Ukishangaa ya musa

vukani

JF-Expert Member
Dec 30, 2009
245
165
Hivi unajua kisa cha huu msemo wa "ukishangaa ya Musa utakutana na ya Firauni?

Haya ungana na mimi katika simulizi ya kisa hiki……

Hapo zamani sana enzi za himaya ya Firauni (Farao) kulikuwa na mivutano ya kimamlaka kati yake na Musa.(Yule Musa anyesimuliwa katika Biblia, aliyewatoa wana wa Israel kule utumwani Misri na kuwapeleka katika nchi ya ahadi)
Firauni alikuwa akishidana na Musa ambaye alikuwa akiongozwa na Mungu.
Basi ilikuwa ni kawaida watu kwenda kwa Firauni kupeleka mashauri yao inapotokea kutofautiana.


Firauni alikuwa akitolea maamuzi mashauri hayo, ambapo maamuzi yake mengi hayakuwa na haki na yalijaa utata mtupu. Lakini ikatokea baadhi ya watu wakawa hawaendi tena kwa Firauni kwa kuwa walipoteza imani kwake na badala yake wakawa wanaenda kwa Musa ambaye alikuwa akisifika sana kwa kutoa maamuzi ya haki na yaliyokubalika na pande mbili.

Basi ilitokea mtu mmoja alikuwa akisafiri kwa miguu, kutoka mji mmoja kwenda mji mwingine, na kama unavyojua zamani kulikuwa hakuna usafiri wa magari au ndege, sana sana ilikuwa ni ngamia tu.

Wakati akiwa njiani akiendelea na safari yake alijisikia njaa na kwa mbali aliona shamba la mahindi, alipofika katika shamba hilo akakata mahindi mawili matatu na kukoka moto pale pale shambani na kuyachoma kisha akala na baada ya kushiba akaondoka zake na kuendela na safari yake…
Mara mwenye shamba akafika katika shamba lake na kukuta kuna mahindi yame katwa na kuchomwa pale pale shambani na kuliwa, akaamu kufuatilia nyayo za mwizi wake..

Yule mtu alikuwa akiendelea na safari yake bila kujua kuwa kuna mtu anamfuatilia nyuma.
Wakati akiendelea na safari yake mara akaona njiwa mzuri aliyenona yuko juu ya mti, akaokota jiwe na kumrushia yule njiwa na kumpiga sawia.
Akamchukua na na kumchinja, shida ikawa ni wapi atapata moto ili amchome njiwa wake na kumla.

Alipoangalia kwa mbali aliona kuna moshi unafuka, akaamua kuufuata ule moshi mpaka akatokea kwenye kijumba kimoja cha masikini mmoja na mkewe, alipobisha hodi akatoka mama moja mjamzito kwenye hiyo nyumba. Mama huyo alikuwa peke yake kwani mumewe alikuwa hayupo alikwenda kuhemea kijiji cha jirani.
Yule mama alikuwa amekoka moto nje ya nyumba kwa ajili ya kupikia, yule bwana akaomba ambanike njiwa wake, akaruhusiwa.

Wakati anambanika yule njiwa alikuwa akinukia ile mbaya, kiasi cha kumtamanisha yule mama mwenye mji,lakini kutokana na kutomjua yule bwana akaogopa kumuomba.
Basi yule bwana alipomaliza kubanika njiwa wake na kuiva akaaga zake na kuondoka huku akitafuna njiwa wake na kuendelea na safari.

Huku nyuma yule mama kutokana kutamani sana yule njiwa akapata uchungu sana kwa kitendo cha yule bwana kuondoka bila hata kumpa kipande cha nyama,na kutokana na kuwa na kisirani na hasira mimba ikatoka.
Mumewe aliporudi akamkuta mkewe amelala nje ya nyumba akiugulia kwa maumivu ya tumbo,alipomchunguza akagundua kuwa mimba imetoka.

Alipomdadisi, mkewe akamsimulia kisa cha yule mpita njia na njiwa wa kubanika kuwa ndio sababu ya mimba kutoka. Yule bwana akawa anamuhudumia mkewe, na mara yule bwana aliyeibiwa mahindi katika shamba lake akafika pale na kukuta yale matatizo, na baada ya kusimuliwa habari ya mpita njia na njiwa wa kubanika ndipo na yeye alipoeleza kisa cha kuibiwa na mahindi na kumtuhumu mpita njia na njiwa wa kubanika kuwa ndiye muhusika.

