Ukimya wa rais unatia shaka

SONGOKA

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
1,843
1,841
Ni jambo lakushangaza, kustaajabisha na kuchukiza kwamba Toka alipowasili jumamosi JK hajasema lolote kuhusu kashfa ya escrow zaidi ya ule mzaha aliofanya pale airport.

Hata kutwambia amelichukuliaje swala hili licha ya BUNGE kuthibitisha kuwa pesa ya UMMA imeibwa. Hajalaani, hajashtushwa, hajakasirika, wala kushangazwa (hamna kauli yeyote kutoka IKULU)


Billion 321 zimeibwa na wahuni nchini mwake, leo siku ya tatu toka mapendekezo yamepitishwa lakini JK yuko kimya, kajifungia IKULU. TUKUELEWEJE?

Hata kutoa press release ya kulaani kitendo hiki umeshindwa. Au umeanzisha uchunguzi mpya???hata umeogopa kuhutubia nchi mwanzo wa mwezi

Kwa rais serious na mwenye uchungu na nchi yake Jumatatu angeshatangaza kuwatimua woote waliofanya kadhia hii kwa mujibu wa maadhimio ya BUNGE, hivi bado unajiuliza nini?Hivi ni Kweli hii nchi iko auto pilot?

MH rais hatukuelewi na hueleweki
.
 
1.hamumuelewi wewe na nni? Usitusemee, wengine tunamuelewa, au wewe ni msemaji wa watz? Kama ndio, tangu lini?
2. Acha kihere here, soma magazeti ya leo kama shida yako ni tamko la ikulu
3.rais hafanyi mambo kwa kukurupuka
 
1.hamumuelewi wewe na nni? Usitusemee, wengine tunamuelewa, au wewe ni msemaji wa watz? Kama ndio, tangu lini?
2. Acha kihere here, soma magazeti ya leo kama shida yako ni tamko la ikulu
3.rais hafanyi mambo kwa kukurupuka

umerupuka wewe,
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Uelewe! Tatizo si JK; tatizo ni katiba, tatizo ni watanzania! Kashifa hii inamkumba JK mwenyewe lakini nani amguse? Katiba hairuhusu, na hata hiyo iliyopendekezwa na ccm inamwendelezo huo huo na hatujakoma kusikia majigambo ya ubora wa katiba hiyo. Anayo madaraka makubwa ya udikiteta wa kukataa au kukubali mapendekezo ya bunge, atakalo changua ndo hilo...kuwa tayali kupokea maamuzi yake...ila asisurutishwe cha nini afanye.
 
Uelewe! Tatizo si JK; tatizo ni katiba, tatizo ni watanzania! Kashifa hii inamkumba JK mwenyewe lakini nani amguse? Katiba hairuhusu, na hata hiyo iliyopendekezwa na ccm inamwendelezo huo huo na hatujakoma kusikia majigambo ya ubora wa katiba hiyo. Anayo madaraka makubwa ya udikiteta wa kukataa au kukubali mapendekezo ya bunge, atakalo changua ndo hilo...kuwa tayali kupokea maamuzi yake...ila asisurutishwe cha nini afanye.
Wewe unapiga mayowe tu, Bunge lina mamlaka ya kupiga kura ya kutokuwa na imani na rais, angekuwa anahusika hakuna aliyekuwa anawazuia.
 
Kukaa kimya kuna maana nyingi na mwenye busara huwa hana haraka, MAVUVUZELA tu ndiyo wanawez kukurupuka
 
1.hamumuelewi wewe na nni? Usitusemee, wengine tunamuelewa, au wewe ni msemaji wa watz? Kama ndio, tangu lini?
2. Acha kihere here, soma magazeti ya leo kama shida yako ni tamko la ikulu
3.rais hafanyi mambo kwa kukurupuka
Mkuu umeandika kwa busara sana.

Kuna watu wanajifanya wao ndio wasemaji wa watanzania.
 
1.hamumuelewi wewe na nni? Usitusemee, wengine tunamuelewa, au wewe ni msemaji wa watz? Kama ndio, tangu lini?
2. Acha kihere here, soma magazeti ya leo kama shida yako ni tamko la ikulu
3.rais hafanyi mambo kwa kukurupuka

kwan ww unamuelewa na nan mbona nawe umewasemea wenzako.
hta hvo angeonyesha hta kush2shwa na hli jambo ka anajali!
 
Ni jambo lakushangaza, kustaajabisha na kuchukiza kwamba Toka alipowasili jumamosi JK hajasema lolote kuhusu kashfa ya escrow zaidi ya ule mzaha aliofanya pale airport.

Hata kutwambia amelichukuliaje swala hili licha ya BUNGE kuthibitisha kuwa pesa ya UMMA imeibwa. Hajalaani, hajashtushwa, hajakasirika, wala kushangazwa (hamna kauli yeyote kutoka IKULU)


Billion 321 zimeibwa na wahuni nchini mwake, leo siku ya tatu toka mapendekezo yamepitishwa lakini JK yuko kimya, kajifungia IKULU. TUKUELEWEJE?

Hata kutoa press release ya kulaani kitendo hiki umeshindwa. Au umeanzisha uchunguzi mpya???hata umeogopa kuhutubia nchi mwanzo wa mwezi

Kwa rais serious na mwenye uchungu na nchi yake Jumatatu angeshatangaza kuwatimua woote waliofanya kadhia hii kwa mujibu wa maadhimio ya BUNGE, hivi bado unajiuliza nini?Hivi ni Kweli hii nchi iko auto pilot?

MH rais hatukuelewi na hueleweki
.


Mkuu kwani hukumsikia profesa alipokuwa anaongea kwenye ile press conference? Prof. alisema wazi kabisa mshono wa "tezi dume" bado haujapona hivyo anatakiwa kupumzika, mpe muda auguze operation ya tezi dume.
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom