Ukipiga Simu Huku Unaendesha Gari Unatozwa 200,000 Hapo Kwa Hapo.

Domo Kaya

JF-Expert Member
May 29, 2007
531
59
Majira
Na Rehema Mwakasese.

Jeshi la Polisi nchini kupitia kikosi cha Usalama barabarani, limepiga marufuku madereva kupokea simu au kupiga simu wakati wakiendesha magari na watakao bainika kufanya hivyo watatozwa faini ya sh, 200,000/= papo hapo.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Kamanda wa Kikosi cha usalama wa Barabarani , Bw. James Kombe, alisema zipo sababu nyingi zinazosababisha ajali barabarani ikiwemo madereva kupokea au kupiga simu wanapoendesha magari.

Kamanda Kombe alisema watu wengi wamekuwa na tabia ya kuendesha magari huku wakizungumza na simu, hivyo husababisha ajali za kizembe.

Alisema askari wa Usalama Barabarani wataanza operationi hiyo mara moja kwa kushirikiana na Mamlaka ya udhibiti wa usafiri wa Nchi kavu na Majini (SUMATRA).

Mbali na hilo Kamanda Kombe alisema madereva wanaondesha magari yaendayo mikoani waongezwa muda wa kuendesha magari usiku ambapo mwisho utakuwa ni saa sita na si saa nne.

Alisema kuwa mwanzo madereva walikuwa wanaendesha mwisho saa nne, lakini wameona abiria wengi wanalalamika ndio maanda wakaongeza hadi saa sita, ili waweze kufika mapema zaidi.

Pia alisema kuanzia sasa dereva wa basi la abiria atapewa leseni la daraja 'C' akiwa na umri wa miaka 30 na mwisho wa kuendesha ni miaka 60.
 
wapumbavu wakubwa hawa,naona wanataka kujitengenezea rushwa tuu hapo,tangu lini Polisi wakatunga sheria? ....kuna utaratibu wa kutunga na kupitisha sheria sio huu uwendawazimu!
 
kweli hii ni kali kuliko, wameshindwa kudhibiti Ujambazi sasa wanatafuta njia zisizo na maana.
 
wapumbavu wakubwa hawa,naona wanataka kujitengenezea rushwa tuu hapo,tangu lini Polisi wakatunga sheria? ....kuna utaratibu wa kutunga na kupitisha sheria sio huu uwendawazimu!

Mkuu ukiiangalia vizuri hii inamaanisha hawa jamaa wanataka waongeze kiwango cha rushwa!! Kwa faini ya 20,000/= ktk makosa ya barabarani walikuwa wanapata 5,000/= hadi 10,000/= ila sasa kwa kuwa wameona life tight wanataka kupiga gap! badala ya mtu kulipa faini ya 200,000/= atatoa rushwa ya 50,000/= hadi 100,000/= na hivyo basi hawa Trafiki wataneemeka!!!

Huu ni upumbavu wa hali ya juu!!! Ufisadi day in day out!!!!! baaahhh!!
 
wapumbavu wakubwa hawa,naona wanataka kujitengenezea rushwa tuu hapo,tangu lini Polisi wakatunga sheria? ....kuna utaratibu wa kutunga na kupitisha sheria sio huu uwendawazimu!

duh!!! Inaonekana wewe unaongeaga na simu barabarani
 
Usalama Wa Raia Ni Muhim Na Usalama Wa Chombo Pia...hakuna Mtu Anaependa Ajali Zitokee Kizembe...sijui Ni Study Gani Imefanyika Kujua Kama Wakipiga Au Kupokea Simu Ajali Ngapi Zishatokea...??

Kwa Uzoefu Wangu Ajali Nyingi Ni Zile Za Gari Za Abiria Hasa Waondeo Mikoani Na Huwa Si Kwasimu, Lkn Pia Za Hapa Dsm Nyingi Ni Uzembe Au Kiburi Cha Madalala Na Wanaojiita Madereva Wazoefu....

