kakuruvi
JF-Expert Member
- Sep 2, 2009
- 770
- 256
''Ukisikia paaa jua imekukosa, aliyepiga amefanya makosa'', ni nini hii, ni risasi.
Kuna kitu kimoja kinakera sana, nilijaribu kuuliza nikaambiwa si hitilafu ni makusudi tu, kitu hicho ni mlio wa pikipiki unaosikika kama risasi, wajuvi wanasema kuna kitu waendesha pikipiki wanafanya wanapoingiza gia namba mbili kutokee mlio wa risasi.
Kinachokera ni usumbufu wanaopata watu hasa wazee, wajawazito na watoto lakini hata baadhi ya wagonjwa na wasio wagonjwa milio hiyo inastusha kama hukuitarajia, tunaomba vyombo husika vitoe onyo kama jambo hili linafanyika makusudi. Mwenye ujuzi zaidi juu ya hili atuelimishe zaidi kama ni hitilafu au kusudi, nawatakia siku njema.
Kuna kitu kimoja kinakera sana, nilijaribu kuuliza nikaambiwa si hitilafu ni makusudi tu, kitu hicho ni mlio wa pikipiki unaosikika kama risasi, wajuvi wanasema kuna kitu waendesha pikipiki wanafanya wanapoingiza gia namba mbili kutokee mlio wa risasi.
Kinachokera ni usumbufu wanaopata watu hasa wazee, wajawazito na watoto lakini hata baadhi ya wagonjwa na wasio wagonjwa milio hiyo inastusha kama hukuitarajia, tunaomba vyombo husika vitoe onyo kama jambo hili linafanyika makusudi. Mwenye ujuzi zaidi juu ya hili atuelimishe zaidi kama ni hitilafu au kusudi, nawatakia siku njema.