Ikabidi waungane muibiwa mahindi na yule, mkewe aliyepoteza ujauzito kumfuatilia yule mpita njia.
Hawakwenda umbali mrefu wakamkuta mpita njia amejipumzisha chini ya mti akipunga upepo, wakamkamata na kumweleza makosa yake, mpita njia akajitetea kuwa hakuiba mahindi bali alikata na kuchoma pale pale shambani kutokana na njaa na kuhusu mimba kutoka alikanusha kuhusika kwa sababu yeye alijichomea njiwa wake na kujiondokea zake baada ya kuruhusiwa na yule mama mwenye nyumba na wala hakujua lililotokea nyuma yake.

Wale watu hawakumuelewa na wakakata shauri wampeleke kwa Musa ili kumshitaki.
Walipofika kwa Musa, wote walisikilizwa kila mtu kwa nafasi yake na baadaa ya Musa kutafakari akatoa hukumu kuwa yule bwana aadhibiwe kwa kuchapwa bakora kisha aondoke zake….

Duh!! Ile hukumu haikuwaridhisha wale jamaa, ikabidi waende kwa Firauni, wakitegemea kupata haki zaidi kwani hukumu ya Musa waliiona kama imempendelea yule mpita njia.

Walipofika kwa Firauni, kama kawaida yake aliwasikiliza wote kila mtu kwa nafasi yake, kisha akatoa hukumu.

Hukumu nyenyewe inasemaje…soma hapa chini…

Firauni akasema yule mpita njia akabidhiwe shamba avune mazao yote kisha apande upya na kuyatunza mpaka yafikie katika hatua kama ile aliyoikuta ndipo amkabidhi mwenye shamba lake. Na kuhusu yule bwana ambaye mkewe alipoteza ujauzito, akasema yule mke akabidhiwe kwa mpita njia akakae nae mpaka apate ujauzito, ukishafikia miezi kama ile iliyotoka amrejeshe kwa mwenyewe….

Duh!!! Jamaa wakachanganyikiwa na ile hukumu wakaondoka pale kwa Firauni kimya kimya na wakamua kumsamehe mpita njia kwani hakuna aliyekuwa tayari kutekeleza ile hukumu.
Na hapo ndipo ulipozuka msemo wa "Ukishangaa ya Musa utakutana na ya Firauni"
 
Hivi unajua kisa cha huu msemo wa “ukishangaa ya Musa utakutana na ya Firauni?

Haya ungana na mimi katika simulizi ya kisa hiki……

Hapo zamani sana enzi za himaya ya Firauni (Farao) kulikuwa na mivutano ya kimamlaka kati yake na Musa.
Firauni akitaka kushindana na Musa ambaye alikuwa akiongozwa na Mungu.
Basi ilikuwa ni kawaida watu kwenda kwa Firauni kupeleka mashauri yao inapotokea kutofautiana na Firauni alikuwa akitoles maamuzi hayo, ambapo maamuzi yake mengi hayakuwa na haki na yalijaa utata mtupu. Lakini ikatokea baadhi watu wakawa hawaendi tena kwa Firauni kwa kuwa walipoteza ikani kwake na badala yake wakawa wa\nenda kwa Musa ambaye alikuwa akisifika sana kwa kutoa maamuzi ya haki na yaliyokubalika na pande mbili.

Basi ilitokea mtu mmoja laikuwa akisafiri kwa miguu, kutoka mji mmoja kwenda mji mwingine, na kama unavyojua zamani kulikuwa hakuna usafiri wa magari au ndege, sana sana ilikuwa ni ngamia tu.
Wakati akiwa njiani akiendelea na safari yake alijisikia njaa na kwa mbali aliona shamba la mahindi, alipofika katika shamba hilo akakata mahindi mawili matatu na kukoka moto pale pale shambani na kuyachoma kasha akyana na baada ya kushiba akaondoka zake na kuendela na safari yake…
Mara mwenye shamba akfika katika shmba lake na kukuta kuna mahindi yame katwa na kuchomwa pale pale shmbani na kuliwa, akaamu akufuatilia nyayo za mwizi wake..

