Ukisema Jini tayari kuna majini miatatu karibu yako. Kila mtoto mchanga huguswa na jini dakika moja bada ya kuzaliwa. Vitabu vya dini vinasemaje?

UHUSIANO ULIOPO KATI YA BINADAMU NA MAJINI,UNAJUA VITABU VYA DINI VINAWAZUNGUMZIAJE MAJINI?






VIUMBE MAJINI NI NINI?NA WANAFANYA NINI?VIPI MAHUSIANO KATI YA MAJINI NA BINADAMU?VITABU VITAKATIFU VINAZUNGUMZIAJE HILI SUALA?

Majini ni viumbe ambao wameumbwa kwa Moto na walikuwa wakiishi duniani kabla ya binadamu miaka Milioni nyingi iliyopita.
Viumbe hawa wana tabia kubwa mbili;

Yaani ya kibinadamu kwa maana wanakuwa wanafanya mapenzi, wanazaa na wanakufa.
Tabia nyingine ni ya Kimalaika ambayo ni kwamba wana uwezo wa kujigeuza katika umbo lolote wanalotaka na vile

vile wanaruka na kwenda wanakotaka au kupita wanakotaka bila kutumia chombo chochote.
Taifa la Majini limegawanyika katika makabila Milioni Sabini na mbili (72,000,000) na wana uwezo wa kujifunza lugha yeyote wanaoitaka.

Idadi ya Majini ni kila Binadamu mmoja kuna Majini 300 na wanaishi katika Majumba yetu, kwenye Miti, Majangwani, Kwenye Mapango na Sehemu zenye Misitu Mikubwa.

Majini wako katika aina Mbili (2); Maruhani na Mashetani.
Maruhani ni Majini wema ambao wanamtii Mwenyezi Mungu na wanawasaidia Binadamu katika mambo mengi.
Mashetani ni Majini Waovu ambao ni wakorofi na wanawaletea Watu madhara na Matatizo mara kwa mara.
Baba wa Majini anaitwa JANN ambaye kimaumbile yeye ana tofauti ndogo na wenzie kwamba yeye ameumbwa kwa ulimi wa Moto.

Pamoja na mambo mengi wanayoyafanya Majini na kujihusisha na binadamu, Majini vilevile wanafanya kazi za Malaika hasa zile za mambo ya kupeleka Habari na kuwalinda Binadamu, mambo ya doria za Angani. Kazi hizi siyo zao lakini kwa vile wanapenda kuiga mambo basi huiga hata kazi ambazo siyo zao.

Majini na Binadamu wana sifa zinazofanana kwani wote wana akili na wote watahesabiwa siku ya Kiama na watazawadiwa kwa mema yao na maovu yao, wote wanakula na kuzaa.
Kama ilivyo, kuna wataalamu wa Kijini wenye fani sawa na Wataalamu wa Kibinadamu wenye kufanya kazi zinazofanana.

Tofauti kubwa iliyopo kati ya Majini na Binadamu ni kwamba; Majini hawana maumbile maalum na wana uwezo wa kujibadilisha katika maumbile mbalimbali ingawa wengi wa Majini wapo katika maumbile ya paka, nyoka na ndege.
Binadamu wao wana umbile maalum ambalo halibadiliki.
Majini wana uwezo wa kuwaingia Binadamu wakati Binadamu hawana uwezo wa kuwaona Majini isipokuwa kwa ufundi maalum.

Namna Majini wanavyowaingia Binadamu iko katika njia tatu:-
1.
2. Njia ya kwanza (1): ni kama Remote Control; Hii inamfanya yule aliyedhibitiwa kuweza kuelewa au kuwa na fahamu zake lakini anakuwa hawezi yeye mwenyewe kuudhibiti mwili wake na anasema yale anayotaka yule Jini.
3. Njia ya Pili (2); Jini humwingia Binadamu ndani ya utosi na kuingia katika Mfumo wa Damu. Hii inamfanya yule Binadamu kupoteza fahamu na anakuwa haelewi kabisa kinachoendlea na anafanya yote anayotaka yule Jini.
4. Njia ya Tatu (3) ni ile ya Jini kukaa nyuma ya Binadamu. Njia hii humfanya yule Binadamu anakuwa hapotezi fahamu ila anakuwa hawezi kufanya lolote na mwili wake.

