Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,597
- 215,268
Ukiona Rais wa nchi analindwa kwa ulinzi wa hali ya juu sana, kwa mitutu na wanajeshi wengi, ujue huyo Rais hayupo hapo alipo kwa kura za wananchi wa Taifa hilo. Hivyo muda wote ana wasiwasi ya kuondolewa kwenye kiti alichakalia kibatili.
Ukiona Rais analazimisha kila mwananchi amuimbe yeye tu. Ujue hana uhakika na kuchaguliwa tena na Wananchi kwa awamu inayofuata, hivyo analazimika kulazimisha kila raia kumuimba yeye ili kuaminisha watu kuwa anakubalika.
Ukiona Rais wa nchi analazimisha watumishi wa Umma (wanaolipwa kodi za Wananchi) kumuimba yeye na kuwalazimisha Watumishi hao kujiunga na chama chake yeye, maana yake Rais huyu anajua kabisa kuwa hajawatimizia mahitaji muhimu watumishi hawa hivyo ili kutokumsumbua katika madai ni kuwatisha na kuwalazimisha wote wawe waimbaji wake wa mapambio.
Ukiona Rais wa nchi analazimisha kupendwa na kila mtu kwenye Taifa, ujue Rais huyo ana matatizo binafsi. Haelewi hata anachokifanya, maana anapingana na nature na ukweli wenyewe wa mambo kuwa, watu hawawezi kuwa na mtazamo sawa.
Ukiona Rais wa nchi hataki wapinzani wake wazungumze, wahoji na kuwachukulia Wapinzani wake kama "wahaini" katika Taifa, ujue Rais huyu katika Serikali aliyopo imefanya maovu mengi sana kuliko kawaida. Ikiwemo, mauaji ya raia, wizi, ubadhirifu n.k
Ukiona Rais wa nchi analazimisha watu wote kuikubali Serikali na kumkubali Rais kwa kila anachokifanya, ujue Rais huyo hajatekeleza mambo ya Wananchi badala yake ametekeleza matamanio yake na kuacha mahitaji ya Wananchi. Hivyo anawalazimisha Wananchi wakubali kuwa, matamanio ya Rais huyo ndio mahitaji ya Wananchi.
Unaweza kuongeza na wewe ndugu msomaji!!
Mohonia Joseph
Ukiona Rais analazimisha kila mwananchi amuimbe yeye tu. Ujue hana uhakika na kuchaguliwa tena na Wananchi kwa awamu inayofuata, hivyo analazimika kulazimisha kila raia kumuimba yeye ili kuaminisha watu kuwa anakubalika.
Ukiona Rais wa nchi analazimisha watumishi wa Umma (wanaolipwa kodi za Wananchi) kumuimba yeye na kuwalazimisha Watumishi hao kujiunga na chama chake yeye, maana yake Rais huyu anajua kabisa kuwa hajawatimizia mahitaji muhimu watumishi hawa hivyo ili kutokumsumbua katika madai ni kuwatisha na kuwalazimisha wote wawe waimbaji wake wa mapambio.
Ukiona Rais wa nchi analazimisha kupendwa na kila mtu kwenye Taifa, ujue Rais huyo ana matatizo binafsi. Haelewi hata anachokifanya, maana anapingana na nature na ukweli wenyewe wa mambo kuwa, watu hawawezi kuwa na mtazamo sawa.
Ukiona Rais wa nchi hataki wapinzani wake wazungumze, wahoji na kuwachukulia Wapinzani wake kama "wahaini" katika Taifa, ujue Rais huyu katika Serikali aliyopo imefanya maovu mengi sana kuliko kawaida. Ikiwemo, mauaji ya raia, wizi, ubadhirifu n.k
Ukiona Rais wa nchi analazimisha watu wote kuikubali Serikali na kumkubali Rais kwa kila anachokifanya, ujue Rais huyo hajatekeleza mambo ya Wananchi badala yake ametekeleza matamanio yake na kuacha mahitaji ya Wananchi. Hivyo anawalazimisha Wananchi wakubali kuwa, matamanio ya Rais huyo ndio mahitaji ya Wananchi.
Unaweza kuongeza na wewe ndugu msomaji!!
Mohonia Joseph