Yule mtu alikuwa akiendelea na safari yake bila kujua kuwa kuna mtu anfuatilia nyuma.
Wakati akiendelea na safari yake mara akona njiwa mzuri aliyenona yuko juu yamti, akokota jiwe na kumrushia yule njiwa na kumpiga sawia.
Akamchukua na na kumcjinja shida ikawa ni wapi atapata moto ili amchome njiwa wake na kula.
Alipoangalia wka mbali aliona kuna moshi unafuka, akaamua kuufuata ule moshi mpaka akatokea kwenye kijumba kimoja cha masikini mmoja na mkewe, alipobisha hodi akatoka mama moja mjamzito kwanye ya nyumba, mumewealikuwa hayupo amekwenda kuhemea kijiji cha jirani.
Yule mama alikuwa amekoka moto nje ya nyuma kwa ajili ya kupikia, yule bwana akaomba ambanike njiwa wake, akaruhusiwa.

Wakati anambanika yule njiwa alikuwa akinukia ile mbaya, kaisi cha kumtamanisha yule mama mwenye mji,lakini kutokana na kutomjua yule bwana akaogopa kumuomba.
Basi yule bwana alipomaliza kubanika njiwa wake na kuiva akaaga zake na kuondoka huku akitafuna njiwa wake.
Huku nyuma yule mama kutokana kutamani san yule njiwa kapata uchungu san kw kitendo cha yule bwana kuondo abila hata kumpa kipande cha nyama,a kuytokamna na kuwa na kisirani mamba ikatoka.
Mumewe aliporudi akamkuta mkewe amelala nje ya nyumba akiugulia kw maumivu ya tumbo,alipomchnguza akagundua kuwa mamba imetoka.

Alipomdadisi, mkewe akamsimulia kisa cha yule mpita njai na njiwa wa kubanika kuwa ndio sababu ya mimba kutoka. Yule bwana akawa anmuhudumia mkewe, na marayule bwana aliyeibiwa mahindi yake shamba akafika pale na kukuta yale matatiz na baada ya kusimuliwa habari yam pita njia na njiwa wa kubanika ndipo nay eye alipodai kuwa anamtafuta mtu huyo huyo kwa kosa la kumuibia mahindi yake katika shamba lake .

Ikabidi waungane muibiwa mahindi na yule, mkewe aliyepoteza ujauzito kufuatilia yule mpita njia.
Hawakukwenda umbali mrfu wakmkuta mpita njia amjipumzisha chini yamti akipunga upepo, wakamkamata na kumwelza makosa yake, mpta nijia akajitetea kuwa hakuiba mahindi bali alikata na kuchoma ple pale shambani kutokana na njaa na kuhusu mamba kutoka alikanusha kuhusika kwa sababi yeye alijichomea njiwa wake na kujiondoke zake na wakla hakun=jua lililotokea nyuma yake.

Wale watu hawakumuelewa na wakakata shauri wampeleke kwa Musa ili kumshitaki.
Walipofika mkwa Musa, wote walisikilizwa kila mtu kwa nafasi yake na baadaa ya Musa kutafakari aktoa hukumu kuwea yule bwana aadhibiwe kwa kuchapwa bakora kasha aondoke zake….
Duh!! Ile hukumu haikuwaridhisha wale jamaa, ikabidi waende kwa Firauni, wakitegemea kupata haki zaiedi kwani hukumu ya Musa waliiona kama imempendelea yule mpita njia.