{mospagebreak}

Majini vilevile wana uwezo wa Kusafiri kwa kasi ya upepo bila kutumia chombo chochote; Binadamu hana uwezo huo isipokuwa kwa msaada wa Majini.

Hiyo ni kusema kwamba mambo yote yanayofanywa na Wachawi na Wanga hayawezekani isipokuwa kwa msaada wa Kijini.

Jambo la muhimu ni kwamba pamoja na uwezo mkubwa walionao Majini, Wanadamu wana uwezo wa Kumtawala na Kumdhibiti Jini na vivyo hivyo Majini nao wanaweza kumtawala na kumdhibiti Binadamu wote kwa kutumia utaalamu maalum.
Wako Majini wa kila Dini na kila Kabila, na kuna watu wanaofuga Majini kwa kujikinga, na kwa kuboresha kazi zao au kujipatia utajiri. Pia kuna watu wanaofunga ndoa na Majini kwa kutumia utaalamu au kwa hiari za Majini hao.

Wabaya wa Majini ni Mashetani ambao wengi hawana Dini na ndio wanaoharibu mimba za Wazazi na kufanya mapenzi na watu usingizini bila hiari zao.
Kuepuka usichafuliwe kimapenzi, kabla ya kulala piga Bismillahi kwa Muislamu au taja jina la Yesu mara tatu kwa Mkristo.

MAUMBILE YAO YAKOJE?


• Majini wana maumbile makuu manne (4);
• Wanakuwa katika maumbile ya Nyoka.
• Wanakuwa katika maumbile ya Nge.
• Wanakuwa katika maumbile ya Mbwa.
• Wanakuwa katika maumbile ya Paka (Mweusi).
• Kuna Majini wengine hawana maumbile yeyote na hawa shughuli yao ni kuruka hewani kuzunguka huku na kule na husafiri mbali kwa mara moja yaani kufumba na kufumbua.


SURA ZA MAJINI NA MASHETANI:

Majini sura zao ni za kutisha na mfano wake ni kama Matunda ya Mti wa Zaqum ambao unatoa matunda yenye sura mbaya na yanayofanana na mawe.
Majini wanakuwa na mkutano kila siku nyakati za kuchomoza na kuzama Jua na nyakati hizo ndizo ambazo wanafanya maasi yao.

Fitna na Maasi yao mengi wanafanyia upande wa Mashariki.
Majini vilevile wanaweza kujigeuza kama mbwa mweusi au paka mweusi kwa sababu Majini wanapenda Rangi Nyeusi kwa sababu ya kiza.

WANAKULA NINI?

Subscribe uzi huu mengi hujayajua bado


Itaendelea

Asalaam kudo
Mkuu! Naomba nikurekebishe hapa unaposema majini yanakufa unakuwa unakosea sana simply because hawa majini ni roho na hawana mwili na siku zote kinachokufa ni kile chenye umbo, maada au (matter) na chenye umbo pekee ni binadamu ndio maana tunakufa ila majini na malaika wameundwa kwa space and time bila kuwa na umbo maalumu wale ni spiritual energy pekee na laws of nature zinasema energy can neither be created nor destroyed it can only be transformed or transferred, hivyo unaposema majini wanakufa unakuwa unakosea wale wana roho tu na hawana miili sasa wanakufaje ilhali wao ni roho tu?

Malaika, majini hawa ndio pekee Mungu aliwapendelea na kuwapa roho pekee kama vile yeye alivyo ila sisi binadamu ndio tukapewa mwili, roho na nafsi.. Sasa tunakiona cha mtema kuni kwenye huu mwili uliobeba deni la Dunia almaarufu kama tumbo usipochakarika kutafuta maisha unahadhirika mchana kweupe tu.

