehemu ya jiji la Dar es Salaam ambayo tofauti na maeneo mengine ilichelewa kuendelezwa kimiundombinu mpaka kufika miaka ya 90 .Watu walichelea kuishi huko kutokana na kupaona ni maporini palipostahili kuishi wanyama.

Hivi leo,mambo ni tofauti sana,mji unakua kwa kasi ya ajabu, barabara zinajengwa kutangulia makazi ya watu,ni sehemu pekee katika jiji la Dar es Salaam ambako ukiingia unasahau kuhusu foleni za barabarani , hali ya hewa ni nzuri kutokana kutokuwepo kwa ujenzi holela wa nyumba, ni karibu sana na city centre na kuna fursa nyingi za kuanzisha biashara.

Binafsi nilifika kwa mara ya kwanza na kuhamia kigamboni mwaka 2015 kutoka Survey maeneo ya karibu na Mlimani city nilipoishi kwa takribani miaka minne,ila mpaka kufikia leo sijawahi kujutia kuishi huku wala kuwaza kuhamia mahali pengine katika mji huu kutokana na sifa nilizozitaja hapo juu na kwa bahati nzuri Mungu amenijaalia kujenga kakibanda huku huku.

Kwa ambao hawajawahi kufika huku hudhani kwamba Kigamboni ni kisiwa na kwamba usafiri pekee wa kufika huku ni wa kuvuka maji kwa pantoni, la hasha! Kigamboni si kisiwa bali imetenganishwa na sehemu nyingine ya jiji kwa sehemu ya bahari iliyoingia nchi kavu (ghuba) ambayo ni bandari ya Dar es Salaam na Kwa sasa ukiachilia usafiri wa wa pantoni kuna daraja na baraba mbili ambazo unaweza kupita bila hata kuiona hiyo bahari.

Karibuni sana Kigamboni.
hapana mku, kigamboni hapafai kabisa, kama ni kwa sababu ya bahari tu sawa lkn kuna changamoto ya usafiri sana, nilifikia huko niliona tabu zake, nilitakiwa kuamka saa 9 usiku kwenda stendi ya Magufuli mbezi, siwezi kuishi mbali na kituo cha mabasi ya kwenda mikoani.
Mpango mzima sasa ni Mbezi, Luguruni, kibamba, kiluvya na kibaha.
 
wadaslam kuwaondolea kigamboni ni Temeke kichwani ni ngumu sana ila uzuri wake inakuzwa na middle income class na real estate projects, baada ya muda itakuwa ni habari nyingine maana vitu kama tatizo la usafiri si kitu permanent
 
Shida kweli kweli na ma gharama yani ina maana wewe kuvuka itakulazimu upoteze 90-100K per months kwenda na kurudi kwako! Huu ujinga ndio unanifanya kigamboni sitaki hata kupasikia

Kabisa mkuu ukipita darajani kule unaacha 1500 go and return
 
Ukitaka mwisho wako wa Kutembea kutokana na Vibaka na Majambazi kuwa wengi na Kula Kwako Bata ( Kustarehe ) kuwe ni Saa 12 Jioni, basi kaishi Kigamboni.
Acha fix wewe. Mimi kuna siku nakaa huko Juliana,samaki samaki Hadi saa Saba nane na ninarudi Kigamboni usiku sina mlinzi geti nafungua mwenyewe. Niliishi miaka mitatu bila geti
 
hapana mku, kigamboni hapafai kabisa, kama ni kwa sababu ya bahari tu sawa lkn kuna changamoto ya usafiri sana, nilifikia huko niliona tabu zake, nilitakiwa kuamka saa 9 usiku kwenda stendi ya Magufuli mbezi, siwezi kuishi mbali na kituo cha mabasi ya kwenda mikoani.
Mpango mzima sasa ni Mbezi, Luguruni, kibamba, kiluvya na kibaha.

Uber hazipo, bajaj za shida hasa usiku ukipata uber ubhatike feri ila anaweza asije. Bora niishi buza sio kigamboni
 
Wakati mwingine foleni ya magari kuingia kwenye kivuko inapita ofisi ya waziri mkuu hadi chuoni
Yan mm ndo nafikiria kuhama huku kigamboni nihamie tegeta nyuki maana stress za kuvuka na ma panton haya imenishinda aiseehh. sometimes bora folen kulko ule ujinga wa kuvuka maji
 
Kigamboni imebadilika sana mkuu huku mambo moto na hayo mambo yalikua miaka nyuma.Kigamboni ndo mji utakao kua umepangika vizuri sana hata masaki huko na obey watapasikia tu ...
Kigamboni panamfaa kwanza mtu asiye na Mambo mengi uwe saa 1 usiku upo kwako nje ya Hapo uwe na usafiri wako. Gari za abiria zinakata saa mbili tu .
 
Back
Top Bottom