Kamanda
Senior Member
- Dec 5, 2007
- 150
- 176
WAKATI gumzo kuu nchini kwa sasa ni juu ya hali mbaya ya kifedha ya Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (Tanesco) mazungumzo yanaendelea kuhusu Tanesco kukodisha sehemu ya mfumo wake wa gridi ya taifa ya usambazaji umeme kwa kampuni binafsi ya kimataifa ili iusambaze katika mikoa ya kusini.
Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Dk. Idris Rashid, aliyathibitisha hayo jana na kueleza kuwa shirika hilo kwa sasa linashauriana na kampuni ya Canada ya Artumas Group Inc., kuhusu mkataba wa muda mrefu wa ukodishaji miundombinu ya usambazaji umeme.
Chini ya makubaliano ya miaka 20 yanayojadiliwa sasa, Artumas itakodi miundombinu ya usambazaji umeme katika mikoa ya Mtwara na Lindi na kuwapatia wateja umeme.
Hii itakuwa mara ya kwanza Tanesco inakodisha miundombinu yake kwa kiwango kikubwa hivyo tena kwa muda mrefu kwa kampuni binafsi.
Mtwara na Lindi ni mikoa ambayo ina eneo la Kilometa za mraba 24,000 na wakaaji wapatao milioni 2.
Taarifa kamili za ukodishaji huo bado hazijapatikana, lakini maofisa wa serikali wamesema ukodishaji huo utaisaidia kifedha Tanesco inayokabiliwa na ukata.
Kwa sasa Tanesco ina ukiritimba wa biashara wa sekta ya umeme na lengo hilo la serikali la kuunda taasisi tatu tofauti za kufua umeme, kuusafirisha na kuusambaza bado liko mbali kutimia.
Haijaeleweka vizuri ni lini majadiliano baina ya Tanesco na Artumas yanatarajiwa kukamilika.
Vilevile haijafahamika kama kampuni hiyo ya kigeni ya Artumas itaweka viwango vyake vya kulipia umeme au itaendelea kutumia viwango vinavyotozwa na Tanesco vilivyoidhinishwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura).
Tanesco inazalisha megawati 560 za umeme nyingi zikiwa kwa nguvu ya maji na pia inanunua megawati 200 za umeme kutoka kwa wazalishaji binafsi.
Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Dk. Idris Rashid, aliyathibitisha hayo jana na kueleza kuwa shirika hilo kwa sasa linashauriana na kampuni ya Canada ya Artumas Group Inc., kuhusu mkataba wa muda mrefu wa ukodishaji miundombinu ya usambazaji umeme.
Chini ya makubaliano ya miaka 20 yanayojadiliwa sasa, Artumas itakodi miundombinu ya usambazaji umeme katika mikoa ya Mtwara na Lindi na kuwapatia wateja umeme.
Hii itakuwa mara ya kwanza Tanesco inakodisha miundombinu yake kwa kiwango kikubwa hivyo tena kwa muda mrefu kwa kampuni binafsi.
Mtwara na Lindi ni mikoa ambayo ina eneo la Kilometa za mraba 24,000 na wakaaji wapatao milioni 2.
Taarifa kamili za ukodishaji huo bado hazijapatikana, lakini maofisa wa serikali wamesema ukodishaji huo utaisaidia kifedha Tanesco inayokabiliwa na ukata.
Kwa sasa Tanesco ina ukiritimba wa biashara wa sekta ya umeme na lengo hilo la serikali la kuunda taasisi tatu tofauti za kufua umeme, kuusafirisha na kuusambaza bado liko mbali kutimia.
Haijaeleweka vizuri ni lini majadiliano baina ya Tanesco na Artumas yanatarajiwa kukamilika.
Vilevile haijafahamika kama kampuni hiyo ya kigeni ya Artumas itaweka viwango vyake vya kulipia umeme au itaendelea kutumia viwango vinavyotozwa na Tanesco vilivyoidhinishwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura).
Tanesco inazalisha megawati 560 za umeme nyingi zikiwa kwa nguvu ya maji na pia inanunua megawati 200 za umeme kutoka kwa wazalishaji binafsi.