Huwa namshangaa sana kiongozi anayewashauri watu wajiajiri!
Kujiajiri Tanzania inabidi kwanza ujitoe ufahamu kabla ya kupata faida!
Ebu fikilia haya malipo ya serikali yalivyo hayana uhalisia!
Yapo mengi sana wafanyabiashara tunadhulumiwa na selikali kuna wakati natamani katiba iseme wazi kabisa! KIONGOZI YOYOTE LAZIMA AWE MFANYABIASHARA Mwenye biashara ya jina lake iliyofanya kazi angalau miaka 10 na kuendelea! Labda itasaidia kutuelewa tunavyoumia wafanyabiashara.
Manispaa wanapata pesa za bure sana na sielewi kwanini LESENI ZAO zisiwe bure au wapunguze anagalau bei ya juu kabisa kwa duka,yard au kampuni isizidi lakimoja!
Na ikiwrzekana makao makuu ya ofisini ilipo ndipo inatakiwa kulipiwa leseni na huko kwenye matawi ipelekwe nakala au walipie kwa nusu bei!
Ndiyo maana VIONGOZI wakitumbuliwa au kustaafu hutamani tena teuzi kwasababu mazingira ya biashara wanajua yalivyo magumu sana!
Kujiajiri Tanzania inabidi kwanza ujitoe ufahamu kabla ya kupata faida!
Ebu fikilia haya malipo ya serikali yalivyo hayana uhalisia!
- Unatafta wazo la biashara,mtaji na fursa lakini TRA hawanaga grace period kwa wafanyabiashara wadogo kama ilivyo kwa uwekezaji mkubwa
- TRA hawana muda wa kufikilia TIN zenye msamaha wa kodi kwa wafanya biashara wanaoanza!
- Malipo ya pango la biashara lazima mfanyabiashara ukalipie 10% ...wakati aliyetakiwa kutoa hiyo ni mwenye nyumba ulipo panga wewe! Lakini kwasababu mfanyabiashara unashida wanakubana wewe!
- HATA mtu hujafanya biashara mwaka huo wa usajili TRA ikifikia kufaili return za mwaka lazima mahesabu yako yahakikiwe na kampuni ya uhasibu editor firm ambako gharama zipo juu sana hadi laki tano au zaidi hata kama UNAFAILI NIL (yaani hujafanya biashara), sijui kwanini Sera na sheria ya TRA wasingeweka utaratibu mrahisi kwa biashara changa ufaili hata kwa mhasibu personal wa kawaida kwa miaka 5 ya kwanza
- Halmashauri na manispaa pasipo kukupa msaada wowote, ukifuata leseni wanakutoza pesa kuanzia elf 80 hadi laki tano kulingana na biashara yako! Tena kibaya zaidi unawafuata ofisini kwao ukapange foleni hata juisi ya kufuta jasho la nauli kwa kuwapelekea pesa ofisini hawakupi, sasa ebu jiuloze pesa zote hizo manispaa wanachukua kwa mchango UPI waliompa mfanyabiashara kama siyo dhulma?
- Malipo ya leseni yanaumiza sana kwasababu kwanza hawajishughulishi hata kukupa elimu ya biashara, hawakutaftii wateja hawakupi ofa yoyote zaidi ya kukukamua tena wakiwa ofisini kwao.
- Ukifanikiwa kufungua matawi ya biashara yako, ajabu kila manispaa utaombwa kulipia mfano! Kama leseni ni tsh 350000 ukiweka tawi kila wilaya utatakiwa kuilipa pesa hiyo kila wilaya utazani ni nchi tofauti wakati uko Tanzania moja
- Yote tisa kote pesa wamechukua pasipo hata grace period, ukitaka kuweka bango la kujitangaza biashara yako watakuja Kudai ULIPIE BANGO Lako la kujitangaza, wanakuchaji kwa square meter.
- Ukishalipa bei ya leseni manispaa bado unatakiwa kulipia TOZO ya leseni hiyo hiyo kila mwezi
- Brela ukilipa na kusajiliwa bado wanataka Uendelee kuilipia TOZO certificate ya brela (Return au faini kila mwezi wakati wameshakusajili)
- Ukituma unakatwa makato
- Ukipokea unakatwa
- Ukinunua kiwanja unakatwa VAT na ukitoa pesa kwenye akaunti unakatwa TOZO
- Ukinunua umeme Tozo, ukilala Giza TOZO ya pango
Yapo mengi sana wafanyabiashara tunadhulumiwa na selikali kuna wakati natamani katiba iseme wazi kabisa! KIONGOZI YOYOTE LAZIMA AWE MFANYABIASHARA Mwenye biashara ya jina lake iliyofanya kazi angalau miaka 10 na kuendelea! Labda itasaidia kutuelewa tunavyoumia wafanyabiashara.
Manispaa wanapata pesa za bure sana na sielewi kwanini LESENI ZAO zisiwe bure au wapunguze anagalau bei ya juu kabisa kwa duka,yard au kampuni isizidi lakimoja!
Na ikiwrzekana makao makuu ya ofisini ilipo ndipo inatakiwa kulipiwa leseni na huko kwenye matawi ipelekwe nakala au walipie kwa nusu bei!
Ndiyo maana VIONGOZI wakitumbuliwa au kustaafu hutamani tena teuzi kwasababu mazingira ya biashara wanajua yalivyo magumu sana!