Ushauri Wangu Ipo Haja Ya Kujifunza Kutoka Kwa Wenzetu Ambao Technology Ya Simu Iliingia Mda Mrefu Na Pia Traffic Yao Ni Kubwa Kuliko Yetu. Binafsi Nimeona Sehem Fulani Ya Nchi Nilizowahi Kutembea, Wao Wameweka Sheria Kama Hii, Ila Wao Wameiboresha, Walichosema Ni Kuwa Wanaruhusiwa Kupokea Au Kupiga Lkn Wasiwe Wameshika Simu, Simu Inaweza Kuwa Free Au Kwa Ear Phones Au Kwa Blue Tooth....sijui Wadau Mnaonaje Hizi...

Japo Tabia Za Viongozi Si Wa Kujifunza Yalio Mema Na Mazuri...
 
Usalama Wa Raia Ni Muhim Na Usalama Wa Chombo Pia...hakuna Mtu Anaependa Ajali Zitokee Kizembe...sijui Ni Study Gani Imefanyika Kujua Kama Wakipiga Au Kupokea Simu Ajali Ngapi Zishatokea...??

Kwa Uzoefu Wangu Ajali Nyingi Ni Zile Za Gari Za Abiria Hasa Waondeo Mikoani Na Huwa Si Kwasimu, Lkn Pia Za Hapa Dsm Nyingi Ni Uzembe Au Kiburi Cha Madalala Na Wanaojiita Madereva Wazoefu....

Ushauri Wangu Ipo Haja Ya Kujifunza Kutoka Kwa Wenzetu Ambao Technology Ya Simu Iliingia Mda Mrefu Na Pia Traffic Yao Ni Kubwa Kuliko Yetu. Binafsi Nimeona Sehem Fulani Ya Nchi Nilizowahi Kutembea, Wao Wameweka Sheria Kama Hii, Ila Wao Wameiboresha, Walichosema Ni Kuwa Wanaruhusiwa Kupokea Au Kupiga Lkn Wasiwe Wameshika Simu, Simu Inaweza Kuwa Free Au Kwa Ear Phones Au Kwa Blue Tooth....sijui Wadau Mnaonaje Hizi...

Japo Tabia Za Viongozi Si Wa Kujifunza Yalio Mema Na Mazuri...

Kuna miji mingi katika nchi za magharibi haziruhusu hata kutumia ear phones. Ni uamuzi mzuri ili kupunguza ajali, lakini utatumika kuongeza rushwa.
 
wapumbavu wakubwa hawa,naona wanataka kujitengenezea rushwa tuu hapo,tangu lini Polisi wakatunga sheria? ....kuna utaratibu wa kutunga na kupitisha sheria sio huu uwendawazimu!

Na hapa wamepewa dili, maana kusa lenyewe faini ni 200,000/= sasa ukitaka mazungumzo lazima wakunyofoe si chini 50,000/=
 
Na yale malori ya mizigo inayokufa kila siku na kila sehemu barabarani na kusababisha foleni isiyo na kichwa wala miguu je? watayatungia sheria?. Hizo tu zinasababisha ajali ile mbaya!
 
Ile Card ya gari yenye 2000 ndani yake sasa inatakiwa hiwe na 20000 badala ya 2000 jiandaeni kunenepesha mifuko ya Trafick
 
Wangetengeneza barabara zao kwanza .. mashimo kama tuko tayari kaburini ... halafu mengine yatafuata ... kwani wanahitaji huwo mchango wa 200,000/- kuongezea wapi kama si kutanua matumbo yao
 
Bubu Nchi gani....kama faini ya 200,000 umesema unatoa mwanya wa rushwa..wape ushauri wafanyeje....?

Nimeuliza is there any statistics za SIMU Vs Ajali za barabarani?...
 
Hivi wanafikiri watanzania wote ni mafisadi, kiasi kwamba ni rahisi kupata kiwango hicho kirahisi?