Majini ni immortal ila binadamu ni mortal being.
 
Mkuu! Naomba nikurekebishe hapa unaposema majini yanakufa unakuwa unakosea sana simply because hawa majini ni roho na hawana mwili na siku zote kinachokufa ni kile chenye umbo, maada au (matter) na chenye umbo pekee ni binadamu ndio maana tunakufa ila majini na malaika wameundwa kwa space and time bila kuwa na umbo maalumu wale ni spiritual energy pekee na laws of nature zinasema energy can neither be created nor destroyed it can only be transformed or transferred, hivyo unaposema majini wanakufa unakuwa unakosea wale wana roho tu na hawana miili sasa wanakufaje ilhali wao ni roho tu?

Malaika, majini hawa ndio pekee Mungu aliwapendelea na kuwapa roho pekee kama vile yeye alivyo ila sisi binadamu ndio tukapewa mwili, roho na nafsi.. Sasa tunakiona cha mtema kuni kwenye huu mwili uliobeba deni la Dunia almaarufu kama tumbo usipochakarika kutafuta maisha unahadhirika mchana kweupe tu.

Majini ni immortal ila binadamu ni mortal being.
Ukisoma vema kuhusu majini utaona kabisa ni viumbe wanaokufa kwa sababu wameumbwa na mungu na kiumbe chochote kinachozaliana lazima kife,ukisema hawafi unamaanisha hawazaliani,pia ukisema hawafi inamaana mungu aliwapa uwezo sawa na wake na Kama ndivyo wasingeliweza kuishi kwa kuogopa neno la mungu mana hawafi hivyo hata kuwakemea wsingelikimbia mana hawafi na mungu Hana uwezo wa kuwaua.
Jini anakufa ila anaishi miaka kuanzia 400 na kuendelea na hii ni kwa sababu hana umbo maalumu......

Elimu hii ni pana sana na kwa sababu ya muda ndio maana niliishia hapo Chief ila ahsante kwa elimu yako pia hakika tunajifunza sote
 
Ukisoma vema kuhusu majini utaona kabisa ni viumbe wanaokufa kwa sababu wameumbwa na mungu na kiumbe chochote kinachozaliana lazima kife,ukisema hawafi unamaanisha hawazaliani,pia ukisema hawafi inamaana mungu aliwapa uwezo sawa na wake na Kama ndivyo wasingeliweza kuishi kwa kuogopa neno la mungu mana hawafi hivyo hata kuwakemea wsingelikimbia mana hawafi na mungu Hana uwezo wa kuwaua.
Jini anakufa ila anaishi miaka kuanzia 400 na kuendelea na hii ni kwa sababu hana umbo maalumu......

Elimu hii ni pana sana na kwa sababu ya muda ndio maana niliishia hapo Chief ila ahsante kwa elimu yako pia hakika tunajifunza sote
Mkuu, wanakufaje wakati wao ni roho pekee? Wao wana sifa nyingi sana zinazofanana na malaika tu, ishu ni kwamba wao ni malaika waliohasi ufalme na neno la Mungu.

Hizi story za hizi njemba jini kufa ni hadithi tu za kusadikika hazina ukweli wowote. Majini ni roho na roho haijawahi kufa bali mwili hufa.

For a simple reason ya wao kuishi rohoni, hivyo hawafi Mkuu. Asante.
 
Mkuu, wanakufaje wakati wao ni roho pekee? Wao wana sifa nyingi sana zinazofanana na malaika tu, ishu ni kwamba wao ni malaika waliohasi ufalme na neno la Mungu.

Hizi story za hizi njemba jini kufa ni hadithi tu za kusadikika hazina ukweli wowote. Majini ni roho na roho haijawahi kufa bali mwili hufa.

