Ukiona vyaelea ujue vimeundwa..................... ..

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,172
Mwanadamu alivyoumbwa ni mwepesi kughafilika na kupagawa...
Hupenda vya mvunguni lakini masharti yake hayawezi........
Hupenda vya kunyonga lakini vya kuchinja huvikwepa.......
Hupenda vya mteremko lakini vya kuhenya kuvigwaya.......
Lakini ukiona vyaelea ujue fika vimeundwa.


Nashangaa kumwona kijana mtanashati akimfukuzia binti hata hamjui......
Kisa binti kapendeza, nguo zimemkaa huku akimeremeta.......
Kijana damu humchemka na kujipiga moyo konde.......
Bila hata ya kujiuliza hivi ni yeye tu mwenye macho ya kuangaza-angaza?
Lakini ukiona vyaelea ujue fika vimeundwa.

Kijana wa watu hupoteza hamu ya kula..........
Shughuli zake zote kuziona ni nuksi.......
Kisa ni kuwa bila ya kumpata yule binti yeye sasa mfu............
Kijana kuhangaika usiku na mchana kumnasa mrembo.....
Lakini ukiona vyaelea ujue fika vimeundwa.

Siku ya siku kijana akutana na binti......
Kiroho kikimdunda na kijasho kumdondoka amwaga sera.............
Mrembo amwelewa lakini ampa pole.............
Ukweli wafichuka kumbe mrembo ana mwenyewe.................
Lakini ukiona vyaelea ujue fika vimeundwa.
 
Nashangaa kumwona kijana mtanashati akimfukuzia binti hata hamjui......
Kisa binti kapendeza, nguo zimemkaa huku akimeremeta.......
Kijana damu humchemka na kujipiga moyo konde.......
Bila hata ya kujiuliza hivi ni yeye tu mwenye macho ya kuangaza-angaza?
Lakini ukiona vyaelea ujue fika vimeundwa.

hapa mkuu umegonga penyewe kabisa, na hii imeshatukuta vijana wengi sana, unamkuta binti unaanza kumbabakia kumbe hujui background yake na hujui kwanini umemkuta katika hali uliyomkuta nayo, na baadae ukija kugundua hali halisi tunaanza kulia lia tu, naikumbuka thread moja ilikuja last week inasema I will never trust any woman may be my Mom, mshikaji alifunguka vizuri na kweli alipenda mtoto wa chuo na alikutana nae katikati ya jiji...
akatoa simu na pesa kumbe alikua hajui kuna msemo unasema Ukiona vyaelea ujue vimeundwa

 
hapa mkuu umegonga penyewe kabisa, na hii imeshatukuta vijana wengi sana, unamkuta binti unaanza kumbabakia kumbe hujui background yake na hujui kwanini umemkuta katika hali uliyomkuta nayo, na baadae ukija kugundua hali halisi tunaanza kulia lia tu, naikumbuka thread moja ilikuja last week inasema I will never trust any woman may be my Mom, mshikaji alifunguka vizuri na kweli alipenda mtoto wa chuo na alikutana nae katikati ya jiji...
akatoa simu na pesa kumbe alikua hajui kuna msemo unasema Ukiona vyaelea ujue vimeundwa

mara nyingi huwa tunajisahau.........tukifikiri ni sisi tu wenye meno kumbe wenye nayo tuko wengi na vingine vilikwishatafunwa na wengine..................kwa hiyo tunatakiwa twenda polepole...tukisoma khali ya upepo.....[MENTION]@Manyanza[/MENTION]
 
hahha.....nyie si mnadhani vyote vinavyoelea ni vyepesi

Vaislay.................kwani hamtujui tulivyo mabwege tukikamatwa na vimbwanga vyenu....wakati mwingine mnapendeza mno na kutuchanganya.......[MENTION]@Vaislay[/MENTION]
 
huenda kweli vimeundwa ila aliyeviunda labda hajui kuvitumia..au havitumii ipasavyo
basi, huenda ikawa ndiyo bahati yako hapo kwamba wewe ndiye uliyekuwa ukingojewa to make a full utilization of kile kilichokuwa chaelea mtoni ilhali kilitakiwa kuwa chaelea baharini!
never give up dat easily..
ukiona vyaelea jua fika vimeundwa, ila je VYAELEA PANAPOSTAHILI!??
 