Inatakiwa watoe statistics hili tuweze kuona kama kweli kuna uhusiano kati ya ajari na upigaji wa simu.
 
Hivi huo utaratibu wa kulipa hio "penalty" umesimama vipi?, na unapolipa kwa huyo polisi unapewa stakabadhi au ..

Kwa nini pasiwepo utaratibu wa kulipia mahakamani ndani ya siku saba badala ya hao polisi wa barabarani?

Ila kiwango hicho ni kikubwa na kina malengo yake ya kifisadi.

Tatizo ni lilelile hakuna system ya maana, period.

Mambo haya yanakwenda na polisi kutoa maelezo kwa nini wamepanga kiasi hicho na vipi sheria inasemaje kuhusu hilo endapo mtu unaamua kupinga penalty hio?

Je "road safety act" inajumuisha kosa hilo na ni lini imekuwa updated?

Halafu hapa SUMATRA inaingiaje naomba mwenye kuelewa anifahamishe hili.
 
Ufisadi sasa umehamia barabarani. Laki mbili nyingi jamani, Mie mwenzenu naenda kununua EAR Phone. nakuwa naongea huku mikono yote inaendesha wala hawanipati ng'oo.
 
Bubu Nchi gani....kama faini ya 200,000 umesema unatoa mwanya wa rushwa..wape ushauri wafanyeje....?

Nimeuliza is there any statistics za SIMU Vs Ajali za barabarani?...

By Michael Santo
Contributing Writer, RealTechNews

Lawrence, Kansas has proposed a complete cell phone ban while driving … the first of its kind in the country. There have been other laws put into place, but this would be the first one that also bans hands-free devices as well.

The proposal, which goes before the Lawrence’s Traffic Safety Commission on Monday, would ban the use of hand-held cell phones and hands-free cell phone devices by all drivers.

“If you pass a ban that just prohibits the hand-held devices, you’re sending a message that the hands-free devices are safe,” said Paul Atchley, associate professor of psychology at the University of Kansas. “And that is false.” Source: AP via MSNBC

We Say: I use a Bluetooth headset when I drive, and even then, I know I get distracted when I talk on the phone while driving. Sometimes the phone won’t voice dial properly, and I have to pull it off my belt to look at it, or since it’s a PDA phone, sometimes I have to boot it. I’ve even used the contacts list to look up info like my VIN while talking to the DMV. All while driving. So I’ll be the first to admit, I definitely am distracted even with a headset.
 
Laki 2 hatoi mtu hapa maisha yenyewe haya...ya kimagumashi!! taenda mahakamani wakanionyeshe hiyo sheria inayosema ukiongea na simu faini laki 2. watafute suluhisho la kudumu, kama wanajifanya wanafuata sheria kwanini hizo stk, stj. su, nk mbona hayakamatwi?? kwanza madereva wake na wa daladala hatofautiani wanaweza kupaki popote pale na kwenda mwendo wowote na hao yange yange wanawaangalia tu??.
 
hakuna atakayelipa hio 200,000/- na wenyewe wanajua.Matrafic wanachekelea sasa hivi.
Sasa hao polisi wenyewe barabarani utawaona wanasoma au kutuma text wakati wanaongoza magari,sasa wao watalipa fine kiasi gani.
Na hao wenye magari ambayo yako tinted je? Coz if thats the case,they should outlaw tinted cars,vinginevyo kila mtu sasa hivi atakimbilia kuweka tint kwenye gari yake,na kuendelea kuongea kwenye simu kama kawaida
 
Watupatia utafiti waliofanya na kuonesha simu zinachangia kwa kiasi gani, otherwise bullshit. Barabara zenyewe hazipitiki kwa jam unakaa barabarani kwa masaa matatu kwenda mwenge utapataje ajali wakati gari inakwenda less than 10km/h?
 
Back
Top Bottom