For a simple reason ya wao kuishi rohoni, hivyo hawafi Mkuu. Asante.
Mkuu jini sio malaika muasi ila wanaongozwa na malaika muasi tena mwenye cheo cha tatu,jini anaumbo lake kamli ila anao uwezo wa kujibadilisha atakavyo,ukisema jini ni hadithi inamaana hata mungu utasema ni hadithi,
Hawa viumbe utasema pia hawazaliani au utasemaje?!
Hawa ni viumbe wa mungu waliopata kuishi duniani kabla ya mwanadamu hajaumbwa kureplace uwepo wao....
Natamani tujadili kiupana zaidi ila sina muda kwa sasa na pia ninapojifunxa au kutaka kujifunza zaidi huwa naogopa sana watu wanaohitimisha kitu kwa kusema neno HADITHI mana hana jipya la kuweza kusaidina kuchanganua jambo

Hivyo basi niseme wewe ndie unahadithi za kusema jini ni roho wakati sio kweli jini sio roho jini ni kiumbe anaeishi nje ya uwezo wa mwanadamu kupata kumshuhudia na hii ni adhabu ya mungu juu yao baada ya kusema mwanadamu akiumbwa basi wao watamuua (soma vizuri biblia ama Quran)
Lakini pia soma kuhusu mfalme Suleiman alieishi na kuwaongoza majini hadi kifo chake na walimsaidia kujenga mahekalu kadhaa je roho inaeeza fanya kazi za kibinadamu mana roho ni kama upepo tu hauonekani na hauna umbo.

Soma vitabu vingi uwezavyo na utaachana na neno HADITHI
 
Tusidanganyane hapa mkuu, hakuna tofauti kati ya Majini na Mashetani, wote ni hao hao tu. Hakuna tofauti kati ya Mapepo na Maruhani. Kwa kifupi ni kwamba malaika wote walioasi Mbinguni na kufukuzwa ndiyo hao leo hii wanaitwa majina tofauti tofauti, wengine wanawaita Majini, Mapepo, Mashetani, Vibwengo, Maruhani, Mizimu, Mazimwi, Mapopobawa n.k.

Hawa wote ni malaika walioasi Mbinguni na kiongozi wao ni mmoja tu ndiye Lusiferi. Huyu Lusiferi moja ya mbinu yake ni kuwachanganya Wanadamu akili zao kwa kuwadanganya kuwa kuna tofauti kati ya Majini na Mashetani. Kwa kifupi tu ni kwamba Lusiferi amekuja na majina ya aina mbali mbali ambayo amewapa wale malaika waliomfuata ili kuwapoteza Wanadamu waone kuna tofauti kumbe kitu ni kile kile!

Mbinu hii ya Lusiferi inaitwa "divide and rule" yaani "watenganishe na uwatawale". Lusiferi amewatenganisha hawa malaika wake kwa kuwapatia majina tofauti tofauti ili waweze kuwatawala Wanadamu kirahisi na hilo wamefanikiwa sana kwani leo hii kuna Mamilioni ya Wanadamu wanaamini kuna Majini wazuri na Majini mabaya. Leo hii Wanadamu wanaamini kuna Mizimu na Mashetani.

Tena Lusiferi amefanikiwa sana kuwatenganisha Wanadamu pia, YESU alipokuja na Mafundisho ya INJILI, Lusiferi akaja na QUARAN(Waislamu mtanisamehe kwani huo ndiyo UKWELI ulivyo). Tena ndani ya Ukristo Lusiferi amefanikiwa kuwagawa sana kwani kuna waabudu JUMAPILI na waabudu siku ya JUMAMOSI, kote huko amevuruga vuruga ili kuwatenganisha. Lipo kundi dogo sana linaloshika mafundisho ya KWELI ya MUNGU linaitwa KANISA LA MUNGU.

Hili nalo Lusiferi amefanikiwa kulivuruga mno kiasi limegawanyika sana na kamebakia kakikundi kadogo sana kanakoshikilia Amri za MUNGU na Imani ya KWELI ya YESU. Hii yote ni ili yatimie yale maneno ya YESU kuwa watakaokolewa ni KUNDI DOGO SANA!

