Ukistaajabu ya Professor Lipumba utakutana na Professor Bana

si huyo wako wengi wanaopotosha kuna siku nilimsikia mtu ameitwa kuja TBC1 naye anasema mfumo wa vyama vingi umeanza mwaka 1992 wakati wote tunajua vyama vingi vilikuweo maka tunaata uhuru vikaja kupigwa marufuku baadae inawezekana ni zao la walimu wa sasa ambao hata historia ya nchi hawaijui
 
Yaani nikisikia tu mwandishi wa habari anamhoji huyu Bana kuhusu uchambuzi fulani!nahama kabisa hiyo station ya radio,yaani hawezi kabisa kuficha hisia zake kwa kupendelea upande fulani
 
Ukistaajabu ya Profesa Lipumba ambae ni Alhaji utakutana nayo ya Profesa Bana ambae pia ni Mhadhiri wa siasa wa Chuo Kikuu Dar es Salaam lakini kwa bahati mbaya zaidi hajui historia ya Zanzibar wala haijui vizuri Katiba ya Jamhuri ya Muungano wala Katiba ya Zanzibar.

Jana wakati anahojiwa na kituo cha redio ya Ujerumani DW mada miaka 54 ya Muungano wetu Demokrasia na Haki za Binadamu anasema muungano wetu huu ndio ulioleta mfumo wa vyama vingi kabla ya muungano hakukuwa na mfumo wa vyama vingi amesahau kama Zanzibar.

Siasa za vyama vingi zimeanza toka mwaka 1954 kabla ya Tanganyika haijapata uhuru kulikuwa na ZPP ASP ZNP sijui alikusudia wingi gani huyu Profesa wakati huo Zanzibar hata idadi ya watu laki mbili haijatimia hapo hapo Profesa huyo anasema ikiwa mtu hajaridhika na matokeo ya uchaguzi ya urais anaweza kwenda Mahakamani.

Amesahau kama Katiba zote mbili ya Zanzibar na Muungano zinasema kwamba matokeo yote ya urais hayatohojiwa na Mahakama yeyote ile ya rufaa sijui katiba ipi aliyoisoma Profesa huyu Bana.

Nilimsikia kwa bahati mbaya nikasikitika sana!
 
Huyu bwana nilisoma naye pale UD, yeye alijiunga chuoni akiwa mtu mzima. Sijui kama alitokea kazini au mtaani. Alidharaulika na kila mmoja, kwanza kutokana na masomo aliyokuwa akisomea yaani somo la Development Studies (ndiyo lilikuwa major subject yake). Wengine wote somo hilo lilikuwa subsidiary, na kwa ujumla tulilazimishwa kusoma.

Pili tulimdharau sana kutokana na uwezo wake mdogo wa kujenga hoja, na kupenda kuongea sana mambo yasiyokuwa ya maana. Tulimchukulia kama comedian.

Leo na yeye eti ni doctor wa huo upuuzi aliokuwa anasomea kiasi cha kupewa nafasi ya kuchambua masuala ya siasa!
Mkuu Bams,nakumbuka siku moja pale Container - UDSM,Bana aliambiwa na "Khamis Kichaa" (hope UDSM Alumni wa early 1990s mwamfahamu) kuwa kama huyu naye anakuwa msomi basi Taifa lina hasara.
 
Kuna watu wanamudu masomo ya darasani vizuri mpaka kufikia uprofesa (Lipumba, Bans etc). Lakini kutumia elimu yao kwa manufaa ya jamii na taifa kwa ujumla ni ZERO. Na hasa unapojifanya kada!!!!
Kumkosoa mtu ni rahisi kuliko kumsifia. Prof. Bana hata kama alikosea siyo kwa sababu haijui Historia. Amenifundisha PS & PA, he is highly knowledgeable on Tanzania's politics especially Public Administration. Wangekuwa wanaikosoa Serikali ndo mgewasifia siyo? Ndiyo maana watu wanawaona wapinzani kuwa mpaka Leo hii bado wanafanya uanarakati, badala ya kujijenga kufanya siasa za kitaasisi. Anyway mtafanyaje siasa za kitaasisi wakati hamtaki kujenga Ofisi yenu sasa za Wilaya zitajengwa lini?
 
Bana ni moja kati ya wasomi wachumia tumbo, wabinafsi na wasiyo na huruma! Nidhani km anawafundisha vizuri wanafunzi wake kwa weledi stahiki, bila shaka atakuwa anawalisha matango poli kwa makusudi. Nchi haiwezi kujikomboa kupitia aina hii ya wasomi km Bana, Lipumba na Kitila Mkumbo, bado tuna safari ndefu mno
 
Ukistaajabu ya Profesa Lipumba ambae ni Alhaji utakutana nayo ya Profesa Bana ambae pia ni Mhadhiri wa siasa wa Chuo Kikuu Dar es Salaam lakini kwa bahati mbaya zaidi hajui historia ya Zanzibar wala haijui vizuri Katiba ya Jamhuri ya Muungano wala Katiba ya Zanzibar.

Jana wakati anahojiwa na kituo cha redio ya Ujerumani DW mada miaka 54 ya Muungano wetu Demokrasia na Haki za Binadamu anasema muungano wetu huu ndio ulioleta mfumo wa vyama vingi kabla ya muungano hakukuwa na mfumo wa vyama vingi amesahau kama Zanzibar.