Walipofika kwa musa liwasikiliza wote kila mtu na nafasi yake, kasha akatoa hukumu.
Hukumu nyenyewe inasemaje…tega sikio…

Firauni akasema yule mpita njia akbiziwe shamba avune mazao yote kisha apande upya na kuyatunza mpaka yafikie katika hatua kama ile aliyoikuta ndipo amkabidhi mwenye shamba lake. Na kuhusu yule mkewe aliyepoteza ujauzito, yule mke akabidhiwe kw mpita njia akakae nae mpaka apate ujauzito, ukishafikia miezi kama ile iliyotoka amrejeshe kwa mwenyewe….
Duh!!! Jamaa wakachnganyikiwa na ile hukumu wakondoka pale kwa Firauni kimya kimya na wakamua kumsamehe mpita njia kwani hakuana aliyekuwa tayari kutekeleza ile hukumu.
Na hapo ndipo ulipozuka msemo wa “Ukishangaa ya Musa utakutana na ya Firauni”

Imenichekesha saaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaana tu jamani!!!!!
 
ha ha very nice lol lakini mi nilikuwa najua huu msemo umetokana na ile story ya kwenye bible pale Musa alipoenda kwa Firauni na kumuomba awaachie wana wa israel wakamtumikie Mungu wao naye akasema toa ishara Musa akaweka fimbo yake chini ikageuka nyoka watu wakashaaa maajabu ya musa lkn firauni akaauru waganga wake na wenyewe wafanye mambo nao wakaangusha fimbo zao na kugeuka nyoka watu wakashangaa tena haaaa


"am just thinking"
 
Hivi unajua kisa cha huu msemo wa “ukishangaa ya Musa utakutana na ya Firauni?

Haya ungana na mimi katika simulizi ya kisa hiki……

Hapo zamani sana enzi za himaya ya Firauni (Farao) kulikuwa na mivutano ya kimamlaka kati yake na Musa.(Yule Musa anyesimuliwa katika Biblia, aliyewatoa wana wa Israel kule utumwani Misri na kuwapeleka katika nchi ya ahadi)
Firauni alikuwa akishidana na Musa ambaye alikuwa akiongozwa na Mungu.
Basi ilikuwa ni kawaida watu kwenda kwa Firauni kupeleka mashauri yao inapotokea kutofautiana.


Firauni alikuwa akitolea maamuzi mashauri hayo, ambapo maamuzi yake mengi hayakuwa na haki na yalijaa utata mtupu. Lakini ikatokea baadhi ya watu wakawa hawaendi tena kwa Firauni kwa kuwa walipoteza imani kwake na badala yake wakawa wanaenda kwa Musa ambaye alikuwa akisifika sana kwa kutoa maamuzi ya haki na yaliyokubalika na pande mbili.

Basi ilitokea mtu mmoja alikuwa akisafiri kwa miguu, kutoka mji mmoja kwenda mji mwingine, na kama unavyojua zamani kulikuwa hakuna usafiri wa magari au ndege, sana sana ilikuwa ni ngamia tu.

Wakati akiwa njiani akiendelea na safari yake alijisikia njaa na kwa mbali aliona shamba la mahindi, alipofika katika shamba hilo akakata mahindi mawili matatu na kukoka moto pale pale shambani na kuyachoma kisha akala na baada ya kushiba akaondoka zake na kuendela na safari yake…
Mara mwenye shamba akafika katika shamba lake na kukuta kuna mahindi yame katwa na kuchomwa pale pale shambani na kuliwa, akaamu kufuatilia nyayo za mwizi wake..

Yule mtu alikuwa akiendelea na safari yake bila kujua kuwa kuna mtu anamfuatilia nyuma.
Wakati akiendelea na safari yake mara akaona njiwa mzuri aliyenona yuko juu ya mti, akaokota jiwe na kumrushia yule njiwa na kumpiga sawia.
Akamchukua na na kumchinja, shida ikawa ni wapi atapata moto ili amchome njiwa wake na kumla.

Alipoangalia kwa mbali aliona kuna moshi unafuka, akaamua kuufuata ule moshi mpaka akatokea kwenye kijumba kimoja cha masikini mmoja na mkewe, alipobisha hodi akatoka mama moja mjamzito kwenye hiyo nyumba. Mama huyo alikuwa peke yake kwani mumewe alikuwa hayupo alikwenda kuhemea kijiji cha jirani.
Yule mama alikuwa amekoka moto nje ya nyumba kwa ajili ya kupikia, yule bwana akaomba ambanike njiwa wake, akaruhusiwa.

Wakati anambanika yule njiwa alikuwa akinukia ile mbaya, kiasi cha kumtamanisha yule mama mwenye mji,lakini kutokana na kutomjua yule bwana akaogopa kumuomba.
Basi yule bwana alipomaliza kubanika njiwa wake na kuiva akaaga zake na kuondoka huku akitafuna njiwa wake na kuendelea na safari.

