Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,172
Mwanadamu alivyoumbwa ni mwepesi kughafilika na kupagawa...
Hupenda vya mvunguni lakini masharti yake hayawezi........
Hupenda vya kunyonga lakini vya kuchinja huvikwepa.......
Hupenda vya mteremko lakini vya kuhenya kuvigwaya.......
Lakini ukiona vyaelea ujue fika vimeundwa.
Nashangaa kumwona kijana mtanashati akimfukuzia binti hata hamjui......
Kisa binti kapendeza, nguo zimemkaa huku akimeremeta.......
Kijana damu humchemka na kujipiga moyo konde.......
Bila hata ya kujiuliza hivi ni yeye tu mwenye macho ya kuangaza-angaza?
Lakini ukiona vyaelea ujue fika vimeundwa.
Kijana wa watu hupoteza hamu ya kula..........
Shughuli zake zote kuziona ni nuksi.......
Kisa ni kuwa bila ya kumpata yule binti yeye sasa mfu............
Kijana kuhangaika usiku na mchana kumnasa mrembo.....
Lakini ukiona vyaelea ujue fika vimeundwa.
Siku ya siku kijana akutana na binti......
Kiroho kikimdunda na kijasho kumdondoka amwaga sera.............
Mrembo amwelewa lakini ampa pole.............
Ukweli wafichuka kumbe mrembo ana mwenyewe.................
Lakini ukiona vyaelea ujue fika vimeundwa.
Hupenda vya mvunguni lakini masharti yake hayawezi........
Hupenda vya kunyonga lakini vya kuchinja huvikwepa.......
Hupenda vya mteremko lakini vya kuhenya kuvigwaya.......
Lakini ukiona vyaelea ujue fika vimeundwa.
Nashangaa kumwona kijana mtanashati akimfukuzia binti hata hamjui......
Kisa binti kapendeza, nguo zimemkaa huku akimeremeta.......
Kijana damu humchemka na kujipiga moyo konde.......
Bila hata ya kujiuliza hivi ni yeye tu mwenye macho ya kuangaza-angaza?
Lakini ukiona vyaelea ujue fika vimeundwa.
Kijana wa watu hupoteza hamu ya kula..........
Shughuli zake zote kuziona ni nuksi.......
Kisa ni kuwa bila ya kumpata yule binti yeye sasa mfu............
Kijana kuhangaika usiku na mchana kumnasa mrembo.....
Lakini ukiona vyaelea ujue fika vimeundwa.
Siku ya siku kijana akutana na binti......
Kiroho kikimdunda na kijasho kumdondoka amwaga sera.............
Mrembo amwelewa lakini ampa pole.............
Ukweli wafichuka kumbe mrembo ana mwenyewe.................
Lakini ukiona vyaelea ujue fika vimeundwa.