Siasa za vyama vingi zimeanza toka mwaka 1954 kabla ya Tanganyika haijapata uhuru kulikuwa na ZPP ASP ZNP sijui alikusudia wingi gani huyu Profesa wakati huo Zanzibar hata idadi ya watu laki mbili haijatimia hapo hapo Profesa huyo anasema ikiwa mtu hajaridhika na matokeo ya uchaguzi ya urais anaweza kwenda Mahakamani.

Amesahau kama Katiba zote mbili ya Zanzibar na Muungano zinasema kwamba matokeo yote ya urais hayatohojiwa na Mahakama yeyote ile ya rufaa sijui katiba ipi aliyoisoma Profesa huyu Bana.
Duh! Domo lake bana.
 
Siioni tofauti kati ya Dr Bana na Lusinde.
Nadhani kwa hapa hujamtendea haki Lusinde. Heri ya Lusinde kwani hajajiita profesa na anakiri kabisa kuwa alitoroka umande lakini huyu...wewe acha tu! Mimi hofu yangu ni kwa vijana anaowafundisha, kweli hawajazi ujinga kama huu tunaoushuhudia kila leo? Kama UDSM ingekuwa ile ya miaka ileee, ubao wa historia (punch) ya wakati huo ungemfunza adabu.
 
Niliwahi kutoa orodha ya maprofesa na ma PhD holders wengi tu jinsi wanavyoshusha hamasa ya vijana kusoma hadi ngazi hiyo. Yaani wengi wao wana upeo mdogo was ufahamu na ueledi huwezi amino kuwa ni profesa. Sasa huyu dk Bana ndio walewale PhD holders wa kitanzania ambao upeo wao no finyu na wanadhalilisha taaluma zao.
 
Ukistaajabu ya Profesa Lipumba ambae ni Alhaji utakutana nayo ya Profesa Bana ambae pia ni Mhadhiri wa siasa wa Chuo Kikuu Dar es Salaam lakini kwa bahati mbaya zaidi hajui historia ya Zanzibar wala haijui vizuri Katiba ya Jamhuri ya Muungano wala Katiba ya Zanzibar.

Jana wakati anahojiwa na kituo cha redio ya Ujerumani DW mada miaka 54 ya Muungano wetu Demokrasia na Haki za Binadamu anasema muungano wetu huu ndio ulioleta mfumo wa vyama vingi kabla ya muungano hakukuwa na mfumo wa vyama vingi amesahau kama Zanzibar.

Siasa za vyama vingi zimeanza toka mwaka 1954 kabla ya Tanganyika haijapata uhuru kulikuwa na ZPP ASP ZNP sijui alikusudia wingi gani huyu Profesa wakati huo Zanzibar hata idadi ya watu laki mbili haijatimia hapo hapo Profesa huyo anasema ikiwa mtu hajaridhika na matokeo ya uchaguzi ya urais anaweza kwenda Mahakamani.

Amesahau kama Katiba zote mbili ya Zanzibar na Muungano zinasema kwamba matokeo yote ya urais hayatohojiwa na Mahakama yeyote ile ya rufaa sijui katiba ipi aliyoisoma Profesa huyu Bana.
Wameshachoka sana hata uwezo wa kufikiri ni zero
 
Ukistaajabu ya Profesa Lipumba ambae ni Alhaji utakutana nayo ya Profesa Bana ambae pia ni Mhadhiri wa siasa wa Chuo Kikuu Dar es Salaam lakini kwa bahati mbaya zaidi hajui historia ya Zanzibar wala haijui vizuri Katiba ya Jamhuri ya Muungano wala Katiba ya Zanzibar.

Jana wakati anahojiwa na kituo cha redio ya Ujerumani DW mada miaka 54 ya Muungano wetu Demokrasia na Haki za Binadamu anasema muungano wetu huu ndio ulioleta mfumo wa vyama vingi kabla ya muungano hakukuwa na mfumo wa vyama vingi amesahau kama Zanzibar.

Siasa za vyama vingi zimeanza toka mwaka 1954 kabla ya Tanganyika haijapata uhuru kulikuwa na ZPP ASP ZNP sijui alikusudia wingi gani huyu Profesa wakati huo Zanzibar hata idadi ya watu laki mbili haijatimia hapo hapo Profesa huyo anasema ikiwa mtu hajaridhika na matokeo ya uchaguzi ya urais anaweza kwenda Mahakamani.

Amesahau kama Katiba zote mbili ya Zanzibar na Muungano zinasema kwamba matokeo yote ya urais hayatohojiwa na Mahakama yeyote ile ya rufaa sijui katiba ipi aliyoisoma Profesa huyu Bana.
Profesa Domo la kumwaga
 
Siioni tofauti kati ya Dr Bana na Lusinde.
Yaani unajua hata Profesa Maji Marefu anawazidi hawa jamaa kwa logic? Profesa Bana, Profesa Lipumba na Profesa Kitila, hawa jamaa ni balaa tupu. kwa uprofesa wa aina hii, hata Lusinde ni Profesa. Profesa Kibajaji.
 
Toka lini Dr. Bana ameshakuwa Profesa? Kwa merit zipi? UDSM is now a dieying donkey. Kuna yule Profesa wa kujibizana na Maaskofu kwa mabarua utafikiri yeye ni msemaji wa serikali.
Nahisi u professor uliishia kwa akina Haroub Othman.Napendekeza Generali Ulimwengu tumpe u professor hapa jamii forum kwa hawa wa vyuo vikuu noma tu sijui njaa
 
Back
Top Bottom