UKWELI ni kwamba hakuna tofauti yoyote ile kati ya hao viumbe niliowataja, wote hao ni wale malaika walioasi Mbinguni na kuja duniani wakimfuata Lusiferi, wote ni kitu kimoja na tabia zao ni moja isipokuwa tu wanajifanya kuwa tofauti ili kuwapotosha Wanadamu na kuwadanganya.

Ndiyo maana Yesu alisema itafuteni KWELI nayo hiyo KWELI itawaweka huru kweli kweli. Mwenye masikio na asikie!

Cc. Kudo Da'Vinci Mshana Jr zitto junior Che mittoga Tz mbongo Sky Eclat Otorong'ong'o SALA NA KAZI mitale na midimu Dejavu Shubiri Pori nyabhingi Mr Q
 
Tusidanganyane hapa mkuu, hakuna tofauti kati ya Majini na Mashetani, wote ni hao hao tu. Hakuna tofauti kati ya Mapepo na Maruhani. Kwa kifupi ni kwamba malaika wote walioasi Mbinguni na kufukuzwa ndiyo hao leo hii wanaitwa majina tofauti tofauti, wengine wanawaita Majini, Mapepo, Mashetani, Vibwengo, Maruhani, Mizimu, Mazimwi, Mapopobawa n.k.

Hawa wote ni malaika walioasi Mbinguni na kiongozi wao ni mmoja tu ndiye Lusiferi. Huyu Lusiferi moja ya mbinu yake ni kuwachanganya Wanadamu akili zao kwa kuwadanganya kuwa kuna tofauti kati ya Majini na Mashetani. Kwa kifupi tu ni kwamba Lusiferi amekuja na majina ya aina mbali mbali ambayo amewapa wale malaika waliomfuata ili kuwapoteza Wanadamu waone kuna tofauti kumbe kitu ni kile kile!

Mbinu hii ya Lusiferi inaitwa "divide and rule" yaani "watenganishe na uwatawale". Lusiferi amewatenganisha hawa malaika wake kwa kuwapatia majina tofauti tofauti ili waweze kuwatawala Wanadamu kirahisi na hilo wamefanikiwa sana kwani leo hii kuna Mamilioni ya Wanadamu wanaamini kuna Majini wazuri na Majini mabaya. Leo hii Wanadamu wanaamini kuna Mizimu na Mashetani.

Tena Lusiferi amefanikiwa sana kuwatenganisha Wanadamu pia, YESU alipokuja na Mafundisho ya INJILI, Lusiferi akaja na QUARAN(Waislamu mtanisamehe kwani huo ndiyo UKWELI ulivyo). Tena ndani ya Ukristo Lusiferi amefanikiwa kuwagawa sana kwani kuna waabudu JUMAPILI na waabudu siku ya JUMAMOSI, kote huko amevuruga vuruga ili kuwatenganisha. Lipo kundi dogo sana linaloshika mafundisho ya KWELI ya MUNGU linaitwa KANISA LA MUNGU.

Hili nalo Lusiferi amefanikiwa kulivuruga mno kiasi limegawanyika sana na kamebakia kakikundi kadogo sana kanakoshikilia Amri za MUNGU na Imani ya KWELI ya YESU. Hii yote ni ili yatimie yale maneno ya YESU kuwa watakaokolewa ni KUNDI DOGO SANA!

UKWELI ni kwamba hakuna tofauti yoyote ile kati ya hao viumbe niliowataja, wote hao ni wale malaika walioasi Mbinguni na kuja duniani wakimfuata Lusiferi, wote ni kitu kimoja na tabia zao ni moja isipokuwa tu wanajifanya kuwa tofauti ili kuwapotosha Wanadamu na kuwadanganya.

Ndiyo maana Yesu alisema itafuteni KWELI nayo hiyo KWELI itawaweka huru kweli kweli. Mwenye masikio na asikie!

Cc. Kudo Da'Vinci Mshana Jr zitto junior Che mittoga Tz mbongo Sky Eclat Otorong'ong'o SALA NA KAZI mitale na midimu
Ni kundi gani hilo litakalo okolewa pekee?
 
