Mindi
JF-Expert Member
- Apr 5, 2008
- 3,523
- 4,991
Usikimbie hoja. Hoja hapa ni nini hasa maana ya "maendeleo". Wewe umeeleza maendeleo kama ni ujenzi wa miundombinu. Sasa hapo juu ndio umefafanua zaidi. Hoja yangu ni kwamba uhuru wa watu ni muhimu zaidi. Watu ndio waamue wanataka nini hasa.Tatizo la Tanzania vijana wengi ukiwemo ww mwenyew elimu zenu zimeshindwa kuwasaidia kuchanganua mambo ya msingi sababu ya siasa. Cha kusikitisha hao waliowafanya mshindwe kuchanganua mambo sababu ya siasa uchwara kama vile kina Mbowe, Lisu, Lema nk watoto wao wanasoma na kukaa mbali sana na siasa kwa ajili ya faida zao na vizazi vyao. Kwani washagundua kwamba ukiendekeza au kuingiza siasa katika kila jambo la msingi basi kuna nafasi kubwa ya kuharibikiwa katika maisha na elimu yao itakuwa haina maana tena kwao. Ebu fikiria mtu mwenye elimu yako unatoaje mfano wa kipuuzi hivi bila kuishirikisha akili yako vizuri? Makaburu walitoka ulaya kuja kuiba, kubagua na kutawala wenyeji. Lakini serikali ya Tanzania inatokea Tanzania na inaongozwa na Watanzania halisi. Makaburu (kama wageni) waliwabagua weusi (wenyeji) wasifanye kazi katika serikali na ofisi za umma kwa sababu ya rangi zao. Tanzania watu wanafanya kazi katika mashirika mbali mbali ya serikali na kibinafsi bila kujali vyama vyao, rangi zao, dini zao na jinsia zao ilimradi tu uwe na vigezo vya utanzania, elimu au uzoefu. Makaburu hawakutaka weusi (wenyeji) wafike mjini au sehemu wanazoishi weupe bila kibali maalumu. Tanzania mtu yoyote, wa chama, dini, jinsia au rangi yoyote yupo free kuishi mahali popote bila bughudha yoyote. Makaburu hawakujenga, shule, barabara wala miundo mbinu mizuri sehem waliyoishi watu weusi. Sisi huku raisi anataka kusambaza umeme, maji, barabara, shule na hospital nchi nzima ili iwe rahisi watanzania kuzipata huduma hizo karibu na maeneo yao na kwa haraka zaidi. So ni ujinga kufananisha yaliyotokea kaburu na yanayoendelea Tanzania kwani kuna utofauti mkubwa mno. Swala la katiba linataka kutumiwa na wapinzani kama kichochoro cha kupiga hela katika vikao vya katiba na kuvimbisha account zao kwa ajili ya future za watoto wao na familia zao, huku huduma za maji, umeme, barabara, hospital nk zikiwa zimekufa kwa sababu ya kuelekeza hela zote katika vikao hivyo. So swala la katiba kwa sasa msahau maana halina tija. Ni bora mkaliweka kwenye ilani yenu ya mwaka 2025.
Tanzania hakuna Uhuru wa kutoa maoni. Kuna magazeti mengi yamefutwa kabisa, mengine yamefungiwa. Kisa? Yalisema UKWELI ambao hauifurahishi serikali.
Tanzania pia kuna ubaguzi mkubwa sana. Raia daraja la kwanza ni wale wanaoshabikia ccm na serikali yake. Raia daraja la TANO ni wale wanaoshabikia UPINZANI. Na ukumbuke, hii ni nchi ya Demokrasia ya Vyama Vingi, kwa mujibu wa katiba, Sheria na Kanuni. Lakini bado, kwa UDHAIFU wa Katiba yetu, hawa wa daraja la TANO wanaweza kuteswa, kunyanyaswa, kupotezwa, kuuwawa, kirahisi tu na hakuna anayetaharuki au kushangaa.
Nimesema habari ya Magazeti kufungiwa. Kuna gazeti la Uhuru karibuni limefanya kosa kubwa sana. Limeandika habari ya uchochezi dhidi ya Rais. Angalia adhabu yao: kufungiwa wiki mbili!
Tunachotaka hii ni nchi yetu sote. Wote ni watanzania. Kukiwa na uhuru wa maoni, Magazeti yafumue uozo. Yakikosea si mahakama zipo? Serikali ifungue shauri. Bunge liwe kweli Bunge la vyama vingi. Sio wapinzani wanahujumiwa kihunihuni tu, na mambo yanakwenda.
Msikilize Bashiru Ali kuhusu Katiba Mpya: