James Martin
JF-Expert Member
- Apr 2, 2016
- 1,206
- 1,509
Siku chache za nyuma nilimsikia mgombea wa urais wa CCM akiwaonya wapiga kura. Aliwaambia kwamba wasipomchagua mgombea wa CCM watakosa maendeleo. Pia alisema kwamba sababu iliyofanya eneo lao kukosa lami ni kutokana na wao kumchagua mbunge wa upinzani.
Kutokana na kauli hizo kuna mambo mawili nimejifunza. Kwanza, uwezo wake wa kufikiri ni hafifu. Pili, ni mtu asiyeaminika.
Kwa kuanza na sababu ya kwanza ni kwamba, huyu mtu anafikiri pesa ya serikali ni yake binafsi. Ana mawazo finyu mpaka anajisahau kwamba hata wanaowapigia kura wapinzani pia wanalipa kodi na wanastahili kuona matunda ya jasho lao.
Nimetaja pia kuwa huyu bwana ni mtu asiyeaminika. Hii ni kwasababu kauli zake zinapingana. Wakati mwingine utamsikia akisema maendeleo hayana chama halafu anajisahau na ku wa "blackmail" wapiga kura ili kuwashurutisha wawachague wagombea wa CCM.
Kwa tabia hizi mbili alizo nazo anakosa kabisa sifa za kuwa rais.
Kutokana na kauli hizo kuna mambo mawili nimejifunza. Kwanza, uwezo wake wa kufikiri ni hafifu. Pili, ni mtu asiyeaminika.
Kwa kuanza na sababu ya kwanza ni kwamba, huyu mtu anafikiri pesa ya serikali ni yake binafsi. Ana mawazo finyu mpaka anajisahau kwamba hata wanaowapigia kura wapinzani pia wanalipa kodi na wanastahili kuona matunda ya jasho lao.
Nimetaja pia kuwa huyu bwana ni mtu asiyeaminika. Hii ni kwasababu kauli zake zinapingana. Wakati mwingine utamsikia akisema maendeleo hayana chama halafu anajisahau na ku wa "blackmail" wapiga kura ili kuwashurutisha wawachague wagombea wa CCM.
Kwa tabia hizi mbili alizo nazo anakosa kabisa sifa za kuwa rais.