Tusidanganyane hapa mkuu, hakuna tofauti kati ya Majini na Mashetani, wote ni hao hao tu. Hakuna tofauti kati ya Mapepo na Maruhani. Kwa kifupi ni kwamba malaika wote walioasi Mbinguni na kufukuzwa ndiyo hao leo hii wanaitwa majina tofauti tofauti, wengine wanawaita Majini, Mapepo, Mashetani, Vibwengo, Maruhani, Mizimu, Mazimwi, Mapopobawa n.k.

Hawa wote ni malaika walioasi Mbinguni na kiongozi wao ni mmoja tu ndiye Lusiferi. Huyu Lusiferi moja ya mbinu yake ni kuwachanganya Wanadamu akili zao kwa kuwadanganya kuwa kuna tofauti kati ya Majini na Mashetani. Kwa kifupi tu ni kwamba Lusiferi amekuja na majina ya aina mbali mbali ambayo amewapa wale malaika waliomfuata ili kuwapoteza Wanadamu waone kuna tofauti kumbe kitu ni kile kile!

Mbinu hii ya Lusiferi inaitwa "divide and rule" yaani "watenganishe na uwatawale". Lusiferi amewatenganisha hawa malaika wake kwa kuwapatia majina tofauti tofauti ili waweze kuwatawala Wanadamu kirahisi na hilo wamefanikiwa sana kwani leo hii kuna Mamilioni ya Wanadamu wanaamini kuna Majini wazuri na Majini mabaya. Leo hii Wanadamu wanaamini kuna Mizimu na Mashetani.

Tena Lusiferi amefanikiwa sana kuwatenganisha Wanadamu pia, YESU alipokuja na Mafundisho ya INJILI, Lusiferi akaja na QUARAN(Waislamu mtanisamehe kwani huo ndiyo UKWELI ulivyo). Tena ndani ya Ukristo Lusiferi amefanikiwa kuwagawa sana kwani kuna waabudu JUMAPILI na waabudu siku ya JUMAMOSI, kote huko amevuruga vuruga ili kuwatenganisha. Lipo kundi dogo sana linaloshika mafundisho ya KWELI ya MUNGU linaitwa KANISA LA MUNGU.

Hili nalo Lusiferi amefanikiwa kulivuruga mno kiasi limegawanyika sana na kamebakia kakikundi kadogo sana kanakoshikilia Amri za MUNGU na Imani ya KWELI ya YESU. Hii yote ni ili yatimie yale maneno ya YESU kuwa watakaokolewa ni KUNDI DOGO SANA!

UKWELI ni kwamba hakuna tofauti yoyote ile kati ya hao viumbe niliowataja, wote hao ni wale malaika walioasi Mbinguni na kuja duniani wakimfuata Lusiferi, wote ni kitu kimoja na tabia zao ni moja isipokuwa tu wanajifanya kuwa tofauti ili kuwapotosha Wanadamu na kuwadanganya.

Ndiyo maana Yesu alisema itafuteni KWELI nayo hiyo KWELI itawaweka huru kweli kweli. Mwenye masikio na asikie!

Cc. Kudo Da'Vinci Mshana Jr zitto junior Che mittoga Tz mbongo Sky Eclat Otorong'ong'o SALA NA KAZI mitale na midimu Dejavu Shubiri Pori nyabhingi Mr Q
Mkuu sijataka watu waamini uzuri wa jini au ubaya wake ila nilileta mada tujifunze pamoja bila kuingilia muhimili wa dini zetu

Lakini naomba nikuulize ni malaika wangapi walimwasi mungu?! Na kwanini katika wingi huo ulioutaja ila Bible inamtaja Lucifer kama ndie malaika alie muhasi Mungu na si hao makabila 72 elfu wa majini?!

Je unaamini kwamba shetani ni kiumbe yeyote mwenye kufanya yasiopendeza akiwemo mwanadamu?!