mara nyingi huwa tunajisahau.........tukifikiri ni sisi tu wenye meno kumbe wenye nayo tuko wengi na vingine vilikwishatafunwa na wengine..................kwa hiyo tunatakiwa twenda polepole...tukisoma khali ya upepo.... Manyanza

na sijui kama nini wanaume tumekua dhaifu sana mbele ya wanawake? mkuu kwenda pole pole haiwezekani bana ukiona totozi lazima uanze kujipanga ili kuing'oa
 
Last edited by a moderator:
huenda kweli vimeundwa ila aliyeviunda labda hajui kuvitumia..au havitumii ipasavyo
basi, huenda ikawa ndiyo bahati yako hapo kwamba wewe ndiye uliyekuwa ukingojewa to make a full utilization of kile kilichokuwa chaelea mtoni ilhali kilitakiwa kuwa chaelea baharini!
never give up dat easily..ukiona vyaelea jua fika vimeundwa, ila je VYAELEA PANAPOSTAHILI!??

haya pia yaezekana kwani hata maandiko husema nayepnda siye atakayevuna.................lakini aliyepanda si ni mzazi na huyu aliyenaye si ndiye mvunaji au wataka kusema havuni vizuri?[MENTION]@Mentor[/MENTION]
 
na sijui kama nini wanaume tumekua dhaifu sana mbele ya wanawake? mkuu kwenda pole pole haiwezekani bana ukiona totozi lazima uanze kujipanga ili kuing'oa

angalia isije kukun'oa meno yako mwenyewe...............[MENTION]@manyanza[/MENTION]
 
mara nyingi huwa tunajisahau.........tukifikiri ni sisi tu wenye meno kumbe wenye nayo tuko wengi na vingine vilikwishatafunwa na wengine..................kwa hiyo tunatakiwa twenda polepole...tukisoma khali ya upepo.... Manyanza

Vipi kuhusu kina kaka? Unamuona kaka mtanashati.......... usafiri mzuri...... anapendeza, tunaanza kumrembulia macho na kutikisa makalio...... kumbe ana mkewe ambaye wamesota naye sana tu. Na pengine ungemuona kipindi anachapa lapa na bahasha ya kazi yenye CV na vyeti, kikwapa kwa mbali ......wala usingemuangalia mara mbili.....

My point is ni pande zote!
 
Last edited by a moderator:
ishinde tamaa....tatizo wanaume wa sasa macho manne

mnajipamba mno kwa malengo ya kututia tamaa............khalafu mwatuambia tuishinde tamaa....... Vaislay
 
Last edited by a moderator:
Mkuu siku hizi nani anafanya hii kazi ya kukufundisha haya mambo
Naomba unipe no ya huyo mtaalam uliyempata maana aise naona vtu vinashuka tuu bila hata mgogoro
Asante sana mkuu kwa hii useful post
 
Mkuu siku hizi nani anafanya hii kazi ya kukufundisha haya mambo
Naomba unipe no ya huyo mtaalam uliyempata maana aise naona vtu vinashuka tuu bila hata mgogoro
Asante sana mkuu kwa hii useful post

Mwenyezi Mungu kanijaza roho Mtakatifu.................na hizi busara zinatoka mbinguni
 
Vipi kuhusu kina kaka? Unamuona kaka mtanashati.......... usafiri mzuri...... anapendeza, tunaanza kumrembulia macho na kutikisa makalio...... kumbe ana mkewe ambaye wamesota naye sana tu. Na pengine ungemuona kipindi anachapa lapa na bahasha ya kazi yenye CV na vyeti, kikwapa kwa mbali ......wala usingemuangalia mara mbili.....

My point is ni pande zote!

Kaunga uko juu sana.........sikupenda kuangalia upande wa pili wa shilingi kwa sababu zilizodhahiri..........msije mkalalama ya kuwa mwamba ngoma huvutia kwake..............[MENTION]@Kaunga[/MENTION]
 
Back
Top Bottom