Huku nyuma yule mama kutokana kutamani sana yule njiwa akapata uchungu sana kwa kitendo cha yule bwana kuondoka bila hata kumpa kipande cha nyama,na kutokana na kuwa na kisirani na hasira mimba ikatoka.
Mumewe aliporudi akamkuta mkewe amelala nje ya nyumba akiugulia kwa maumivu ya tumbo,alipomchunguza akagundua kuwa mimba imetoka.

Alipomdadisi, mkewe akamsimulia kisa cha yule mpita njia na njiwa wa kubanika kuwa ndio sababu ya mimba kutoka. Yule bwana akawa anamuhudumia mkewe, na mara yule bwana aliyeibiwa mahindi katika shamba lake akafika pale na kukuta yale matatizo, na baada ya kusimuliwa habari ya mpita njia na njiwa wa kubanika ndipo na yeye alipoeleza kisa cha kuibiwa na mahindi na kumtuhumu mpita njia na njiwa wa kubanika kuwa ndiye muhusika.

Ikabidi waungane muibiwa mahindi na yule, mkewe aliyepoteza ujauzito kumfuatilia yule mpita njia.
Hawakwenda umbali mrefu wakamkuta mpita njia amejipumzisha chini ya mti akipunga upepo, wakamkamata na kumweleza makosa yake, mpita njia akajitetea kuwa hakuiba mahindi bali alikata na kuchoma pale pale shambani kutokana na njaa na kuhusu mimba kutoka alikanusha kuhusika kwa sababu yeye alijichomea njiwa wake na kujiondokea zake baada ya kuruhusiwa na yule mama mwenye nyumba na wala hakujua lililotokea nyuma yake.

Wale watu hawakumuelewa na wakakata shauri wampeleke kwa Musa ili kumshitaki.
Walipofika kwa Musa, wote walisikilizwa kila mtu kwa nafasi yake na baadaa ya Musa kutafakari akatoa hukumu kuwa yule bwana aadhibiwe kwa kuchapwa bakora kisha aondoke zake….

Duh!! Ile hukumu haikuwaridhisha wale jamaa, ikabidi waende kwa Firauni, wakitegemea kupata haki zaidi kwani hukumu ya Musa waliiona kama imempendelea yule mpita njia.

Walipofika kwa Firauni, kama kawaida yake aliwasikiliza wote kila mtu kwa nafasi yake, kisha akatoa hukumu.

Hukumu nyenyewe inasemaje…soma hapa chini…

Firauni akasema yule mpita njia akabidhiwe shamba avune mazao yote kisha apande upya na kuyatunza mpaka yafikie katika hatua kama ile aliyoikuta ndipo amkabidhi mwenye shamba lake. Na kuhusu yule bwana ambaye mkewe alipoteza ujauzito, akasema yule mke akabidhiwe kwa mpita njia akakae nae mpaka apate ujauzito, ukishafikia miezi kama ile iliyotoka amrejeshe kwa mwenyewe….

Duh!!! Jamaa wakachanganyikiwa na ile hukumu wakaondoka pale kwa Firauni kimya kimya na wakamua kumsamehe mpita njia kwani hakuna aliyekuwa tayari kutekeleza ile hukumu.
Na hapo ndipo ulipozuka msemo wa “Ukishangaa ya Musa utakutana na ya Firauni”


....Utastaajabu ya Firauni.
It is very nice.
 
Mi nikitazama naona wote wawili Musa na Firauni walikuwa bogus katika maamuzi yao!..Musa nae, how come mtu aliyetenda kama huyu mgeni aadhibiwe kuchapwa viboko?
Anyway, ni hadithi hii!
Aksante Mkuu!
 
Mi nikitazama naona wote wawili Musa na Firauni walikuwa bogus katika maamuzi yao!..Musa nae, how come mtu aliyetenda kama huyu mgeni aadhibiwe kuchapwa viboko?
Anyway, ni hadithi hii!
Aksante Mkuu!
PJ tupe uamuzi wako ingekuwa wewe ungefanyaje!??
 
Back
Top Bottom