Sijajua lengo lako ni nini hasa mana mada imeeleza maisha ya viumbe hao na si wema ama ubaya wao na bado nimeonesha njia za kukukabiliana nao lakini pia hat
 
Lakini naomba nikuulize ni malaika wangapi walimwasi mungu?! Na kwanini katika wingi huo ulioutaja ila Bible inamtaja Lucifer kama ndie malaika alie muhasi Mungu na si hao makabila 72 elfu wa majini?!
Mkuu malaika waliomuasi MUNGU kwa idadi yao ni theluthi ya malaika wote na kiongozi wao ni Lusiferi(UFUNUO 12:3-4). Alianza Lusiferi kuasi na akaweza kuwashawishi theluthi ya malaika wengine nao pia wakaasi. Hakuna tofauti yoyote ile ya malaika waasi na majini, hao ni kitu hicho hicho kimoja.

Malaika hawa walioasi pamoja na Lusiferi mwenyewe ndiyo hao wanaitwa mashetani, maana ya "shetani" ni "adui" au tunaweza kusema ni "adui ya MUNGU". Kwa udanganyifu wa Shetani amewadanganya na kuwafanya muamini kuna tofauti kati ya shetani na jini, wakati ukweli ni kwamba hakuna tofauti yoyote ile, shetani ndiyo huyo huyo jini na jini ndiyo huyo huyo shetani.
 
Nataka unitajie wewe ni kundi gani/linaitwaje?
Wewe na elimu yako yote ya "Theology" hulijui kundi la KWELI la MUNGU?? Theology uliyosoma inakusaidia nini mkuu? Kweli sasa nimeamini maarifa ya Wanadamu ni upumbavu mbele ya MUNGU(1 WAKORINTHO 3:19-20).

Mkuu kama unataka kuunganishwa na hilo Kanisa la kweli la MUNGU basi wewe zishike Amri zote za MUNGU na imani ya YESU KRISTO kisha Roho Mtakatifu atakuongoza kwenye hilo kanisa. Imeandikwa hakuna anayekuja kwa BABA pasipo kuvutwa na Baba(YOHANA 6:44). Pia YESU alisema yeye atakayenipenda na kuzishika Amri zangu, tutakuja kwake na kufanya makao kwake(YOHANA 14:23-24).
 
Wewe na elimu yako yote ya "Theology" hulijui kundi la KWELI la MUNGU?? Theology uliyosoma inakusaidia nini mkuu? Kweli sasa nimeamini maarifa ya Wanadamu ni upumbavu mbele ya MUNGU(1 WAKORINTHO 3:19-20).

Mkuu kama unataka kuunganishwa na hilo Kanisa la kweli la MUNGU basi wewe zishike Amri zote za MUNGU na imani ya YESU KRISTO kisha Roho Mtakatifu atakuongoza kwenye hilo kanisa. Imeandikwa hakuna anayekuja kwa BABA pasipo kuvutwa na Baba(YOHANA 6:44). Pia YESU alisema yeye atakayenipenda na kuzishika Amri zangu, tutakuja kwake na kufanya makao kwake(YOHANA 14:23-24).
Mkuu mimi nimeshika sheria zake zote Mungu (hua nazivunja muda mwingine coz sijakamilika) nafuata mafunzo ya Yesu kristo je nimeunganishwa na hilo kanisa?
 
Nilitegemea nitaona kanisa la kule Ileje Mbeya kumbe bado unaleta story za kimishionari kwamba Africa hakuna Mungu?

Sijui waafrika sisi tuna kazi gani hapa Duniani kama hata Mungu mwenyewe hatutambui!
Mkuu nani kakuambia NENO la MUNGU limetokea Ileje Mbeya? wewe ingia hapa www.ccog.org ujisomee UKWELI ulivyo.
 
Nilitegemea nitaona kanisa la kule Ileje Mbeya kumbe bado unaleta story za kimishionari kwamba Africa hakuna Mungu?

Sijui waafrika sisi tuna kazi gani hapa Duniani kama hata Mungu mwenyewe hatutambui!
Nimeona nisiendelee kubishana nae mkuu bora nawe umeliona hilo
 
Back
Top Bottom