Shayu
Platinum Member
- May 24, 2011
- 608
- 1,653
Ukiona watu wanapenda pesa kuliko utaifa ujue taifa ndio lina angamia! Moyo wa utaifa umotoweka, hii changamoto kwa kiongozi yeyote makini na mzalendo, umoja wetu ndio nguvu yetu, tulitumikie taifa letu kwa nguvu moja.
Ufisadi hutugawa, lakini haki hutuleta pamoja, tunahitaji kiongozi atakayetuunganisha na kutumikia taifa letu, ili tujitegemee na tutengeneze mamlaka mpya duniani.
Ubinafsi Mwisho wake tutapigana wenyewe kwa wenyewe, nchi yetu imekuwa na magenge ambayo yanasuguana sio kwa maslahi ya taifa hili, bali ubinafsi, wameligawa taifa hili kwa uroho, lakini Sisi tunahitaji kujenga taifa imara kwa vizazi vyetu, tunahitaji kujitegemea na kujenga uchumi wetu wenyewe ili watu wetu wawe wenye kuheshimika. Ni Aibu kwa viongozi wetu kusaka uongozi hadi kwa waganga wa kienyeji mtu kama huyu hafai kuongoza wananchi ni mbinafsi na mroho anataka uongozi kwa faida zake binafsi na anasa, Kiongozi wa kweli ni yule anaye organize watu kutumikia taifa lao wenyewe, sio yule anayetumia nafasi hiyo kujinufaisha na kuisha maisha ya anasa wakati watu wake wakiteseka.
Tumekuwa taifa lisilokuwa na mwelekeo, wananchi hawajui wanapoelekea ni nini mission ya taifa, tumekuwa watu wa binafsi na wenye choyo. Ubinafsi huondoa mantiki ya watu kuishi katika taifa, kama taifa ni lazima tujue nini kimetuunganisha na wapi tunataka kuelekea, Kujumuika kwetu kwa pamoja ni ili tuwe na maisha mazuri kuliko haya tuliyo nayo, ili tuishi kwa amani, undugu na upendo, ili kulinda taifa letu dhidi ya maadui wa kigeni. Haki za kila mmoja wetu ni muhimu ili kujenga taifa lenye umoja. Tuna taifa ambalo watu wake hawajui wajibu wao kwa nchi yao wenyewe , hii ni hali ya hatari sana. Ni lazima tujenge taifa amabalo vijana watajua wajibu wao kwa taifa, hili ni jambo muhimu sana. Taifa huvunjika na kusambaratika kabisa, msifikiri kwamba mtaishi milelele katika nchi hii kama hatukujenga misingi ya umoja na mshikamano wetu. Ni lazima tufikirie upya juu ya ujenzi wa taifa letu na mustakabali wetu kama taifa.
Ufisadi hutugawa, lakini haki hutuleta pamoja, tunahitaji kiongozi atakayetuunganisha na kutumikia taifa letu, ili tujitegemee na tutengeneze mamlaka mpya duniani.
Ubinafsi Mwisho wake tutapigana wenyewe kwa wenyewe, nchi yetu imekuwa na magenge ambayo yanasuguana sio kwa maslahi ya taifa hili, bali ubinafsi, wameligawa taifa hili kwa uroho, lakini Sisi tunahitaji kujenga taifa imara kwa vizazi vyetu, tunahitaji kujitegemea na kujenga uchumi wetu wenyewe ili watu wetu wawe wenye kuheshimika. Ni Aibu kwa viongozi wetu kusaka uongozi hadi kwa waganga wa kienyeji mtu kama huyu hafai kuongoza wananchi ni mbinafsi na mroho anataka uongozi kwa faida zake binafsi na anasa, Kiongozi wa kweli ni yule anaye organize watu kutumikia taifa lao wenyewe, sio yule anayetumia nafasi hiyo kujinufaisha na kuisha maisha ya anasa wakati watu wake wakiteseka.
Tumekuwa taifa lisilokuwa na mwelekeo, wananchi hawajui wanapoelekea ni nini mission ya taifa, tumekuwa watu wa binafsi na wenye choyo. Ubinafsi huondoa mantiki ya watu kuishi katika taifa, kama taifa ni lazima tujue nini kimetuunganisha na wapi tunataka kuelekea, Kujumuika kwetu kwa pamoja ni ili tuwe na maisha mazuri kuliko haya tuliyo nayo, ili tuishi kwa amani, undugu na upendo, ili kulinda taifa letu dhidi ya maadui wa kigeni. Haki za kila mmoja wetu ni muhimu ili kujenga taifa lenye umoja. Tuna taifa ambalo watu wake hawajui wajibu wao kwa nchi yao wenyewe , hii ni hali ya hatari sana. Ni lazima tujenge taifa amabalo vijana watajua wajibu wao kwa taifa, hili ni jambo muhimu sana. Taifa huvunjika na kusambaratika kabisa, msifikiri kwamba mtaishi milelele katika nchi hii kama hatukujenga misingi ya umoja na mshikamano wetu. Ni lazima tufikirie upya juu ya ujenzi wa taifa letu na mustakabali wetu kama taifa.